DON’T BE AFRAID WHEN YOU GO DOWN.

Nifanyeje niwe mwombaji mzuri, wa masafa marefu?

SWALI: Nifanyeje niwe mwombaji mzuri, wa masafa marefu na sio mtu wa kuomba omba tu, ilimradi?


JIBU: Katika vita lazima ujue adui wako mkuu ni nani.. Bwana Yesu alisema maneno haya;

Mathayo 26:40-41

[40]Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja?

[41]Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.

Hapa  Bwana alitarajia, wakeshe, Yaani waombe naye masafa marefu, (kama vile wewe unavyotamani uwe na nguvu hata ya kukesha katika maombi mpaka asubuhi), lakini kinyume chake, hawakuweza kumaliza hata Saa moja..matumaini yao yaliishia katikati..

Lakini Bwana Yesu alipowakuta wamelala hakuwaambia kemea pepo hilo la uchovu, au wachawi hao waliotumwa kuwafanya mpige pige miayo ya usingizi, muda wote muombapo..

Bali aliwaambia maneno haya “ROHO I RADHI, LAKINI MWILI NI DHAIFU”..Akiwa na maana roho zao kweli zilikuwa zinatamani kukesha naye kule bustanini…na ndio maana walitii wito wa kwenda kuomba..kama roho zao zisingekuwa  radhi kufanya vile muda ule wangekuwa vitandani mwao wamelala..

Lakini Bwana anawaambia kikwazo ni nini.? Kikwazo ni MIILI yao.. Huyo ndio adui wao wa kwanza wanapaswa wamuangalie, sana

Tunashindwa kuomba, hata wakati mwingine kusoma Neno,..kwasababu ya mwili,..Lakini kama tukishindana na mwili ipasavyo basi tutaweza fungua milango mingi ya rohoni.

Sasa tutawezaje kuwa hivyo?

Ni kujitengenezea ”pumzi ya kiroho”..Kama vile wanariadha wafanyavyo katika mwili, kwa kawaida yule anayefanya mazoezi sana, huwa anajiongezea pumzi ya kukimbia umbali mrefu zaidi kuliko yule asiyefanya mazoezi yoyote, Atakimbia mzunguko mmoja tayari hoi.

Unapotaka uwe mwombaji mzuri, hata wa masafa marefu, ni lazima uanze kidogo kidogo, ukikumbuka kuwa adui wako wa kwanza sio shetani bali ni mwili wako..

Hivyo unaanza siku ya kwanza kuomba  dakika 15,  kesho huna budi kuongezea nyingine 5, kesho kutwa yake nyingine 5, hivyo hivyo, bila kurudi nyuma, Sasa kwa jinsi utakavyozidi kuongeza muda wako katika maombi ndivyo utakavyoona wepesi wa kuomba..

Kipindi cha mwanzoni utaona ni shida kumaliza saa moja katika maombi…lakini kama utakuwa ni mtu wa kuomba kila siku, utaona ni jepesi sana kama tu vile unavyoomba dakika 10..

Hautatumia nguvu kufikia huo muda, kwasababu tayari pumzi ya maombi ipo ndani yako.

Pengine jambo usilolijua ni kuwa wewe usiyeomba unaweza  kudhani yule anayeweza kukesha saa nyingi katika kuomba, anapata shida sana..lakini ukweli ni kwamba wewe ambaye unasali dakika chache, ndio unayechoka sana kuliko yule..kwasababu kuna kilele fulani mtu anayeomba  huwa anakifikia ile raha ya maombi inaingia ndani yake..wala haoni ugumu wa kuendelea mbele.

Hivyo jitahidi sana..Kushindana na mwili wako, ondoa mawazo yako sana kwa shetani, ni kweli upo wasaa ibilisi atataka kuvuruga ratiba zetu za maombi, lakini si jambo la kila siku…pindi unaposikia tu kuomba unalala, halafu unasema ni shetani…Ni huo mwili wako ndugu..

Anza leo kujizoeza kuomba. Shindana na usingizi, shindana na uchovu, shindana na uvivu.

Na hatimaye utakuwa mwombaji bora..Pia usingoje kuombewa, ombewa tu muda wote, vilevile usiseme Namwachia Mungu mwenyewe afanye, na ilihali hutaki kuomba..utapata hasara..Muda mwingine Kristo anasimama kutuombea..lakini wakati mwingine anataka kusimama na sisi kuomba, Kama alivyowaambia mitume wake hapo. Kesheni pamoja nami.

Mambo muhimu yatakayoweza kukupeleka rohoni haraka sana katika uombaji wako, Ni yapi?

  • Hakikisha kabla ya maombi..pata muda kidogo kukaa katika utulivu ukiwa umefunga macho..tafakari mambo yote mazuri, Mungu aliyokufanyia tangu utotoni mpaka hapo ulipofikia, kisha mpe shukrani, tafakari, uumbaji wa Mungu, tafakari, mbinguni siku ile utakapofika, tafakari mambo yote mazuri ya Mungu. N.k.
  • Pata muda tena wa kumsifu na kumwabudu kwa kinywa chako..imba nyimbo chache za shukrani na za kumtukuza Mungu.
  • Baada ya hapo mimina moyo wako mbele za Bwana, kwa kumwomba rehema na msamaha kwa makosa yako yote..

Kisha baada ya hapo ndio uingie moja kwa moja katika vipengele vyako vya maombi.

Zingatia hayo, na Mungu atakutia nguvu, katika hatua zako za maombi.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

TUTAWEZAJE KUMZALIA MUNGU MATUNDA?

YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

Kuna tofauti gani kati ya SALA na DUA?

Marago ni nini? ( Waamuzi 10:18)

MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.

Ijumaa kuu ni nini? Na kwanini iitwe kuu?

FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

Midiani ni nchi gani kwasasa?.

Midiani kwasasa ni eneo la Mashariki mwa nchi ya Saudi-Arabia, Kusini mwa nchi ya Yordani. Asili ya waMidiani ni Ibrahimu.

Maandiko yanaonyesha baada ya Sara kufa, Ibrahimu alimwoa mwanamke mwingine aliyeitwa Ketura, na huyu Ketura, alikuja kuzaa Watoto 6 wa kiume , na mmojawapo wa Watoto hao aliitwa Midiani, ambaye ndiye Baba wa wa-Midiani.

Mwanzo 25:1 “Ibrahimu alioa mke mwingine jina lake akiitwa Ketura.

2 Akamzalia Zimrani, na Yokshani, na Medani, na MIDIANI, na Ishbaki, na Sua”.

Wamidiani walikuwa wanamwabudu Mungu wa Ibrahimu isipokuwa si katika sheria za Musa kama Israeli walivyofanya, kwasababu Torati ilikuja miaka mingi baada ya Midiani kuwa Taifa kubwa.

