DON’T BE AFRAID WHEN YOU GO DOWN.

KUONGOZWA SALA YA TOBA

Kuongozwa sala ya toba.


Ikiwa leo upo tayari kufanya uamuzi wa kumgeukia Yesu Kristo, na kutaka akuokoe na kukusamehe dhambi zako kabisa, Basi ni uamuzi wa busara sana ambao, utaufurahia maisha yako yote, kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Kumbuka..

  • Kwa Yesu lipo tumaini la uzima wa milele.
  • Kwa Yesu Unapata utulivu wa nafasi na faraja. Alisema.

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.

  • Kwa Yesu zipo Baraka.
  • Na kwa Yesu upo msahama wa kweli:

Isaya 1:18 “Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu”.

Kwa hiyo unapokuja kwake leo hii kwa kumaanisha, ujue kuwa hiyo mizigo ya dhambi uliyonayo haijalishi ni mingi kiasi gani ataitua mara moja, haijalishi uliuwa watu wengi namna gani, haijalishi ulizini nje ya ndoa mara nyingi kiasi gani, haijalishi ulikwenda kwa waganga mara nyingi namna gani..Ikiwa tu upo tayari leo kumkaribisha Yesu moyoni mwako basi ataitua, na kukusamehe kabisa kana kwamba hakuna chochote ulichowahi kumkosea..Na atakupa amani.

Hivyo kama leo ni siku yako ya kuyasalimisha maisha yako kwake, jambo la kwanza unalopaswa kufahamu ni kwamba, unapaswa umaanishe kutoka katika moyo wako, kuwa kuanzia sasa, wewe na dhambi basi, wewe na ulimwengu basi kabisa..

Hivyo kama umeshakuwa tayari kufanya hivyo basi..

Basi, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuwa na uhalali kwa kuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako.

Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Hongera kwa kuokoka.

Hivyo ikiwa utahitaji msaada zaidi basi, wasiliana nasi kwa namna hizi hapa chini..+255 789001312

Pia unaweza ukatutumia ujumbe tukuunge kwenye magroup yetu ya Whatsapp ya kujifunza Neno la Mungu.

Vile vile tunakualika kutembelea website hii, yenye mafundisho ya Neno la Mungu zaidi ya 1000, na maswali na majibu mengi sana yaliyojibiwa. Tazama chini, usome baada ya hayo.

Na Bwana akubariki sana.

Group la whatsapp jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.

RABI, UNAKAA WAPI?

TAZAMA, MWISRAELI KWELI KWELI, HAMNA HILA NDANI YAKE!

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

KWANINI AWE NI PUNDA NA MWANA-PUNDA?

UNYAKUO.

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

Rudi Nyumbani:

Print this post

BWANA WA MAJESHI.

Kwanini Mungu aitwe Bwana wa majeshi? Je! Ni kweli anayo majeshi au ni cheo tu amependa kujivika?

Watu wengi hatufahamu kuwa Mungu anayo majeshi yake…Ni kweli hili jina limekaa sana ulimini mwetu, lakini bado hatufahamu vizuri ni kiwango gani Mungu anajiita Bwana wa majeshi..Naamini siku tukilifahamu hilo vema basi tutaishi maisha yasiyo na woga na wasiwasi hata kidogo hapa ulimwenguni.

Kumbuka hajiiti Mungu wa “Jeshi” kana kwamba ni moja hapana bali anajiita Mungu wa “Majeshi” ikiwa na maana ni mengi.

Ni majeshi ambayo yaanzia mbinguni mpaka duniani. Na kama tunavyojua sikuzote majeshi kazi yake, kulinda usalama, kutunza amani, na kuupigania ufalme, kinyume na maadui zao.

Mungu alijitambulisha kama Bwana wa Majeshi, sio kwamba alitaka  sisi tumwogope, Hapana, bali alitaka sisi tujue nguvu aliyonayo katika kutupigania watu wake dhiki maadui zao (Shetani na mapepo yake). Embu Jaribu kutengeneza picha Mungu angejiita tu  majina haya, ingekuwaje?

  • Bwana wa Amani(Jehova-Shalom), au
  • Bwana mpaji wetu, (Yehova-yire), Au
  • Bwana atuponyaje(Yehova-Rafa), Au
  • Bwana atuonaye (Yehova-Shama) N.K.

Unadhani hiyo ingetosha tu?..Kwamfano tungekuwa tunapitia katika vita vikali tumezungukwa na maadui wa mwilini na rohoni, kilichobaki ni kufa na kupona, unadhani Bwana mpaji wetu(Yehova yire), tungemuhitaji wakati huo? Wakati unaona unakaribia kuchinjwa Je, utamwambia Mungu nipatie mali?..Jibu la, kinyume chake atamuita Bwana kwa nguvu  zote asimame mwenyewe akupiganie na kuwasambaratisha  maadui zako ili upone.

Hapo ndipo jina la BWANA WA MAJESHI linapoitwa (Yehova-Saboati)

Ilifika wakati Daudi alikuwa anakwenda kupigana na adui yake mkubwa Goliathi, moyoni alijua kabisa mtu kama huyu wa vita, haiwezekani kumshinda, Lakini alipogundua kuwa yupo Bwana wa Majeshi Mungu wa vita,karibu naye ndipo aliposimama kwa ujasiri na kwenda kupigana naye..tusome..

1Samweli 17:43 “Mfilisti akamwambia Daudi, Je! Mimi ni mbwa hata umenijia kwa fimbo? Mfilisti akamlaani Daudi kwa miungu yake.

44 Mfilisti akamwambia Daudi, Njoo huku kwangu; nyama yako nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni.

45 Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe KWA JINA LA BWANA WA MAJESHI, MUNGU WA MAJESHI ya Israeli uliowatukana.

46 Siku hii ya leo Bwana atakuua mkononi mwangu, nami nitakupiga, na kukuondolea kichwa chako, nami leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya majeshi ya Wafilisti, ili kwamba dunia nzima wajue ya kuwa yuko Mungu katika Israeli.

47 Nao jamii ya watu wote pia wajue ya kwamba Bwana haokoi kwa upanga wala kwa mkuki; maana vita ni vya Bwana, naye atawatia ninyi mikononi mwetu”.

Unaona hapo Daudi alimuita Bwana wa Majeshi, aje kumsaidia..

Ndugu fahamu kuwa, Unapokuwa mkristo, hupaswi kuwa woga wa kitu chochote, Inasikitisha kuona ni mkristo wa muda mrefu halafu bado anaogopa wachawi na washirikina, pamoja na mapepo na majini.

