DON’T BE AFRAID WHEN YOU GO DOWN.

Sifa ni nini?

Sifa ni kitendo cha kumshuhudia Mungu, au kuyasimulia matendo makuu ambayo ameyafanya au aliyonayo, na huwa inaambata na mguso wa ndani unaomfanya mtu arukeruke, acheze, afurahie, aimbe, ashangalie, apige kilele kwa nguvu, kwa hayo aliyoyaona kwa Mungu wake.

Kwamfano tunapoona jinsi, mbingu na nchi, jua na mwezi, na milima na bahari, vilivyoumbwa kwa uweza na ukuu wa ajabu, hapo tunapata sababu ya kumshuhudia Mungu, au kumtangaza kwa namna zote aidha kwa kumwimbia, kushangalia kwa sauti ya juu,

Au labda ulikuwa na shida Fulani labda ugonjwa, ukaponywa, au hitaji la kazi, nyumba, chakula ukapatiwa na yeye. Hapo ndipo unapopata sababu ya kuyatangaza maajabu yake, kwa kumwimbia kwa nguvu sana. Hizo ndio sifa.

Mungu anasema..

Zaburi 68:32 “Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu, Msifuni Bwana kwa nyimbo”.

Zaburi 117:1 “Haleluya. Enyi mataifa yote, msifuni Bwana, Enyi watu wote, mhimidin.

Zaburi 147:1 “Haleluya. Msifuni Bwana; Maana ni vema kumwimbia Mungu wetu, Maana kwapendeza, kusifu ni kuzuri”.

Biblia inatuambia viumbe vyote na uumbaji wote, vinamsifu Mungu. Kwanini na sisi tusimwimbie yeye sifa zetu?.  Embu tazama pumzi uliyopewa bure, embu tazama mapigo ya moyo yanayodundishwa ndani yako bila tozo lolote, embu tafakari jua unaloangaziwa na Yehova. Kwanini usimsifu yeye?

Bwana anaketi juu ya sifa.. (Zaburi 22:3), Na yeye pekee ndiye anayestahili kuabudiwa.

Hivyo wote wamsifuo kwa Roho na Kweli, yeye yupo juu yao. Katika sifa kuta za Yeriko zilianguka, , \vifungo vya Gereza vililegezwa Paulo na Sila walipokuwa gerezani, katika sifa maadui waliuliwa bila vita yoyote kipindi cha Mfalme Yehoshafati.  Nasi pia tukiwa watu wa sifa, ni maombi tosha ya kutuweka huru na kutufungua.

Bwana atupe macho ya kuliona hilo.

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kuhimidi ni nini?(Zaburi 31:21)

Mwana haramu ni nani kibiblia? (Kumbukumbu 23:2).

Uchaga ni nini? (Luka 12:24)

Kinubi ni nini katika biblia? (1Samweli 16:16, 23)

BARAGUMU NI NINI?

Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?

Ulafi ni nini kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

Kuhimidi ni nini?(Zaburi 31:21)

Kuhimidi kibiblia ni kumpa Mungu sifa iliyochanganyikana na heshima na unyenyekevu wa hali ya juu sana,

Neno hili limeonekana  mara nyingi sana katika biblia,

Kwamfano hivi ni baadhi ya vifungu, ambavyo utakutana na Neno hilo;

Mwanzo 14:19 “Akambariki, akasema, Abramu na abarikiwe na Mungu Aliye juu sana, Muumba mbingu na nchi. 20 Ahimidiwe Mungu Aliye juu sana, aliyewatia adui zako mikononi mwako. Abramu akampa fungu la kumi la vitu vyote”.

Waamuzi 5:3 “Sikieni, enyi wafalme; tegeni masikio, enyi wakuu; Mimi, naam mimi, nitamwimbia Bwana; Nitamhimidi Bwana, Mungu wa Israeli”.

Zaburi 31:21 “Bwana ahimidiwe; kwa maana amenitendea Fadhili za ajabu katika mji wenye boma”.

Zaburi 34: 1 “Nitamhimidi Bwana kila wakati, Sifa zake zi kinywani mwangu daima”.

Warumi 15:10 “Na tena anena, Furahini,Mataifa,pamoja na watu wake.

11 Na tena, Enyi Mataifa yote,msifuni Bwana; Enyi watu wote,mhimidini.

Ikiwa wewe ni mwanadamu mwenye pumzi huna budi kumuhimidi Mungu muumba wako sikuzote za  maisha yako. Ni lazima ujishushe, upige magoti, na kwa kumaanisha kabisa, umsifu kwa nguvu zako zote, umtukuze kwa wema wake wako, na kuliadhimisha jina lake.

Moja ya mambo ambayo yalimfanya Daudi awe kipenzi cha Mungu, ni tabia yake, ya kumuhimidi Mungu, tena mbele ya makusanyiko ya watu.

Zaburi 26:12 “Mguu wangu umesimama palipo sawa; Katika makusanyiko nitamhimidi Bwana”.

Bwana atusaidie sote, tuwe na matamanio kama haya.  Kwasababu kama ilivyo chakula chetu sisi ni Neno la Mungu, halikadhalika chakula cha Mungu wetu ni Sifa. Hatuna budi kumlisha kila siku sifa zake, kwa kumuhimidi yeye.

Bwana akubariki.

Je umeokoka? Kama la unafahamu kuwa tunaishi katika vizazi ambacho unyakuo ni wakati wowote?. Tubu dhambi zako mgeukie Mungu, naye atakusaidia. Ikiwa utahitaji msaada ya kumkaribisha Kristo maishani mwako/ kubatizwa, basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi;

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Wana wa Asafu ni akina nani katika biblia?

Ibada ni nini,Na je ili ikamilike inapaswa iwe na nini na nini?

