DON’T BE AFRAID WHEN YOU GO DOWN.

NI KIPI MUNGU ANACHOKITAZAMA ZAIDI, MOYO AU MWILI?

Je! ni kipi Mungu anachokitazama zaidi, moyo au mwili?

Shalom. Jina la Bwana Yesu libarikiwe.

Karibu tujifunze Biblia. Neno la Mungu linasema katika..Waefeso 5:9-10 “kwa kuwa tunda la nuru ni katika wema wote na haki na kweli; mkihakiki ni nini impendezayo Bwana”.

Hivyo kila siku ni wajibu wetu kuhakiki ni nini impendezayo Bwana. Kila tunachokifanya, kila tunachokisema na kila tunalichopanga kukifanya. Ni lazima tuwe na uhakika kwamba Je! kinampendeza Mungu.

Leo tutajifunza kuhusu mambo Mungu anayoyaangalia ndani ya mtu. Kama wengi wetu tunavyofahamu kuwa kuna usemi ambao upo kila mahali miongoni mwa wakristo wengi usemao kwamba “Mungu haangalii mambo ya nje kama mavazi bali anaangalia moyo”. Usemi huo upo kila mahali kama hujawahi kuusikia jaribu kufanya mahojiano na watu 5 au 10 hususani mabinti utalisikia Neno hilo likitoka vinywani mwao.

Kwanza kabisa ni muhimu kufahamu kuwa Mwanadamu kaumbwa katika sehemu kuu mbili ambazo ni UTU WA NDANI na UTU WA NJE. Utu wa ndani ndio unajumuisha Nafsi na Roho ya mtu. Na utu wa Nje ndio hii miili tuliyonayo. Hivyo kuna utu wa ndani na utu wa nje. Soma (Warumi 7:22, Waefeso 3:16),

Sasa aliyeufanya utu wa ndani ndio huyo huyo aliyeufanya utu wa nje. Hivyo vyote viwili kwake anavitazama. Lakini tukija katika suala la Ibada zetu sisi binafsi na Mungu ni ukweli usiopingika kwamba Mungu anatazama utu wetu wa ndani, na si nje. Ingekuwa anatazama miili yetu basi asingesikiliza sala zetu tunapojifungia vyumbani mwetu na kuomba tukiwa kifua wazi, au asingesikia sala zetu au sifa zetu tuwapo bafuni tunaoga. Hivyo hiyo ni wazi kuwa Mungu anaitazama mioyo yetu zaidi ya miili yetu.

Lakini linapokuja suala la kuwepo nje mahali ambapo pana mkusanyiko wa watu wengi. Kama kanisani au barabarani. Ni lazima ujifunike kwasababu haupo wewe na Mungu hapo..Bali upo wewe, Mungu pamoja na watu wengine. Mungu anatazama kweli moyo wako lakini hao wengine hawaoni moyo wako bali mwili wako, na wanapokuona upo nusu-uchi, au umevaa mavazi yasiyostahili au yasiyo na heshima, mioyoni mwao kutatokea tamaa, kutatoka shuku mbaya, kutatoka aibu, kutatokea kukwazika na wakati mwingine hasira na matusi.

Sasa mambo hayo ndiyo yanayomchukiza Mungu kwasababu unawakosesha wengine. Na ndio maana katuambia tuvae mavazi ya kujisitiri kila mahali tunapokwenda. 1Timotheo 2:9 “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi;”

Usipofanya hivyo, utakuwa unatenda dhambi kwa kuwakosesha wengine. Na Biblia inasema katika..

Marko 9.42 “Na ye yote atakayemkosesha mmojawapo wa wadogo hawa waniaminio, afadhali afungiwe jiwe la kusagia shingoni mwake, na kutupwa baharini.”..

Wewe hujali mwingine anatenda dhambi kwaajili yako. Lakini Mungu anajali sana, adhabu yake ndio hiyo hapo kwamba ni afadhali “kufungiwa jiwe la kusagia na kutupwa baharini”, kuliko kumfanya mtu mmoja akutamani kutokana na uvaaji wako.Kuliko kumfanya mtu mmoja aige uvaaji wako utahukumiwa kwaajili ya hayo.

Kama unasikia joto na unataka kuomba au kuabudu huku umevaa nguo fupi, basi nenda nyumbani kwako peke yako, vaa nguo zako fupi. Jifungie peke yako mahali asipoweza mtu hata mmoja kukuona omba unavyotaka na Sali unavyotaka. Hapo Mungu kweli hataangalia mavazi yako bali roho yako. Lakini unapotoka nje! Hiyo ni habari nyingine kabisa. Mavazi yako na mwonekano wako unajalisha sana. Bwana Yesu alisema..

Mathayo 5:16 “Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni”.

Sasa Ikiwa kuangaza kwako ni nusu-uchi barabarani, ni nani atayayatazama matendo yako na kumtukuza Mungu mbinguni?

Mtu mmoja tu unapomkosesha! Kumbuka sio watu 20, biblia inasema mmoja tu!! Ni huzuni kubwa sana kwa Mungu. Hakuna mtu anayeweza kukutamani ukivaa nguo za kujisitiri mwili wako wote. Usidanganyike na Semi za kishetani zinazokwambia na kukufundisha utembee nusu uchi barabarani au uingie ibadani na vimini hakuna shida. Huo ni uongo wa shetani 100%, ambao unatokana na upambanuzi mbaya wa maandiko…maswali ya moyo au mwili kwamba Mungu anaangalia moyo zaidi ya mwili yakatae.

Na tunapozungumzia uvaaji, tunalenga mavazi..sio mapambo!. Mapambo kama lipstick, wigi, hereni, make-up zote kama kujipaka hina, kuchora tattoo,kupaka wanja.kuchonga nyusi, kujichubua… hayo ni machukizo kabisa ambayo biblia imeyakataza (Soma 1Timotheo 2:9-10, Walawi 19:28). Hupaswi hata kujipamba na kumwomba Mungu ukiwa chumbani mwako peke yako. Kwasababu ni sanamu umeziweka juu ya mwili wako, na hivyo huwezi kumwomba Mungu na huku kuna sanamu kichwani mwako au mwilini mwako.

2Wakoritho 6:16 “Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.

17 Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha”.

Bwana akubariki sana.

Kama hujaokoka! Mlango wa Neema upo wazi, ila si karibuni, na ile njia ya uzima inazidi kuwa nyembamba. Kuokoka kesho ni ngumu kuliko leo, hivyo ni vyema ukafanya uamuzi leo, kwasababu biblia inasema saa ya wokovu ni sasa. Amua kwa dhati kutubu dhambi zako zote huku ukimaanisha kuziacha kabisa, na kisha baada ya kutubu tafuta ubatizo sahihi, ambao huo utakufanya ukamilishe wokovu wako. Ubatizo sahihi ni wa maji mengi na kwa Jina la Yesu kulingana na Matendo 2:38. Na kwa kufanya hivyo Roho Mtakatifu atakutia muhuri na kuwa wake milele, na kukupa uwezo wa kushinda dhambi.

Maran atha!

Mada Nyinginezo:

SAMEHE KUTOKA NDANI YA MOYO WAKO.

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

KAMA MUNGU ANABORESHA KAZI ZAKE, KWANINI WEWE USIBORESHE ZA KWAKO?.

Mpagani ni nani?

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE! MTUMISHI KUTOKUWA NA FEDHA NI ISHARA KUWA KUNA TATIZO KATIKA IMANI YAKE?

Jina kuu la Bwana wetu YESU KRISTO libarikiwe. Ni siku nyingine tena Bwana ametupa neema ya kuiona, Hivyo ninakukaribisha tujifunze tena maneno ya uzima maadamu siku ile inakaribia.

Watumishi wengi wa Mungu wameshakutana na changamoto kama hii ya watu kuwauliza mbona huyo Mungu wenu mnayemtumikia hawafanyi kuwa matajiri ikiwa yeye ni Tajiri…

Lakini mtu huyu huyu anayeuliza swali kama hili na yeye ukimuuliza Je! Wewe ni mkristo?. Atakuambia ndio, ukimuuliza Je unaiamini biblia unayoisoma atakuambia ndio ninaiamini.