Shetani mwenyewe anawashaangaa, anapoona watu wa Bwana wa majeshi kama sisi, nasi tunamwogopa yeye..

Kuna wakati Elisha alikuwa anatembea na mtumishi wake Gehazi, wakafika mahali wakajikuta wamezungukwa na majeshi mengi ya maadui zao, yule mtumishi akawa anatetemeka na kuogopa sana..Lakini Elisha hakuogopa kwasababu alijua majeshi ya Mungu wa Israeli aliyo nayo ni mengi kuliko ya wale wengine..Bwana wa majeshi ndio nguvu yake.. Ndipo Elisha akamwomba Mungu amfungue macho alione hilo.

2Wafalme 6:17 “Elisha akaomba, akasema, Ee Bwana, nakusihi, mfumbue macho yake, apate kuona. Bwana akamfumbua macho yule mtumishi; naye akaona; na tazama, kile kilima kilikuwa kimejaa farasi na magari ya moto yaliyomzunguka Elisha pande zote.

18 Na walipomtelemkia Elisha akamwomba Bwana, akasema, Uwapige, nakusihi, watu hawa kwa upofu. Akawapiga kwa upofu sawasawa na neno la Elisha.

19 Elisha akawaambia, Njia hii siyo, na mji huu sio, nifuateni mimi, nami nitawapeleka kwa mtu yule mnayemtafuta. Akawapeleka Samaria”.

Hivyo hata wewe ukiwa unapitia mahali ambapo, unaona vita vikali vipo mbele ya basi mwite Bwana wa Majeshi atakusaidia,..

Lakini ikiwa wewe bado upo nje ya wokovu, nataka nikuambie hata umwite vipi Mungu katika vita vyako hawezi kukusikia wala kukusaidia, kwasababu wewe sio wa ufalme wake. Wachawi watakutesa, mapepo yatakutesa, ibilisi atakutesa,.. Lakini ukitaka leo awe upande wako, basi ni sharti kwanza umpokee YESU KRISTO katika moyo wako. Akusemehe dhambi zako, ndipo pale utakapoliita jina la Bwana wa majeshi atakusikia na kukusaidia.

Ikiwa upo tayari Kumpa YESU leo  maisha yako basi bofya hapa, kwa Sala ya toba >>> SALA YA TOBA.

Pia yapo mafundisho mengi unahitaji kujua juu ya majeshi ya mbinguni(malaika) wanavyofanya kazi na sisi(tuliookoka), hivyo nakusihi fungua na masomo mengine hapa chini, ufahamu zaidi juu ya ulimwengu wa roho wa malaika wa Bwana na utendaji kazi wao.

Zaburi 24: 10 Ni nani huyu Mfalme wa utukufu? Bwana wa majeshi, Yeye ndiye Mfalme wa utukufu.

Mungu akubariki.

Mada Nyinginezo:

HUDUMU YA MALAIKA WATAKATIFU.

 KUWAHUDUMIA MALAIKA PASIPO KUJUA.

ZIFAHAMU HUDUMA KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.

WAKAMCHA BWANA, NA KUITUMIKIA MIUNGU YAO WENYEWE.

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MASERAFI NI NANI?

Yapo makundi tofauti tofauti ya Malaika wa Mbinguni.  Wapo Maserafi ambao ndio tutakaowazungumzia leo, wapo Makerubi (ambao ndani yake ndio alikuwa shetani), wapo wenye uhai wanne, wapo wazee ishirini na nne.. na wapo Malaika wa vita ambao ndani yake ndio  wakina Mikaeli na wenzake.

Na katikati ya hayo makundi, yamegawanyika vipengele vingi!..wapo malaika wenye mbawa na wasio na mbawa, wapo wenye maumbo kama ya wanadamu lakini pia wapo wenye maumbo kama ya wanyama na ndege.

Kwa ufafanuzi kuhusu makundi hayo ya Malaika,  mwisho kabisa wa somo hili utaona LINK za masomo hayo, zifungue ili uweze kuzisoma.

Sasa Maserafi ni kundi la Malaika ambao kazi yao ni kumsifu na kumtukuza Mungu mbinguni, Wamekizunguka kiti cha enzi kwa maelfu yao, wakimsifu Mungu usiku na mchana. Maserafi wana mabawa sita kila mmoja. Mawili yanakifunika kichwa kufunua kuwa KUFUNUA MAMLAKA YA MUNGU, NA UTAWALA WA KIMUNGU. Kwamba Mungu ndiye kichwa cha mambo yote. Na pia wanafunika kichwa kwasababu wanaona hata hawastahili kumtazama Mungu, wala Mungu kuwatazama wao kwajinsi yeye Mungu alivyo mtakatifu sana.

Na pia hawaishii tu! Kufunika kichwa..bali wanafunika pia Miguu, kufunua jambo kufunua kuwa hawastahili hata Mungu aliye mtakatifu kuona miguu yao.

Na mabawa mawili yaliyosalia ni kwaajili ya kuruka (yaani kupaa).

Kundi hili la malaika tunaona limetajwa katika Kitabu cha Isaya.

Isaya 1: 1 “Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, na pindo za vazi lake zikalijaza hekalu.

2 Juu yake walisimama maserafi; kila mmoja alikuwa na mabawa sita; kwa mawili alifunika uso wake, na kwa mawili alifunika miguu yake, na kwa mawili aliruka.

 3 Wakaitana, kila mmoja na mwenzake, wakisema, Mtakatifu Mtakatifu, Mtakatifu, ni Bwana wa majeshi, dunia yote imejaa utukufu wake”.

Bwana aliwaumba malaika hawa kwa lengo hilo la kumsifu yeye na kuufunua utakatifu wake kwa viumbe vyake vyote…ndio maana katika sifa zao wanaanza na neno.. “Mtakatifu mtakatifu”.  

Na malaika hawa (maserafi) wanatufundisha na sisi jinsi ya kumsifu Mungu..Kwamba tuwapo mbele zake tujisitiri!..

Hebu tujifunze kitu hapa!..sio malaika wote wanaofunika vichwa mbele za Mungu…lakini kundi hili linafanya hivyo? kwanini?…Huoni pia katika kanisa kuna kundi la watu ambao ni lazima lifunike vichwa liwapo ibadani?..na sio tu kufunika kichwa bali hata kujisitiri mwili mzima ikiwemo na miguu.