Kujazi ni nini? (Mathayo 6:4)

Panda/ Sauti ya panda ni nini kibiblia?(Danieli 3:5)

Matoazi na Matari ni nini? (Kutoka 15:20)

Uchaga ni nini? (Luka 12:24)

Rudi nyumbani

Print this post

Mwana haramu ni nani kibiblia? (Kumbukumbu 23:2).

Mwana-haramu, au mwana wa haramu ni mtu aliyezaliwa nje ya Ndo Takatifu.

Zamani katika jamii ya Israeli, Mungu aliwakataza wana wa Israeli, wasioane na watu wa mataifa. (Kumbukumbu 7:2-3). Wala wasioane ndugu kwa ndugu..

Walawi 18:5 “Kwa ajili ya hayo mtazishika amri zangu na hukumu zangu; ambazo mtu akizitumia ataishi kwa hizo; mimi ndimi Bwana.

6 Mtu ye yote aliye wa kwenu ASIMKARIBIE MWENZIWE ALIYE WA JAMAA YAKE YA KARIBU ili kumfunua utupu; mimi ndimi Bwana”.

Vile vile Bwana aliwakataza watu wasiingie kwa wake wa Jirani zao (Kumbukumbu 5:21, Kutoka 20:17).

Kwahiyo mtoto yeyote aliyepatikana kwa mojawapo ya hizo njia tatu, yaani kwa njia ya kukutana ndugu kwa ndugu, au kuoana mtu wa Israeli na mtu wa mataifa, au kwa kuzaa na mke wa Jirani yako au ambaye hamjaoana, mfano wa Yuda katika Mwanzo 38:24. Mtoto huyo aliyezaliwa aliitwa MWANA-HARAMU, Au MWANA WA HARAMU.

Na Mwana haramu, enzi za agano la kale hakuruhusiwa kuingia katika MKUTANO WA BWANA MILELE, na hata kizazi chake chote..

Kumbukumbu 23:2 “Mwana wa haramu asiingie katika mkutano wa Bwana; hata kizazi cha kumi asiingie aliye wake katika mkutano wa Bwana”.

Lakini swali ni je! Mpaka sasa, wana wa Haramu,(yaani waliozaliwa nje ya ndoa, kimwili) hawakubaliwi na Bwana?

Jibu ni la!, katika Agano la kale, si tu wana haramu waliokuwa wanatengwa, bali hata walemavu na watu wenye ukoma, hawakuruhusiwa kuingia katika mkutaniko wa Bwana. Na Bwana aliruhusu vile, ili kufundisha Uana haramu wa kiroho jinsi ulivyo mbaya, ambao utakuja kufunuliwa mbeleni(katika Agano jipya). Ambao huo utatufanya sisi tusikubalike mbele za Mungu, milele!!.

Mwana wa Haramu kibiblia ni mtu ambaye Hajazaliwa mara ya Pili.

Je umewahi kujiuliza ni kwanini “Wokovu” unafananishwa na “kuzaliwa mara ya pili”.. jiulize kwanini biblia haijatumia neno “kutengenezwa upya” lakini imetumia neno “kuzaliwa mara ya pili”.. Tafsiri yake ni kwamba “hali tuliyopo” sasa ni “u-haramu”… hivyo tunapozaliwa upya, ili ule uharamu unaondoka, na kuwa wana HALALI!!.. Na hivyo tunakuwa na uwezo wa kushiriki baraka zote za Mungu kwasababu tumefanyika kuwa Watoto wa Mungu halali.

Wana wa Haramu, (ambao hawajazaliwa mara ya pili), wanafananishwa na mbegu zinazoharibika.. maana yake!, hazina uzima wa milele, lakini wana halali (yaani wale waliozaliwa mara ya pili), wanafananishwa na mbegu zidumuzo.

1Petro 1:23 “Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima, lidumulo hata milele”.

Na tabia ya mtoto halali, (asiye haramu), huwa baba yake anamfunza, ikiwemo pia kumwadhibu pale anapokosea..

Mtume Paulo aliliandika hilo kwa uweza wa roho na kusema…

Waebrania 12.5 “tena mmeyasahau yale maonyo, yasemayo nanyi kama kusema na wana, Mwanangu, usiyadharau marudia ya Bwana, Wala usizimie moyo ukikemewa naye;

6 Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi, Naye humpiga kila mwana amkubaliye.

7 Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye?

8 Basi kama mkiwa hamna kurudiwa, ambako ni fungu la wote, ndipo MMEKUWA WANA WA HARAMU NINYI, WALA SI WANA WA HALALI.

9 Na pamoja na hayo tulikuwa na baba zetu wa mwili walioturudi, nasi tukawastahi; basi si afadhali sana kujitia chini ya Baba wa roho zetu na kuishi?

10 Maana ni hakika, hao kwa siku chache waliturudi kama walivyoona vema wenyewe; bali yeye kwa faida yetu, ili tuushiriki utakatifu wake.

11 Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani”.

Je umezaliwa mara ya pili?

Maana ya kuzaliwa mara ya pili, ni Kutubu kwa kumaanisha kuacha dhambi, na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi (Kwa jina la Yesu) na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu. (Matendo 2:38).

Yohana 3:3 “Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, MTU ASIPOZALIWA MARA YA PILI, HAWEZI KUUONA UFALME WA MUNGU.

4 Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?

5 Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.

6 Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.

7 Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili”.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

MJUE SANA YESU KRISTO.

AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

Hema ya kukutania ni nini, na ilikuwaje?

Rudi nyumbani

Print this post

Uchaga ni nini? (Luka 12:24)

Jibu: Tusome,

Luka 12:24 “Watafakarini kunguru, ya kwamba hawapandi wala hawavuni; hawana GHALA wala UCHAGA, na Mungu huwalisha. Bora ninyi mara nyingi kuliko ndege!”

