(1Samweli 23:1-14)
Keila ni moja ya miji midogo iliyokuwa Israeli, lakini kuna wakati ulipitia taabu kubwa sana ya kuvamiwa na wafilisti, wakateswa wakaibiwa nafaka zao, hivyo wakiwa katika mahangaiko hayo, na mateso hakuna wa kuwasaidia, Maandiko yanatuonesha akatokea Daudi katika maficho yake, alipokuwa anamkimbia Sauli..Akapita katikati ya mji huo,akasikia, kuwa wafilisti wapo huko wanawatesa watu wa Keila.
Lakini Daudi aliguswa sana moyo, hakujali Maisha yake na kuendelea na safari yake ya mafichoni bali alichokifanya ni kukiita kikosi chake kidogo, na kukiambia adhima yake ya kuwasaidia, japokuwa watu wake walikuwa wachache, walijitia nguvu, ndipo Daudi akaenda kumuuliza Mungu, kama akiwapigania watu wa Keila atashinda au hatashinda, Mungu akamwambia, hakika atashinda, akauliza tena na mara nyingine Mungu akamjibu hivyo hivyo kuwa watashinda.
Tengeneza picha, wenyeji wa mtu huyo wanasikia, Shujaa Daudi amekuja kuwasaidia, walifurahi kiasi gani, Na ndivyo ilivyokuwa Daudi akaenda kuwapigania watu hao, akashinda na kurejesha mateka yote, tena na Zaidi akawarejeshea.
Wanawake, wazee, vijana wa Keila wakahuika mioyo yao, wakafurahia kuona ng’ombe zao, ngano zao, watumwa wao, mali zao zimerudi.. Waliruka ruka na kucheza, na kumpenda sana Daudi.
Lakini habari mbaya ziliwafikia kwa ghafla watu wa Keila, biblia inasema, Sauli aliyekuwa anamwinda Daudi alipata taarifa kuwa adui yake amefika Keila, kuwasaidia watu wale. Hivyo, akatuma vikosi vyake, kwenda kumkamata. Lakini safari hii sio tena kumtafuta, bali kwenda kuwafuata wakuu wa mji huo, na kuwaambia wamkamate Daudi wamfikishe kwa Sauli ili amuue.
Lakini kabla Sauli hajatuma vikosi vyake, Daudi naye akapata taarifa kuwa Sauli amejua yupo kule, hivyo alichokifanya ni kwenda kumuuliza Mungu kama ilivyokawaida yake, kuhusiana na jambo hilo kama kweli watu wa Keila watamtoa na kumpa Sauli au La..
Matarajio ya Daudi yalikuwa ni hapana, akiamini kuwa wale watu aliowaokoa kwa mkono mkuu, watampa hifadhi watamficha, hawawezi kumsaliti, Lakini Bwana akamwambia Daudi kuwa, hao watu watakutoa kwa Sauli. Hapo Daudi akawa hana jinsi Zaidi ya kuingia tena maporini kwenda kutafuta mahali pa kujificha.
1Samweli 23:7 “Kisha Sauli aliambiwa ya kwamba Daudi amefika Keila. Sauli akasema, Mungu amemtia mkononi mwangu; kwa maana amefungwa ndani, kwa vile alivyoingia katika mji wenye malango na makomeo. 8 Basi Sauli akawaita watu wote waende vitani, ili waishukie Keila, na kumhusuru Daudi na watu wake. 9 Naye Daudi alifahamu ya kuwa Sauli amemkusudia mabaya; akamwambia Abiathari, kuhani, Lete hapa hiyo naivera. 10 Ndipo Daudi akasema, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mimi mtumwa wako nimesikia hakika ya kuwa Sauli anataka kuja huku Keila, ili kuuharibu mji kwa ajili yangu. 11 Je! Watu wa Keila watanitoa, nitiwe mkononi mwake? Je! Sauli atashuka, kama mtumwa wako alivyosikia? Ee Bwana, Mungu wa Israeli, nakusihi, umwambie mtumwa wako. Naye Bwana akamjibu, Atashuka. 12 Ndipo Daudi akasema, Je! Watu wa Keila watanitia mimi na watu wangu mkononi mwake Sauli? Bwana akasema, Watakutia. 13 Basi Daudi na watu wake, ambao wapata kama mia sita, wakaondoka na kutoka Keila, wakaenda po pote walipoweza kwenda. Kisha Sauli akaambiwa ya kwamba Daudi amekimbia toka Keila; akaacha kutoka nje. 14 Basi Daudi alikuwa akikaa nyikani ngomeni, akakaa katika nchi ya milima milima kwenye nyika ya Zifu. Naye Sauli alikuwa akimtafuta kila siku, lakini Mungu hakumtia mikononi mwake.”
1Samweli 23:7 “Kisha Sauli aliambiwa ya kwamba Daudi amefika Keila. Sauli akasema, Mungu amemtia mkononi mwangu; kwa maana amefungwa ndani, kwa vile alivyoingia katika mji wenye malango na makomeo.
8 Basi Sauli akawaita watu wote waende vitani, ili waishukie Keila, na kumhusuru Daudi na watu wake. 9 Naye Daudi alifahamu ya kuwa Sauli amemkusudia mabaya; akamwambia Abiathari, kuhani, Lete hapa hiyo naivera.
10 Ndipo Daudi akasema, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mimi mtumwa wako nimesikia hakika ya kuwa Sauli anataka kuja huku Keila, ili kuuharibu mji kwa ajili yangu.
11 Je! Watu wa Keila watanitoa, nitiwe mkononi mwake? Je! Sauli atashuka, kama mtumwa wako alivyosikia? Ee Bwana, Mungu wa Israeli, nakusihi, umwambie mtumwa wako. Naye Bwana akamjibu, Atashuka.
12 Ndipo Daudi akasema, Je! Watu wa Keila watanitia mimi na watu wangu mkononi mwake Sauli? Bwana akasema, Watakutia.
13 Basi Daudi na watu wake, ambao wapata kama mia sita, wakaondoka na kutoka Keila, wakaenda po pote walipoweza kwenda. Kisha Sauli akaambiwa ya kwamba Daudi amekimbia toka Keila; akaacha kutoka nje.
14 Basi Daudi alikuwa akikaa nyikani ngomeni, akakaa katika nchi ya milima milima kwenye nyika ya Zifu. Naye Sauli alikuwa akimtafuta kila siku, lakini Mungu hakumtia mikononi mwake.”
Maana yake ni nini habari hii?
Wenyeji waliona ni heri mmoja wao aangamie lakini mji wote upone mikononi mwa jeshi la Sauli. Hawakujali msaada mkubwa aliowapatia, wakamwogopa mtu ambaye hakuwajali hata kidogo walipokuwa katika mateso yao. Mfano Dhahiri wa watu wa kipindi kile cha Bwana Yesu..
Hawakujali miujiza waliyotendewa, hawakujali wafu waliofufuliwa, pepo waliotolewa, vipofu walioona, habari njema za faraja zilizohubiriwa na Yesu, Watoto wao walioponywa. Lakini Waliposikia tu kuna hatari ya Herode kuja kuwaangamiza.. Wakasema ni heri Mmoja afe ili taifa zima lisiangamie.