1Wakorintho 11:5 “Bali kila mwanamke asalipo, au anapohutubu, bila kufunika kichwa, yuaaibisha kichwa chake; kwa maana ni sawasawa na yule aliyenyolewa”

Na ukiendelea kusoma mistari hiyo utaona suala la wanawake kufunika vichwa ibadani limehusishwa na “Malaika”..kasome 1Wakorintho 11:10.

Kwahiyo pia si vyema mwanamke kuingia kanisani bila kufunika kichwa wala kujisitiri mwili..Utakuta mwanamke anaingia ibadani kichwani kaweka wigi, chini kavaa kimini au suruali. Jiulize hapo unakwenda kumwabudu Mungu gani?..Maserafi wasio na dhambi wanajisitiri wewe uliye na dhambi inakupasaje?

Mwisho, Kumbuka Malaika yoyote yule sio wa kuabudiwa!..wala hatupaswi kuweka picha au sanamu ya malaika yoyote yule na kuisujudia, ni Mungu pekee ndiye anayestahili kuabudiwa na kusujudiwa.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

MAKERUBI NI NINI?

WALE WAZEE ISHIRINI NA WANNE (24), WANA KAZI GANI?

Kuna Malaika wangapi?

Je! mbinguni kuna malaika wa kike?. Na je! tukifika mbinguni tutafanana wote?

Malaika wa maji ni yupi na Je kuna aina ngapi za malaika?

Nitaitofautishaje sauti ya Malaika na ya Roho Mtakatifu?

HUDUMU YA MALAIKA WATAKATIFU.

MAJESHI YA PEPO WABAYA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MJUMBE ASIYEKUWA NA UJUMBE.

Mjumbe asiyekuwa na ujumbe:

Ukisoma katika biblia utakumbuka habari ile ya Daudi na mwanawe Absalomu, jinsi walivyoingia katika mapambano makali,.mpaka kuepelekea vita vizito kupiganwa kule msituni..Kama wengi wetu tunavyofahamu, katika vita vile Daudi hakuwepo bali alimtuma amiri jeshi wake mkuu aliyeitwa Yoabu, kupigana nao. Lakini kabla ya kuanza vita Daudi alimwagiza Yoabu, kuwa ahakikishe kijana hawamuui bali wanamleta mikononi mwake akiwa mzima.

Lakini Yoabu alipomkamata Absalomu, alimuua, na kisha akamtupa kwenye shimo refu sana. Na Israeli walipoona kiongozi wao Absalomu amekufa, vita vikaishia pale pale, watu wote wakatawanyika na kwenda makwao.

Sasa kilichokuwa kimebakia, ni kumpelekea Daudi taarifa za vita, Lakini ni nani wa kumpelekea Daudi Habari ya kifo cha mwanawe. Hapo ndipo wakatokea wajumbe wawili mmoja aliitwa, Ahimaasi, mwana wa Sadoki na mwingine, alikuwa ni mkushi.

Sasa huyu Ahimaasi, akamwomba Yoabu, akimbie ampelekee ujumbe Mfalme Daudi kuhusu vita, lakini Yoabu alimwambia, kwasasa wewe huwezi kupeleka ujumbe, na sababu ya kutopeleka ujumbe ni kwasababu zile sio Habari njema apelekazo..

Ndipo Yoabu akamwita kijana mwingine mkushi akamtuma badala yake akamwambia nenda ukamwambie mfalme uliyoyaona..

2Samweli 18:21 “Ndipo Yoabu akamwambia Mkushi mmoja, Nenda ukamwambie mfalme hayo uliyoyaona. Na huyo Mkushi akajiinamisha mbele ya Yoabu, akaenda zake mbio.”

Ndipo huyu mkushi akatii akaondoka mbio mara moja..Lakini yule Ahimaasi, alipoona mwenzake katumwa halafu yeye bado kabaki, akaendelea kumsisitiza Yoabu na yeye aende..Tusome.

2Samweli 18:22 “Ndipo Ahimaasi, mwana wa Sadoki, akamwambia Yoabu mara ya pili, Haidhuru, tafadhali nipe ruhusa, nipige mbio na mimi nyuma ya huyo Mkushi. Naye Yoabu akasema, Mbona wewe unataka kupiga mbio, mwanangu, kwa maana hutapata kitu kwa habari hizo unazopeleka?

23 Akasema, Haidhuru, nitapiga mbio. Akamwambia, Haya, piga mbio. Ndipo Ahimaasi akapiga mbio, akishika njia ya uwandani, akampita yule Mkushi”.

Hivyo wote wawili wakaanza safari, lakini tofauti ya mjumbe wa kwanza na yule wa pili ni kuwa yule mkushi, alikuwa na ujumbe wa kupeleka kwa yale aliyoyaona vitani jinsi Absalomu alivyouliwa, lakini yule mwingine hakuona chochote, alisikia tu..

Sasa biblia inatuambia yule wa pili alipiga mbio Zaidi ya yule wa kwanza na kufika kwa mfalme, (hatujui alipiga short-cut au vipi), lakini alifikia wa kwanza kuliko yule mwingine.

Akafika mpaka malangoni mwa mfalme, akaulizwa, umeleta ujumbe gani? Akasema, Mungu ashukuruwe kwa kuwa maadui zako wametawanyishwa.

Lakini Daudi alipomuuliza Habari za kijana? … sikiliza majibu yake.

2Samweli 18:29 “Mfalme akauliza, Je! Yule kijana, Absalomu, yu salama? Ahimaasi akajibu, Yoabu aliponituma mimi mtumishi wa mfalme, mimi mtumishi wako, NALIONA KISHINDO KIKUBWA, LAKINI SIKUJUA SABABU YAKE”.

Daudi aliposikia hivyo akamwambia simama pembeni, akamngojea yule mwingine afike.. Ndipo alipofika yule mwingine na kuulizwa..naye akajibu, “wote wainukao ili kukudhuru, na wawe kama alivyo yule kijana”(akimaanisha kuwa Absalomu Amekufa).

Ndipo Daudi aliposikia vile alienda kulia sana, akimwombolezea mwanawe..

NI NINI BWANA ANATAKA TUJIFUNZE?.

Kama haujafikiria, kuwa mhubiri, au mchungaji, au nabii au mwinjilisti au mtume, au mjumbe yoyote wa Mungu, kwa njia yoyote ile,iwe katika uimbaji, au uandishi n.k. ni vizuri kwanza ukafahamu na kuuelewa vizuri ni ujumbe gani unakabidhiwa kuupeleka..