“Ghala” ni chumba/nyumba ndogo ya kuhifadhia nafaka, lakini “Uchaga” ni jengo kubwa lililotengenezwa kwaajili ya kuhifadhia nafaka pamoja na aina nyingine ya vyakula vya mifugo na binadamu.

Hivyo Bwana Yesu aliposema, tuwatafakari kunguru, kwamba hawana “Ghala” wala “Uchaga”, alimaanisha kunguru hawana mahali pa kuhifadhia chakula kwaajili ya vipindi vigumu vinavyokuja mbeleni, Lakini muujiza ni kwamba ijapokuwa hawana sehemu za kuweka akiba ya chakula, unapokuja msimu wa kiangazi bado hawafi kwa njaa, wanaishi!!

Utakumbuka kisa cha Nabii Eliya, kipindi ambacho mbingu zimefungwa miaka mitatu na Nusu, kipindi ambacho watu na Wanyama wanakufa kwa kukosa chakula, utaona kunguru bado walikuwa wanaishi na wanakula vizuri, na hata Mungu kuwatumia hao kumpelekea chakula mtumishi wake.

1Wafalme 17:2 “Neno la Bwana likamjia, kusema,

3 Ondoka hapa, geuka, uende upande wa mashariki, ujifiche karibu na kijito cha Kerithi kinachokabili Yordani.

4 Itakuwa utakunywa maji ya kile kijito; NAMI NIMEWAAMURU KUNGURU WAKULISHE HUKO.

5 Basi akaenda akafanya kama alivyosema Bwana; kwa kuwa akaenda akakaa karibu na kijito cha Kerithi, kinachokabili Yordani.

6 KUNGURU WAKAMLETEA MKATE NA NYAMA ASUBUHI, na mkate na nyama jioni, akanywa maji ya kile kijito”.

Umeona?.. wakati watu wanakufa kwa njaa, Kunguru na Watoto wao wanakula mpaka wanasaza, mpaka wanakuwa na akiba ya kumpelekea Eliya, mtumishi wa Mungu.

Lakini sasa Bwana Yesu anakuja kusema katika Luka 12:24, kwamba TUWATAFAKARI HAO!!.. Kama Baba wa mbinguni anawapa chakula hao, na ijapokuwa hawana maghala wa uchaga, si Zaidi sisi endapo tukimwamini na kumtegemea yeye?.. Kwasababu sisi ni bora kuliko kunguru mara nyingi.

Baba yetu anatuhurumia sisi mara nyingi Zaidi, kuliko anavyowahurumia kunguru!. Tunapomtegemea yeye, hata kama tutapitia hali ngumu na za ukame kiasi gani, basi Bwana Yesu hatatuacha tupungukiwe kabisa…atakuwa na sisi na kutuhudumia kuliko anavyowahudumia kunguru.

Waebrania 13:5 “Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa.

6 Hata twathubutu kusema, Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?”

Je umempokea Yesu leo?, je umefanyika mtoto wake?, kama bado kumbuka dunia si salama, wala haina mshahara wowote Zaidi ya mauti, dunia itakususha thamani Zaidi ya kunguru siku ya mateso, kipindi cha Eliya wote waliokuwa wanaitumainia dunia, walikufa kwa njaa, lakini kunguru wakawa wanaishi…wote waliokuwa wanaabudu mabaali waliangamia, lakini kunguru waliishi!..Lakini waliomtegemea Mungu waliishi na kudumu,

Mpokee Yesu leo kama bado hujampokea, pia ukabatizwe katika ubatizo sahihi kwaajili ya ondoleo la dhambi na upokee kipawa cha Roho Mtakatifu.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

KAMA MKRISTO FAHAMU ZIPO HATUA UTAPIGISHWA NA MUNGU.

JIHADHARI NA ROHO ZIDANGANYAZO.

TUSIWE WATU WA KUPUNGUKIWA AKILI.

Biblia inamaana gani iliposema “Dhambi ilipozidi, Neema ilizidi kuwa nyingi Zaidi”.

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

Rudi nyumbani

Print this post

NIFANYE NINI ILI MUNGU AYAJIBU MAOMBI YANGU?

Ukienda kuomba kazi yoyote halali, kikawaida huwezi kupewa majibu ya papo kwa papo na kuambiwa anza kazi leo, bila ya kutaka kwanza taarifa Fulani kutoka kwako, hata kama ni ile ndogo ya kufagia, vipo vigezo  vitaambatanishwa tu na kazi hiyo, aidha utaulizwa umri wako, au hali yako ya kiafya, au fani uliyonayo, au jinsia yako, au elimu yako n.k. Lakini ikiwa hujasoma vigezo vyao, halafu ukapeleka maombi yako kienyeji, Ni wazi kuwa barua yako itatupwa kapuni.

Vivyo hivyo na kwa Mungu, tunapopeleka maombi yetu, ni sharti tujue vigezo vya kujibiwa, vinginevyo, tutabakia kumlaumu Mungu, mbona tulifunga, na kukesha lakini hujasikia maombi yetu.

Hivi ndio vigezo kivuu vya maombi yetu kujibiwa na Mungu

  1. Kaa mbali na dhambi:

Hili ndio jambo la kwanza na la msingi; Dhambi ndiyo inayomdhoofisha Mungu, na kumdumaza kwenye eneo la kujibiwa maombi yetu.

Isaya 59:1 “”Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;

2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia”.

Hakikisha unakaa mbali na mambo yote yanayomchukiza Mungu, yaliyo ndani yako, mfano uzinzi, ulevi, uongo, rushwa, wivu, matusi n.k.

  1. Omba vizuri:

Kuomba vizuri, sio kupangalia maneno katika uombaji, hapana, bali kuomba jambo linalotimiza mapenzi ya Mungu.