Yohana 11:47 “Basi wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakakusanya baraza, wakasema, Tunafanya nini? Maana mtu huyu afanya ishara nyingi. 48 Tukimwacha hivi, watu wote watamwamini; na Warumi watakuja, watatuondolea mahali petu na taifa letu. 49 Mtu mmoja miongoni mwao, Kayafa, aliyekuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, akawaambia, Ninyi hamjui neno lo lote; 50 wala hamfikiri ya kwamba yafaa mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, wala lisiangamie taifa zima”
Yohana 11:47 “Basi wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakakusanya baraza, wakasema, Tunafanya nini? Maana mtu huyu afanya ishara nyingi.
48 Tukimwacha hivi, watu wote watamwamini; na Warumi watakuja, watatuondolea mahali petu na taifa letu.
49 Mtu mmoja miongoni mwao, Kayafa, aliyekuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, akawaambia, Ninyi hamjui neno lo lote;
50 wala hamfikiri ya kwamba yafaa mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, wala lisiangamie taifa zima”
Wakamsulibisha mwokozi wao.. Hata Sasa hatushangai kuona, watu wakimfurahia Kristo anapowasaidia tu nyakati za mateso yao, anapowabariki, anapowalinda, anapowaponya.. Lakini ikija tu tufani ndogo ya ibilisi kwa ajili ya Kristo, tayari wanamsaliti, wanautupilia mbali wokovu, akiambiwa anafukuzwa kazi kisa Yesu wake, anasahau, mema yote aliyofanyiwa na Bwana siku zote za Maisha yake. Anamwacha. Akiona umri umeenda haolewi, anasema huku kuvaa magauni ya nini tena, ngoja nivae vimini nitembee nusu uchi, ili nipate mchumba.
Tusiwe kama watu Keila, ambao walimsaliti shujaa wao kisa mtu asiyewajali, tusimwache Yesu kisa vitisho vya shetani vidogo vinavyopita mbeleni yetu. Kisa wazazi hawapendezwi na Imani yetu. Tukumbuke yeye ndio jemedari wetu, kama alitupigania vipindi vya nyuma atatupigania hata sasa.
Tumpende Bwana Mungu wetu kwa mioyo yetu yote, kwa nguvu zetu zote, kwa roho zetu zote, na kwa akili zetu zote.
Bwana atusaidie.
Shalom.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
KWANINI DAUDI ALIKUWA NI MTU ALIYEUPENDEZA MOYO WA MUNGU?
Naivera ni nini? Kwanini Daudi aliihitaji alipomtafuta Mungu?
Je! aliyemwua Goliathi ni Daudi au Elhanani.
WALA HAKUSIMAMA MTU PAMOJA NAYE, YUSUFU ALIPOJITAMBULISHA KWA NDUGUZE
UKIOKOKA, JIANDAE KUPITISHWA USIPOPATAZAMIA.
Je tunaruhusiwa kushirikiana na wasanii wa kidunia katika kumwimbia Mungu?
Rudi nyumbani
Print this post
Haya ni Mafundisho maalumu kwa ajili ya wanawake..
JIBU: Ni vema kujua mfungo ni nini na madhumuni yake ni yapi.
Mfungo ni kitendo cha kujizuia kufanya jambo fulani la lazima kwa kipindi fulani kwa lengo la kumkaribia Mungu zaidi..
Kwamfano mfungo hasaa hulenga kujizuia kula au kunywa , wengine huzuia usingizi, wengine kazi, wengine mawasiliano n.k. inategemea unalenga nini.
Hivyo pale unapojizuia kula au kunywa lengo lako ni upate utulivu wa kuwa karibu zaidi na Mungu katika maombi na kumtafakari.
Kwahiyo kwa jinsi unavyojiweka mbali zaidi na masuala ya mwili ndivyo unavyoupa zaidi mfungo wako nguvu.
Hivyo tukirudi katika swali je tunaruhisiwa kushiriki tendo la ndoa tuwapo katika mfungo?
Jibu ni kuwa hakuna katazo lolote..kwasababu shabaha ya mfungo wako lilikuwa katika kujizuia kula au kunywa..
Lakini ikiwa utapenda kuzuia pia tendo la ndoa, ni vizuri lakini hapo ni jambo la makubaliano na mwenzi wako, ikiwa ataliridhia kwa wakati huo msafanye tendo la ndoa, ili mwelekeze fikra zenu zote kwa Bwana…hapana shida. Ni vema.
Lakini ikiwa mmoja wenu hajaridhia, hapo hupaswi kuzuia, kwasababu uolewapo au uoapo, huna amri juu ya mwili wako, isipokuwa mwenzako, kwahiyo akikataa hupaswi kupinga.Ni lazima ufanye.
Biblia inasema..
1 Wakorintho 7:3-5
[3]Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.
[4]Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe.
[5]Msinyimane isipokuwa MMEPATANA kwa muda, ili mpate faragha kwa kusali; mkajiane tena, Shetani asije akawajaribu kwa kutokuwa na kiasi kwenu.
Vilevile ikiwa nyote hamjaridhia…pia bado hakuharibu mfungo wenu.
Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa kushiriki tendo la ndoa, ndani ya mfungo, hakubatilishi mfungo wa mtu. Isipokuwa tu maandiko yanatuelekeza iwe ni kwa kiasi ili mpate na muda wa kusali
Bwana akubariki.
Je unaruhusiwa kufanya tendo la ndoa ukiwa katika mfungo?
JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?
MASWALI NA MAJIBU: YAHUSUYO NDOA- Sehemu ya 2.
Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?
SIKU ZA MWISHO ZA UHAI WANGU.
Tunajua kuwa vya Kaisari tunavyopaswa tumpe ni “kodi” lakini je! Na Vya Mungu ambavyo tunapaswa tumpe ni vipi kulingana na Luka 20:25?
Tuanze kusoma mstari wa 21 ili tuelewe vizuri zaidi..
Luka 20:21 “Wakamwuliza, wakisema, Mwalimu, twajua ya kwamba wasema na kufundisha yaliyo ya haki, wala hujali cheo cha mtu, bali unafundisha njia ya Mungu kwa kweli 22 Je! Ni halali tumpe Kaisari kodi, au sivyo? 23 Lakini yeye alitambua hila yao, akawaambia, 24 Nionyesheni dinari. INA SURA NA ANWANI YA NANI? Wakamjibu, Ya Kaisari. 25 Akawaambia, Basi, vya Kaisari mpeni Kaisari, NA VYA MUNGU MPENI MUNGU. 26 Wala hawakuweza kumshitaki kwa maneno yake mbele ya watu; wakastaajabia majibu yake, wakanyamaa”.
Luka 20:21 “Wakamwuliza, wakisema, Mwalimu, twajua ya kwamba wasema na kufundisha yaliyo ya haki, wala hujali cheo cha mtu, bali unafundisha njia ya Mungu kwa kweli
22 Je! Ni halali tumpe Kaisari kodi, au sivyo?
23 Lakini yeye alitambua hila yao, akawaambia,
24 Nionyesheni dinari. INA SURA NA ANWANI YA NANI? Wakamjibu, Ya Kaisari.
25 Akawaambia, Basi, vya Kaisari mpeni Kaisari, NA VYA MUNGU MPENI MUNGU.
26 Wala hawakuweza kumshitaki kwa maneno yake mbele ya watu; wakastaajabia majibu yake, wakanyamaa”.
Nataka tujifunze ni vigezo gani Bwana Yesu alitumia hapo kuhalalisha kuwa Kodi ni haki ya Kaisari, hiyo itatusaidia na sisi kujua vilivyo vya Mungu ni vipi?.. Na tunaona hakutumia kitu kingine chochote isipokuwa ile “Sura” inayoonekana kwenye ile sarafu pamoja na ‘Anwani” inayosomeka pale. Kwani Dinari ile ilikuwa na sura ya Kaisari na Anwani ya Kaisari, hivyo ni haki kuwa mali ya Kaisari.