Ujumbe/ Agizo kuu tulilopewa na Bwana Yesu kwa mtu yeyote anayetaka kuifanya kazi ya Mungu ni hili..

Mathayo 28:19 “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;

20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi;..”

Sasa jiulize, Je, katika kujibidiisha kwako kuwahubiria watu, Je! Lengo lako ni kuwafanya watu kuwa wanafunzi wa Kristo?, Je! Ni kuwafundisha kuyashika yale yote Yesu aliyotuamuru au mambo ya kidunia tu?..

Wengine wakiulizwa kwanini auhubiri injili kama ile ya mitume injjili kamilifu na ya utakatifu, watakwambia, mimi sikuitwa kuhubiri injili hiyo! Mimi nimeitwa kuwa mfariji tu!! ..Nataka nikuambie ndugu hapo ni sawa na unakimbia bure bila ujumbe wowote kama yule Ahimaasi. Kumbuka hapo kwenye Mathayo 28, agizo hilo lilipewa kwa watu wote kiujumla, hapo Bwana alikuwa hazungumzi na Petro peke yake, au Mathayo peke yake, au Filipo…alikuwa anazungumza na wote waliokuwepo pale Pamoja na sisi wote tunaosoma.

Ikiwa mafundisho yako, hayalengi kuwavuta watu wa Kristo, kinyume chake, ni kuwahubiria tu jinsi ya kufanikiwa hapa duniani..Basi ujue wewe ni mjumbe usiyekuwa na ujumbe.. Na kazi yako haina faida yoyote, haijalishi utakuwa unawakusanya maelfu ya watu kiasi gani kukusikiliza, au wanakusifia kiasi gani.

Ujumbe tuliopewa ni mmoja tu, nao ni kuwafanya “mataifa yote kuwa wanafunzi wake”. Na unamfanyaje mtu kuwa mwanafunzi, Bwana Yesu alishasema katika Luka 14:27

Hivyo chochote tukihubiricho hakipaswi kwenda mbali na kiini hicho cha agizo..Hata kama tutahubiri hayo mengine lakini kiini hicho kionekane, na hiyo ni kwa faida yetu wenyewe ili kazi yetu isiwe bure mbele za Mungu.

Bwana akabariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Je! hizi roho saba za Mungu ni zipi? na je zinatofautiana na Roho Mtakatifu?

SADAKA YA MALIMBUKO.

KUOTA UNACHEZA MPIRA.

MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.

WAKATI WA KRISTO KUSIMAMA,UMEKARIBIA SANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

IJUE NGUVU YA IMANI.

ijue Nguvu ya Imani ipo wapi?


Imani ni ufunguo wa mambo yote.. Ukiwa na Imani timilifu Bwana Yesu alisema unaweza ukauambia hata Mlima Kilimanjaro uondoke pale, na ukajitupe Baharini, na ukakutii..

Watu wanadhani maneno hayo alimaanisha  milima ya rohoni, kwamba unaweza ukayaambia matatizo ondoka hapa uende kule, hapana, bali  maneno yale ni ya mwilini kabisa.. Jambo ambalo wengi hatukubali kukiri ni kuwa hatuna Imani timilifu ya kufanya hivyo (Nami pia sina).

Joshua aliweza kusimamisha Jua, ambalo ni kubwa Zaidi ya dunia, kwanini leo hii isiwezekane, kuamini kuwa mlima ambao ni sehemu ndogo sana ya dunia unaweza kuhamishwa.

Hivyo hakuna jambo lolote linaloshindikana ukiwa na Imani timilifu. Bwana Yesu alisema hivyo katika Marko 9:23.

Lakini kutoweza kuhamisha milima haimaanishi kuwa huna Imani kabisa, hapana, Imani zinatofautiana viwango..Ili kufahamu vizuri juu ya hilo fungua hapa >>> IMANI MAMA NI IPI?

Embu ngoja nikupe mfano wangu mdogo sana..naamini utakuongezea kitu..

Kuna wakati nilikuwa nimepanga jumba sehemu fulani, sasa ilikuwa kila mwisho wa mwezi, tunalipia bili ya maji sh. 7000, na  bili ya umeme sh.15,000. Na sehemu hiyo hao wanaokuja kuchukua bili hizo walikuwa ni wakali kweli, haziwezi pita siku mbili bila kuja kukugongea hodi..

ujue nguvu ya Imani..

Ilikuwa ni mwezi wa pili, wakati huo hali kwangu haikuwa nzuri sana, lakini nilimwambia Mungu nitakuamini wewe, na ni wewe ndiye utakayenipa hifadhi mimi na ndugu yangu..Hivyo ulipofika mwisho wa mwezi tulishangaa, wale hawakuja kutugongea wakati ilikuwa ni desturi yao, mpaka ukaanza mwezi mwingine wa tatu, lakini hatukuwaona..zikawa zinapita tu tarehe, bado tunashangaa hatuwaoni, wapangaji wengine walienda kulipia lakini sisi hatujafuatwa..Ikaendelea hivyo hivyo, hapo mfukoni hatuna kitu, mpaka ikafika tarehe 25,..kipindi hicho na gesi nayo ikaisha ndani, tukawa kama vile hatuna kitu na mwezi mwingine unakwenda kuishia bado tunayo madeni ya nyuma na hatuna pesa ya matumizi..

Lakini siku hiyo tulikuwa tumekaa, tukajikuta tunaangalia tu M-pesa, cha ajabu tukashangaa kule kulikuwa ni sh.50,000 na hiyo namba hatujawahi kuitumia kwa miamala yoyote ya kifedha, tukaenda kutoa ili tukanunue gesi sh. 20,000, lakini tulipomaliza tu kutoa , mara wale watu wa umeme, wanakuja kutugongea mlango, na kutuambia tuwalipe pesa ya umeme wa mwezi uliopita.. Ndipo tukatoa ile hela tukawapa saa ile ile, tukafiria kwamba kama  tusingewapa siku ile sijui hali ingekuwaje!.

Lakini tulimwamini Mungu, tukajua kweli nguvu ya Imani ni kubwa. Yapo na mambo mengine mengi Mungu aliyonitendea kwa kumwamini tu..

ijue Nguvu ya Imani.

Hiyo yote ni kutaka kukupa moyo na wewe, ukimwamini Mungu, basi anaweza kukufanyia mambo makubwa katika Maisha yako.

Mifano mingi sana ipo katika biblia, ambayo ukiisoma itaikuza Imani yako sana.. Na ndio maana tunaambiwa..