Yakobo 4:2 “Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi!

3 Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu”.

Jiulize unachokiomba je kina  lengo gani, ni ili umkomoe yule adui yako?, au ili ukaongezee mtaji wa ile biashara yako ya bar?, au ili uonekane mwanamke wa kisasa mfano wa Yezebeli? Kama sivyo  ni Ili nini?..Fahamu kuwa Mungu anachunguza mioyo. Hakikisha unachokiomba ni kwa utukufu wa Mungu. Vinginevyo hutapokea chochote.

    3. Usiombe ili utazamwe na watu unajua kuomba:

Bwana Yesu alisema..

Mathayo 6:5 “Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao.

6 Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.

Mawazo yako yanapaswa yamwelekee Mungu, na sio Mungu Pamoja na wanadamu. Ukilijua hilo, basi hutaona sababu ya kujionyesha kwa watu ili wakupe utukufu.

     4. Omba kwa bidii:

Ukweli ni kwamba yapo maombi utahitaji kuonyesha bidii kwa Mungu ili uyapate, na sio kuomba dakika 5 halafu basi, hapo unaweza usipokee chochote, bali yakupasa kung’ang’ana mbele za Mungu ndipo yaje kutokea.

Yakobo 5:16 “… Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.

17 Eliya alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja na sisi, akaomba kwa bidii mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya nchi muda wa miaka mitatu na miezi sita.

18 Akaomba tena, mbingu zikatoa mvua, nayo nchi ikazaa matunda yake.

Hivyo ongeza misuli yako ya maombi. Hata ya masafa mrefu na mikesha.

    5.  Usikate tamaa:

Yakupasa ujifunze uvumilivu. Uvumilivu ni muhimu sana ikiwa hujajibiwa leo, haimaanishi kuwa Mungu hajakusikia, bali omba tena kesho, na kesho kutwa, kwasababu ipo sababu kwanini hujakipata kwa muda huo.

Luka 18 : 1-8

18:1 “Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa.

2 Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu.

3 Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, Nipatie haki na adui wangu.

4 Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu,

5 lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima.

6 Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu.

7 Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao?

8 Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani”?

    6. Jifunze kumtolea Mungu:

Ni jambo dogo, lakini linamatokeo makubwa sana rohoni. Sio kwamba Mungu anahaja na fedha zetu hapana, lakini umtoleapo unaonyesha upendo wako kwake. Ukipelekea maombi yako kwake, jijengee utaratibu pia wa kuambatanisha na sadaka, kwa kile ulichojaliwa, ikiwa ni senti mbili, au milioni 10, mpelekee Bwana. Wengi waliotenda hivi walifanikiwa.

Malaki 3:10 “”Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la”.

Hivyo kwa kuzingatia, mambo hayo sita, basi ni hakika Mungu atakujibu maombi yako. Na utamfurahia yeye.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

Nifanyeje niwe mwombaji mzuri, wa masafa marefu?

Namna ya kuomba

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

JINSI YA KUPOKEA UPONYAJI, TUNAPOMWOMBA BWANA ATUGUSE MARA YA PILI.

Tofuati kati ya kifo na mauti ni ipi?

UNYAKUO WA KANISA UMEPITA LEO!!

Rudi nyumbani

Print this post

Kujazi ni nini? (Mathayo 6:4)

Kujazi maana yake ni kulipa.

Kwamfano tusome Neno hilo jinsi lilivyotumika na kumaanisha katika maandiko;

Mathayo 6:2 “Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu.

3 Amin, nawaambieni, Wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe utoapo sadaka, hata mkono wako wa kushoto usijue ufanyalo mkono wako wa kuume;

4 sadaka yako iwe kwa siri; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.

Maana yake ni kwamba, unapokuwa mtu wa kutoa sadaka bila kuwa na nia ya kuonekana mbele za watu, basi Mungu atakulipa kwa utoacho.

Mathayo 6:6 “Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.

Mathayo 6:17 “Bali wewe ufungapo, jipake mafuta kichwani, unawe uso;

18 ili usionekane na watu kuwa unafunga, ila na Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi”.

Vilevile unapokuwa mtu wa kuomba na kufunga, lengo lako likuwa ni kujisogoza mbele za Mungu na sio kufanya mashindano, au kuonekana na watu kuwa ni wa kiroho sana, basi Mungu atakulipa kwa hicho ukifanyacho.

Ruthu 2:11 “Naye Boazi akajibu, akamwambia, Nimeelezwa sana yote uliyomfanyia mkweo, tangu alipokufa mumeo; na jinsi ulivyowaacha baba yako na mama yako, na nchi yako uliyozaliwa, ukawafikilia watu usiowajua tangu hapo.

12 Bwana akujazi kwa kazi yako, nawe upewe thawabu kamili na Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye umekuja kukimbilia chini ya mabawa yake”.

Tunaona pia hapa Boazi akimbariki Ruthu, kwa wema wake aliomfanyia mkwewe, na kumwambia Bwana akulipe kwa kazi yako njema.

Lakini ni ujumbe gani Bwana anapitisha katika haya?

Ni kuonesha kuwa hakuna tendo jema tutakalomfanyia Mungu asirudishe malipo, endapo tutafanya ipasavyo. Kama kweli utaomba mbele zake, utafunga kwa ajili yake, utamtolea sadaka zako, kama kweli utatenda wema wowote, fahamu kuwa hilo Bwana atakulipa tu kwa wakati wake, thawabu yako haitakupita.

Hivyo atukuzwe Mungu awezaye kutuona na kuturehemu na kutubariki. Sifa, heshima na utukufu vina yeye milele na milele. Amina.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Sadaka ya kutikiswa ilikuwaje?

Nini maana ya ampokeaye Nabii atapata thawabu ya Nabii? (Mathayo 10:41).