Wamidiani walimtumikia Mungu katika mfumo wa sadaka za kafara kama alivyofanya Ibrahimu, hawakumjua Mungu kwa mapana ( yaani katika sheria kama Israeli walivyomjua walipokuwa jangwani). Na hiyo ni kwasababu ahadi ya agano Mungu aliyompa Ibrahimu,  ilikuwa ni kwa Ibrahimu na mwanaye  Isaka mwana wa Sara na si kwa wana wa Ketura.

Hivyo wamidiani walimtumikia Mungu wa Ibrahimu lakini si kwa usahihi wote. Ndio maana tunakuja kumwona Mkwewe Musa aliyeitwa Yethro (au Reuli) ambaye alikuwa ni Mmidiani kwa asili, maandiko yanasema alikuwa ni “kuhani” wa nchi hiyo ya Midiani (soma Kutoka 2:16).

Ikiwa na maana kuwa alikuwa anafanya kazi za kikuhani kama Haruni lakini si katika ukamilifu wote kama walivyokuwa wanafanya akina Haruni na wanawe.

Hivyo kwaasili waMidiani walikuwa ni ndugu ya Israeli kupitia Ibrahimu. Lakini baadaye tunakuja kusoma wamidiani waligeuka na kuwa madui wa kubwa wa Israeli, kipindi Israeli wanatoka Misri kuelekea Kaanani hawa wamidiani walijiunga na WaMoabu na kumwajiri mtu aliyeitwa Balaamu ambaye alikuwa ni mchawi kutoka Midiani kuja kuwalaani, jambo ambalo lilimchukiza sana Mungu, na kufanya Mungu awalipize kisasi wamidiani kwa kosa hilo.

Hesabu 31:1 “Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,

2 Walipize kisasi wana wa Israeli juu ya Wamidiani; kisha baadaye utakusanywa uwe pamoja na watu wako.

3 Basi Musa akanena na watu, na kuwaambia, Wavikeni silaha watu miongoni mwenu waende vitani, ili waende kupigana na Midiani, wapate kumlipiza kisasi Bwana, juu ya Midiani”.

Lakini Ijapokuwa Mungu aliwapiga waMidiani karibia wote, lakini hawakuisha wote.. Wamidiani walikuja kunyanyuka tena na kuwa Taifa kubwa, na lenye nguvu kuliko hata Israeli.

Na miaka kadhaa baadaye Israeli walipomwacha Mungu, na kwenda kuabudu miungu mingine, Mungu aliwatia waisraeli mikononi mwa hawa Wamidiani wawatese, na Waisraeli wakateswa miaka 7 na waMidiani, mpaka walipomlilia Bwana, na kupelekewa mwokozi awaokoe (ambaye alikuwa ni Gideoni).

Waamuzi 6:1 “Kisha wana wa Israeli walifanya yaliyo maovu mbele za macho ya Bwana; Bwana akawatia mikononi mwa Midiani muda wa miaka saba

2 Mkono wa Midiani ulikuwa na nguvu juu ya Israeli; tena kwa sababu ya Midiani wana wa Israeli walijifanyia hayo mashimo yaliyo milimani, na hayo mapango, na hizo ngome.

3 Basi ikawa, hapo Israeli walipokuwa wamepanda mashamba, Wamidiani wakakwea, na Waamaleki, na hao wana wa mashariki; wakakwea juu yao;

4 wakapanga marago juu yao, na kuyaharibu hayo maongeo ya nchi, hata ufikapo Gaza, wala hawakuacha katika Israeli riziki ziwazo zote; kondoo, wala ng’ombe, wala punda.

5 Kwa maana walikwea na ng’ombe zao na hema zao, wakaja mfano wa nzige kwa wingi; wao na ngamia zao pia walikuwa hawana hesabu; nao waliingia katika hiyo nchi ili kuiharibu.

6 Israeli walitwezwa sana kwa sababu ya Wamidiani; nao wana wa Israeli wakamlilia Bwana.

7 Kisha ikawa, hapo wana wa Israeli walipomlilia Bwana kwa sababu ya Midiani,

8 Bwana akamtuma nabii aende kwa hao wana wa Israeli; naye akawaambia, Bwana, yeye Mungu wa Israeli, asema hivi, Mimi niliwaleta ninyi mkwee kutoka Misri, nikawatoa katika nyumba ya utumwa;

9 nami niliwaokoa na mikono ya Wamisri, na mikono ya wote waliokuwa wakiwaonea, nami niliwafukuza watoke mbele zenu, nami niliwapa ninyi nchi yao;

10 kisha niliwaambia, Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu; msiiche miungu ya Waamori, ambayo mwaketi katika nchi yao; lakini hamkuitii sauti yangu.

11 Malaika wa Bwana akaenda akaketi chini ya mwaloni uliokuwa katika Ofra, uliokuwa mali yake Yoashi, Mwabiezeri; na mwanawe Gideoni alikuwa akipepeta ngano ndani ya shinikizo, ili kuificha machoni pa Wamidiani.

12 Malaika wa Bwana akamtokea, akamwambia, Bwana yu pamoja nawe, Ee shujaa”.

Jamii ya Wamidiani kwasasa haipo, bali imemezwa na jamii nyingine za Arabia na Yordani na Misri, kiasi kwamba kwasasa hakuna ajijuaye kama yeye ni mmidiani au la!.

Lakini tunachoweza kujifunza kwa Habari ya Wamidiani ambao walikuwa ni maadui wa Israeli kwa kipindi chote, ni kuwa “maadui wanatabia ya kuchipuka tena”.

Wamidiani waliuawa karibia wote na mali zao kutekwa nyara na wa Israeli, kwaufupi ni kama vile walifutwa juu ya uso wa nchi, lakini tunaona walikuja kuchipuka tena na kuwa Taifa kubwa tena lenye nguvu kuliko Israeli, na tena likawatawala Israeli. Lakini hiyo yote ni matokeo ya Waisraeli kumwacha Mungu.

Vile vile na sisi tukimwacha Mungu, haijalishi yale magonjwa ambayo yalikuwa yameondoka miaka mingi na hatuyaoni tena, yatarudi tena na kuchipuka kwa nguvu na kutuangamiza!.

 Tukimwacha Mungu haijalishi tulikuwa na ushindi mkubwa kiasi gani dhidi ya mapepo na wachawi!, tukimwacha Mungu Watanyanyuka tena na kutudhuru na kututesa!.

Tukimwacha Mungu na kurudia ulevu, uzinzi, wizi, uvaaji mbaya, utukanaji…haijalishi tulikuwa na ushindi mkubwa dhidi ya shetani hapo kabla…atanyanyuka tena na jeshi lake kwa nguvu na kuteka nyara… Israeli hawakutegemea kama Taifa walilopiga na karibia kulitowesha kabisa, leo lingekuja kuwatawala kwa miaka 7 tena kwa utumwa mkali.

Na sisi hatuna budi kujifunza katika haya, ili tusifanya makosa waliyofanya Israeli.

1Wakorintho 10:11 “Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.

12 Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke”.