Warumi 10:17  “Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo”.

Hivyo unapoitafakari mifano mingi ya Imani katika Biblia ndivyo unavyoikuza Imani yako. Na ndio mpaka huko huko unajikuta unafanya mambo makubwa ya ki-imani yasiyoelezeka kibinadamu.

Lakini yote hayo ni mpaka uwe katika wokovu?

Je! Umeokoka?

Je! Unajua kuwa tunaishi katika siku za mwisho, na Yesu yupo karibuni kurudi? Na kwamba kanisa hili ndio kanisa la mwisho lijulikanalo kama Laodikia na kwamba hakutakuwa na kanisa lingine Zaidi ya hili? Unasubiri nini usimkaribishe Yesu maishani mwako akuokoe?

Fanya maamuzi upesi, kabla ya mlango wa neema haujafungwa.

Bwana akubariki.

ijue Nguvu ya imani ni kuu.

Mada Nyinginezo:

KIWANGO CHA TATU CHA IMANI.

ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.

IMANI NI KAMA MOTO.

NGUVU YA SADAKA.

UNYAKUO.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

NGUVU YA SADAKA.

Ijue nguvu ya sadaka.


Kuna nguvu ya kipekee  iliyo ndani ya sadaka ambayo watu wengi hawaifahamu.

Mungu anaweza kweli akawa ni Rafiki yako mkubwa sana, anaweza kweli akawa anazungumza na wewe, na ukaisikia sauti yake, ikikwambia nimekusikia mwanangu na nitakupa kitu Fulani..Lakini ukashangaa kitu hicho hujakipata japokuwa alikuahidia kabisa atakuwa na wewe..

Hiyo ni kutokana na kuwa ulichomwomba Mungu, hukukiambatanisha na sadaka..Leo hii nitakuonyesha mfano wa watu wa namna hiyo katika biblia ambao walimwomba Mungu sana Na Mungu akawasikia na kuwaahidia kuwa anatakuwa nao, lakini majibu yalikuja tofauti na walivyokitarajia mpaka walipogundua kuwa tatizo ni nini?….

Bwana atusaidie tuifahamu Nguvu ya Sadaka.

Hiyo ni Habari ya wana wa Israeli siku ile walipotaka kwenda kupigana na ndugu zao Benyamini kutokana na wao kuwa na tabia ya kuutamia uovu wa wazinifu, bila kuwashaadhibu. Hivyo vita vikapangwa dhiki yao na waisraeli wengine wote waliosalia, Sasa Israeli wote walimwomba Mungu aende nao ili wakawapige Benyamini, mara ya kwanza, Mungu akawajibu akawaambia nitakuwa Pamoja nanyi, nanyi mtashinda, Lakini walipokwenda walipigwa mapigo makubwa sana..

Wakamrudia Mungu wakamuuliza tena, Je utakwenda Pamoja nasi mara hii nyingine?, Mungu akawaambia ndio nitakuwa Pamoja nanyi, lakini walipoenda kapigwa, tena wakafa watu wengi kweli.

Wakamrudia tena Mungu kwa mara ya tatu, lakini safari hii hawakumrudia mikono mitupu, walimrudia kwa kufunga, na kwa sadaka nyingi sana, jambo ambalo hapo Mwanzo hawakulifanya..Kisha wakamuuliza Mungu tena Je! Utakwenda Pamoja na sisi, ndipo Mungu akawaambia, Hakika nitakwenda Pamoja na nyie..

Na kweli walipokwenda waliwapiga Wabenyamini wengi sana, wakatoka na ushindi mnono (Waamuzi 20:22-29)..Hapo ndipo walipojua nguvu ya sadaka ipo wapi!

Kwa marefu ya Habari hiyo na fundisho lake fungua  hapa usome. >>> UMUHIMU WA SADAKA.

Hata wewe, inawezekana unamtii Mungu sana, unajibidiisha sana katika kumwomba kwa bidii, lakini kwenye suala la kumtolea Mungu, hulizingatii sana, unaona kama halina umuhimu kwa mkristo, ni pengine kwasababu hukujua nguvu ya sadaka…

Ndugu Ijue nguvu ya sadaka..

Umekuwa ukimwomba Mungu akupe kitu Fulani, na muda mrefu umepita..Leo hii fahamu kanuni za kupokea kutoka kwa Mungu. Kumbuka Mungu hana shida na fedha zako..Kwasababu vyote ni mali yake, alishasema hivyo (Hagai 2:8) , lakini anataka kuona mtu anayemwomba anao moyo wa kujali..Hicho tu..

Pale unapomtolea kinono, ndipo unapougusa moyo wake Zaidi na kuona sababu ya kwanini wewe akujibu haraka kuliko yule mwingine asiyemjali?. Fedha unazomtolea Mungu, zinakwenda katika kuwabariki wengine pia rohoni,

Hivyo unapomwomba Mungu akupe, au akutendee jambo lolote, hakikisha kwa uwezo ulio nao, ambatanisha sadaka yako tena iliyo  NONO ya hicho unachomwombea… Usiombe tu Mungu nipe, gari, nipe nyumba, nipe hiki, nipe kile halafu huna mpango wa wewe pia kumtolea Mungu, nataka nikuambie, ukiwa na tabia hiyo  majibu yako yatakuwa ni ya kuchelewa sana.

Hivyo anza leo, kujifunza kuambatanisha sadaka ya kila unachomwomba Mungu, kwa jinsi Mungu alivyokujalia…

Ijue nguvu ya sadaka..

Na kumbuka pia sadaka hiyo haipaswi kupelekwa sehemu nyingine yoyote Zaidi ya madhabahuni pa Mungu.. Haipaswi kupelekwa kwa watoto yatima, au watu wasiojiweza, au kwa mtu mwingine yoyote hapana..Inapaswa ifikishwe madhabahuni pa Mung utu! yaani Kanisani kwako.

Hivyo zingatia vigezo hivyo, Na hakika utaona matokeo chanya, katika maombi yako.

Hiyo ndiyo nguvu ya sadaka.

Bwana akubariki.

Soma masomo mengine chini…

Mada Nyinginezo:

TUMTOLEE MUNGU VILE VINAVYOTUGHARIMU ZAIDI.

HALI ZETU JINSI ZINAVYOWEZA KUATHIRI UTOAJI WETU.

HISIA YA MUNGU ILIYO MBAYA KULIKO ZOTE.

FUKUZA TAI WOTE JUU YA SADAKA YAKO.

KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?

NGUVU YA MSAMAHA

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

WHAT WE BELIEVE.

CLOUD OF WITNESSES, (BRETHRENS)

We believe that Jesus Christ is the God manifested in human flesh for the purpose of man’s redemption, and he is the Alpha and Omega (Rev.22: 13).

Jesus Christ


We believe Brother William Branham is the messenger of God to our generation, sent as the Prophet of this generation and his ministry fulfills a prophecy given by the prophet Malachi.

Prophet William Branham

Malachi 4: 5-6 “Behold, I will send you Elijah the prophet before the coming of the great and dreadful day of the Lord: And he shall turn the heart of the fathers to the children, and the heart of the children to their fathers, lest I come and smite the earth with a curse”

William Branham fulfilled Malachi 4: 6b. And Brother Branham also fulfills John’s prophecy concerning the 7th Angel, on Revelation 3:14 & 10: 7

So with all our hearts, we firmly believe that He is the Messenger of the last church that we are living now (i.e Laodicean church), and there will be no other church after this, so there will be no other messenger after this one.

We do not believe that William Branham is God or Jesus. To do so is to cultivate idolatry, and to equate man with God, which is an abomination in his sight and blasphemy.

We believe in inner and outer holiness, and that, it is the duty of every Christian to live a holy life according to the Word of God as it is written in the Holy Bible.

We believe in zealously preaching the message of the last days, and baptizing people in the correct baptism, by immersion in the name of Jesus Christ according to (Acts 2:38, 8: 16,10: 48 and 19: 5).

We also believe that we are living in the last days, and Our Lord Jesus Christ will appear soon.


Other Topics:

EVERY ONE SHALL GIVE ACCOUNT OF HIMSELF

WHAT IS THE EVERLASTING GOSPEL?

Is it sin to charge interest (unsury)?

Is masturbation a sin?

Home:

Print this post

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

Fahamu jinsi ya kusoma biblia.


Awali ya yote ninakupongeza kwa nia yako kutamani kujua jinsi ya kusoma biblia. Hapo mwanzoni kabla sijamjua vizuri Mungu, kati ya  vitabu ambavyo nilikuwa ninaona ni vigumu kuvielewa, basi kimojawapo kilikuwa ni BIBLIA.

Lakini siku, na miaka ilivyozidi kwenda niligundua kuwa sio, nataka nikuambie hakuna kitabu kilicho kirahisi kama Biblia. Kwanini ninakuambia hivyo?.. Kwasababu ni kitabu kinachoweza kusomwa na watu wa makundi yote.  Mzee anaweza kukisoma, kijana anaweza kukisoma, asiye na elimu anaweza kukisoma mwenye PH.D anaweza kukisoma..Na wote wakafaidika na kilichoandikwa mule. Vilevile hakina ngazi yoyote ya awali kukipitia ndio uelewe kama vilivyo vitabu vingine. Leo hii ukihitaji kusoma kitabu cha Fizikia, itakugharimu kwanza upitie elimu za chini uwe na msingi, vinginevyo hutaweza kukielewa..Lakini biblia haina misingi hiyo.

Tena na cha kushangaza Zaidi ni kwamba, biblia imetoa nafasi ya kueleweka na watu wasio na elimu kuliko wenye hekima na ujuzi..(Luka 10:21)

Jinsi ya kusoma biblia.

Mambo ya kuzingatia kabla hujaanza kusoma biblia.

  • Kwanza: Omba Kabla hujaanza kusoma Habari yoyote, hata kama unaifahamu, mshirikishe kwanza Roho Mtakatifu, na mwombe msaada akusaidie kuyaelewa maandiko. Siri moja ya maandiko ni kuwa Habari ile ile inaweza ikawa na mafunuo mengi sana..Hivyo usipokuwa mnyenyekevu na kujiona kwamba Habari Fulani unaijua, nakuambia utabakia kuwa hivyo hivyo. Lakini ukimwomba kwanza Roho Mtakatifu akufunulie, maandiko basi utashangaa mambo mengi sana ambayo hukuwahi hata kuyafikiria.
  • Pili: Hakikisha upo katika utulivu wa kutosha. Mahali palipo na machafuko siku zote hata akili haiwezi kukaa katika utulivu wa kuzingatia kile kinachosomwa, na hivyo Roho Mtakatifu anakosa wigo wa kukufunulia, yale anayotaka kukufunulia. Hivyo kama upo kwenye makelele basi, subiri uwe katika utulivu, tenga muda wako, hususani usiku ni muda mzuri Zaidi.
  • Tatu: Tafakari Neno, Kumbuka Neno la Mungu halisomwi kama gazeti tu, Chukua muda mrefu kuyatafari maandiko Zaidi ya kuyasoma, ikiwa na maana mtu yule anayeitafakari sura moja vizuri, ni Zaidi na mtu yule atakayesoma kitabu kizima bila kutafakari chochote kilichoandikwa. Roho Mtakatifu anazungumza kwa kasi sana, pale mtu anapojibiisha kuitafakari Habari husika.
  • Nne: Endelea kutumia muda mwingi, katika kutafakari hilo Neno, kwa jinsi unavyokaa sana katika uwepo huo ndivyo unavyompa Roho Mtakatifu wigo wa kukufunulia maandiko katika uelewa mzuri zaidi. Mpaka dakika ya mwisho unamaliza, unatoka kitu ambacho hapo kabla hukuwahi kukijua, tena moyo wako ukiwa na amani ya kutosha.
  • Tano: Kuwa na daftari na kalamu. Hiyo itakusaidia kuandika kile Mungu anachokufundisha, kwa kumbukumbu la baada usije ukasahau, Kumbuka mwanafunzi mzuri ni yule anaandika chini kile mwalimu wake anachomfundisha, kila anapomfundisha. Hivyo na wewe hakikisha unakuwa na daftari lako.

Hivyo ukizingatia hizo hatua, utakuwa umeshajua jinsi ya kusoma biblia. Pia kumbuka, kwenye suala la kitabu kipi uanzane nacho, au kipi usianzane nacho, hilo halina umuhimu sana, unaweza kuanza na kitabu chochote kile na  huko huko Roho Mtakatifu mwenyewe atakufunulia mambo ya ajabu, Na kukufikisha pale anapotaka ufike kwa siku hiyo, kwasababu hiyo ndio kazi yake aliikusudia juu yetu.

Yohana 16:13  “Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake”.

Jinsi ya kusoma biblia.