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)

HERI WAPATANISHI, MAANA HAO WATAITWA WANA WA MUNGU

Mapooza ni nini? Na je! Twawezaje kuepukana nayo?

Nini maana ya huu mstari? “Yeye mwenyewe ataokolewa lakini ni kama kwa moto”

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI YA KUPOKEA UPONYAJI, TUNAPOMWOMBA BWANA ATUGUSE MARA YA PILI.

Wingu la Mashahidi
Wingu la Mashahidi
JINSI YA KUPOKEA UPONYAJI, TUNAPOMWOMBA BWANA ATUGUSE MARA YA PILI.
/

Jina kuu la Bwana na Mwokozi wa Ulimwengu, Simba wa kabila la Yuda, na Mkuu wa wafalme wa dunia, Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia, neno la Mungu wetu, lililo mwanga wa njia yetu, na taa iongozayo miguu yetu.

Upo wakati wakati ambao tutahitaji Bwana atuguse mara ya pili, lakini ni vizuri kujua kanuni ya kupokea Uponyaji pindi tunapomsihi Bwana atuguse tena…

Hebu tusome kisa kimoja katika biblia na kisha tutafakari na tujifunze, kanuni ya kupokea uponyaji mkamilifu.

Tusome Marko 8:22-26, (Zingatia maneno yaliyoanishwa kwa herufi kubwa).

Marko 8:22 “Wakafika Bethsaida, wakamletea kipofu, wakamsihi amguse.

23 Akamshika mkono yule kipofu, akamchukua nje ya kijiji, AKAMTEMEA MATE YA MACHO, akamwekea mikono yake, akamwuliza, Waona kitu?

24 AKATAZAMA JUU, AKASEMA, NAONA WATU KAMA MITI, INAKWENDA.

25 Ndipo akaweka tena mikono yake juu ya macho yake, NAYE AKATAZAMA SANA; akawa mzima, akaona vyote waziwazi.

26 Akampeleka nyumbani kwake, akisema, Hata kijijini usiingie”.

Katika kisa hichi hebu tujiulize swali lifuatalo, kisha tuendelee mbele..

Je inawezekana mtu atazame juu halafu aone watu?, tena watu wenyewe wanatembea? Na tena wanatembea kwa kasi kama miti?… Nilitegemea hata angesema anaona “ndege wanaruka, wanakimbia kama miti”!! Lakini yeye anasema anaona watu!!……Bila shaka ulishawahi kusafiri na basi linalokwenda kasi, na njiani ukaona namna miti inavyoonekana kama inarudi nyuma kwa kasi sana…Ndivyo alivyoona huyu mtu alipotazama juu..aliona watu!..

Kwa kawaida, huu sio uponyaji!!.. Huyu mtu hakuwa amepata uponyaji wowote, bali alikuwa katika hatua za mwanzo za kupokea uponyaji..ni kama tu TV iliyowashwa ambayo bado haijakamata mawimbi!!..inakuwa inaonyesha tu chenga chenga…

Lakini tunaona tabia ya kipekee ya huyu kipofu baada ya kuguswa na Bwana mara ya pili.

Utaona huyu kipofu mara ya kwanza alipoguswa, alitazama juu hakutumia muda mrefu kutazama, badala yake, kwa haraka haraka akakimbilia kumjibu Bwana kwa kusema “anaona watu kama miti”….. lakini baada ya kuguswa na Bwana mara ya pili, ni kama alijifunza kitu kuwa hana budi kutokuwa na haraka ya mambo…utaona alitulia na KUTAZAMA SANA!! (pengine alitumia dakika kadhaa kutazama juu), akawa bado anaona ile ile miti, lakini hakuacha kutazama…..

Na alipozidi KUTAZAMA SANA, pengine akaanza kuona  ile miti inafutika kidogo kidogo, akaanza kuona anga linakuwa jeupe na kidogo kidogo akaanza kuona mawingu, na pengine akaanza kuona ndege wanaruka, na alipotazama mbele akamwona Bwana Yesu, ndipo akasema sasa ninaona!!! Haleluya.

Na sisi hatuna budi KUTAZAMA SANA!!..Tusiishie kutazama kidogo tu! tusiishie kuzungumza, wala kunung’unika, wala kukosoa, wala kutoa hitimisho, pale tunapoona uponyaji haujakamilika….bali turuhusu uponyaji wa Bwana ufanye kazi!… Tuwe na Subira huku tukiliamini Neno lake.

Kutazama sana, ni kudumu katika kumwamini Mungu, hata kama unaona lile tatizo bado halijatatuka… wewe endelea kumwamini Bwana na kusubiri, bila kutoa uso wako juu mpaka muujiza wako utakapokamilika..

Pengine ulimwomba Bwana kuhusu hali unayopitia ya kiroho au kimwili,  lakini uliishia kuona chenga chenga katika huo ugonjwa, au hilo tatizo..lakini sasa umeijua kanuni..Msii Bwana akuguse tena kwa mara nyingine, lakini safari hii USIRUHUSU IMANI YAKO IPUNGUE, WALA USIUKIRI UGONJWA.…Utaona muujiza wa ajabu, ukitendeka!!.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

JINSI YA KUMSIKIA MUNGU, NA KUPOKEA MAFUNUO AU JUMBE KUTOKA KWAKE.

Mwerezi ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

USIISHIE TU KUPATA HAKI, BALI PATA NA WOKOVU.

Jina kuu la Bwana na Mwokozi wetu, Yesu Kristo libarikiwe!. Karibu tuyatafakari maandiko,

Neno la Bwana wetu, lililo chakula cha roho zetu linasema hivi..

Warumi 10:10 “Kwa maana KWA MOYO mtu huamini HATA KUPATA HAKI, na KWA KINYWA hukiri HATA KUPATA WOKOVU”.