Bwana atusaidie nasi pia tusirudi nyuma.. kusudi tusije tukampa nguvu adui yetu shetani.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Je ni kweli Musa alikuwa mtu mpole kuliko wote duniani?

Ninawi ni nchi gani kwasasa?

Babeli ni nchi gani kwasasa?

Moabu ni nchi gani kwasasa?

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?.

Rudi nyumbani

Print this post

Marago ni nini? ( Waamuzi 10:18)

Marago ni mahali ambapo watu wanaweka makao ya muda kwa makusudi maalumu.

Kwamfano watu zamani walipokuwa wanakwenda vitani, waliweka makempu au makambi au mahema mahali mahali…hayo ndio yaliitwa marago..

Kwamfano ukisoma..

Waamuzi 10:17-18 inasema..

[17]Wakati huo wana wa Amoni walikutana pamoja, wakapanga marago huko Gileadi. Wana wa Israeli nao wakajikusanya wakapanga marago Mispa.

[18]Na hao watu, wakuu wa Gileadi, wakaambiana wao kwa wao, Je! Ni mtu yupi atakayeanza kupigana na wana wa Amoni? Yeye atakuwa ni kichwa juu ya wenyeji wote wa Gileadi.

Ikiwa na maana wote waliweka kambi zao za kijeshi huko Mispa.

Hali kadhalika Wana wa Israeli walipokuwa katika safari yao ya kuelekea nchi  ya ahadi waliweka makazi ya muda sehemu kadha wa kadha..

Kwamfano ukisoma..

Kutoka 29:13-14

[13]Kisha twaa mafuta yote yafunikayo matumbo, na kitambi kilicho katika ini, na figo mbili, na mafuta yaliyo juu yake, uyateketeze yote juu ya madhabahu.

[14]Lakini nyama yake huyo ng’ombe, na ngozi yake, na mavi yake, utayachoma kwa moto nje ya marago; ni sadaka kwa ajili ya dhambi.

Akiwa na maana hivyo viungo vya ndani watavichoma mbali na pale wana wa Israeli walipoweka makambi..

Neno hilo italisoma pia katika vifungu hivi;

Kutoka 36:6, Walawi 4:21, 10:5, Waamuzi 21:12.

Ni nini twajifunza kwa habari za marago.

Hata sisi hapa duniani ni kama tupo maragoni..Hatuna makazi ya kudumu..tumewekwa kwa makusudi maalumu..kusudi hilo likiisha..hakuna kukutanika tena..

Ibrahimu alilijua hilo..Kiasi kwamba japokuwa alikuwa na tajiri na mwenye mali nyingi..Moyo wake hakuuweka hapa duniani, hata kidogo..Bali kule kwenye mbingu mpya na nchi mpya(YERUSALEMU MPYA)..Na hiyo ndio ilikuwa sababu ya kuitwa Baba wa imani..Aliishi kama mpitaji hapa duniani..

Waebrania 11:9-10

[9]Kwa imani alikaa ugenini katika ile nchi ya ahadi, kama katika nchi isiyo yake, akikaa katika hema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi pamoja naye wa ahadi ile ile.

[10]Maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu….

[14]Maana hao wasemao maneno kama hayo waonyesha wazi kwamba wanatafuta nchi yao wenyewe.
[15]Na kama wangaliikumbuka nchi ile waliyotoka, wangalipata nafasi ya kurejea.
[16]Lakini sasa waitamani nchi iliyo bora, yaani, ya mbinguni. Kwa hiyo Mungu haoni haya kuitwa Mungu wao; maana amewatengenezea mji.

Je na sisi twaweza fanana na Ibrahimu?

Je tunaweza kuwa kama Ayubu ambaye japo alipoteza kila kila hakutetereka katika imani yake..kinyume chake ndio analibariki jina la Bwana.?

Hivyo nasi tuishi kama wapitaji. Kwasababu tukiwa ni watu wa namna hii, tunapata faida zote mbili kwanza ulimwengu hauwezi kutuzomba tukamsahau Mungu. Na pili Bwana atatubariki hata kwa hivyo tusivyovitazama..Kwasababu mioyo yetu haipo huko.

Bwana atusaidie.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Shetri ni nini kama tunavyosoma katika Marko 3:38?

Neno Buruji lina maana gani katika biblia?

Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)

Gumegume ni nini? (Isaya 50:7)

HERI WAPATANISHI, MAANA HAO WATAITWA WANA WA MUNGU

Easter ni nini?..Na je tunaruhusiwa kuisheherekea?

JIHUDHURISHE, ILI AANZISHE MAZUNGUMZO NA WEWE

Rudi nyumbani

Print this post

Shetri ni nini kama tunavyosoma katika Marko 3:38?

Jibu: Tusome,

Marko 4:35 “Siku ile kulipokuwa jioni, akawaambia, Na tuvuke mpaka ng’ambo.

36 Wakauacha mkutano, wakamchukua vile vile alivyo katika chombo. Na vyombo vingine vilikuwako pamoja naye

37 Ikatokea dhoruba kuu ya upepo, mawimbi yakakipiga chombo hata kikaanza kujaa maji.

38 Naye mwenyewe alikuwapo katika SHETRI, amelala JUU YA MTO; wakamwamsha, wakamwambia, Mwalimu, si kitu kwako kuwa tunaangamia?”.

Katika kisa hicho tunaona Wanafunzi walimchukua Bwana Yesu kama alivyo (yaani bila ya kitu chochote cha njiani kama vile chakula, au mavazi). Walimchukua kama alivyo..Na kumchukua kunakozungumziwa hapo ni kumchukua, kama vile mtu anavyomchukua mwenzake na kumpa lifti ya gari, ndivyo wanafunzi walivyomchukua Bwana Yesu..

Lakini tunaona walipokuwa njiani ndani ya ile Merikebu, Bwana Yesu alienda kulala katika Shetri ya Merikebu.

Sasa “SHETRI” au kwa lugha nyingine “TEZI”, ni sehemu ya Nyuma ya Meli au Merikebu, ambayo ni pana, na ndiyo iliyotumika katika kuwekea mizigo, na pia ndipo palipotengenezewa vyumba vya kulala watu. Sehemu ya mbele ya Meli au Merikebu inaitwa “OMO”, ambayo ni nyembamba ili kuisiaidia meli kukata mawimbi.

Sasa Bwana Yesu alienda kulala kwenye Shetri, mahali ambapo kulikuwa na nafasi ya kulala, na akawa amelala juu ya mto! (Mto unaozungumziwa hapa sio mto wa kutiririsha maji, bali ni ule mto wa kulalia kitandani, kuupatia shingo egemeo bora). Na akiwa Dhoruba ikaanza, na chombo kikakaribia kuzama..na Baadaye wanafunzi wakamwamsha Bwana na Bwana Yesu akaikemea ile Dhoruba ikatulia.