Pia Kujifunza biblia ni Pamoja na kusikiliza na mafundisho mengine ya Neno la Mungu yanayohubiriwa.. Yale yanakuwa kama TUTION kwako. Hivyo hapa pia yapo mafundisho mengi ya kukusaidia kuielewa biblia, kwenye website hii yapo mafundisho Zaidi ya 1000 ya mada mbalimbali, na Maswali na Majibu mengi sana, ambayo ukiyasoma naamini utapiga hatua kubwa sana katika kuielewa biblia..Hivyo kama upo tayari bofya hapa uende moja kwa moja katika orodha hiyo….>> MAFUNDISHO

                                                                                >> MASWALI NA MAJIBU

Bwana akubariki sana.

Jinsi ya kusoma biblia.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au tutumie ujumbe kwa namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Mihimili mikuu (4) ya mkristo katika safari yake ya wokovu.

USIPOLITENDEA KAZI NENO LA MUNGU.

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.

NENO LA MUNGU NI DAWA ILIYO TOFAUTI NA DAWA NYINGINE.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

KABLA YA MAANGAMIZI, KRISTO HUWA ANAONYESHA KWANZA NJIA YA KUTOROKEA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

UTAFIKA WAKATI WA WEWE KUACHWA NYIKANI.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia leo tena.

Vipo vipindi tofauti tofauti ambavyo kila mkristo atavipitia…maana biblia inasema katika..

Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa; ….

4 Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza”.

Hata uwe unampendeza Mungu kiasi gani/ hata uwe mkamilifu mbele za Mungu kiasi gani..ni lazima utapitia vipindi vya kulia tu katika Maisha yako!..ni kweli asilimia kubwa ya Maisha yako itatawaliwa na furaha na amani..lakini ni lazima utapitia tu vipindi tofauti tofauti vya kulia na vya huzuni.

Sasa katika Imani pia vipo vipindi ambavyo utamwona Mungu sanaaa..na vipindi ambavyo hutamwona (utaona kuna ukimya Fulani maishani mwako)!…Sio kwamba atakuwa amekuacha kabisa! Au hakufuatilii wala kukusaidia…Hapana atakuwa yupo anakuona na kukujua lakini atakuwa kama amejiepusha na wewe”. Bwana Yesu kuna kipindi alisema “Mungu wangu, Mungu wangu mbona umeniacha”…hivyo huo wakati wa kuachwa upo!…Wengi hawalijui hili, ndio maana wanapopitia kipindi Fulani cha Maisha wanarudi nyuma na kuuacha wokovu…

Sasa leo tutajifunza hicho kipindi ni kipi lakini kabla ya kuendelea mbele zaidi hebu usome mfano huu taratibu sana, kisha tutaendelea…

Luka 15:3  “Akawaambia mfano huu, akisema, 

4  Ni nani kwenu, mwenye kondoo mia, akipotewa na mmojawapo, asiyewaacha wale tisini na kenda NYIKANI, aende akamtafute yule aliyepotea hata amwone? 

5  Naye akiisha kumwona, HUMWEKA MABEGANI PAKE AKIFURAHI. 

6  Na afikapo nyumbani kwake, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimekwisha kumpata kondoo wangu aliyepotea. 

7  Nawaambia, Vivyo hivyo kutakuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu”.

Mfano huo unaonyesha ni jinsi gani..Bwana anaweza akawaacha kondoo 99 nyikani na kwenda kumtafuta kondoo mmoja aliyepotea. Umewahi kujiuliza kwanini awaache wale kondoo 99, na kwanini asiende nao?..na kwanini awaache NYIKANI na si kwenye zizi, mahali palipo salama?…

Maana yake ni kwamba anawaacha peke yao sehemu ya wazi isiyo na uzio, ambayo inaonekana ni sehemu hatari, lakini ni salama….Sehemu ambayo Wanyama wakali wanapita, sehemu ambayo inaogopesha!…na mbaya zaidi wanaachwa peke yao…Na lengo la Bwana kuwaacha ni ili akatafute kondoo wengine..

Sasa hao kondoo walioachwa nyikani pengine ni wewe unayepitia ukame sasa, humwoni Bwana kama ulivyomwona wakati umeokoka. Sasa ufanye nini katika hiyo nyika yenye utata?

Kumbuka hapo ni nyikani, mahali pasipo na uzio.. hivyo sio wakati wa kuzunguka zunguka huko na kule…kaa hapo hapo ulipo ndio mahali salama!…hapo hapo mahali Bwana alipokuacha!..(maana yake ni kwamba anaelewa kabisa mahali alipokuacha  utakuwa salama mpaka atakaporudi) tulia hapo hapo hata kama ukitazama kushoto humwoni Bwana, ukitazama kulia umwoni Bwana kama ilivyokuwa hapo kwanza…wewe tambua kuwa hapo ulipo upo sehemu salama..lishike Neno lake lile lile na Imani!…

Haupo ndani ya uzio, ikiwa na maana kuwa  vishawishi vya kukuvuta utoke kwenye mstari wa wokovu, utaviona, usianze kuzurula…wala kuhama hama…tulia hapo hapo….Hali kadhalika pembeni unaweza kuona dalili ya kudhurika na wanyama wanaopita kule, na unaweza kuona kama vile hakuna ulinzi, usiogope! Kaa hapo hapo ndio sehemu salama (aliyekuacha hapo sio mjinga)….Hivyo tumia muda wako kujifunza Neno na kuwaimarisha wengine na kuwalinda wasitoke kwenye hifadhi ya Mungu..kwa kuwafundisha wokovu na kuwafariji mpaka wakati wa Bwana kurudi.

Kumbuka tena kuna wakati Fulani Kristo alikuweka mabegani alipokupata…lakini si wakati wote utakuwa mabegani mwake…wakati ukiwa mabegani mwake ulikuwa unamwona kwenye ndoto kila siku, ulikuwa unauhisi uwepo wake kila mahali, ulipomwomba kitu ulikipata papo kwa hapo…(wakati huo ulikuwa mabegani mwake, mbingu ilifurahia kukupata) lakini hautakuwa hivyo siku zote…utafika wakati utashushwa mabegani na wewe utakwenda kuungana na wenzako nyikani na Bwana atakwenda kutafuta kondoo wengine waliopotea.

Kama ni leo umempa Kristo Maisha yako, basi uwe tayari kwa hicho kipindi kuja mbele yako. Jifunze kumwelewa sana Bwana wakati huu wa sasa, ambao unamwona sana… kwasababu wakati wa ukame utafika!..kama hutamwelewa sana wakati huu, wakati wa kuachwa nyikani utaikimbia na kuiacha nyika.