Ipo sababu kwanini Biblia imetenganisha hayo mambo mawili, HAKI na WOKOVU. Watu wengi leo wameishia kupata HAKI tu, lakini si WOKOVU.. Wapo wengi leo waliomwamini Bwana Yesu mioyoni mwao na kuishia kupata haki sawasawa na Warumi 5:1 na Wagalatia 2:16, lakini hawana WOKOVU, maishani mwao, Na Wokovu unakuja kwa kumkiri Yesu na maneno yake kwa kinywa!.

Wakati Bwana Yesu akiwa duniani, walikuwepo Mafarisayo na wakubwa wengi waliomwamini mioyoni mwao, lakini katika Vinywa vyao, hawakumkiri..na hivyo Imani yao ikahesabika si kitu!.

Yohana 12:42 “Walakini hata katika wakuu WALIKUWAMO WENGI WALIOMWAMINI; lakini kwa sababu ya Mafarisayo HAWAKUMKIRI, wasije wakatengwa na sinagogi”.

Umeona?. walivifunga vinywa vyao, kuhofia kutengwa na dini zao, au madhehebu yao, au wakubwa wenzao, au kuonekana washamba na waliorukwa na akili!!..

Ndugu unapomwamini Bwana Yesu na maneno yake, ndani ya moyo wako, hiyo bado haitoshi kukupa wewe wokovu.. Huna budi kumkiri kwa kinywa chako kila siku katika Maisha yako..  Wokovu wa siri siri, na wakujificha ficha huo sio wokovu kibiblia!!.. Bwana Yesu alisema mtu yeyote akimwonea yeye na maneno yake, yeye naye atamwonea haya mtu huyo mbele za baba yake na malaika zake.

Luka 9:26 “Kwa sababu kila ATAKAYENIONEA HAYA MIMI NA MANENO YANGU, Mwana wa Adamu ATAMWONEA HAYA MTU HUYO, atakapokuja katika utukufu wake na wa Baba na wa malaika watakatifu”.

Soma tena..

Mathayo 10:32 “Basi, kila mtu atakayenikiri mbele ya watu, NAMI NITAMKIRI MBELE ZA BABA YANGU ALIYE MBINGUNI”.

Umeona?..kumbe unaweza kuwa umemwamini Bwana Yesu moyoni mwako, lakini kwasababu tu! Humkiri maishani mwako, siku ile naye akakukana!!..kumbe wokovu wetu unakamilika pia kwa kumkiri Bwana Yesu.

Wakati Fulani, Bwana Yesu alimponya kipofu mmoja, ambaye alizaliwa katika hali hiyo ya upofu.. Na baada ya kumponya..Wazazi wake yule kipofu, walimwamini Bwana Yesu kuwa ni Kristo, lakini kwa hofu ya kutengwa hawakumkiri kwa vinywa vyao, lakini mwanao ambaye alikuwa kipofu, alimwamini Bwana Yesu na kumkiri..

Yohana 9:18 “Basi Wayahudi hawakusadiki habari zake, ya kuwa alikuwa kipofu, kisha akapata kuona; hata walipowaita wazazi wake yule aliyepata kuona.

19 Wakawauliza wakisema, Huyu ndiye mwana wenu, ambaye mnasema kwamba alizaliwa kipofu? Amepataje, basi, kuona sasa?

20 Wazazi wake wakawajibu, wakasema, Tunajua ya kuwa huyu ndiye mwana wetu, tena ya kuwa alizaliwa kipofu;

21 lakini jinsi aonavyo sasa hatujui; wala hatujui ni nani aliyemfumbua macho. Mwulizeni yeye mwenyewe; yeye ni mtu mzima; atajisemea mwenyewe.

22 Wazazi wake waliyasema hayo kwa sababu WALIWAOGOPA WAYAHUDI; kwa maana Wayahudi walikuwa wamekwisha kuafikiana kwamba MTU AKIMKIRI KUWA NI KRISTO, ATATENGWA NA SINAGOGI.

23 Ndiyo sababu wale wazazi wake walisema, Ni mtu mzima, mwulizeni yeye”.

Umeona hawa wazazi, walikuwa na Imani mioyoni mwao, lakini Imani yao haikuwasaidia..Bwana Yesu hakuwafuata…lakini mbele kidogo, utaona Bwana anamfuata yule kipofu, na kujidhihirisha kwake kwasababu alimkiri..

Yohana 9:33 “Kama huyo asingalitoka kwa Mungu, asingeweza kutenda neno lo lote.

34 Wakajibu, wakamwambia, Ama! Wewe ulizaliwa katika dhambi tupu, nawe unatufundisha sisi? Wakamtoa nje.

35 YESU AKASIKIA KWAMBA WAMEMTOA NJE; NAYE ALIPOMWONA ALISEMA, WEWE WAMWAMINI MWANA WA MUNGU?

36 NAYE AKAJIBU AKASEMA, NI NANI, BWANA, NIPATE KUMWAMINI?

37 YESU AKAMWAMBIA, UMEMWONA, NAYE ANAYESEMA NAWE NDIYE.

38 AKASEMA, NAAMINI, BWANA. AKAMSUJUDIA”.

Leo Bwana Yesu ajidhihirishi kwa wengi, kwasababu hiyo moja tu!.. ya KUTOMKIRI YEYE!!.. Tunampenda na kumwamini kweli Yesu, lakini hatuwezi kumkiri mbele ya mabosi zetu, hatuwezi kumkiri mbele ya wanafunzi wenzetu, hatuwezi kumkiri mbele ya wafanyakazi wenzetu, hatuwezi kumkiri mbele ya ndugu zetu…huku tukidhani kuwa ndio tunao wokovu..kumbe bado hatuna wokovu!!!.