Sasa kikubwa tunachoweza kujifunza katika tukio hilo ni kuwa, Bwana Yesu anaweza kuwa yupo ndani yetu lakini amelala!. Tusipopaza sauti zetu kwa nguvu kwa maombi, basi tutahangaika na Dhoruba zilizopo nje, na wala yeye hatasema chochote.

Hii inatukumbusha kuwa waombaji, na si waombaji tu, bali waombaji wenye bidii, wenye kupaza sauti mpaka majibu ya maombi yatokee.

Bwana atusaidie katika hayo.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Ahera ni wapi? Kama tunavyosoma katika biblia.

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Bustani ya Edeni ipo nchi gani?

MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.

NI NINI TUNAJIFUNZA KWA DEMA NA MARKO?

Rudi nyumbani

Print this post

Je tunaruhusiwa kushirikiana na wasanii wa kidunia katika kumwimbia Mungu?

Swali: Je Ni sahihi  kimaandiko kwa mwimbaji wa nyimbo za injili kufanya collaboration na wasanii wa kidunia?..


Kabla ya kujibu swali hili, hebu tujiulize kwanza swali lifuatalo!. Je ni sahihi Mchungaji kumwalika mtu wa kidunia ambaye hajaokoka kabisa aje kuhubiri madhabahuni?. Kama jibu ni Ndio!, basi pia ni sahihi Mwimbaji wa nyimbo ya Injili kushirikiana na msanii wa kidunia katika kuimba, lakini kama jibu ni hapana!! basi pia si sahihi mwimbaji wa nyimbo za injili kushirikiana na mwimbaji wa nyimbo za kidunia kumwimbia Mungu.

Jambo moja lisilofahamika na wengi, hususani waimbaji wa nyimbo za Injili, ni kwamba hawajui kuwa Huduma ya kumwimbia Mungu, ni huduma kama ya Uchungaji tu!..Unaposimama kumwimbia Mungu, ni sawasawa na umesimama madhahabuni unahubiri, na unaonya na unawajenga watu kiroho, sawasawa na uchungaji tu, au uinjilisti….

Sasa Unaposhirikiana na mtu ambaye hajaokoka utakuwa unaiharibu kazi ya Mungu, badala ya kuijenga, umempandisha shetani madhabahuni ahubiri..kwasababu yule mtu ambaye hajaokoka anazo roho ndani yake, ambazo ni za mashetani…maisha yake yanaongozwa na shetani, aidha kwa kujua au kwa kutokujua..kama ni hivyo atawezaje kusimama kuwahubiria wengine waokoke, wakati yeye mwenyewe hajaokoka, atawashaurije wengine waache ulevi wakati yeye mwenyewe ni mlevi na mzinzi, atawaambiaje watu wawe wasafi mwilini wakati yeye mwenye mwili mzima umejaa tattoo?.

Umeona? Tunaweza kushirikiana na watu ambao hawajaokoka katika kufanya mambo mengine ya kimaisha kama kazi (ukiwa ofisini au shuleni, utashirikiana na watu ambao hawajaamini, haina madhara), au unaweza kuishi nao, au kula nao… lakini SI KUFANYA NAO KAZI ZA MADHABAHUNI!!!.

Bwana Yesu alikuwa anakula na watoza Ushuru, na makahaba na wenye dhambi wote… lakini hakuwahi kuwatuma Pamoja na wakina Petro wakahubiri Injili!!.. Hakuna mahali Bwana Yesu kamtupa Adrea na Farisayo mmoja au kahaba wakafanye collaboration katika kuhubiri Injili!.. Kwasababu hilo kundi bado lilikuwa linahitaji kwanza kuhubiriwa liokoke na si kwenda kufanya huduma!.

Kwahiyo na sisi kama Watumishi tulioitwa katika kuutangaza ufalme wa Mungu kwa njia ya nyimbo na nyinginezo.. na kama tunataka kushirikiana Pamoja na watu wengine ambao kwasasa ni wa kidunia, (bado hawajaokoka)..Sharti kwanza TUWABADILISHE WAOKOKE!!!, watubu dhambi zao na kubadilisha Maisha yao, na baada ya kuokoka na kupata wokovu kamili, wakae kwenye madarasa ya kumjua Mungu kwa kitambo Fulani, na wakishafikia kiwango Fulani cha ufahamu wa kumjua Mungu, ndipo tushiriki nao katika kufanya huduma ya kumwimbia Mungu au uinjilisti, Ili kazi ya Mungu isiharibike wala kutukanwa!!.

Kwahiyo kwa hitimisho, ni kwamba sio sahihi kushiriki Pamoja na wasio amini kutangaza Habari za ufalme wa mbinguni..

Bwana atubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Je ni sahihi kusikiliza miziki ya kidunia?.

USIWE ADUI WA BWANA

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

Je! Ni kanisa lipi sahihi kumuabudia Mungu?

Zaburi maana yake nini, katika Biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako.

SWALI: Je? Daudi na Yonathani walikua wanashiriki mapenzi ya jinsia moja?

Kufuatana na vifungu hivi;

1 Samweli 20:30

[30]Basi hasira yake Sauli ikawaka juu ya Yonathani, akamwambia, Wewe, mwana wa mke mkaidi, asi, je! Mimi sijui ya kuwa umemchagua huyo mwana wa Yese, kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako.


JIBU: Andiko hilo halina uhusiano wowote wa Yonathani na Daudi kuwa na mahusiano ya jinsia moja..

Wazo kama hilo linakuja kichwani mwa watu kufuatana na lile andiko linalosema upendo wa Jonathan kwa Daudi ulikuwa zaidi ya upendo wa mwanamke (2Samweli 1:26).Ambalo nalo halihusiani na jambo hilo kabisa.

Katika andiko hilo tunaona Sauli alipoona kwamba mwanawe Jonathani anashikamana sana na Daudi na kwamba yupo tayari hata kumwachia ufalme wake ambao alistahili yeye kuumiliki..ilimfanya Sauli aghadhibike sana juu yake ndipo akamwambia maneno hayo..

1 Samweli 20:30 “… je! Mimi sijui ya kuwa umemchagua huyo mwana wa Yese, kwa aibu yako mwenyewe, na kwa aibu ya uchi wa mama yako”.

“Aibu ya uchi wa mama yake”..Akiwa na maana “aibu ya mama yake aliyemzaa” na si vinginevyo .

Yaani kwa tendo lile la kumruhusu Daudi aje kuwa mfalme wa Israeli badala yake italeta aibu kubwa na fedheha kwa mama yake, kwa kuzaa mtoto ambaye haendelezi ufalme katika familia

Na ikumbukwe kuwa wa-mama wa wafalme enzi zile walikuwa wanapewa heshima kubwa kiasi cha kuwekewa kiti cha enzi pembezoni mwa wafalme . Na ndio maana utaona sehemu nyingi mfalme mpya atajwapo huwa anaambatanishwa na jina la mama yake, na sio mke au mtoto kwasababu walipewa heshima yao, kipekee. ( soma 2Wafalme 21:19, 22:1).