Ukimuuliza tena Je! unamwamini Bwana Yesu? atakuambia ndio, Na vipi kuhusu mitume wake. Je unawaamini nao? atakuambia ndio ninawaamini asilimia mia kuwa walikuwa ni watumishi walioitwa na Mungu kutuletea sisi Imani ya kikiristo..

Lakini ukimwambia Je! Unajua hao unaowaamini sasa kuna wakati hawakuwa na chochote mfukoni mwao lakini Mungu alikuwa anawatumia bila matatizo yoyote. Atakuambia huo ni uongo..

Matendo 3:1 “Basi Petro na Yohana walikuwa wakikwea pamoja kwenda hekaluni, saa ya kusali, saa tisa.

2 Na mtu mmoja aliyekuwa kiwete toka tumboni mwa mamaye alichukuliwa na watu, ambaye walimweka kila siku katika mlango wa hekalu uitwao Mzuri, ili aombe sadaka kwa watu waingiao ndani ya hekalu.

3 Mtu huyu akiwaona Petro na Yohana wakiingia hekaluni aliomba apewe sadaka.

4 Na Petro, akimkazia macho, pamoja na Yohana, akasema, Tutazame sisi.

5 Akawaangalia, akitaraji kupata kitu kwao.

6 Lakini Petro akasema, MIMI SINA FEDHA, WALA DHAHABU, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, simama uende”.

Embu jaribu kifikiria kwa ukaribu mistari hiyo. Omba-omba huwa hahitaji pesa nyingi kama vile mtu wa kawaida anavyoweza kuomba. omba-omba huna wanahitaji vichenchi chenchi tu, vilivyobakia mfukoni shilingi 100, mia 200, mia 300 basi ikizidi sana 500. Na ukiwapa wanashukuru sana na kuona kama siku yao imekuwa nzuri sana. Ni hela ambazo mtu wa kawaida haziwezi kumshinda kutoa..

Lakini mitume wa Bwana Yesu Kristo, hawakuwa nazo, walikiri kwa vivywa vyao kuwa hawana fedha wala dhahabu, hawana chochote. Sio kwamba walikuwa nazo wakawa wanazuia kumpa hapana, ni kweli hawakuwa na kitu mfukoni… Lakini hilo halikuwafanya wajione kuwa sio watu walioitwa na Mungu..Badala yake wakamweleza walicho nacho…ambacho ni Jina la YESU KRISTO, na hilo ndilo waliloliona kuwa lina thamani kubwa kuliko fedha zote duniani.

Mtumishi wa kweli wa Mungu anacho kitu ambacho fedha haiwezi kufikia thamani yake, anazo habari za uzima. Injili inayoweza kumfanya mtu apate uzima wa milele jambo ambalo fedha haiwezi kufanya. Hakuna mtu anayeweza kuongeza muda wa Maisha yake kwa fedha. Na ndio maana na sisi tunaoujasiri kusema..Hatuna fedha wala dhahabu lakini tunalo Neno la Mungu linaloweza kuokoa roho za watu.

Hivyo kama mtumishi wa Mungu kwa fedha alizonazo kama uthibitisho wa utume wake, Na si kwa Neno la Mungu. Nataka nikuambie umepotea njia..kwasababu ni kweli wanaweza wasiwe na hicho unachotamani kukiona kwao..Lakini hao ndio watiwa Mafuta wa Mungu wanaokuletea wewe habari njema za wokovu..na uponyaji wa Roho yako, usiwadharau!.

Yule kiwete ambaye tangu kuzaliwa alikuwa hawezi kutembea. Laiti angewadharau wale Mitume na kulazimisha apate fedha kutoka kwao. Angekufa na hali yake, hata angepewa fedha za mchango na watu wote wa dunia nzima. Hakuna matibabu yoyote duniani ambayo yangeweza kumfanya atembee.

Biblia inasema siku za mwisho kutatokea kundi kubwa la watu watakaokuwa wanapenda fedha (2Timotheo 3:2)..Yaani kwao fedha itakuwa ni kipimo cha kila kitu, hadi katika mambo ya rohoni. kama mchungaji huna gari basi hakuna mtu atakayekuja kusikilza Neno la Mungu kanisani kwako hata kama unafundisha kweli kiasi gani..

Kama ukisimama barabarani kuhubiri upo na biskeli na spika yako, hata kama uwepo wa Mungu upo hapo kuwaokoa watu kiasi gani, na ishara na miujiza vinatendeka, watu watageuza vichwa upande wa pili na kuondoka zao. Lakini wakimuona nabii fulani wa uongo anatembea na walinzi, anafundisha mafundisho yake mwenyewe na kuuza chupa za maji ya upako, na Zaidi ya yote hawaambiwi chochote kuhusu Maisha yao ya dhambi. ndio anakuwa wa kwanza kwenda kumsikiliza na kukunua.

Sisemi watumishi wa Mungu wanapaswa wawe maskini, lakini leweke hilo akilini kuwa mambo ya ufalme wa mbinguni hayapimwi kwa mizani ya fedha au utajiri,..Tukilijua hilo tutaweza kujipima sisi na kuchagua ni wapi pa kudumu kujifunza na ni wapi tusidumu, kwa ajili ya usalama wa Roho zetu.. Hizi ni siku zile za hatari ambazo shetani amejikita Zaidi kuwapotosha watu nyuma ya vazi la uzuri na urembo, na utanashati, na mafanikio..lakini ndani yake ni shimo la kuzimu..Hivyo Bwana atusaidie sote.

Ubarikiwe sana.

 

 

Mada Nyinginezo:

ALIYE MKUU KATIKA UFALME WA MBINGUNI.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

CHUKIZO LA UHARIBIFU

NGURUMO SABA

Rudi Nyumbani:

Print this post

UWE MWAMINIFU HATA KUFA.

Uwe mwaminifu hata kufa…

Ufunuo 2:2 “Nayajua matendo yako, na taabu yako, na subira yako, na ya kuwa huwezi kuchukuliana na watu wabaya, tena umewajaribu wale wajiitao mitume, nao sio, ukawaona kuwa waongo;

3 tena ulikuwa na subira na kuvumilia kwa ajili ya jina langu, wala hukuchoka”.

Wengi wanasema Kristo hatujali.. Lakini kiuhalisia ni kwamba anatujali kuliko sisi tunavyodhani. Kila kitu tunachokifanya anakiona, na anakihesabu. Hakuna kinachoenda bure mbele zake. Alisema katika Neno lake “lakini ninyi, hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote.( Mathayo 10:30)”. Sasa mtu anayejua idadi ya nywele zetu zote na hakuna hata moja inayopotea bila yeye kujua ataachaje kufahamu kila tendo jema tunalolifanya?

Ukiona mtu anasema naijua tabu yako. Ni wazi kuwa ni mtu anayejali….tena anakuambia najua Taabu yako na shida zako unazozipitia, anajua uvumilivu wako, na subira yako…Na anajua jitihada zako na jinsi gani huchoki kufanya mema. Ni wazi kuwa ni mtu anayekujali sana na anap moyo wa upendo na wewe.

Ndio maana tunasoma katika kitabu cha Ufunuo, Bwana Yesu alipotoa ujumbe kwa kila kanisa alianza na Neno hili “Nayajua matendo yako,”. Ikifunua kuwa Bwana anatujua sana, kila dakika anatuangalia..Kama ni mabaya tunayafanya anayaona, vile vile kama mema tunayafanya anayaona..Leo ulimhurumia mtu Fulani mnyonge anaona!. Na anarekodi, leo ulimsamehe mtu aliyekuudhi ingawa alikuumiza sana kiasi kwamba ilikuwa hata ni ngumu kumsamehe lakini ulimsamehe tu hivyo hivyo, anakuona. Na atalitaja tukio hilo siku ile mbele ya malaika wake watakatifu.

Ulimhurumia mtu Fulani na kumsaidia katika hali aliyokuwepo. Analiona tendo hilo.