Vile vile ukiyaonea haya maneno yake yote ya kwenye biblia..bado hauna wokovu!!.. Haijalishi unalijua Neno kiasi gani, au unaijua biblia kiasi gani…

Siku zote kumbuka hilo, Wokovu wetu unakamilika na KUMKIRI BWANA YESU NA MANENO YAKE!!!!..(Usilisahau hilo kamwe).

Warumi 10:8 “Lakini yanenaje? Lile neno li karibu nawe, KATIKA KINYWA CHAKO, na katika MOYO WAKO; yaani, ni lile neno la imani tulihubirilo.

9 Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka

10 Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu”

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

HIZO NDIZO ROHO ZA MASHETANI.

USIMLAANI KIZIWI, WALA USITIE KWAZO MBELE YA KIPOFU.

Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?

Ni nani aliye kipofu, ila mtumishi wangu?

NJIA YA KUPATA WOKOVU.

Rudi nyumbani

Print this post

JIFUNZE KUDUMU UWEPONI MWA MUNGU.

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tena tuyatafakari maneno matukufu ya mola wetu. Leo napenda tuutafakari huu mstari kwa ukaribu sana, kwasababu una maana kubwa nyuma yake huwenda tofauti na vile tunavyoufahamu.

Biblia inasema..

Mithali 23:29 “Ni nani apigaye, Yowe? Ni nani aliaye, Ole? Ni nani mwenye ugomvi? Ni nani mwenye mguno? Ni nani aliye na jeraha zisizo na sababu? Ni nani aliye na macho mekundu?

30 NI WALE WAKAAO SANA KWENYE MVINYO; Waendao kutafuta divai iliyochanganyika”.

Mwandishi anaeleza matokeo, ya mtu kufikiwa na hayo mambo yote sita(6) mabaya kwa mpigo ni nini.. Yaani Yowe, ole, ugomvi, mguno, jeraha zisizo na sababu, na macho mekundu.. ni nini..

> Anaposema Yowe, sote tunafahamu, mpaka mtu apige yowe, ni matokeo ya kakumbwa na jambo baya sana, ambalo linamfanya ahitaji msaada wa haraka sana, pengine labda anafukuzwa auawe,  au anapigwa vikali , au amekumbwa na taarifa za kushtusha sana..Hivyo kwa kawaida hakuna yowe inayotokana na mema.

> Vilevile anaposema ni nani aliaye ole..Tunafahamu ole ni baada ya kutahadharishwa kwa mabaya. Lakini mpaka mtu analia ole, “kusema ole wangu mimi,” ni mtu ambaye tayari ameshakumbwa na mabaya hayo,aidha vifungo, magonjwa, taabu, mateso n.k.

> Halikadhalika anaposema, ni nani mwenye mguno; Anamaanisha mtu mwenye malalamiko, mwenye maneno yasiyofaa, au kueleweka, mtukanaji, mtu wa kashfa. Jambo hili nalo haliji kutoka katika mema.

> Vilevile aliye na jeraha zisizo na sababu, ni mtu aliyejiingiza katika matatizo ambayo hakustahili au hakupaswa kukumbwa nayo. Pengine amrukwa na akili, au uzembe uliopitiliza usio wa kibinadamu.

> Anaposema tena ni “nani mwenye ugomvi”..Yaani mtu anayezua ugomvi, malumbano, yasiyo na maana au sababu, kufoka, na ukorofi.

> Na pia mwenye macho mekundu, .Yaani macho yaliyolegezwa na pombe.

Sasa ukisoma kwa makini, vyote hivyo sita (6), haviji hivi hivi kwa wanywaji pombe kidogo, wanaweza wakafikia kiwango Fulani..Lakini mpaka tabia hizo zitokee kwa mlevi ni lazima awe ni mtu wa “KUKAA SANA KWENYE MVINYO” kama maandiko yanavyosema..Walevi waliopitiliza, ndio huwa wanaanguka mitaroni na kujiumiza miza wenyewe ovyo bila sababu, ndio wenye macho yaliyolegea mpaka kuwa mekundu, ndio wanaopiga piga makelele njiani na majumbani, ndio wanaopata hasara ya mali zao, na kupiga mayowe, anayetapika ovyo n.k… Hii hali mpaka afikie mtu, ni lazima atukuwa mule mlevi wa kishinda kilabuni usiku kucha.

Hii inafunua nini?

Ni kutuonyesha jinsi kitu chenye ulevi kinapotumiwa kwa muda mrefu na sanaa, kinavyoweza kuleta matokeo yakubwa Zaidi..

Lakini biblia inatuambia kuwa  ipo DIVAI MPYA. Ambayo sisi wakristo, tunakunywa na katika hiyo, tunalewa. Lakini kanuni ni ileile hatutaweza kulewa vema na kutoa matokeo yake, kama hatutakaa sana katika kuinywa..

Na divai yenyewe si mwingine Zaidi ya ROHO MTAKATIFU.

Siku ile ya Pentekoste mitume walipojazwa Roho Mtakatifu, walionekana kama walevi, waliolewa kwa mvinyo mpya..Kumbe hawakujua kuwa alikuwa ni Roho Mtakatifu kawafanya vile. Kuonyesha kuwa Roho naye huwa anawalewesha watu wake pia katika roho.

Matendo 2:12 “Wakashangaa wote wakaingiwa na shaka, wakiambiana, Maana yake nini mambo haya?

13 Wengine walidhihaki, wakisema, wamelewa kwa mvinyo mpya.

14 Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu.

15 Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana;

16 lakini jambo hili ni lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Yoeli,

17 Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto”.

Na matokeo ya kuleweshwa kisawasawa na Roho Mtakatifu, ni kutoa matunda yake.. ambayo tunayasoma katika, Wagalatia 5:22 na pia kufanya kazi kama za mitume, walizofanya baada ya kupokea Roho..

Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,

23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria”.

Hivyo hatuwezi kuwa na Upendo, kama hatutakaa sana uweponi mwa Mungu tulewe mema yake kisawasawa, hatutakaa tufikie furaha timilifu, kama tutakuwa tunamtafuta Mungu jumapili kwa jumapili, na sio muda wote.. Hatutakaa tuwe na kiasi, na upole na amani, kama hatujibidiishi, kuutafuta uso wa Mungu, kwa wakati mrefu. Hatuwezi kuzidhihirisha karama za Roho kama hatutampa muda wa kutosha mioyoni mwetu.

Tukae sana kwenye mvinyo wetu (Roho Mtakatifu), ili tumzalie Bwana matunda ya haki.

Hivyo, tukiwa na bidii katika Mungu, kusali, kufunga, kutafakari sana, maneno ya Mungu Pamoja na wapendwa wenzetu, Kidogo kidogo tunakuwa walevi, na kwa jinsi tunavyozidisha ndivyo tutakavyoyatoa hayo matunda ya Roho kirahisi sana ndani yetu.

Hivyo sote kwa Pamoja tuanze kuzidisha bidi zetu kwa Bwana. Ili Bwana naye apate nafasi ya kutuponya

Bwana akubariki.

Ikiwa hujaokoka, kumbuka kuwa hizi ni siku za mwisho, siku yoyote Yesu anarudi kulinyakua kanisa lake. Kumbuka injili iliyobakia sasa sio ya kubembelezewa wokovu, ni wewe mwenyewe kuona hali halisi na kujiokoa nafsi yako. Ikiwa upo tayari kutubu leo na kumpa Yesu Maisha yako, basi utakuwa umefanya uamuzi wa busara, katika dakika hizi za majeruhi tulizopo.

Hivyo kama utapenda kupata msaada huo. Basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi, ili tuweze kuomba na wewe na pia kukuongoza sala ya Toba (Bure). >>> +255693036618/  +255789001312 .

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko siku elfu”?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Mapooza ni nini? Na je! Twawezaje kuepukana nayo?

Kwanini Bwana Yesu alisema “Msimwamkie mtu njiani”?

Roho Mtakatifu ni nani?

Bwana alimaanisha nini kusema “kila mtu atatiwa chumvi kwa moto”

Je! Bwana Yesu alikunywa kileo mpaka watu wakasema ni mlafi na mlevi? Kulingana na Mathayo 11:19?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini tofauti ya Mtumwa, Mjakazi na kijakazi?

      1. MTUMWA

Mtumwa ni mfanyakazi wa jinsia ya kiume. Kawaida ya mtumwa, anakuwa anatawaliwa uhuru wake na maamuzi yake kwa asilimia kubwa na yule anayemtumikisha au aliyemwajiri. Hivyo mwanaume yeyote anayetumika chini ya bwana wake kwa namna hiyo anaitwa MTUMWA.

Sisi tuliokoka tunakuwa ni watumwa wa Bwana Yesu (2Timetheo 2:24)..na wote ambao hawajamwamini Bwana Yesu, wanakuwa ni watumwa wa dhambi.

Yohana 8:33 “Wakamjibu, Sisi tu uzao wake Ibrahimu, wala hatujawa watumwa wa mtu wakati wo wote; nawe wasemaje, Mtawekwa huru?

34 Yesu akawajibu, Amin, amin, nawaambia, KILA ATENDAYE DHAMBI NI MTUMWA WA DHAMBI.

35 Wala mtumwa hakai nyumbani sikuzote; mwana hukaa sikuzote.

36 Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli”.

2. MJAKAZI.

Mjakazi ni mtumwa wa kike, sifa zile zile  alizonazo mtumwa wa kiumbe, ndizo hizo hizo alizonazo mjakakazi.

Mfano wa aliyekuwa Mjakazi katika biblia ni Hajiri.

Mwanzo 16:1 “Basi Sarai mkewe Abramu hakumzalia mwana, naye alikuwa na mjakazi, Mmisri, JINA LAKE HAJIRI”.

 3. KIJAKAZI.

Kijakazi ni Mjakazi wa hadhi ya chini Zaidi. Ni sawa na kutumia neno “kitoto” badala ya “mtoto”..ndivyo ilivyo kwa “Kijakazi” na “Mjakazi”..Mfano wa vijakazi katika biblia ni BILHA NA ZILPA.

Mwanzo 35:25 “Wana wa Bilha, KIJAKAZI WA RAHELI, ni Dani na Naftali.

26 Wana wa Zilpa, KIJAKAZI WA LEA, ni Gadi na Asheri”.

Biblia inatushauri tusiwe “watumwa wa wanadamu”, bali wa Bwana.

1Wakorintho 7:23 “Mlinunuliwa kwa thamani; msiwe watumwa wa wanadamu”.

Vile vile tusiwe watumwa wa dhambi ambao ndio Mbaya Zaidi.. Dhambi inapomtumikisha mtu, mshahara wake ni MAUTI!!. Heri mwadamu akiisha kutumikisha atakulipa fedha, au mali..lakini dhambi inakulipa Mauti.

Warumi 6:23 “Kwa maana MSHAHARA WA DHAMBI NI MAUTI; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Sasa ili kuondokana na utumwa wa dhambi, tunafanyaje?

Bwana Yesu alisema maneno yafuatayo..

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.

Jitie Nira ya Bwana Yesu, ufanyike mtumwa wake, kwasababu Mshahara wake ni UZIMA WA MILELE!!!.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA FILEMONI.

MJUE SANA YESU KRISTO.

LEO WOKOVU UMEFIKA NYUMBANI HUMU

Tofauti kati ya maandiko na Neno ni ipi?

Rudi nyumbani

Print this post