Sasa kama vya Kaisari vilitambulika kwa sura iliyokuwa inaonekana juu ya Sarafu, ni wazi kuwa na vya Mungu vitatambulika kwa njia hiyo hiyo, Maana yake chochote chenye Sura ya Mungu hicho ni cha Mungu, na anapaswa apewe.. Sasa hebu tusome maandiko yafuatayo..
Mwanzo 1:27 “Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba”.
Umeona?..Kumbe! sisi tumeumbwa kwa Mfano wa Mungu, Nyuso zetu ni nyuso za Mungu, na kama tumeumbwa kwa mfano na Sura ya Mungu basi ni wazi kuwa sisi (yaani miili yetu na roho zetu) ni mali ya Mungu na si yetu! na hivyo ni LAZIMA TUMPE MUNGU VILIVYO VYAKE…Biblia inasema hivyo kuwa sisi si mali yetu wenyewe..
1Wakorintho 6:19 Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? WALA NINYI SI MALI YENU WENYEWE”
Na tena inasema Miili yetu ni MALI INAPASWA ITOLEWE KWA BWANA..
1Wakorintho 6:13 “Vyakula ni kwa tumbo, na tumbo ni kwa vyakula; lakini Mungu atavitowesha vyote viwili, tumbo na vyakula. LAKINI MWILI SI KWA ZINAA, BALI NI KWA BWANA, naye Bwana ni kwa mwili”
Hiyo ikiwa na maana kuwa ni lazima tuitoe miili yetu kwa Bwana, ni lazima tumpe MUNGU vilivyo vyake, Tusipofanya hivyo tutakuwa tunafanya makosa makubwa sana..
Sasa tunampaje Mungu vilivyo vyake?
1.KWA KUOKOKA!
Kuokoka maana yake ni kumkabidhi Bwana roho zetu, kwa kutubu dhambi na kubatizwa kwa maji na kwa Roho.(Marko 16:16). Unapomwamini Bwana Yesu na kumkabidhi maisha yako, hapo umempa Mungu vilivyo vyake, na hivyo utakuwa umeyafanya mapenzi ya Mungu.. kwasababu Utu wako wa ndani umeumbwa kwa mfano wake.
2. KWA KUJITENGA NA DHAMBI.
1Wakorintho 6:13 “…LAKINI MWILI SI KWA ZINAA, BALI NI KWA BWANA, naye Bwana ni kwa mwili” Hapa maandiko yanaonesha dhahiri kuwa “mwili si kwa zinaa bali kwa Bwana ” maana yake mtu anayefanya zinaa inaiharibu mali ya Mungu, ambayo ni mwili wake.. Kwasababu mwili wake umeumbwa kwa mfano wa MUNGU, una anwani ya Mungu!!..
Hivyo si ruhusa kuuharibu kwa zinaa, au kwa pombe, au kwa sigara, au kwa kuuandika tattoo au kwa kuuvisha jinsi mtu atakavyo (nguo za kubana au zisizo za maadili) au kwa mambo mengine yote yanayofanana na hayo..
Hivyo kwa hitimisho ni kwamba.. Vya Mungu anavyopaswa apewe ni ROHO ZETU, na MIILI YETU. Kwasababu vitu hivyo vina sura na anwani ya Mungu mwenyewe, kama vile dinari iliyokuwa na sura na anwani ya Kaisari.
Nini maana ya tumeumbwa kwa mfano na sura ya Mungu?
Tofauti kati ya mtu na mwanadamu ni ipi?
Naomba kufahamu maana ya “sura ya kijiti” katika Marko 12:26.
Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?
Nuru yetu inapaswa iangaze au isiangaze kulingana na Mathayo 5:16 na Mathayo 6:1?
Mwanzo 45:1 “Hapo Yusufu hakuweza kujizuia mbele yao wote waliosimama karibu naye. Akapiga kelele, na kusema, Mwondoeni kila mtu mbele yangu. Wala hakusimama mtu pamoja naye, Yusufu alipojitambulisha kwa nduguze. 2 Akapaza sauti yake akalia, nao Wamisri wakasikia. Watu wa nyumba ya Farao nao wakasikia. 3 Yusufu akawaambia ndugu zake, Mimi ndimi Yusufu; baba yangu angali hai bado? Wala ndugu zake hawakuweza kumjibu, maana waliingiwa na hofu mbele yake”.
Nakusalimu katika jina kuu sana la mwokozi wetu Yesu Kristo.
Yusufu baada ya kuuzwa na ndugu zake kwa watu wa mataifa, akidhaniwa kuwa ndio habari yake imeishia pale, lakini kama tunavyoifahamu habari, mambo yalikuwa ni kinyume chake, badala ya kuwa mtumwa akawa msaada na nguzo kubwa sana sio kwa wa-Misri peke yao bali pia kwa dunia nzima.
Lakini nachotaka tuone leo, ni ile siku alipojitambulisha kwa ndugu zake, ambao hawakumtambua siku zote ijapokuwa alikuwa ni ndugu yao kabisa wa damu, utaona siku hiyo Yusufu hakujidhihirisha mbele ya kila mtu tu ilimradi, hakujidhihirisha mbele ya watu wake Misri waliompokea, bali aliwaondoa kwanza wote, akabaki yeye kama yeye pamoja na wale ndugu zake 11 tu.
Ulishawahi kujiuliza ni kwanini iwe vile? Kwani kuna ubaya gani yeye kujifunua mbele ya kila mtu?..Kulikuwa hakuna ubaya wowote, lakini upo ufunuo mkubwa sana nyuma yake, kuhusiana na mpango wa wokovu wa Mungu.
Kibiblia habari ya Yusufu ni picha halisi ya Bwana wetu Yesu Kristo. Yeye alipokuja duniani kama mfalme, biblia inasema watu wake (Wayahudi), hawakumkubali, bali kinyume chake ndio wakamuua, ili tu asiwe mfalme wao.
Yohana 1:11 “Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea”
Lakini neema walioikataa ilipohubiriwa kwetu sisi (watu wa mataifa), tuliipokea kwa shangwe, na ndio maana tunaona mpaka sasa Bwana Yesu ndio msingi na ngome ya mataifa yote ulimwenguni. Lakini cha ajabu ni kwamba Yesu ambaye alitoka kwa wayahudi, mpaka sasa hawamtambui, ijapokuwa miaka 2000, inakaribia kuisha.. Bado hawaoni kuwa huyu Yesu ndiye tegemeo la dunia yote, wala hakutakuwa na masihi mwingine atakayekuja kuwaokoa zaidi ya huyo. Hilo hawalioni, ukienda kumuhubiria sasa Rabi wa kiyahudi habari za Yesu, anakuona kama wewe ni kafiri.
Lakini maandiko yanatabiri kuwa, wakati wao wa kurudiwa tena utafika, na Yesu atajitambulisha kwao kwa mara nyingine, macho ya mioyo yao yatatiwa Nuru, wakati huo, wayahudi wote, watalia na kuomboleza kwa maombolezo makuu pale Israeli, watalia sana ni kwanini walimsulibisha Bwana wao na mfalme wao, waliyekuwa wanamsubiria..