Ulimwombea mwingine katika maombi yako, ingawa yeye hakuna lolote analokufanyia. Bwana anaona na analiandika katika kumbukumbu isiyoweza kusahaulika. Ulitukanwa ukavumilia na wala hukurudisha tusi anaandika. Ulimtolea sadaka yako ingawa ndio hiyo tu uliyokuwa nayo huna nyingine. Ameliweka moyoni mwake zitapita siku kadhaa wewe utasahau lakini yeye lipo moyoni mwake. Kila siku kila dakika linamrudia rudia katika mawazo yake milele na milele.

Wakati mwingine ingawa unaomba lakini majibu yanachelewa, lakini bado unamvumilia. Jambo hilo analiona na uvumilivu wako kwake, upo akilini mwake kila dakika. Mateso na dhiki unazopitia ambazo bado hujaona tumaini na bado hujaiachilia Imani. Nataka nikuambia anaona! Na inamwingia moyoni kuliko hata wewe inavyokusumbua.

Sehemu nyingine anasema “Nayajua matendo yako na upendo na imani na huduma na subira yako; tena kwamba matendo yako ya mwisho yamezidi yale ya kwanza. (Ufunuo 2:19)”

Ufunuo 2:8 “Haya ndiyo aneneyo yeye aliye wa kwanza na wa mwisho, aliyekuwa amekufa, kisha akawa hai.

9 Naijua dhiki yako na umaskini wako, (lakini u tajiri) najua na matukano ya hao wasemao ya kuwa ni Wayahudi, nao sio, bali ni sinagogi la Shetani.

10 Usiogope mambo yatakayokupata; tazama, huyo Ibilisi atawatupa baadhi yenu gerezani ili mjaribiwe, nanyi mtakuwa na dhiki siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima.”

Wakati mwingine huyu huyu Yesu wetu mwema anaruhusu tujaribiwe kwa dhiki na vifungo. Na wakati mwingine anakaa mbali kama vile hayupo. Tambua ya kwamba yupo pembeni yako hata wakati wa tabu. Na anaiona shida yako, Anasema Uwe mwaminifu tu hata kufa. Naye atakupa Taji ya Uzima,Usianze kunung’unika nung’unika kama walivyofanya wana wa Israeli kule jangwani. Ukifanya hivyo utapoteza Taji yako.

Bwana Yesu naye alipitia majaribu mazito kuliko hata sisi. Yeye alitiwa mikononi mwa shetani ili ajaribiwe, akatundikwa msalabani. Na wakati akiwa msalabani japo kuwa alikuwa ni mwana wa Mungu lakini alisikia hali Fulani ya ukame wa kiroho isiyokuwa ya kawaida mpaka akasema Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?. Lakini alikuwa mwaminifu mpaka kufa hakuikana imani wala kunung’unika akiwa pale msalabani. Na Mungu akampa Taji ya Uzima ambayo leo hii tunamtukuza kama MFALME MKUU ASIYESHINDWA. Haleluya!.

Kwahiyo na sisi wakati mwingine Mungu ataruhusu tujaribiwe. Ila tunapaswa na sisi tuwe waaminifu mpaka kufa. Tukifahamu kuwa Mwangalizi wetu yupo mbinguni akirekodi kila tukio na kila tendo jema tunalolipitia, akirekodi kila chozi, na kila tendo tunalolivumilia. Akirekodi kila jeraha tunaloumizwa na tunaposamehe. Tukilitambua hilo itatufanya tuishi maisha ya kujipa moyo kila siku Kuwa mateso ya Ulimwengu huu ni ya kitambo tu. Ipo taji tumewekewa mbinguni. Na upo wakati wa kufutwa machozi.

Malaki 3:13 “Maneno yenu yamekuwa magumu juu yangu, asema Bwana. Lakini ninyi mwasema, Tumesema maneno juu yako kwa namna gani?

14 Mmesema, Kumtumikia Mungu hakuna faida; na, Tumepata faida gani kwa kuyashika maagizo yake, na kwa kwenda kwa huzuni mbele za Bwana wa majeshi?

15 Na sasa twasema ya kwamba wenye kiburi ndio walio heri; naam, watendao uovu ndio wajengwao; naam, wamjaribuo Mungu ndio waponywao.

16 Ndipo wale waliomcha Bwana waliposemezana wao kwa wao. Naye Bwana akasikiliza, akasikia; na kitabu cha ukumbusho kikaandikwa mbele zake, kwa ajili ya hao waliomcha Bwana, na kulitafakari jina lake.

17 Nao watakuwa wangu, asema Bwana wa majeshi, katika siku ile niifanyayo; naam, watakuwa hazina yangu hasa; nami nitawaachilia, kama vile mtu amwachiliavyo mwanawe mwenyewe amtumikiaye”.

Bwana akubariki.

Mada Nyinginezo:

KITABU CHA UKUMBUSHO

UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.

PENGINE MUNGU ALISHASEMA NAWE KWA NJIA HII.

INJILI YA KRISTO HAITANGAZWI KWA HATI MILIKI.

SIKU ILE NA SAA ILE.

WOKOVU NI SASA

Rudi Nyumbani:

Print this post

KARAMA YA MUNGU NI UZIMA WA MILELE.

 Kwanini karama ya Mungu ni uzima wa milele?

Ukikaa chini ukajaribu kutafakari kwa umakini hili Neno UZIMA WA MILELE, utashangaa sana, wakati mwingine utajiuliza hili jambo linawezekanaje kanaje, na ukilitafari sana utaona kama akili yako inafika sehemu inagota. Eti unaishi tu siku zote bila kuwa na kikomo, unaishi leo, miaka mia inapita bado unaendelea tu kuishi.

Miaka elfu inapita bado unaendelea kuishi, miaka milioni moja inapita bado unaendelea kuishi, miaka bilioni moja inapita bado unaendelea kuishi. Miaka trilioni moja inapita ndio bado hata maisha hayajaanza…unaendelea tu, miaka kuadrilioni moja (ambayo ni sawasawa na miaka trilioni elfu moja), inapita bado unaendelea kuishi, miaka kuintilioni moja inapita ndio bado hata hakuna dalili ya kufika mwisho, miaka seksitilioni moja, wewe bado unaendelea tu kuishi. Miaka oktilioni na nonilioni, na desilioni na anidesilioni inapita, hapo bado utaendelea tu,..miaka dodesilioni, na tradesilioni na kuatuordesilioni na kuindesilioni na seksidesilioni bado tu safari inaendelea ukiwa bado kama kijana mdogo tu, n.k. n.k. tukiziandika namba zote hapa tunaweza kujaza ukurasa mzima na bado zisitoshe….

Embu jaribu kufikiria hayo ni maisha marefu kiasi gani, leo hii tu ikipita miaka 20 au 30 unaona kama ilikuwa ni zamani sana, na tena unaiita enzi hizo, sasa hapo bado haijatapita miaka milioni moja sijui hiyo utaiitaje labda utaaita kama ile ya historia zama za mawe za kwanza, pengine hata kumbukumbu zake utakuwa umezipoteza..

Sasa Mungu asiyekuwa na mwisho ametuahidia zawadi hiyo kuu bure, Hata tusingepewa zawadi nyingine hiyo tu ya Uzima wa Milele ingetutosha. Ni zawadi kubwa sana isiyoelezeka.

Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni UZIMA WA MILELE katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Na kumbuka pia Mungu asiye na mipaka, miaka hiyo yote hatutakuwa tunaishi tu kama watu wasiokuwa na mwelekeo “idle”. Au unaishi tu bila maaana yoyote hapana! vinginevyo umilele utakuwa wa ku-boa.

Badala yake kila siku, kila wakati kutakuwa na matukio yake na mambo yake mazuri mapya, yaani tutayafurahia maisha kila iitawapo leo, kwasababu kila siku itakuwa na mambo yake, kutakuwa hakuna magonjwa, kutakuwa hakuna kuzeeka, kutakuwa hakuna shida, kutakuwa hakuna mahangaiko, wala kupigwa na jua hakutakuwepo, wala ulemavu hautakuwepo, wala uchungu, wala kuudhiwa, wala kuumizwa, wala kudaiwa. Siku zote tutaishi katika raha isiyo na kifani, tukiushangaa utukufu wa Mungu na kumwabudu yeye katika raha isiyoelezeka.