Sasa hapa inapotokea Yonathani hapiganii kiti chake cha ufalme kinyume chake ndio yupo tayari kumpa Daudi ufalme wote..Ndio maana Sauli akamwambia tendo analolifanya ni aibu kubwa sana kwa mama yake.

Hii inatufundisha nini?

Upendo usio wa kinafki unakuwa tayari kujishusha pale panapostahili kufanya hivyo.

Hautafuti mambo yake wenyewe..sawasawa na 1Wakorintho 13:5

Unawatanguliza wengine mbele..

Si ajabu ni kwanini Daudi hakuufananisha upendo ule na wa mwanamke yeyote duniani.

Na sisi pia tupendane, kwa kuwa tayari kutangulizana. Kumuhesabu mwingine ni bora zaidi yetu sisi wenyewe, Hiyo itatupa kibali kikubwa sana kwa Mungu. Kama vile Yonathani ambaye hadi leo hii tunazisoma habari zake kwa mema.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAMA, TAZAMA, MWANAO.

HERI WAPATANISHI, MAANA HAO WATAITWA WANA WA MUNGU

Upole ni nini?

Unyenyekevu ni nini?

MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI.

Matulizo ya mapenzi ni nini? (Wafilipi 2:1).

Kiyama ni nini?

YESU NDIYE ATAKAYEKURUSHIA MAWE, USIPOTUBU.

Wakati wakina Shadraka wanatupwa katika tanuru la moto, Danieli alikuwa wapi?

Rudi nyumbani

Print this post

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?.

Tusome,

Yohana 8:56 “Ibrahimu, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi”.

Jibu: Siku aliyoiiona Ibrahimu sio siku Kristo anamwaga damu yake pale Kalvari, kwaajili ya ondoleo la dhambi ya ulimwengu..

Sasa ni lini Ibrahimu aliiona hiyo siku?

Aliiona hiyo siku wakati anakutana na Melkizedeki, mfalme wa Salemu. Melkizedeki  maandiko yanasema alikuwa KUHANI WA MUNGU ALIYE JUU. (Hapa ndipo siri ya furaha ya Ibrahimu ilipokuwepo).

Melkizedeki alimjia Ibrahimu kama mtu, akiwa na mkate na Divai mkononi mwake, na akampatia Ibrahimu mkate ule na divai ile. Sasa Melkizedeki alikuwa ni Bwana Yesu Mwenyewe, aliyemtokea Ibrahimu kwa sura nyingine, na kwa umbile lingine, kabla ya wakati..

Waebrania 6:20 “alimoingia Yesu kwa ajili yetu, mtangulizi wetu, amekuwa kuhani mkuu hata milele kwa mfano wa Melkizedeki”.

Ndio maana, Bwana Yesu aliwaambia Wayahudi, kwamba kabla ya Ibrahimu kuwapo yeye (Yesu) alikuwapo..

Yohana 8:57 “Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe hujapata bado miaka hamsini, nawe umemwona Ibrahimu?

58 YESU AKAWAAMBIA, AMIN, AMIN, NAWAAMBIA, YEYE IBRAHIMU ASIJAKUWAKO, MIMI NIKO.

59 Basi wakaokota mawe ili wamtupie; lakini Yesu akajificha, akatoka hekaluni”

Kwahiyo tumeshaona kuwa aliyekutana na Ibrahimu alikuwa ni Bwana Yesu mwenyewe katika mwili. Lakini utaona huyu Melkizedeki (Kristo), alipokutana na Ibrahimu, hakumpa nyumba, wala mali, wala fedha, wala kingine chochote, bali alimpa MKATE na DIVAI.

Sasa huo Mkate na Divai Ibrahimu aliopewa na Melkizedeki.. ulikuwa ni ufunuo wa Mwili na Damu ya Yesu ambao atakuja kuutoa baadaye kwaajili ya uzima wa ulimwengu..

Yohana 6:51 “Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; mtu akila chakula hiki, ataishi milele. Na chakula nitakachotoa mimi ni mwili wangu, kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.

52 Basi Wayahudi walishindana wao kwa wao wakisema, Awezaje mtu huyu kutupa sisi mwili wake ili tuule?

53 Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu.

54 Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho.

55 Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli.

56 Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake ”.

Hiyo ndiyo sababu kwanini Bwana Yesu siku ile ya pasaka alitwaa Mkate na Divai na kuwapatia wanafunzi wake, na akaagiza tendo lile la kushiriki Mwili wake na damu yake liwe endelevu.

Kwahiyo Ibrahimu alipata ufunuo wa Melkizedeki, kuwa ni Melkizedeki ni Kuhani wa Mungu ambaye atakuja kuleta upatanisho kupitia Mwili wake na Damu yake, ambao unafananishwa na ule Mkate na Divai.

Kwahiyo kitendo hicho cha Ibrahimu kupata ufunuo wa ukuhani wa Melkizedeki, atakaokuja kuufanya siku za mbeleni, ndicho kilichomfanya ashangilie.

Na alishangilia kwasababu aliona Ulimwengu unakwenda kupatanishwa, unakwenda kuokolewa na Kuhani Mkuu, unakwenda kumkaribia Mungu kupitia huyu Melkizedeki..

Ndio maana utaona Ibrahimu hakumwona Melkizedeki kama Mfalme tu!, bali alimwona kama Kuhani Mkuu..

Sasa kabla ya kuendelea mbele hebu tujikumbushe kwa ufupi kuhani ni nani na kazi ya kuhani ni ipi?

Kuhani ni mtu Maalumu aliyeteuliwa na Mungu, kuwaunganisha watu na Mungu wao. Kwasababu katika kumkaribia Mungu kuna kanuni.. katika kumtolea kuna kanuni, vile vile katika kumwomba au kupeleka haja zetu kwake kuna kanuni. Sasa Mtu asipozijua hizi kanuni na akamwendea Mungu hataambulia chochote, au hata anaweza kujitia katika laana badala ya baraka kutokana na kutokujua kanuni.

Hivyo Makuhani ni watu maalumu waliokuwa wanazijua kanuni za kusogelea Mungu na kumsogeza Mtu kwa Mungu.. Ndio maana utaona wana wa Israeli walipotaka kumtolea Mungu, kulikuwa na taratibu za Namna ya kumtolea Mungu ili sadaka hiyo ikubalike, kwamba ilikuwa ni lazima Mwanakondoo achinjwe ipatikane damu, na kupitia ile damu kuhani anaingia nayo ndani ya hema na kufanya upatanisho wa yule mtu na muumba wake..

Sasa Ibrahimu alikuwa anajua umuhimu wa Ukuhani na Makuhani. Ndio maana siku hii alipokutana na Melkizedeki alifurahi.