Zekaria 12:10 “Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimchoma; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza. 11 Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika bonde la Megido. 12 Nayo nchi itaomboleza, kila jamaa peke yake; jamaa ya nyumba ya Daudi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Nathani peke yao, na wake zao peke yao; 13 jamaa ya nyumba ya Lawi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Shimei peke yao, na wake zao peke yao. 14 Jamaa zote zilizosalia, kila jamaa peke yake, na wake zao peke yao”.
Zekaria 12:10 “Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimchoma; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza.
11 Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika bonde la Megido. 12 Nayo nchi itaomboleza, kila jamaa peke yake; jamaa ya nyumba ya Daudi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Nathani peke yao, na wake zao peke yao;
13 jamaa ya nyumba ya Lawi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Shimei peke yao, na wake zao peke yao. 14 Jamaa zote zilizosalia, kila jamaa peke yake, na wake zao peke yao”.
Hapo ndipo neema itarudi Israeli, ambapo inafananishwa ni lile tendo la Yusufu kujifunua tena kwa ndugu zake na kumtambua..Wakalia pamoja.
Lakini kabla hayo yote hayajatokea, ni sharti kwanza, watu wa nyumbani mwa Yusufu “WAONDOLEWE”.
Yusufu hawezi, kuwahudumia wote wawili kwa mpigo..Alikuwa na utaratibu wake. Na ndivyo hata Kristo atakavyofanya pindi neema inarudi Israeli, sisi watumishi wake, (tulio katika mataifa), atatuondoa kwanza, kwa tukio lijulikanalo kama unyakuo, ndio ajifunue kwa Israeli.
Ndugu yangu, kama hujui mpango huu wa Mungu ni kwamba mpaka sasa Israeli imeshakuwa taifa tangu 1948, ni taifa huru linalojitegemea, na hivi karibuni neema hii ya injili itarejea kwao. Hivyo mimi na wewe hatuna muda mwingi, Unyakuo upo karibu, tunachokisubiria hapa ni parapanda tu, hakuna kingine, dalili zote Yesu alizozisema zimeshatimia,(hilo kila mtu anajua) Kama unadhani, dunia itaendelea kuwepo kwa miaka mingine elfu, hilo wazo lifute,
Ikiwa unyakuo utapita leo, maana yake ni kuwa hii dunia itakuwa imebakiwa na miaka saba(7) tu mpaka iishie, na ndani ya hicho kipindi, Israeli itampokea Kristo, kisha mpinga-Kristo atanyanyuka mahususi kupigana nao, na baada ya hapo, Mungu ataiadhibu hii dunia kwa wote watakaopokea chapa ya Mnyama. Kisha Bwana atawaokoa watu wake Israeli, kwa kurudi kwake mara ya pili duniani, na dunia itakuwa imeisha.
Ndugu yangu, angalia maisha yako, angalia unapoelekea, angalia mpango wa Mungu ulivyojidhihirisha wazi mbele yetu, utaendelea mpaka lini kudumu katika dhambi? Au katika maisha ya uvuguvugu?. Ikiwa hujazaliwa mara ya pili ni heri ufanye hivyo sasa katika hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho. Na mtu anazaliwa mara ya pili kwanza kwa kutubu dhambi zake kwa kumaanisha kuziacha, na pili kwa kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi, na kwa jina la Yesu Kristo, na mwisho kupokea Roho Mtakatifu.
Hivyo ikiwa utahitaji msaada ya Toba, au ubatizo sahihi wa maji mengi, basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi nasi tutakusaidia.
Maran Atha.
WATAMTAZAMA YEYE AMBAYE WALIMCHOMA; NAO WATAMWOMBOLEZEA.
SIKU YA TAABU YA YAKOBO.
MZEITUNI HALISI UTAKAPOPACHIKWA.
ALIPO NA ATAKAPOKUWEPO BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
MIHURI SABA
UNAWAZA NINI SASA, JUU YA UFALME WA MBINGUNI?
Mafundisho maalumu kwa ajili ya waajiriwa: Sehemu 1
“Wewe U Mungu uonaye“
Kwa kuwa tupo katika huu ulimwengu, na hivyo Bwana ametuagiza tufanye kazi za mikono (kwa sisi ambao hatuna huduma ya kudumu madhabahuni kwa Bwana). tumeona ni vema pia tuwe na madarasa, ambayo, yatatupa mwongozo, wa namna ya kuishi katika maisha ya kazi. Na kama tujuavyo, kazi imegawanyika katika makundi mawili
Lakini, watu wengi wameangukia sana katika hilo kundi la pili(Yaani kuajiriwa). Hivyo leo tutaangazia hapo. Kazi ya kuajiriwa maana yake ni kuwa ni sharti mtu awekwe chini ya mwajiri (Boss) wake. Tutatazama kimaandiko, migogoro inayotokea mara nyingi katika kazi za kuajiriwa.
Watu wengi ukiwauliza, shida ni nini? Mbona huna raha na kazi yako? Watakuambia shida ni boss wangu, mwingine atasema haniamini, mwingine atasema ananionea wivu, mwingine atasema ni mbinafsi sana, anawapandisha wengine cheo hanipandishi mimi,mwingine atasema hatujali wafanyakazi, n.k. n.k.
Lakini wewe kama mkristo hupaswi umfikirie kiongozi wako, kwa jicho hilo, kwasababu, hata kama kweli anazo hizo tabia zinazokukwamisha, bado hawezi kuzuia kufanikiwa yako, au maono ambayo Mungu amekuwekea mbele yako.
Embu tutafakari kile Kisa cha Sarai na kijakazi wake Hajiri..Biblia inasema Sarai mwenyewe ndiye, aliyemwambia mumewe Abramu, amwingilie kijakazi wake ili ampatie uzao.. Wazo hilo halikuwa la Hajiri wala Abramu,. Kwa namna nyingine tunaweza kusema, Sarai alikusudia kumpandisha cheo kijakazi wake Hajiri, aonekane na yeye kama ni sehemu ya wake wa Ibrahimu.
Lakini mambo yalikuja kubadilika mbeleni, Hajiri alipoonekana ana mimba, Sarai akaanza kumtesa mama Yule. Na sababu ya kumtesa sio kwamba alimwonea wivu, hapana, bali aliona tabia za Hajiri zimebadilika ghafla hataki tena kuishi kama kijakazi bali anataka kuishi kama mke-mwenza, akiambiwa na Sarai aoshe vyombo anasema embu, niache hujui kama mimi ni mzazi!.
Hivyo Sarai kuona vile akaanza kumtesa, na kufadhaisha, mpaka uzalendo ukamshinda,Yule binti, ikabidi akimbilie jangwani huko akafie mbali. Lakini akiwa njiani, malaika alimtokea, akamwambia unakwenda wapi, akasema ninamkimbia bibi yangu Sarai kwasababu ananitesa nusu aniue,..Malaika akamwambia, Rudi kwa boss wako UKANYENYEKEE..
Tuisome habari..