Mungu kashaipigia mahesabu kila siku moja ya umilele hivyo analijua tukio ambalo litatokea siku Fulani ya mwaka Fulani wa bilioni moja huko mbeleni kwamba wewe utakuwa unafanya kitu Fulani na Yule kitu fulani,..Huyo ndio YEHOVA..hatuishi kumshangaa kwa matendo yake ya ajabu.

Na ndio maana Mungu anasema katika..

Isaya 55:8 “Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema Bwana.

9 Kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu”.

Kauli hiyo ya Mungu inatuthibitishia kuwa mipango ya Mungu aliyotuandalia sisi, hatuwezi kuidhania au kuifikiria ipasavyo hata kwa chembe ndogo sana. Kwasababu ipo mbali sana na upeo wetu wa kufikiri, na ndio maana ni jukumu letu kuhakikisha sisi sote hatuukosi huo uzima wa milele.. Kwasababu hapa ni kama tunaandaliwa tu kwa ajili ya kuishi maisha halisi, hapa duniani hatuna maisha, miaka 70 au 80 sio maisha. Bali tunaandaliwa tu kwa ajili ya kuishi kule ambako Mungu alitukusudia tuishi, tunatengenezwa tu ili tuweze kustahimili huo umilele unaokuja huko mbeleni..

Hivyo tukiwa tunayatafakari hayo kila siku tutapata nguvu ya kutokujali ni nini tunapoteza sasa tukiwa hapa duniani, kwa ajili ya maisha yetu ya umilele ya baadaye…hatutojali tunapoteza fursa ngapi za biashara kwa ajili ya kuhudhuria maombi, hatutojali tunapoteza hiki au kile kwa kwenda ibadani, kwa kujifunza Neno la Mungu…Hatutojali ni mambo mangapi ya kidunia yanatupita, sisi tunatazama maisha ya milele Mungu aliyotuandalia…

Hata mithali ya kidunia inasema, “usiache mbachao kwa msala upitao”. Ikiwa na maana tusiopoteze uzima wetu wa milele kwa vitu vya kidunia vinavyopita, ambavyo mwisho wake ni hapa tu..Itatufaidia nini tuupate ulimwengu mzima, kisha tupate hasara ya nafsi zetu.? Kwasababu mshahara wa dhambi ni mauti…lakini karama ya Mungu ni uzima wa milele.

Lakini uzima wa milele huu kuupata ni bure, nao unakuja kwa kumwamini tu YESU KRISTO, pale unapotubu kwa kudhamiria kwa dhati kutoka moyoni mwako kwamba kuanzia leo unaacha dhambi zako zote..Unafanya maamuzi ya kuacha pombe, kuacha uasherati, kucha uvaaji mbaya, kuacha rushwa, kuacha wizi n.k. Na vitu vyote ulivyokuwa unaviona vinakufaidisha sana vya kidunia unaviacha vyote unavihesabia kama ni mavi. Kama Mtume Paulo alivyovihesabia.

Wafilipi 3.7 “Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, naliyahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo.

8 Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa kama MAVI ili nipate Kristo”

Na baada ya kutubu na kuyahesabia mambo yote uliyokuwa unayafanya machafu kama MAVI. Hatu inayofuata ni kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamwisha katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO, kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako sawasawa na Matendo 2:38,.Kisha Bwana atakupa kipawa cha Roho Mtakatifu..Hivyo Hatua hizo zote zikikamilika juu yako basi na wewe utakuwa umefanyika kuwa mwana wa Mungu na yeye mwenyewe atakupa karama hii ya uzima wa milele bure..

Kumbuka …Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”…Na sio katika Ulimwengu.

Ubarikiwe sana.

Mada Nyinginezo:

UFUNUO: Mlango wa 1

INJILI KULINGANA NA TEKNOLOJIA

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

Rudi Nyumbani:

Print this post

LITANIA YA BIKIRA MARIA JE! NI SALA YA KIMAANDIKO?

Litania ya bikira Maria mtakatifu ni nini?, Je Maria ni Malkia wa Malaika, Malkia wa mitume na malkia wa wakristo?.

Maana ya “LITANIA” ni Mfululizo wa sala ambayo maneno yake ni ya kujirudia rudia, ambayo yanahusisha upande mmoja kuitikia. (Mkusanyiko unaitikia). Mtindo huu wa sala unatumika sana na Kanisa Katoliki.

Sehemu ya baadhi ya Maneno yanayotamkwa katika sala hiyo ya litania ya bikira maria ni haya..

  • Maria Mtakatifu ………. utuombee
  • Mzazi Mtakatifu wa Mungu …….. utuombee
  • Bikira Mtakatifu Mkuu wa Mabikira …….. utuombee
  • Mama wa Kristo ……… utuombee
  • Mama wa Neema ya Mungu ………….. utuombee
  • Mama Mtakatifu sana ……… utuombee
  • Mama mwenye usafi wa Moyo ……….. utuombee
  • Mama mwenye ubikira ……….. utuombee
  • Mama usiye na doa ……….. utuombee
  • Mama mpendelevu ………. utuombee
  • Mama mstajabivu ………. utuombee
  • Mama wa Muumba ………. utuombee
  • Mama wa Mkombozi ………….. utuombee
  • Mama wa Kanisa……….. utuombee
  • Bikira mwenye utaratibu ………….. utuombee
  • Bikira mwenye heshima ………….. utuombee
  • Bikira mwenye sifa ………….. utuombee
  • Bikira mwenye uwezo ………….. utuombee
  • Bikra mweye huruma ………….. utuombee
  • Kioo cha haki ………….. utuombee
  • Kikao cha hekima ………….. utuombee
  • Sababu ya furaha yetu ………….. utuombee
  • Chombo cha neema ………….. utuombee
  • Chombo cha kuheshimiwa ………….. utuombee
  • Chombo bora cha ibada ………….. utuombee
  • Waridi lenye fumbo ………….. utuombee
  • Mnara wa Daudi ………….. utuombee
  • Mnara wa pembe ………….. utuombee
  • Nyumba ya dhahabu ………….. utuombee
  • Sanduku la Agano ………….. utuombee
  • Mlango wa Mbingu ………….. utuombee
  • Nyota ya asubuhi ………….. utuombee
  • Afya ya wagonjwa ………….. utuombee
  • Kimbilio la wakosefu ………….. utuombee
  • Mtuliza wenye huzuni ………….. utuombee
  • Msaada wa waKristo ………….. utuombee
  • Malkia wa Malaika ………….. utuombee
  • Malkia wa Mababu ………….. utuombee
  • Malkia wa Manabii ………….. utuombee
  • Malkia wa Mitume ………….. utuombee
  • Malkia wa Mashahidi ………….. utuombee
  • Malkia wa Waungama dini ………….. utuombee
  • Malkia wa Mabikira ………….. utuombee
  • Malkia wa Watakatifu wote ………….. utuombee
  • Malkia uliyepalizwa Mbinguni ………….. utuombee
  • Malkia wa Rozari takatifu ………….. utuombee
  • Malkia wa amani ………….. utuombee

Lakini je! Sala hii ni ya kimaandiko?.

Kabla ya kuitafakari kama ni sala ya kimaandiko au la..Ni muhimu kufahamu kuwa lengo la ujumbe huu..sio kumshutumu mtu, wala kumhukumu, wala lengo sio kujifanya kuwa upande mmoja unajua zaidi ya mwingine..Lengo kuu ni kujifunza Maandiko, huku tukionyana na kusahihishana kasoro zetu kwa kutumia Biblia. Kama tulivyoagizwa katika Wakolosai 3:16.

Sasa tukirudi kwenye sala hiyo hapo juu..Tunaweza tukahoji mambo machache muhimu..

Je! Ni kweli  Maria Mtakatifu? na ni mama mwenye Ubikira?..

Si kweli  kwasababu Maria Baada ya kumzaa Bwana hakuendelea kuwa Bikira..na pia alipokufa, alizikwa na huko alipo sio bikira, yupo katika roho ambapo yeye naye anasubiri ufufuo ambao utakaokuja katika siku ile ya unyakuo,..ambapo atavaa mwili wa utukufu kama watakatifu wengine na kwenda kumlaki Bwana mawinguni. Hivyo hawezi kuombwa kwa lolote wala haelewi kinachoendelea duniani.