Sasa kwanini alifurahi?.. Ni kwasababu huyu aliyekutana naye..alikuwa ni KUHANI, na sio kuhani tu!, bali kuhani MKUU!, na sio kuhani mkuu tu!, bali kuhani mkuu wa MILELE wa Mungu aliye juu. (Zaburi 110:4).

Mwanzo 14:18 “Na Melkizedeki mfalme wa Salemu akaleta mkate na divai, naye alikuwa KUHANI WA MUNGU ALIYE JUU SANA”

Ibrahimu alipojua kuwa Melkizedeki ni kuhani Milele, maana yake alijua kuwa hata siku yeye atakapokufa!, bado huyu kuhani atakuwepo..kwahiyo alimuona Melkizedeki akija tena miaka mingi baadaye akiwa na Mkate na Divai na kuupa ulimwengu mzima….

Alimuona Melkizedeki akija tena duniani, Pamoja na damu, ili kuwapatanisha watu na Mungu wao..Alimuona akiingia kwenye hema ya kimbinguni akifanya upatanisho, na aliona kupitia damu yake mwenyewe watu wanapatanishwa na Mungu. Hivyo alifurahi na kushangilia..

Waebrania 6:20 “alimoingia Yesu kwa ajili yetu, mtangulizi wetu, amekuwa kuhani mkuu hata milele kwa mfano wa Melkizedeki”.

Waebrania 5:9 “naye alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii;

10 kisha ametajwa na Mungu kuwa kuhani mkuu kwa mfano wa Melkizedeki”.

Hadi leo hii, huyu Kuhani Mkuu, Yesu.. yupo anaishi na ndiye mpatanishi wetu sisi na Baba. Wala hakuna wokovu kwa mwingine yeyote, wala hakuna njia nyingine yeyote ya kufika mbinguni isipokuwa kwa njia yake yeye.

Waebrania 8:1 “Basi, katika hayo tunayosema, neno lililo kuu ndilo hili: Tunaye kuhani mkuu wa namna hii, aliyeketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Ukuu mbinguni,

2 mhudumu wa patakatifu, na wa ile hema ya kweli, ambayo Bwana aliiweka wala si mwanadamu”.

Je umemwamini na kuoshwa dhambi zako naye?..kumbuka dini yako, tabia yako nzuri, sifa zako nzuri, dhehebu lako, na matendo yako havitakufikisha mbinguni kama utakuwa hujamwamini na kufuata kanuni zake za wokovu. Na kanuni yake ni kuamini, kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha, kubatizwa ubatizo sahihi na kupokea Roho Mtakatifu. Kama umeikosa hii kanuni basi wewe upo mbali na Mungu, haijalishi unaona mambo yako yanaenda sawa..

Mkaribie leo Yesu kuhani Mkuu upate wokovu.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

NI NINI BWANA ANATAZAMIA KILA TUNAPOSHIRIKI MEZA YAKE.

HUYU MELKIZEDEKI NI NANI?

KATIKA MLIMA WA BWANA ITAPATIKANA.

Je ni sahihi kumwita mtu “Mkuu”?

TUSIWE WAVIVU WA KUSIKIA.

Je ni lazima kushiriki Meza ya Bwana?

Rudi nyumbani

Print this post

Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.

Swali: Tunasoma katika Warumi 11:4, Mungu anasema kuwa “nimejisazia” lakini katika Wafalme tunasoma Mungu anasema “nitajisazia” kana kwamba ni kitendo kinachokuja mbeleni.. Je hapo mwandishi gani yupo sahihi?

Tusome:

Warumi 11:4 “Lakini ile jawabu ya Mungu yamwambiaje? “NIMEJISAZIA WATU ELFU SABA” wasiopiga goti mbele ya Baali”.

1Wafalme 19:18 “Pamoja na hayo NITAJISAZIA katika Israeli watu elfu saba, kila goti lisilomwinamia Baali, na kila kinywa kisichombusu”.

Jibu: Ni muhimu kufahamu kuwa siku zote biblia haijichanganyi.. isipokuwa fahamu zetu ndizo zinazojichanganya..

Ili kuelewa vizuri labda tuanze kusoma juu kidogo katika mstari huo 1Wafalme 19 ila tuanzie juu kidogo..

1Wafalme 19:14 “Akasema, Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana, Mungu wa majeshi; kwa kuwa wana wa Israeli wameyaacha maagano yako, na kuzivunja madhabahu zako, na kuwaua manabii wako kwa upanga; nami nimesalia, mimi peke yangu; nao wanitafuta roho yangu waiondoe.

15 Bwana akamwambia, Enenda, urudi njia ya jangwa la Dameski; ukifika, mtie mafuta Hazaeli awe mfalme wa Shamu.

16 Na Yehu mwana wa Nimshi mtie mafuta awe mfalme wa Israeli; na Elisha mwana wa Shafati wa Abel-Mehola mtie mafuta awe nabii mahali pako.

17 NA ITAKUWA ATAKAYEOKOKA NA UPANGA WA HAZAELI, YEHU ATAMWUA; NA ATAKAYEOKOKA NA UPANGA WA YEHU, ELISHA ATAMWUA.

18 Pamoja na hayo NITAJISAZIA katika Israeli watu elfu saba, kila goti lisilomwinamia “baali”, na kila kinywa kisichombusu”.

Katika Habari hiyo tunaona kuwa kumbe Mungu alikuwa amekusudia kuwaangamiza watu wote wanaobudu na kumsujudia baali. Lakini utaona wakati anataka kupitisha hukumu hiyo, akasema ATAJISAZIA yaani (atawabakisha) watu elfu 7 ambao hawamsujudii baali TANGU SASA.. yaani wakati wengine wote watakufa kwa upanga wa Hazaeli, Yehu au Elisha, Ambao utakuja baadaye.. hili kundi la watu elfu 7 lililopo sasa, litakuwa salama kwasababu halimsujudii Baali..

Kwahiyo Mwandishi wa Kitabu cha Warumi hajichanganyi na wa kitabu cha Wafalme, wote wapo sahihi

Ili tuelewe Zaidi labda tutafakari mfano huu.

“Umetenga magunia 10 ya makapi, na magunia 7 ya ngano.. na ukamwambia mtu mmoja kuwa “wiki ijayo utayachoma magunia yote ya makapi, na utabakiwa na magunia 7 ya ngano”. Na wakati wakati huo huo ukampa taarifa hiyo hiyo mtu mwingine kwa kusema “umejibakishia magunia 7 ya ngano ambayo hutayachoma moto wakati utakapoteketeza makapi”. Je! Kwa kauli hizo mbili utakuwa umejichanganya?.. jibu ni la!.. utakuwa umeelezea jambo lile lile ila kwa namna nyingine.. Ndicho Mwandishi wa kitabu cha Wafalme na Warumi walichoandika, kauli zao hazijakinzana bali zote zimelenga kitu kimoja na maana ile ile moja.