Mwanzo 16:1 “Basi Sarai mkewe Abramu hakumzalia mwana, naye alikuwa na mjakazi, Mmisri, jina lake Hajiri. 2 Sarai akamwambia Abramu, Basi sasa, Bwana amenifunga tumbo nisizae, umwingilie mjakazi wangu labda nitapata uzao kwa yeye. Abramu akaisikiliza sauti ya Sarai. 3 Sarai mkewe Abramu akamtwaa Hajiri Mmisri mjakazi wake, baada ya kukaa Abramu katika nchi ya Kanaani miaka kumi, akampa Abramu mumewe, awe mkewe. 4 Basi akamwingilia Hajiri, naye akapata mimba. Naye alipoona ya kwamba amepata mimba, bibi yake alikuwa duni machoni pake. 5 Sarai akamwambia Abramu, Ubaya ulionipata na uwe juu yako; nimekupa mjakazi wangu kifuani mwako, naye alipoona kwamba amepata mimba, mimi nimekuwa duni machoni pake. Bwana na ahukumu kati ya mimi na wewe. 6 Naye Abramu akamwambia Sarai, Tazama, mjakazi wako yu mkononi mwako, mtendee lililo jema machoni pako. Sarai akamtesa, naye akakimbia kutoka mbele yake. 7 Malaika wa Bwana akamwona kwenye chemchemi ya maji katika jangwa, chemchemi iliyoko katika njia ya kuendea Shuri. 8 Akamwambia, Hajiri, wewe mjakazi wa Sarai, unatoka wapi, nawe unakwenda wapi? Akanena, Nakimbia mimi kutoka mbele ya bibi yangu Sarai. 9 Malaika wa Bwana akamwambia, Rudi kwa bibi yako, UKANYENYEKEE CHINI YA MIKONO YAKE. 10 Malaika wa Bwana akamwambia, Hakika nitauzidisha uzao wako, wala hautahesabika kwa jinsi utakavyokuwa mwingi. 11 Malaika wa Bwana akamwambia, Tazama! Wewe una mimba, utazaa mwana wa kiume, nawe utamwita jina lake Ishmaeli, maana Bwana amesikia kilio cha mateso yako. 12 Naye atakuwa kama punda-mwitu kati ya watu, mkono wake utakuwa juu ya watu wote na mkono wa watu wote utakuwa juu yake, naye atakaa mbele yao ndugu zake wote. 13 Akaliita jina la Bwana aliyesema naye, WEWE U MUNGU UONAYE, kwani alisema, Hata hapa nimemwona yeye anionaye”?
Tafakari kwa umakini hiyo habari..
Rudi ukanyenyekee, Mungu anajua kuwa unateswa, lakini wakati mwingine ni kwasababu ya kukosa kwako unyenyekevu..Rudi, kwasababu Baraka zako haziwezi kuzuiliwa na mtu yeyote kama mtoto utazaa tu, naye atakuwa taifa kubwa..Na kweli Hajiri akatii, japo hapo mwanzo alidhani kuwa Mungu haoni mateso yake..lakini hapa mpaka akasema, hakika “Wewe U Mungu uonaye”
Ndugu uliyeajiriwa, hakuna mtu anamchukia “mnyenyekevu”, usishindane na boss wako, hata kama ni mkali, wala usimkimbie, ukaacha kazi kwasababu za chuki, na fitina n.k., unaweza usipate nyingine nzuri kama hiyo.. bali kuwa tu mtulivu, kwasababu “Yupo aonaye”..Ukidhulumiwa mshahara “Yupo aonaye”.. Baraka zako zipo palepale. Yusufu alinyanyuliwa visa na boss wake wa kike, akawekwa gerezani, lakini mwisho wake tunaujua.
Hivyo zingatia hilo kama mkristo, katika maisha ya kuajiriwa,kuwa mnyenyekevu, ili uifurahie kazi yako.
na Bwana atakubariki.
Biblia inasemaje kuhusu Kazi?
JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 3)
Biblia inapotumia neno “Bila kazi ya mikono”, ina maana gani?
USIISHI BILA KUIFANYA KAZI YA MUNGU KABISA..
Moyo wake mwenye hekima upo upande wa kuume, maana yake nini?
Maji ya Zamzam yapo kibiblia?
JE! UNAMPENDA BWANA?
MIEZI 13 YA KIYAHUDI.
Je unajua kwamba kuikaribia dhambi ni “DHAMBI”, Hata tu kabla ya kuifanya?.
Mungu hakumpa tu Adamu maagizo ya kutokula yale matunda ya mti wa katikati…bali pia alimwambia “Asiyaguse yale matunda”..asije akafa. Wengi wetu tunaona tu habari ya “kula” kama kosa, lakini hatujui kuwa Mungu aliwaagiza kwamba hata kuyagusa wasiyaguse, (maana yake wakae mbali nayo).
Mwanzo 3:2 “Mwanamke akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula; 3 lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala MSIYAGUSE, msije mkafa”.
Mwanzo 3:2 “Mwanamke akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula;
3 lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala MSIYAGUSE, msije mkafa”.
Kumbe hata wangeyagusa tu yale matunda bila hata ya kuyala, bado Wangekufa!!.
Hii ni hatari sana..na inatupa fundisho kubwa sana..
Kwanini Mungu akataze wasiyaguse?..Je kuna ubaya wowote katika kuyagusa???… Jibu ni ndio!… kwasababu chanzo cha dhambi ya kula tunda ni kulishika lile tunda kwanza, (Hawa asingeweza kulipeleka mdomoni kabla ya kulishika) kabla ya kulichunguza chunguza kwanza, kabla ya kulidadisi dadisi, ndipo akaangukia katika ushawishi wa kulila.
Hivyo Mungu aliona chanzo cha dhambi kuwa ni “kushika” ndipo akatoa maagizo kwamba WASIYAGUSE!! Wasije wakafa… lakini wenyewe (Waligusa, na tena wakala) Hivyo ikawa ni makosa mawili yaliyozaa Mauti kamilifu.
Na hata leo Bwana anatuonya tukae mbali na dhambi, tusiikaribie kabisa dhambi, tusiiguse dhambi licha ya kuitenda!!..
Tukae mbali na Wizi kama ya wizi wenyewe kutendeka,…tukae mbali na Ulevi kabla ya ulevi wenyewe kutendeka… tukae mbali na Utukanaji, Uadui, Kiburi, Uasherati, kabla ya kufanya mambo hayo (Wagalatia 5:19-20)… Tusizikaribie kabisa hizi dhambi!!.. tukae nazo mbali maili nyingi sana, kwasababu kitendo cha kuzikaribia tu tayari ni kosa..
leo hii utaona mtu anasema hazini, wala hafanyi uasherati lakini katika simu yake kumejaa picha zinazochochea mambo hayo, kumejaa miziki inayochochoea mambo hayo, kumejaa filamu zi kidunia zenye maudhui hayo ya kiasherati, simu yake imejaa magroup ya mizaha, na uhuni, unaochochea mambo hayo…pasipo kujua kuwa anafanya makosa makubwa kuisogelea dhambi kwa namna hiyo..
Neno la Mungu linasema kwamba tuikimbie zinaa, sio tuishi nayo, au tuikemee!..bali tuikimbie (Soma 1Wakorintho 6:18 )...kama vile Yusufu alivyoikimbia mbele ya mke wa Potifa, na sisi tunapaswa tuikimbia hivyo hivyo Yusufu hata hakukubali kuzungumza na Yule mwanamke..
Lakini ni kinyume chake katika siku hizi za mwisho, utaona binti anayekiri kumpokea Yesu anapiga maneno na mwanaume anayemtaka, kijana anayekiri kumpokea Yesu anapiga maneno ya kidunia na binti anayemtamani, na hata kufanya naye mizaha..Hii ni hatari kubwa!, kumbuka ushawishi wa Hawa kula tunda haukuanzia mdomoni bali mkononi!..baada ya kulishika ndipo ushawishi ukamwingia..