Kadhalika Maria sio Malkia wa wakristo wala Malkia wa Malaika.  Kwasababu Malaika hawana Malkia,..Na hakuna mahali popote katika maandiko matakatifu panasema hivyo..Isipokuwa wapagani ndio walikuwa wanaabudu kiumbe wanachokiita wao malkia wa mbinguni. Lakini katika maandiko hakuna sehemu yoyote inayoonesha kuwa kulikuwa au kutakuwepo na malkia wa malaika. Hivyo ni dhahiri kuwa kama sala hii haipo katika Biblia basi ni lazima itakuwa imetungwa tu na watu fulani ambao nia yao ni kupoteza wengine.

Pia Maria sio Malkia wa Mitume, wala  wa manabii wala sio malkia wa mababu, wala malkia wa wakristo..

Hivyo sala hii sio sala ya kimaandiko bali ya kibinadamu, ambayo ndani yake upo mpango mkubwa sana wa Ibilisi..kuwafanya watu waabudu sanamu na vitu visivyokuwepo..

Ndugu kama unataka kusali, Bwana Yesu mwenyewe alitufundisha sala..Nayo ni hii..

Luka 11:1 “Ikawa alipokuwa mahali fulani akiomba, alipokwisha, mmoja katika wanafunzi wake alimwambia, Bwana, tufundishe sisi kusali, kama vile Yohana alivyowafundisha wanafunzi wake.

2 Akawaambia, Msalipo, semeni, Baba [yetu uliye mbinguni], Jina lako litakaswe, Ufalme wako uje, [Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.]

3 Utupe siku kwa siku riziki yetu.

4 Utusamehe dhambi zetu, kwa kuwa sisi nasi tunamsamehe kila tumwiaye. Na usitutie majaribuni [lakini tuokoe na yule mwovu]”

Ingekuwa Maria anastahili kuombwa Bwana Yesu angewafundisha wanafunzi wake hapo juu wamwombe Maria..Lakini unaona hajafanya hivyo..Ikimaanisha kuwa sala inastahili kwenda kwa Baba yetu wa Mbinguni basi.

Kama ulikuwa unasali sala hiyo ya “litania ya bikira Maria” na hukujua kuwa ni sala ya uongo, na leo umejua. Usifanye hivyo tena, ni machukizo mbele za Mungu..Ni ibada za sanamu ambazo Mungu amezikataza mara nyingi katika Biblia..Mpe leo Yesu Kristo maisha yako naye atakupa tumaini na moyo mpya wa sala.

Bwana akubariki.

Tafadhali share na wengine. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

JINSI YA KUJIWEKA KARIBU NA MUNGU.

JINSI YA KUJIWEKA KARIBU NA MUNGU.

Hakuna kitu kinachomtamaisha Mungu kama kujiweka karibu na sisi, tunalithitisha hilo katika maandiko haya “Yakobo 4:5 Au mwadhani ya kwamba maandiko yasema bure? Huyo Roho akaaye ndani yetu hututamani kiasi cha kuona wivu?” Unaona? lakini kwa bahati mbaya sisi ndio hatujui kanuni ya jinsi ya kujiweka karibu na Mungu..Na ndio maana tukiendelea mbele kidogo maandiko yanasema:..

Yakobo 4:8 Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi…

Unaona biblia inatupa ufahamu mwepesi wa  namna ya sisi kuwa karibu na Mungu, nao ni kwa kumkaribia tu.. Watu wengi wanadhani wanaweza kuwa karibu na Mungu, au Mungu kuwa rafiki yao wa karibu wakiwa katika hali zao zile zile za kale, na mienendo ile ile wanayoiendea kila siku, na huku hawataki kuonyesha jitihada za kumkaribia Mungu, ndio hapo mwisho wa siku wanaona kama vile Mungu hana faida yoyote maishani mwao, au wanaona kama vile amekufa hayupo, au hawasikii, au hawajali…yote hiyo ni kwasababu hawajajua namna ya kumkaribia Mungu..

SASA TUNAWEZAJE KUMKARIBIA MUNGU?

Tukiendelea kusoma ule ule mstari unasema…

Yakobo 4:8 “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili.

9 Huzunikeni na kuomboleza na kulia. Kucheka kwenu na kugeuzwe kuwa kuomboleza, na furaha yenu kuwa hamu.

10 Jidhilini mbele za Bwana, naye atawakuza”.

Unaona anatoa kanuni kadha wa kadha  hapo ya kwanza na ya msingi ni:

ITAKASENI MIKONO YENU, ENYI WENYE DHAMBI:

Ukiwa mwenye dhambi, yaani kwa ufupi ukiwa hujaokoka, kamwe hutakaa umkaribie Mungu kwa namna yoyote ile, haijalishi, unatoa zaka kiasi gani, haijalishi unasaidia yatima kiasi gani, haijalishi, unahudhuria ibadani kiasi, maadamu upo nje ya Kristo, tayari wewe upo mbali sana na Mungu. Hivyo hatua ya kwanza na ya msingi ya Mungu kukuribia ni kutubu kwa kudhamiria kabisa kuacha dhambi zako zote, kumwambia Bwana Yesu akusamehe dhambi zote ulizomkosea, kisha kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi Kwa jina la Yesu Kristo sawasawa na Matendo 2:38, kisha kupokea  Roho Mtakatifu. Kwa kufanya hivyo utakuwa umeshakamilisha hatua ya kwanza ya kumkaribia Mungu..

JAMBO LA PILI ANASEMA NI : KUISAFISHA MIOYO YENU, ENYI WENYE NIA MBILI:

Wapo watu baada ya kumpa Kristo maisha yao, bado wanayatamani mambo yale yale waliyoyaacha kule nyuma, sasa watu kama hao Mungu hawezi kuwakaribia kwasababu mioyo yao inakuwa imegawanyika, nusu kwa Mungu, nusu kwenye dunia..Ikiwa umedhamiria kweli kumfuata Kristo mfuate kwa kumaanisha kweli kweli, acha kila kitu mfuate, na hiyo inakuja kwa kujikana nafsi yako na kujitwika msalaba wako na kumfuata, unakuwa tayari kukubali kuchekwa, au kudharauliwa, au kutukanwa au kufanyiwa jambo lolote baya kwa ajili ya imani yako bila kutetereka..Na Mungu akishaona moyo wako upo thabiti kwake, hapo ndipo na yeye anaongeza hatua yake nyingine ya kukukaribia.

YA TATU NI: HUZUNIKENI NA KUOMBOLEZA NA KULIA:

Tena anaendelea kusema.. Kucheka kwenu na kugeuzwe kuwa kuomboleza, na furaha yenu kuwa hamu…Hii haimaanishi kuwa ujifanye kuwa mtu wa huzuni kila saa, kama vile mfiwa hapana, bali unaugua kwa kuchukia dhambi, unaomboleza kwa mabaya yanayofanyika, sio unafurahia kuona ubaya, au dhambi zikifanyika, Na kwa kawaida kuugua pamoja na maombolezo kunazaa pia na kuombea wengine, na kuliombea kanisa lote kwa ujumla..na kuwashuhudia wengine habari njema..Sio pale tunapokuwa wakristo ndio basi tena, maadamu sisi tumeshaokolewa hayo mengine hayatuhusu…Tukiwa watu wa namna hiyo basi vilevile tufahamu kuwa Mungu naye atakuwa mbali na sisi lakini kama tukiwa tunahuzunika na kuomboleza kwa ajili yetu sisi na kwa wengine ili waokolewe, na kuchukua hatua stahiki basi tufahamu kuwa Mungu hapo atakuwa tena karibu zaidi na sisi, kwasababu tunaichukua ile huzuni yake tunaifanya ya kwetu..Mungu hafurahii maovu, wala hapendi mtu hata mmoja apotee.

NA MWISHO NI: JIDHILINI MBELE ZA BWANA.