Na hapo ndipo watu wengi walipopotelea. Imani ni ya kuilinda sana.

Bwana atubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MAJARIBU MATATU YA YESU KRISTO

MASHAHIDI 40 WALIOUAWA MJINI SEBASTE, NI UJUMBE KWETU.

IKIMBIE DHAMBI KWA GHARAMA ZOZOTE ZILE!

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

UNYAKUO.

JUMA LA 70 LA DANIELI

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MHUBIRI.

Kitabu cha mhubiri kiliandikwa na mfalme Sulemani.

Kitabu hichi kinaeleza, jumla ya mambo yote, na mwisho kinatoa ushauri ni nini mwanadamu anapaswa achague.

Ikiwa wewe ni mmojawapo wa  wanaojiuliza nini maana ya maisha, ni nini ufanye ili upate mwisho mwema mwenye mafanikio, basi nakushauri ukipitie kitabu hichi cha mhubiri kwa utulivu, Kwasababu Mungu alikiandika mahususi kwa ajili ya watu wenye maswali kama ya kwako.

Kwa ufupi (Mhubiri)Sulemani anajaribu kueleza jinsi alivyoanza safari yake yake ya kutafuta kitu kitakachompa raha maishani, kitu kitakachotatua matatizo yake moja kwa moja, Hivyo akaanza kujaribu kufanya kwa bidii jambo moja hadi  lingine ili aone kama linaweza kumletea jawabu la maisha yake.,

  • Alijaribu kufanya biashara nyingi sana kuliko watu wote waliomtangulia duniani lakini hakupata kile alichokuwa anakitafuta..
  • Alijaribu starehe na anasa zote unaozijua wewe, lakini katika hivyo vyote bado hakupata jumla ya maisha.(Mhubiri 2:1)
  • Akajaribu kwa kujijengea makasri ya kifahari lakini bado hakuipata hiyo jumla ya maisha (Mhubiri 2:4)
  • Alijiongezea elimu kuliko watu wote ulimwenguni, alikuwa na elimu juu ya miti yote, na karibu viumbe vyote duniani lakini katika elimu yake, na hekima yake bado hakupata jumla ya mambo yote.(Mhubiri 1:13)

Mpaka mwisho wa siku akakata tamaa, akaona kila kitu ni sawa na ubatili tu, na kujilisha (kufuata) Upepo. Japokuwa alijusumbua kupata kila kitu roho yake inapenda,  lakini bado kile alichokuwa anakitazamia hakukipata.

Na ndipo mwisho wa siku  akagundua jumla ya mambo yote ambayo  mwanadamu anapaswa kuyafanya chini ya jua nayo si nyingine zaidi ya KUMCHA BWANA, NA KUZISHIKA AMRI ZAKE.

Hivyo mimi na wewe hatupaswi, kuanza tena, kufanya utafiti, wa kitu kitakachotupa jawabu la maisha duniani,..Sulemani alishatusaidia, ukisema leo hii wewe mwenyewe ngoja uanze, kwa akili zako na nguvu zako, kutafuta maana ya maisha, nakawambia utazunguka kote na utarudi pale pale Sulemani alipoishia. Na wakati huo utakuwa umeshachelewa.

Unasema, ngoja nitafute elimu sana, hiyo ndio itanipa raha, Mungu hawezi kunipa raha,..Ni kweli utaisumbukia na kuipata, na kufanikiwa lakini mwisho wa siku utakuja kugundua mbona bado kuna shimo ndani yako? Ile raha ambayo uliitazamia mbona hujaipata?

Unasema, ngoja nitafute mali, nijiwekee miradi, mingi, kwasababu hiyo itanipa raha.. Nataka nikuambie yupo aliyefanya kazi kubwa zaidi yako aliyeitwa Mhubiri Sulemani, lakini hilo mwisho wa siku halikumpa jawabu alilokuwa analitarajia.

Vivyo hivyo na wewe kama unataraji utapata raha, sehemu yoyote, aidha kwa waganga, au kwa wanadamu, na huku umemwacha Mungu nyuma, ukweli ni kwamba mwisho wa siku utakuja kugundua uliacha kitu cha thamani sana nyuma yako.

Sasa mwishoni kabisa mwa kitabu hicho cha mhubiri, maneno hayo ya Mhubiri Sulemani ndio tunayapata,

Anasema..

Mhubiri 12:13 “Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; MCHE MUNGU, NAWE UZISHIKE AMRI ZAKE, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.

14 Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya”.

Unaona, anasema, mche Bwana, uzishike amri zake. Hivyo ikiwa bado angali unao muda ndugu yangu, mimi na wewe tumtafute Mungu, kwasababu huyo ndio atakayetupa furaha yote ya maisha yetu..

Na ndio maana mhubiri juu kidogo  alisema..

Mhubiri 12:1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo 2 Kabla jua, na nuru, na mwezi, Na nyota, havijatiwa giza; Kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua;

3 Siku ile walinzi wa nyumba watakapotetema; Hapo wenye nguvu watakapojiinamisha; Na wasagao kukoma kwa kuwa ni haba; Na hao wachunguliao madirishani kutiwa giza;

4 Na milango kufungwa katika njia kuu; Sauti ya kinu itakapokuwa ni ndogo; Na mtu kusituka kwa sauti ya ndege; Nao binti za kuimba watapunguzwa;

5 Naam, wataogopa kilichoinuka Na vitisho vitakuwapo njiani; Na mlozi utachanua maua; Na panzi atakuwa ni mzigo mzito; Na pilipili hoho itapasuka; Maana mtu aiendea nyumba yake ya milele, Nao waombolezao wazunguka njiani.

6 Kabla haijakatika kamba ya fedha; Au kuvunjwa bakuli la dhahabu; Au mtungi kuvunjika kisimani; Au gurudumu kuvunjika birikani;

7 Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.

8 Mhubiri asema, Ubatili mtupu; mambo yote ni ubatili!”.

Ubarikiwe.

Kwa ziada ya masomo kuhusu kitabu cha Mhubiri, Fungua masomo haya;

ZIKUMBUKE SIKU ZIJAZO ZA GIZA, KWA MAANA ZITAKUWA NYINGI.

FANYA MAAMUZI KABLA HAZIJAKARIBIA SIKU ZA HATARI.

HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

UBATILI.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

habari za ziada.

Rudi Nyumbani:

Print this post