Lakini nini tunachoweza kujifunza hapo katika Habari hiyo?.. Tunachoweza kujifunza ni kuwa Mungu analitimiza neno lake na wala hasemi uongo.. aliwaondoa wote wanaoabudu baali na kuwasaza watu elfu 7 kama alivyosema..wasiopigia goti baali.

Na zama hizi za mwisho, unabii unasema Kristo atarudi kwaajili ya hukumu ya ulimwengu kwa wote wanaotenda maovu. Na neno lake kama alivyosema litatimia. Hivyo ni wajibu wetu sisi kusimama katika Imani kama tumeshampokea Yesu, na kama bado ni wakati wa kumpokea na kuiamini injili yake.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Baali alikuwa nani?

Je kauli ya Bwana Yesu inajichanganya? Katika Yohana 8:14 na Yohana 5:31?

Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?

Ni kiumbe gani kinachosujudiwa hapo katika Warumi 1:25?

Ahera ni wapi? Kama tunavyosoma katika biblia.

Rudi nyumbani

Print this post

TUKIO LA MUSA NA ELIYA KUMTOKEA BWANA, LIMEBEBA UJUMBE GANI?

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze maneno ya Uzima wa Mungu wetu..

Yapo maswali kadhaa ambayo tunaweza kujiuliza, juu ya tukio la Bwana Yesu kutokewa na Musa na Eliya siku ile alipopanda mlimani kuomba pamoja na wale wanafunzi wake watatu (Petro, Yohana na Yakobo)..

Na maswali yenyewe ni haya..

 1) Iweje Bwana Yesu atokewe na Musa ambaye tayari alishakufa miaka mingi?, na Zaidi ya yote maandiko yanasema alizikwa, tena na Mungu mwenyewe?..

2) Kwanini Musa na Eliya wamtokee?.. kulikuwa na umuhimu gani wa wao kumtokea Bwana?

Sasa ili tupate majibu ya maswali hayo vizuri, Labda tusome habari yenyewe kwa ufupi kisha tuendelee

Luka 9:28 “Baada ya maneno hayo yapata siku nane, aliwatwaa Petro na Yohana na Yakobo, akapanda mlimani ili kuomba.

29 Ikawa katika kusali kwake sura ya uso wake ikageuka, mavazi yake yakawa meupe, yakimeta-meta.

30 Na tazama, watu wawili walikuwa wakizungumza naye, nao ni MUSA NA ELIYA;

31 walioonekana katika utukufu, WAKANENA HABARI ZA KUFARIKI KWAKE ATAKAKOTIMIZA YERUSALEMU”

Kiini cha majibu ya maswali yetu tutakipata katika huu mstari wa 31.. “walioonekana katika utukufu, WAKANENA HABARI ZA KUFARIKI KWAKE ATAKAKOTIMIZA YERUSALEMU”

Kumbe Sababu ya Musa na Eliya kumtokea Bwana, ilikuwa ni kuzungumza kuhusu Kufa kwake Bwana Yesu, ambako atakutimiza Yerusalemu.

Sasa swali linakuja?, je ni kwamba Bwana Yesu alikuwa hajui kwamba atakwenda kufa mpaka atokewe na watu hao wawili, wamweleze kuhusu kufa kwake?.. Jibu ni la!.. alikuwa anajua, lakini zipo siri nyingine zihusuzo kufa kwake na kufufuka kwake na kupaa kwake, ambazo hizo Baba alimfunulia siku hiyo kupitia manabii hao wawili.

Kumbuka kabla ya Kristo kufa, roho za watakatifu zilikuwa chini, na shetani alikuwa na uwezo wa kuzileta juu, kama wewe ni msomaji wa biblia utakumbuka lile tukio la Samweli kuletwa juu ya yule mwanamke mwenye pepo la utambuzi, na baada ya kuletwa juu, Samweli aliweza kutoa unabii wa mambo yajayo, ijapokuwa alikuwa ameshakufa na kuzikwa, kwani tunasoma, alimtolewa Unabii Mfalme Sauli kuhusu KUFA KWAKWE, AMBAKO KUTAKWENDA KUTIMIA KIPINDI SI KIREFU KUTOKA PALE. Unaweza kusoma Habari hiyo kwa urefu katika kitabu cha 1Samweli 28:1-19.

Sasa Biblia haijaeleza Musa alikuwa anamweleza nini Bwana Yesu, lakini tunajua kabisa ni kuhusu Habari za kufunguliwa kwao wafu, na kwamba Bwana Yesu atakwenda kusulibiwa na kushuka sehemu ya wafu wao (akina Musa na wengine walipo na kuwaweka huru, na kwamba siku ya tatu atafufuka).

Kwahiyo kumbe kabla ya Bwana Yesu kufa, Wafu waliendelea kuishi, na pia iliwezekana kuwaleta baadhi yao juu na kutoa unabii, kwa njia yoyote ile!..

Kwasababu hiyo basi tumeshapata jibu ni kwanini MUSA, aliletwa juu na Mungu, ili kutoa unabii (Habari za kufa kwake Bwana Yesu, ijapokuwa Musa alikuwa ameshakufa kitambo na kuzikwa)…Ni kama tu vile, Nabii Samweli alivyoletwa juu na yule mwanamke mwenye pepo la utambuzi. (Kumbuka jambo hilo liliwezekana tu kipindi kabla ya Bwana Yesu kufa, lakini baada ya Bwana Yesu kufa na kufufuka, hakuna mchawi yeyote anayeweza kumleta juu mtu aliyekufa, kwasababu Kristo alizichukua funguo za Mauti na kuzimu).

Hapo tumepata jibu kuhusu Musa, sasa vipi kuhusu ELIYA?

Tunajua kabisa Eliya hakufa, bali alipaa..Maana yake Eliya anayajua yaliyo ya Mbinguni.. kama Nabii, Bwana alimtoa huko na kuja kumpasha Habari Bwana Yesu, kuhusu kupaa kwake, na enzi na mamlaka zinazomngojea Mbinguni (labda na siku hiyo alimpa na tarehe ya kupaa kwake, hatujui).

Kwasababu ijapokuwa Eliya alikuwa amepaa mbinguni, lakini bado alikuwa ni Nabii. Kwahiyo ujio wa Eliya ulikuwa ni wa muhimu sana kwa Bwana, kupata taarifa kuhusu kupaa kwake.

Kwahiyo kwaufupi ni kwamba Mungu aliwatumia manabii hawa wawili kama Manabii wa Ushahidi. Na Ushahidi huo ni wa KUFA kupitia Musa, na Kupaa kupitia ELIYA. Kwasababu Kristo naye atakufa kama Musa aliye nabii mkuu, na vile vile atapaa mbinguni kama ELIYA.

Kwahiyo baada ya tukio lile, Bwana Yesu alipokea Ufunuo mkuu kuhusu Mauti yake na kufufuka kwake, na kupaa kwake.. Zaidi sana na kurudi kwake kutakavyokuwa..ndio maana tunaona pia Uso wake uling’aa kama jua, kuashiria siku ya kurudi kwake kutakavyokuwa.