 Kwa namna ya kawaida hakuna mtu asiyempenda mtu mnyenyekevu, Vivyo hivyo na kwa Mungu tukiwa watu wanyenyekevu watu wa kujishusha mbele zake, watu tunaoungama makosa yetu, basi tutamvuta kwa haraka sana aje karibu sana na sisi kama ilivyokuwa kwa Daudi..Lakini tukijiona sisi kila kitu tunajua, hatutaki kuambiwa chochote, hata kama ni kweli, tunajiona tunajua biblia sana, dini zetu na madhehebu yetu yanatutosheleza kama vile mafarisayo na waandishi walivyokuwa, kwa kiburi chao walimkosa Mungu, walidhani wapo karibu na YEHOVA kumbe walikuwa hatua mia mbali na yeye.

FAIDA ZA KUWA KARIBU NA MUNGU NI ZIPI?

Faida kubwa ni kuambukizwa ule utukufu wake, kama tu vile pale unapokaa  karibu na mtu aliyejipulizia marashi makali kwa muda mrefu akiondoka ile harufu bado itabakia katika mwili wako..Vivyo hivyo na kwa Mungu ikiwa umezifuata hizo hatua zote basi ule utukufu wa Mungu unaingia ndani yako, kama vile Musa alivyokaa uweponi mwa Mungu kwa siku zile 40 kule mlimani, aliposhuka uso wake uling’aa kama vile wa malaika..Ni kwasababu alikuwa karibu sana na Mungu…Lakini sisi hatung’ai uso wa mwilini bali uso wa rohoni..

Matokeo yake ni kuwa jambo lolote tutakalomwomba Mungu tutatendewa…

Yohana 15:7 Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa.

Vilevile wewe utakuwa ni wa kwanza kuzipokea zile siri za ndani kabisa za Mungu, kwasababu wewe ni bibi-arusi wa Kristo, na sikuzote bibia-arusi ndiye anayejua siri ya Bwana arusi, halikadhalika hakuna jambo lolote au adui yoyote atakayekushida kwasababu muda wote unaonekana kama miale ya moto duniani..Vilevile Mungu anakufanya kuwa chombo chake kiteule cha kuwachunga kondoo wake wengine.

Hizo ndio faida zake kuu. Kwanini tusitamani kuwa karibu naye? Tufanye bidii sote tufike hapo. Amen.

Ubarikiwe sana.

Mada Nyinginezo:

TUNAMHITAJI SANA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUYAELEWA MAANDIKO.

NITAFUNGUAJE MILANGO ILIYOFUNGWA MBELE YANGU?

ALIYE MKUU KATIKA UFALME WA MBINGUNI.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini Musa alipewa mbao mbili za mawe na sio moja au zaidi

SWALI: Tukisoma Kutoka 34:1-5 Tunaona Musa anaambiwa atengeneze mbao mbili za mawe mfano wa zile za awali. Sasa swali ni kwanini ziwe mbili na sio moja au Zaidi? Na ni kwanini ziwe mbao za mawe. Je kuna ufunuo wowote kuhusu hilo?


KWANINI ZILICHONGWA KWENYE MAWE.

Sababu kuu ya Mungu kuzichonga kwenye mawe na si penginepo ni kuonyesha uthabiti na ubora wa sheria zake., kumbuka kitu chochote kinachochongwa katika mwamba ni tofauti na kile kinachochorwa katika karatasi au kinachochongwa katika ubao..Mwamba wakati wote ni mgumu hivyo hata kile kinachochonga kitahitaji jitihada Zaidi katika kuchongwa, Japo inatumia nguvu zaidi na gharama lakini faida yake mwisho wa siku inakuwa ni kubwa, nayo ni UBORA..tofauti na  kile kinachochorwa katika katarati ambapo kifuto kikipita kidogo tu maandishi yale yanafutika na kazi yote inakuwa bure, au kile kinachochorwa  katika mbao ambacho nacho pia moto kidogo tu ukipita kazi yote inateketea na kumbukumbu lote kufutika….Lakini mwamba hata moto ukipita, ndio kwanza inazidi kuwa imara Zaidi, Na ndio maana utaona baada ya pale zile mbao mbili za mawe zilidumu kwa maelfu ya miaka mbeleni..

Kufunua kuwa upo ubao ulio mgumu Zaidi ya mwamba, ambapo Mungu aliuweka tayari huko mbeleni kuandika amri zake zisizoweza kufutika milele..na ubao huo si mwingine Zaidi ya moyo wa mwanadamu, huo ni bora Zaidi ya mwamba wowote duniani…Mungu akishaandika sheria  zake ndani ya mwaminio, haziwezi kufutika tena milele, wala kupotea, kama ilivyokuwa katika agano la kale watu walikuwa wakizisahau sahau mpaka wakumbushwe vilevile vibao vile vilikuja kupotea baadaye na wala kumbukumbu lake halijulikana lilipo mpaka leo…

Lakini biblia inasema..

Yeremia 31:31 ‘’Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda. 

32 Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa mume kwao, asema Bwana.

 33 Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; Nitatia sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. 

34 Wala hawatamfundisha kila mtu jirani yake, na kila mtu ndugu yake, wakisema, Mjue Bwana; kwa maana watanijua wote, tangu mtu aliye mdogo miongoni mwao hata aliye mkubwa miongoni mwao, asema Bwana; maana nitausamehe uovu wao, wala dhambi yao sitaikumbuka tena’’.

Soma pia..

Waebrania 10:16  ‘’Hili ni agano nitakaloagana nao baada ya siku zile, anena Bwana, Nitatia sheria zangu mioyoni mwao, Na katika nia zao nitaziandika; ndipo anenapo’’,

Unaona huo ndio ubora wa agano jipya..Sheria ile inaandikwa juu ya vibao vya mioyo yetu kwa sisi tulioamini isiyoweza kuharibiwa au kufutwa na mtu yeyote milele.. Hivyo kama wewe upo nje ya Kristo, mlango wa neema bado upo wazi, lakini hautakuwa wazi hivyo milele..Mkaribishe leo ndani ya maisha yako, kwa kutubu na kuacha dhambi zote, kisha baada ya hapo ataanza kukutengeneza na sheria yake ataiandika moyoni mwako, na wala dhambi haitakushinda milele, kwasababu sheria hiyo imechorwa ndani ya vilindi vya moyo wako asipoweza mtu wala shetani kuifikia na kuifuta…sheria hiyo itakulinda mpaka siku ile ya kwenda mbinguni katika Unyakuo.

Tubu dhambi zako sasa, nawe uufurahie wokovu, na neema ya bure ya BWANA YESU.

NA JE! KWANINI ZIWE MBAO MBILI ZA MAWE NA SI PUNGUFU AU ZAIDI?

Fahamu kuwa zile amri kumi za Mungu ziliganyika katika mafungu makuu mawili, la kwanza ni Upendo kwa Mungu wetu, na la pili Ni upendo kwa jirani zetu kama nafsi zetu..Hakuna shaka zile nne za kwanza zilikuwa katika ubao mmoja unaojitegemea ambazo zinamuhusu Mungu, na zile sita za pili zilikuwa katika ubao wa pili ambazo zinatuhusu sisi, …

Na hiyo ndio mihili mikuu miwili  hata katika agano jipya ambayo tunapaswa tutembee nayo, hizo ndizo mbawa zetu mbili tunapaswa turuke nazo kila siku, ya kwanza ni hiyo ya kumpenda Mungu, ambapo tukimpenda Mungu tutafanya yote anayotuagiza, na ya pili ndio hiyo tuwapende jirani zetu kama nafsi zetu tukiwapenda ndugu tutasitiri wingi wa dhambi, na kila tendo ovu dhidi ya majirani zetu na jamii kwa ujumla….Hatuwezi kuruka na mbawa mojawapo katika ya hizo, bali zote mbili zinakwenda pamoja..

Ubarikiwe sana..

Mada Nyinginezo:

UTAJI ULIOKUWA JUU YA USO WA MUSA.

FIMBO YA HARUNI!

UTHABITI WA AGANO LA MUNGU KWA MKRISTO.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

NYIMBO ZA WOKOVU

Utauliza kuna nyimbo za wokovu?. Jibu ni Ndio! Uimbaji ni moja ya karama za Roho kama zilivyo karama nyingine, kama vile Uchungaji, Unabii, ualimu, uinjilisti n.k.