Na sisi tukijishikamanisha na dhambi, basi ni lazima tutazitenda tu!, haijalishi itachukua muda gani ni lazima tutazitenda tu!…Hauwezi kusema umeacha utukanaji, lakini kila kukicha kampani zako ni za watu wanaotukana…ni lazima tu na wewe utatukana, haijalishi itakuchukua muda gani kudumu bila kutukana lakini mwisho wa siku utaishia kurudia matukano tu.
Hauwezi kukaa unasikiliza usengenyaji na wewe usiwe msengenyaji..ni suala la muda tu!, utajikuta na wewe upo kama wao.. Kumbuka Adamu na Hawa waliambiwa “wasiukaribie kabisa ule mti, na hata kuugusa”.. Vile vile na sisi leo hii tunapaswa tusiikaribie miti ya dhambi…wala tusiguse mashina yake wala matawi yake.. maana kugusa ndio chanzo cha kula..
Bwana atusaidie na kutuwezesha katika yote.
Maran atha!
MWENDO UNAOSHANGAZA SANA!
MUME / MKE BORA KUTOKA KWA BWANA UTAMWONA UKIWA KATIKA MAZINGIRA GANI?
HUJAPEWA MBAWA ZA KUKIMBIA MATATIZO
FANYA MAAMUZI KABLA HAZIJAKARIBIA SIKU ZA HATARI.
Mambo yale yaliyo mbali, na yale yaendayo chini sana,
Nini tofauti kati ya Bustani ya Edeni (Mwanzo 2:8) na bustani ya Adeni (Ezekieli 28:13 na Yoeli 2:3)
Jibu:Tusome
Mwanzo 2:8 “Bwana Mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa EDENI, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya”.
Isaya 51:3 “Maana Bwana ameufariji Sayuni; amepafariji mahali pake palipokuwa ukiwa; amefanya jangwa lake kuwa kama BUSTANI YA EDENI, na nyika yake kama bustani ya Bwana; furaha na kicheko zitaonekana ndani yake, kushukuru, na sauti ya kuimba”.
Hapa tunaona ikitajwa bustani ya “Edeni” lakini tukisoma mahali pengine tunaona ikitajwa bustani nyingine ya “Adeni”
Ezekieli 28:13 “Ulikuwa ndani ya ADENI, bustani ya Mungu; kila jiwe la thamani lilikuwa kifuniko chako, akiki, na yakuti manjano, na almasi, na zabarajadi, na shohamu, na yaspi, na yakuti samawi, na zumaridi, na baharamani, na dhahabu; kazi ya matari yako na filimbi zako ilikuwa ndani yako; katika siku ya kuumbwa kwako zilitengenezwa tayari”
Yoeli 2:3 “Moto unakula mbele yao; na nyuma yao miali ya moto inateketeza; hiyo nchi inafanana na BUSTANI YA ADENI mbele yao, na nyuma yao imekuwa jangwa tupu; naam, hakuna aliyeokoka asipatikane nao”.
Na pia katika Ezekieli 31:9, Ezekieli 31:16-18, na Ezekieli 36:35 utaona ikitajwa Adeni na si Edeni, swali je kuna utofauti wowote?
Jibu ni la! hakuna utofauti wowote iliyopo kati kati ya “Adeni” na “Edeni”, hayo ni maneno mawili yenye maana moja, sehemu moja biblia imetaja Edeni, sehemu nyingine Adeni lakini maana ni ile ile..Na maana ya neno Edeni au Adeni ni “paradiso ya raha”.
Mungu alipoiumba dunia, alimweka mwanadamu wa kwanza katika bustani ya Edeni, na alikusudia mahali pale pawe Paradiso yake ya milele. Dunia yote ilikuwa ni nzuri, lakini pale Edeni palikuwa ndio kitovu cha utukufu wa mwanadamu.
Lakini baada ya shetani kumdanganya Hawa, ndipo Uovu ukaingia na kusababisha mwanadamu kuondolewa katika bustani ile, na Mungu kuitowesha kabisa!
Lakini Bwana ameahidi kuumba Mbingu Mpya na Nchi mpya (Isaya 65:17), ambayo itakuja baada ya utawala wa miaka elfu kuisha hapa duniani. Katika mbingu mpya na nchi mpya, Bwana ametuandalia mambo mazuri kuliko yaliyokuwepo Edeni, maandiko yanasema jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia mambo ambayo Mungu kawaandalia wale wampendao..(1Wakorintho 2:9).
Lakini ahadi hiyo kulingana na Neno lake ni kwa wale waliomwamini Yesu Kristo na kuoshwa dhambi zao kwa damu yake.
Je umempokea Yesu?..kama bado unasubiri nini?. Mwamini leo na ukabatizwe katika ubatizo na ujazwe Roho Mtakatifu kulingana na Matendo 2:38.
Maran atha.
Bustani ya Edeni ipo nchi gani?
EDENI YA SHETANI:
Je! Ni kweli Yesu alirejesha kila kitu kama pale Edeni?
MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)
MIGAWANYO MINNE (4), YA HUDUMA YA YESU.
Mwanazuoni ni mtu aliyejikita katika utafiti au usomi wa ndani katika tasnia Fulani, lengo lake likiwa ni kupata uvumbuzi wa yale magumu yenye utata au yaliyojificha.. Hivyo mwanazuoni wa biblia ni mtu anayeingia ndani kujifunza Biblia, ili kuieleza katika urahisi zaidi au katika ufasaha zaidi kwa jamii au kutoa majibu ya mambo magumu yaliyo ndani ya biblia.
Mwanazuoni anajitofautisha na mwana-theolojia, kwa namna ya kwamba mwanatheolojia yeye yupo kisomi zaidi, kusoma kanuni na taratibu za kidini, hivyo anapohitimu, anakuwa amepata maarifa yale yale yaliyokwisha kuandaliwa. Lakini mwanazuoni, ni mtu ambaye hafungwi na taratibu, anaweza jitenga, kuchunguza, kusoma kwa ndani na kujua maana ya mambo.
Si kila mwanazuoni lazima apitie vyuo vya biblia.. Mtu akijikita katika kusoma biblia kwa undani na kujua siri nyingi zilizo ndani yake, huyo huitwa pia mwanazuoni.
Vilevile si kila mchungaji ni mwanazuoni. Mchungaji kazi yake ni kulichunga kundi la kulilisha, lakini ni vizuri pia mchungaji yeyote awe mwana-zuoni wa biblia. Kwasababu katika siku hizi za hatari zenye mafundisho mengi potofu, na udanganyifu mwingi wa dini za uongo, kila mmoja wetu hana budi kuwa mwanazuoni(mwanafunzi) wa biblia, ili awasaidie na wale ambao, hawajui kweli ya Neno la Mungu.
Lakini..
Kuna aina mbili za wanazuoni;
Mfano wa hilo kundi la kwanza, ndio wale waandishi na mafarisayo, waliokuwa kipindi cha Bwana Yesu, hawa waliipokea torati kama vitabu vya kidini tu, na kuvikariri, na kutunga hata na taratibu zao nyingine ambazo Mungu hakuwaagiza kabisa.
Walikuwa wanayachunguza maandiko, lakini wanamweka Mungu nyuma, Matokeo yake wakashindwa hata kumwona Kristo katika kila kipengele cha torati walichosoma, badala ya kumpokea wakampinga..Ndipo hapo Yesu akawaambia..