Na wakati ulipofika kweli Bwana Yesu, alikufa, akafufuka, na akapaa mbinguni.. imesalia hatua moja tu!.. nayo ni KURUDI KWAKE KUTUCHUKUA!..

Je! Umejiandaaje?.. Kama Nabii hizo mbili za kufa na kufufuka kwake na kupaa kwake zilitimia.. Basi hata kurudi kwake kutatimia. Na tupo katika majira ya kurudi kwake, dalili zote zimeshaonekana, muda wowote mambo yanakwisha, Kristo anakuja kuwachukua watakatifu wake, na kitakachokuwa kimesalia kwa wale watakaobaki ni majuto na dhiki kuu.

Je umejiandaaje? Je umemwamini Yesu na kutubu dhambi zako? Je umebatizwa katika ubatizo sahihi?…kama bado unangoja nini?.. Ukiikataa leo injili siku hiyo hutakuwa na la kujitetea. Mpokee Yesu leo, na ukabatizwe na kujazwa Roho Mtakatifu.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?

Je Eliya aliandika waraka baada ya kupaa mbinguni?

Mtu wa kwanza kufa alikuwa nani?

Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki;

Ngome ni nini?  Kwanini Mungu anafananishwa na ngome?

Rudi nyumbani

Print this post

HERI WAPATANISHI, MAANA HAO WATAITWA WANA WA MUNGU

Unajua ni kwasababu gani Bwana Yesu aliitwa Mwana wa Mungu? ..Mungu kukuona wewe kama  mwana wake kweli kweli sio tu uwe umezaliwa na yeye kwa kumkiri na kubatizwa, hapana bali pia kuwa na huduma ya upatanisho ndani yako….

Biblia inasema..

Mathayo 5:9

[9]Heri wapatanishi;

Maana hao wataitwa wana wa Mungu.

Jiulize Kwanini isiseme wataitwa watakatifu, au wataitwa wafalme, au wataitwa makuhani wa Mungu..bali wana wa Mungu.

Hilo jambo ambalo Yesu Kristo alilijua ndio maana kusudi lake kubwa la yeye kuja duniani, lilikuwa ni kutupatanisha sisi na Mungu..Yaani sisi tuliokuwa tumefarakana na Mungu kwasababi ya dhambi, sasa tunawasiliana naye kwa kupitia Yesu Kristo mwana wake..

Tunalithibitisha hilo katika mistari hii..

2 Wakorintho 5:18-19

[18]Lakini vyote pia vyatokana na Mungu, aliyetupatanisha sisi na nafsi yake kwa Kristo, naye alitupa huduma ya upatanisho;

[19]yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao; naye ametia ndani yetu neno la upatanisho.

Umeona? Tendo la Yesu kuacha enzi na mamlaka, na kuja duniani ili kutupatanisha tu sisi hilo ndio lililomfanya Mungu amwone kuwa ni mwana  bora kuliko wana wake wote aliokuwa nao.

Ndio maana akamshuhudia  mwenyewe..Huyu ni mwana wangu, mpendwa wangu, niliyependezwa naye. (Mathayo 3:17)

Akampa kibali cha kipekee kuliko wanadamu wote walioko ulimwenguni.

Hata sisi ili  Mungu atuone ni wana wake kwelikweli hatuna budi kuwa na huduma hii ya upatanisho ndani yetu.

Tuulete ulimwengu kwa Kristo. Lakini jambo ambalo hatujui ni kuwa kuwapatanisha watu waliogombana si jambo rahisi..la kwenda kuwashikanisha mikono tu halafu basi.. Hapana..lina gharama kubwa sana..kama ulishawahi kujaribu utalithibitisha hilo.

Ilimlazimu Yesu aache enzi na mamlaka, aje duniani, na kama hiyo haitoshi akataliwe kwanza na wale anaowapatanisha, (yaani sisi), na bado autoe uhai wake pia kwa ajili wao.

Kwa ufupi ni kwamba alikuwa anafosi upatanisho ambao ulikuwa hauwezekani kwa namna yoyote ile, ni uadui uliokuwa umekomaa..lakini hakukata tamaa, hadi mwisho wa siku ukatokea tu wenyewe.

Na sisi vivyo hivyo anasema ametupa huduma ya upatanisho. Yaani na sisi tukaupatanishe ulimwengu na Mungu kwa kupitia yeye.

Hivyo tufahamu kuwa tunapowahubiria watu, hadi kuokoka halitakuwa jambo rahisi kama sisi tunavyodhani..Watu wengi wamekatishwa tamaa  kuhubiri habari njema..kisa watu wanaowahubiria hawana geuko au badiliko, lolote..wengine ndio wanawatukana na kuwapiga

Hatuna budi kuendelea..kwasababu hakuna upatanisho ulio mwepesi. Ni unajitoa sadaka kwa vita ambayo si yako. Leo atakupuuzia, kesho atakutukana, lakini kesho kutwa ataokoka.

Ukifanikiwa kwa jambo hilo moja. Utajiongezea daraja la juu zaidi mbinguni..La kuwa mwana mpendwa wa Mungu. Na kwa jinsi unavyoendelea kufanya ndivyo kubali chako kinavyoongozeka kwa Mungu, hatimaye..kufikia kilele cha kufanana na Yesu Kristo..Ukimwomba Mungu lolote atakupa, na kazi zake zote utazifanya..Kama yeye alivyosema maneno haya..

Yohana 5:20-21

[20]Kwa kuwa Baba ampenda Mwana, naye humwonyesha yote ayatendayo mwenyewe; hata na kazi kubwa zaidi kuliko hizo atamwonyesha, ili ninyi mpate kustaajabu.

[21]Maana kama Baba awafufuavyo wafu na kuwahuisha, vivyo hivyo na Mwana awahuisha wale awatakao.

Umeona hiyo ndio faida za kuwa mwana wa Mungu kwelikweli.

Nasi pia tuanze kwa kuthamini wengine, kwa kuwahubiri habari njema, hapo tutakuwa tunaukiri UWANA wetu kwa Mungu..Ukimwona jirani yako amepotea basi pambana naye kwa hali na mali mpaka amgeukie Kristo kama wewe…wakati mwingine ugumu utakuwepo japo si kwa wote..

Ukifahamu kuwa hakuna upatanisho usiokuwa na gharama, basi utakuwa na uvumilivu na amani kwa yote utakayokutana nayo.

Bwana akubariki.

Uwe na utumishi mwema wa upatanisho.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MJUE SANA YESU KRISTO.

UVUVI BORA HAUCHAGUI, CHA KUVUA.

Heri maskini wa roho maana ufalme wa mbinguni ni wao.

Kwanini, tuimbe, je! kuna ulazima wowote wa kufanya hivyo?

Injili iliyopo kwa Samaki aina ya Eeli.

Kiyama ni nini?

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.

Rudi nyumbani

Print this post