Na kama vile kulivyo na manabii wa uongo, na waalimu wa uongo na wainjilisti wa Uongo. Kadhalika pia kuna WAIMBAJI WA UONGO. Tabia zinazoonekana kwa manabii wa Uongo ndio zile zile zilizopo kwa waimbaji wa uongo.

Manabii  Uongo wanapenda fedha. Na ndivyo ilivyo kwa waaimbaji wa Uongo. Nabii wa uongo hatahubiri wokovu hata siku moja. Bali atahubiri anavyojua yeye ilimradi tu, asiwaudhi watu ili wawe wepesi kufungua pochi zao na kumpatia chochote. Hawataweza kuvumilia kamwe kufanya kazi ya Mungu bila kupata malipo yoyote kutoka kwa waumini. Na wanajua kitu pekee  kitakachomgeuza mtu na kuwa mkristo ni kumwambia kweli yote ya Biblia.

Waimbaji wa uongo nao ni hivyo hivyo. Kamwe hawataimba nyimbo za wokovu, za watu kutubia dhambi zao na maonyo ya siku za mwisho. Bali wataimba nyimbo za kuwafariji watu hata katika hali za dhambi walizopo. Lengo kuu na madhumuni ni ili wasiwaudhi mashabiki wao na hivyo wakakosa soko/fedha kwa nyimbo zao. Wanajua wakimhubiria mtu wokovu, mtu yule hatafikiria habari za kumpa yeye fedha. Bali atafikiria habari za kuyatakasa maisha yake. Mtu atatoka pale amechomwa moyo wake na mwenye moyo mzito, kitu ambacho wao hawakitaki. Kitawakoseshea mapato. Watakula nini??

Kadhalika Manabii wa uongo wanapenda UMAARUFU.

Na Waimbaji wa uongo ni hivyo hivyo. Leo utaona mtindo fulani umetoka nao pia wamo. Tofauti yao na watu wasanii wa ulimwengu huu haipo. NI WASANII, Kuimba kwao ni SANAA na sio Injili. Malengo yao ni kuwa waimbaji maarufu duniani na sio kitu kingine. Lakini muhubiri wa kweli au mwimbaji wa kweli lengo lake sio kuwa maarufu duniani. Au sio kujulikana duniani kote bali ni kuhakikisha injili inajulikana na watu wote, inawafikia watu wote duniani. Watu watubu na kuokoka na kuacha dhambi na kumgeukia Kristo na kwenda mbinguni. Hiyo ndiyo raha ya mhubiri au mwimbaji wa kweli wa nyimbo za wokovu.

Na kama uimbaji ni moja ya karama za Roho Mtakatifu. Viwango vya Roho ni vile vile. Bwana Yesu alisema mtu yeyote akitaka kuwa mwanafunzi wangu.. “ajikane mwenyewe ajitwike msalaba wake anifuate. (Mathayo 16:24)”. Uanafunzi sio tu uchungaji, au uinjilisti au ualimu..bali ni pamoja na uimbaji.

Na pia anasema katika Luka..

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana.

48 Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, atapigwa kidogo. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na zaidi.”

Umeijua Injili ya kweli. Lakini bado huimbi nyimbo za wokovu na badala yake unaimba tu nyimbo za kuwaburudisha watu. kiasi kwamba hata wakiwa bar! wanaona faraja tu kuipiga au kuisikiliza nyimbo yako. Fahamu kuwa kwako vitatakwa na vya ziada.

Na sifa nyingine ya mwisho ya Mwimbaji wa uongo, ni kufanya kazi kwa kutegemea malipo. Kwamfano utasikia mwimbaji fulani hataki kuimba mpaka ahakikishiwe kiwango fulani cha fedha. Akiahidiwa kiwango kidogo hasimami kuimba. Ukiona mwimbaji yupo hivyo basi fahamu kuwa ni mwimbaji wa uongo.

Ulishawahi kuona wapi, mchungaji anaalikwa kwenda kuhubiri kwa kuahidiwa kiwango fulani cha fedha?. Au mwinjilisti gani anakwenda kuhubiri huku tayari kashapambana na bei ya kupanda madhabahuni. Sasa kama wachungaji ambao karama zao zimewekwa wazi kwenye maandiko hawafanyi hivyo kwanini wewe unayejiita mwimbaji ufanye hivyo?. Huoni kama kutakuwa na kasoro kubwa sana kwako?.

Bwana atusaidie sana. Kama ulikuwa ni mmoja wapo wa wanaofanya hivyo, au wenye malengo ya kufanya hivyo. Na ulikuwa hujui kama ni makosa. Mlango wa kutubu bado upo wazi. Kutubu maana yake ni kugeuka kuacha kile ulichokuwa unakifanya kisicho sawa. Ukiamua tu kugeuka na kuamua kumwimbia Mungu NYIMBO ZA WOKOVU na sio NYIMBO ZA KUSAKA PESA. Bwana atakupokea, Kwasababu hizi ni siku za mwisho ambazo biblia imetabiri kuinuka kwa wimbi kubwa la manabii wa uongo, Ikijumuisha huko huko na waimbaji wa uongo na waalimu wa uongo na waachungaji wa uongo.  Bwana akusaidie usiwe miongoni mwao, Bwana atusaidie tusiwe miongoni mwao.

Maran atha!


Mada Nyinginezo:

YUDA ISKARIOTE! MTUME ALIYECHAGULIWA NA BWANA YESU.

INJILI NI NINI?

SIKU YA HUKUMU ITAKUWAJE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya ”Mizani ya hadaa ni chukizo kwa Bwana”?

Je! katika biblia mstari huu una maana gani? ”Mizani ya hadaa ni chukizo kwa Bwana Bali vipimo vilivyo sawasawa humpendeza’’? (Mithali 11:1)? ..Hiyo mizani ya hadaa ni ipi?


JIBU: Katika maisha ya kawaida Bwana anataka tuwe na haki, katika mambo yetu tunayoyafanya kila siku iwe ni katika biashara zetu au kazi zetu…Unapouza kitu uza kulingana na thamani ya kitu chenyewe unachouza, usizidishe thamani ya kitu kile ili upate faida kubwa vile vile usipunguze kipimo cha kitu kile ili upate faida kubwa…

USIPANDISHE THAMANI.

Kwa mfano kama wewe ni muuzaji wa mchele, na umenunua kilo moja kwa shilingi elfu mbili, na bei inayoziwa sokoni ni shilingi elfu na mia tano kwa wateja…Na unajua kabisa faida yako inapaswa iwe ni shilingi mia tano kwa kila kilo, au ikizidi sana mia 7.

Lakini wewe unakwenda kuuza kwa bei ya juu kuliko inavyotakiwa ili wewe upate faida kubwa bila kujali kuwa unamkandamiza yule unaye muuzia kisa tu anaouhitaji mkubwa wa kitu hicho..Labla tuseme unauuza mchele ule kwa shilingi elfu 4 kwa kilo moja..Hivyo kwa kufanya hivyo, Ni machukizo kwa Bwana. Hiyo ni mizani ya hadaa, hutendi haki.

USIPUNGUZE KIPIMO;

Vilevile Bwana hapendezwi na kupunguza kipimo cha bidhaa ile kwa hila, kwamfano unapunguza kwa makusudi kiwango cha upimaji, aidha katika mizani yako ili usiuze kingi upate faida kubwa..Hilo nalo ni chukizo kwa Bwana…Hiyo nayo ni mizani ya hadaa, hutendi haki.

Vilevile katika kazi nyingine zote tunazozifanya iwe ni kwa Mungu, au mashuleni, au  mahakamani, tunapaswa tuamue kwa haki bila kumpendelea mtu, kwa kutokujali fedha, au heshima, au cheo, au jinsia,..Bwana anapenda haki, na palipo na haki ndipo kiti chake cha enzi kilipo…..(Zaburi 97:2)

Zaburi 89: 14 Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chako, Fadhili na kweli zahudhuria mbele za uso wako.

Na ndio maana biblia inasema .. Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu. (Mathayo 5:48)

Bwana akubariki.