Yohana 5:39 “Mwayachunguza maandiko, kwa sababu mnadhani kwamba ninyi mna uzima wa milele ndani yake; na hayo ndiyo yanayonishuhudia. 40 Wala hamtaki kuja kwangu mpate kuwa na uzima”
Lakini kundi la pili la wanazuoni ni lile ambalo lina nia ya kuujua ukweli, na kiu yao ni wokovu na sio mashindano au usomi, mfano wa hawa ni wale watakatifu wa Beroya, ambao tunawasoma katika..
Matendo 17:10 “Mara hao ndugu wakawapeleka Paulo na Sila usiku hata Beroya. Nao walipofika huko wakaingia katika sinagogi la Wayahudi. 11 Watu hawa walikuwa waungwana kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa walilipokea lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo. 12 Basi watu wengi miongoni mwao wakaamini, na wanawake wa Kiyunani wenye cheo, na wanaume si wachache”.
Mfano tena wa hawa, ni Nabii Danieli.. ambaye pia biblia inatuonyesha alikuwa ni mtafiti (mwanazuoni) aliyekuwa anasoma sana vitabu, na matokeo yake akagundua hesabu ya miaka ambayo wangekaa Babeli, hivyo akajinyenyekeza mbele za Mungu akaomba dua na rehema, na Mungu akamsikia, na kumfunulia zaidi..
Danieli 9:1 “Katika mwaka wa kwanza wa Dario, mwana wa Ahasuero, wa uzao wa Wamedi, aliyetawazwa kuwa mfalme juu ya milki ya Wakaldayo; 2 katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danielii, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini”.
Mwingine ni mtume Paulo ambaye mpaka uzee wake alikuwa anasoma vitabu, soma (2Timotheo 4:13), na ndio maana hatushangai ni kwanini Mungu alimjalia mafunuo mengi namna ile.. mpaka akamuasa na Timotheo naye awe vilevile..
1Timotheo 4:13 “Hata nitakapokuja, ufanye bidii katika kusoma na kuonya na kufundisha”.
Zipo faida nyingi za kila mmoja wetu kuwa mwanazuoni, Kama Apolo asingekuwa mwanafunzi mzuri wa maandiko, asingeweza kuwashinda wayahudi ambao walilisumbua sana kanisa la kwanza kwa imani zao potofu..(Soma Matendo 28:24-28).
Hivyo kuwa mwanazuoni huchangiwa na; kwanza kwa kuwa na bidii ya kusoma biblia binafsi, pili kuhudhuria mafundisho ya biblia kanisani, tatu kusoma vitabu mbalimbali vya Kikristo, Nne kusikiliza mafundisho yenye maudhui ya biblia kwenye radio, televisheni na bila shaka, kwenye tovuti kama yetu hii www.wingulamashahidi.org.
Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyotuhimiza kuwa wasomi/wanafunzi wa biblia..wenye lengo la kujifunza kumjua Mungu, (lakini sio mfano wa waandishi na mafarisayo, ambao lengo lao lilikuwa ni vyeo na ukubwa, na heshima waonekane wanayajua maandiko mengi, wasomi, wakubwa waogopwe). Lakini tukiwa na kiu ya kujua mapenzi ya Mungu katika maandiko, ni bora kwetu na kwa wengine..
Wakolosai 4:6 “Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea munyu, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu”.
Mathayo 4: 4 “Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu”.
Yoshua 1:8 “Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana”
JINSI YA KUSOMA BIBLIA.
TUNAMHITAJI SANA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUYAELEWA MAANDIKO.
Tofauti kati ya maandiko na Neno ni ipi?
UFUNUO NI NINI, NA NITAPOKEAJE UFUNUO KUTOKA KWA MUNGU?
HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?
Biblia ni nini?USIACHE KUJIFUNZA NENO LA MUNGU
Gombo ni nini?
Kitabu cha YASHARI kinachozungumziwa katika 2Samweli 1:17-18, ni kitabu gani?
Wakati ambapo Israeli inapitia manyanyaso makali kutoka kwa wakaanani kwa miaka 20, mpaka yakawafanya wamlilie Mungu kwa nguvu ili awaokoe..Tunasoma kwenye biblia Mungu alisikia kilio chao akawanyanyulia mwamuzi Debora pamoja na baraka..
Hivyo Mungu akawaagiza wana wa Israeli wapange majeshi, ili wakapigane na adui zao, na hakika Bwana atawashindia..makabila mengi yalikubali kupeleka majeshi yao, lakini yapo makabila mengine hayakutaka kujishughulisha na jambo hilo..na hayo si mengine zaidi ya Dani, Asheri, na nusu ya kabila la Manase na Gadi. Haya yote yalikuwa mbali kidogo na eneo la vita, Yaliona kama vile vita haviwahusu wao, hivyo yakawa bize kuendelea na mambo yao..
Waamuzi 5:17
[17]Gileadi alikaa ng’ambo ya Yordani, Na Dani, mbona alikaa katika merikebu? Asheri alikaa kimya penye bandari ya bahari, Alikaa katika hori zake.
[17]Gileadi alikaa ng’ambo ya Yordani,
Na Dani, mbona alikaa katika merikebu?
Asheri alikaa kimya penye bandari ya bahari,
Alikaa katika hori zake.
Kwamfano kama hapo maandiko yanasema Dani alikaa katika merikebu, maana yake ni kuwa alikuwa ni mfanya biashara, aliona kuacha biashara zake za melini, za uchukuzi, na kwenda kujishughulisha na vita, ni upotezaji wa muda, kupigania taifa la Mungu ni kazi kichaa, wacha niendelee na biashara zangu..Na ndivyo hata hayo mataifa mengine yalivyokuwa, yalichowaza ni biashara, na mahangaiko ya hii dunia mpaka Agizo la Mungu likawa halina maana tena kwao, hata utumwa wa taifa lao hawakuuona, mateso na dhihaka taifa lao lilipokuwa linapitia hawakuona kama ni kitu zaidi ya biashara.
Ndipo Debora akaongozwa na Roho kutunga wimbo huo wa kuwashutumu ambao mpaka sasa tunausoma..
Hata sasa, tabia za makabila haya kama Dani zipo miongoni mwa wakristo wengi, ni mara ngapi utamwambia mkristo twende tukashuhudie, kwasababu tumeamuriwa kufanya hivyo na Kristo..lakini atakuambia sina muda, nipo buzy, sina mtu wa kumuacha kwenye biashara yangu…
Anaona biashara yake ni bora kuliko kuokoa roho za watu wanaopotea, huyu ni Dani anayekaa merikebuni..kipaumbele chake ni shughuli za huu ulimwengu, kazi, pesa, ndizo anazozitaabikia kutoka Januari mpaka Disemba, mwaka kwa mwaka, hana rekodi ya kufanya chochote kizuri kwa ajili ya ufalme wa Mungu, lakini yupo tayari kujenga majumba, na mahoteli, na ma-meli ili kutanua wigo wake wa kibiashara..
Ni kweli Mungu anaweza kuokoa watu wake pasipo wewe, lakini vilevile kumbuka Mungu anaweza kubaki na mbingu yake pasipo wewe..usipokwenda mbinguni hakumpunguzii yeye kitu.
Hatushangai hata ni kwanini hili kabila la Dani halionekani miongoni mwa makabila ya Israeli yatakayookolewa siku za mwisho (Ufunuo 7:1-8). Sababu mojawapo ni hii..Na sisi tujichunguze tutambue kipaumbele chetu kwa kwanza ni kipi. Je siku ile tutakuwa na ujasiri wa kusimama mbele ya Kristo?