Mada Nyinginezo:

TWEKA MPAKA VILINDINI.

WALIO NA HEKIMA NDIO WATAKAOELEWA.

UNYAKUO.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

NITAFUNGUAJE MILANGO ILIYOFUNGWA MBELE YANGU?

Nifanye nini ili niifungue milango iliyofungwa mbele yangu?

Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe. Moja ya mada inayozungumzwa na wakristo wengi hususani wa kanisa hili la Mwisho ni juu ya namna ya kufungua milango iliyofungwa mbele yetu.

Na kwa haraka haraka wengi wetu tunatafuta njia za haraka haraka ilimradi tu, Milango iliyopo mbele yetu ifunguke. Ndio hapo utaona baadhi wanaenda kwa watumishi wawaombee, wengine watatafuta mahali panapouzwa Mafuta fulani, au maji fulani ya baraka au upako. Wengine watakwenda kutafuta kwa kuombewa nyota zao na kutabiriwa. Na mambo mengine mengi yanafanyika katikati ya wakristo. Na Bahati mbaya wengi baada ya kufanya hivyo hali inabakia kuwa vile vile. Ni kwanini?. Ni kwasababu hiyo sio njia au Namna Mungu aliyoiweka ya kufungua milango iliyofungwa mbele yetu.

Biblia inasema katika..

Ayubu 22:21 “Mjue sana Mungu, ili uwe na amani; Ndivyo mema yatakavyokujia.”

Kumjua Mungu maana yake ni kutafuta maarifa ya kujua ni nini Mungu anataka, Yakikosekana maarifa ya kumjua Mungu ni rahisi sana kuangamia.

Sasa leo kwa ufupi sana tutatumia biblia kujua namna yakufungua milango iliyopo mbele zetu. Na pia kumbuka kabla ya yote kuwa sio kila mlango uliofungwa mbele yako. Ni shetani kahusika! Hapana mingine ni Mungu mwenyewe kaifunga kwaajili ya makusudi yake. Na tunajua makusudi ya Mungu siku zote ni Mema. Hivyo tutazungumzia kwa ujumla namna ya kufungua milango yote (Iliyofungwa na Mungu au shetani)

Tusome.

Ufunuo 3:7 “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Filadelfia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye mtakatifu, aliye wa kweli, aliye na ufunguo wa Daudi, yeye mwenye kufungua wala hapana afungaye, naye afunga wala hapana afunguaye.

8 Nayajua matendo yako. Tazama, nimekupa mlango uliofunguliwa mbele yako, ambao hapana awezaye kuufunga, KWA KUWA UNAZO NGUVU KIDOGO, NAWE UMELITUNZA NENO LANGU, WALA HUKULIKANA JINA LANGU”.

Kwanza tunaona hapo kumbe Kristo anaweza kufunga kitu na hakuna awezaye kukifungua..Na pia anauwezo wa kufungua na hakuna awezaye kuufunga. (Hiyo ni point ya kwanza ya kuweka akilini). Ili tufahamu kuwa sio kila mlango uliofungwa mbele yetu ni shetani kahusika. Hapana bali mengine ni Kristo mwenyewe ndiye aliyehusika.

Lakini tukiendelea na mstari wa 8 ndio tutapata majibu ya swali letu. “Tutafunguaje milango iliyofungwa mbele yetu?”.

Bwana Yesu mwenye ufunguo wa mambo yote anaanza kwa kusema…Nayajua matendo yako!. Ikifunua kuwa mlango kufunguliwa au kufungwa unahusiana na “Matendo ya Mtu”..Anaendelea na kusema “nimekupa mlango uliofunguliwa mbele yako, ambao hapana awezaye kuufunga, KWA KUWA UNAZO NGUVU KIDOGO, NAWE UMELITUNZA NENO LANGU, WALA HUKULIKANA JINA LANGU”

Umeona sababu za huyu mtu kufunguliwa mlango?. Sababu zipo tatu.

Ya kwanza Kwa kuwa anazo nguvu kidogo. Ya pili Kwa kuwa amelitunza Neno lake. Na ya tatu Hakulikana jina lake.

Kristo hajabadilika sababu zile zile alizozitumia kale ndizo anazozitumia leo kufungua milango iliyofungwa mbele yetu.

Ni lazima kwanza tuwe na nguvu za rohoni. Biblia inasema.

1 Yohana 2: 14 “….Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na Neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu”. Kuliweka Neno la Mungu ndani yetu ndio NGUVU ZA ROHONI. Mtu asiye na Neno la Mungu ndani yake, nguvu zake za rohoni zipo chini sana. Na kumbuka kuliweka Neno moyoni sio kujua vifungu vingi vya Biblia, kwa kuikariri. Hapana bali kuliweka Neno la Mungu moyoni ni kuliishi Neno moja lililoandikwa katika biblia. Ni kuona matokeo ya lile Neno katika maisha yako.

Kwamfano biblia inaposema “wapendeni Adui zenu, waombeeni wanaowaudhi..Mathayo 5:44”. Kama mtu kaushika huo mstari kwa kuukariri na hautendei kazi hicho kilichoandikwa hapo. Mtu huyo hajalishika Neno la Mungu moyoni mwake, lakini kama anakitendea kazi kwa kuwaombea wengine huyo kaliweka moyoni Neno la Mungu.

2) Sababu ya Pili ya Kufunguliwa mlango. Ni kwa kulitunza NENO LA MUNGU.

Kulitunza ni tofauti kidogo na kuliishi. Kulitunza maana yake unalitenda lile Neno kila siku katika maisha. Sio leo unalitenda kesho unaliacha.

3) Na sababu ya tatu na ya mwisho ni Kutolikana JINA lake.

Maana yake ni kutoikana Imani. Kulikana jina la Mungu na kuikana Imani ni kitu kimoja. Kuikana Imani kunajumuisha kurudi nyuma kiimani. Petro alimkana Bwana Yesu maana yake alirudi nyuma kiimani. Kadhalika mtu anayerudi nyuma kiimani ni sababu tosha ya kujifungia milango ya Baraka mbele yake.

Ndugu hatupaswi kukimbilia maji ya Upako kupata kibali mbele yetu. Au kupata fursa Fulani mbele yetu. Njia pekee ya kupata fursa ya kitu Fulani ni kurekebisha MATENDO YETU na KULITUNZA NENO LA MUNGU maishani mwetu. Na ndipo hayo yote yaliyosalia uliyokuwa unamwomba Mungu yanafunguka.

Kama ulikuwa hujampa Kristo maisha yako, unageuka sasa kwa kudhamiria kuacha dhambi kabisa. Na humfuati kwasababu tu unataka fursa Fulani. Hapana bali kwasababu umejigundua wewe ni mwenye dhambi na unahitaji kubadilishwa. Na Kristo mwenyewe anapenda watu wanaotubu dhambi zao na kukiri kuwa ni wakosaji. Yeye anawapa msamaha bure wote wanaokimbilia kwake haijalishi wameasi kiasi gani. Na baada ya kupata msamaha huo ambao utaambatana na AMANI Fulani moyoni isiyokuwa ya kawaida. Moja kwa moja usikawie nenda kakamilishe wokovu wako kwa kubatizwa katika maji tele(Yohana 3:23) na kwa jina la Yesu kulingana na (Matendo 2:38). Na Bwana mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu ambaye atakuongoza katika kuijua kweli yote ya maandiko na kukusaidia kushinda dhambi ambazo ulikuwa huwezi kuzishinda kwa nguvu zako.

Hapo utakuwa umeokoka kwa kuzaliwa mara ya pili. Na utakuwa na tumaini la uzima wa milele. Na kwasababu umeupata kwanza ufalme wa Mungu na Haki yake. Na hizo fursa na milango iliyofungwa ambayo umekuwa ukiitabikia kwa muda mrefu itafunguka yenyewe pasipo stika wala chumvi.

Bwana akubariki. Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

DANIELI: Mlango wa 2

MIHURI SABA

USIPOLITENDEA KAZI NENO LA MUNGU.

Inaruhusiwa Kula nyama ya Nguruwe kwa Mkristo wa Kweli?

Rudi Nyumbani:

Print this post