Bwana atupe kuliona hili.
USIPOLITENDEA KAZI NENO LA MUNGU.
Hori ni nini kibiblia (Waamuzi 5:17, Luka 2:7)?
Tarshishi ni mji gani kwasasa?
NITAJUAJE KAMA MAOMBI YANGU YAMEFIKA (YAMEJITOSHELEZA)?.
NYOTA ZIPOTEAZO.
Kuna tofauti gani kati ya ‘Mungu’ na ‘Mola’?
NI NINI TUNAJIFUNZA KWA YOANA NA MANAENI?
Tofauti na Kalenda ya Kirumi ambayo ndiyo tunayoitumia sasa yenye miezi 12, Kalenda ya kiyahudi yenyewe inakuwa na miezi 13 kwa mara saba kila baada ya miaka 19. (Yaani katika kipindi cha miaka 19, miaka 7 inakuwa na miezi 13, na miaka 12 iliyosalia inakuwa na miezi 12 kama kawaida), Na miaka yenye miezi 13 ni inakuwa ni mwaka wa 3, 6,8,11,14, 17 na 19 na mzunguko wa miaka 19, unapoisha na unapoanza mzunguko mwingine, basi mgawanyo wa miezi unakuwa ni huo huo, wa baadhi ya miaka kuwa na miezi 13 na mingine 12.
Sasa mwezi wa 13, unaoongezeka juu ya miezi 12 ya kiyahudi ni mwezi ujulikanao kama Adari II, Sasa kabla ya kwenda kuutazama huu mwezi wa 13 wa Adari, hebu tuitazame miezi 12, na rejea zao katika biblia.
Mwezi wa 1: Abibu au Nisani.
Mwezi wa Abibu au Nisani ni mwezi wa kwanza katika kalenda ya kiyahudi, mwezi huu unaanza katika mwezi Machi katikati na kuisha mwezi Aprili katikati katika kalenda yetu ya kirumi tunayoitumia..
Mwezi wa Abibu ndio mwezi ambao wana wa Israeli walitoka Misri..
kutoka 13:3 Musa akawaambia hao watu, Kumbukeni siku hii, mliyotoka nchi ya Misri, kutoka nyumba ya utumwa; kwa kuwa Bwana aliwatoa mahali hapa kwa nguvu za mkono wake; na usiliwe mkate uliochachwa. 4 Ninyi mwatoka leo katika MWEZI WA ABIBU.
kutoka 13:3 Musa akawaambia hao watu, Kumbukeni siku hii, mliyotoka nchi ya Misri, kutoka nyumba ya utumwa; kwa kuwa Bwana aliwatoa mahali hapa kwa nguvu za mkono wake; na usiliwe mkate uliochachwa.
4 Ninyi mwatoka leo katika MWEZI WA ABIBU.
Na wakati ambapo Hamani ananyanyuka kutaka kuwaangamiza Israeli yote katika ufalme wote wa Ahasuero, tunasoma wazo hili lilimjia katika Mwezi wa Nisani/ Abibu..
Esta 3:7 “Basi mwezi wa kwanza, ndio MWEZI WA NISANI, mwaka wa kumi na mbili wa mfalme Ahasuero, wakapiga Puri, yaani kura, mbele yake Hamani; siku kwa siku, na mwezi kwa mwezi, hata mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari”.
Na pia tunausoma huu mwezi ukitajwa wakati Nehemia alipoingiwa na wazo la kwenda kuujenga Yerusalemu..
Nehemia 2:1 “Ikawa katika MWEZI WA NISANI, mwaka wa ishirini wa mfalme Artashasta, na divai imewekwa mbele yake, nikaishika ile divai, nikampa mfalme. Nami mpaka sasa sikuwa na huzuni mbele ya mfalme wakati wo wote.”.
Mwezi wa 2: Zivu au Ayari
Mwezi huu unaangukia kati ya mwezi Aprili na mwezi May kwa kalenda yetu tunayoitumia, na ni mwezi wa pili katika kalenda ya kiyahudi.
Mwezi huu ndio mwezi ambao Mfalme Sulemani alianza kulijenga Hekalu la Mungu katika Yerusalemu..
1Wafalme 6:1 “Ikawa katika mwaka wa mia nne na themanini baada ya kutoka wana wa Israeli katika nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa kutawala kwake Sulemani juu ya Israeli, katika MWEZI WA ZIVU, ndio mwezi wa pili, akaanza kuijenga nyumba ya Bwana. 2 Nayo nyumba hiyo mfalme Sulemani aliyomjengea Bwana, urefu wake ulikuwa mikono sitini, na upana wake ishirini, na kwenda juu kwake mikono thelathini”.
1Wafalme 6:1 “Ikawa katika mwaka wa mia nne na themanini baada ya kutoka wana wa Israeli katika nchi ya Misri, katika mwaka wa nne wa kutawala kwake Sulemani juu ya Israeli, katika MWEZI WA ZIVU, ndio mwezi wa pili, akaanza kuijenga nyumba ya Bwana.
2 Nayo nyumba hiyo mfalme Sulemani aliyomjengea Bwana, urefu wake ulikuwa mikono sitini, na upana wake ishirini, na kwenda juu kwake mikono thelathini”.
Mwezi wa 3: Siwani
Huu ni mwezi wa tatu kwa kalenda ya kiyahudi, lakini kwa kalenda yetu ni mwezi unaoangukia kati ya mwezi Mei na mwezi Juni.
Katika mwezi huu ndio mwezi ambao Mfalme Ahasuero, enzi za malkia Esta alitoa ruksa kwa wayahudi kujilipizia kisasi juu ya adui zao.
Esta 8:9 “Basi, waandishi wa mfalme wakaitwa pale pale, siku ya ishirini na tatu ya mwezi wa tatu, ndio MWEZI WA SIWANI; na kama vile Mordekai alivyoamuru, Wayahudi wakaandikiwa, pamoja na maakida na maliwali, na wakuu wa majimbo toka Bara Hindi mpaka Kushi, majimbo mia na ishirini na saba, kila jimbo kwa mwandiko wake, na kila taifa kwa lugha yake; na Wayahudi kwa mwandiko wao na kwa lugha yao”.
Mwezi wa 4: Tamuzi
Huu ni mwezi wa Nne katika kalenda ya kiyahudi, lakini kwetu sisi unaanguka katika ya mwezi Juni na mwezi Juni na mwezi Julai.
Mwezi huu katika bibli unaonekana kutajwa mara moja tu katika kitabu cha Ezekieli.
Ezekieli 8:14 “Ndipo akanileta mpaka mlango wa kuingilia katika nyumba ya Bwana, ulioelekea upande wa kaskazini, na tazama, wanawake wameketi wakimlilia TAMUZI”.
Mwezi huu wa nne umetajwa sehemu nyingine kama kwa namba na si kwa jina (Soma Yeremia 39:1-2, na Yeremia 52:6-7).
Mwezi wa 5: Avu
Huu ni mwezi wa tano kwa wayahudi na kwetu sisi unaangukia kati ya mwezi wa Julai na Mwezi Agosti.. Mwezi huu katika biblia haijatajwa kwa jina bali kwa namba..
Kwamfano tunasoma Ezra aliwasili Yerusalemu katika mwezi wa 5
Ezra 7:8 “Naye Ezra akafika Yerusalemu mwezi wa tano katika mwaka wa saba wa huyo mfalme”
Na pia katika (2 Wafalme 25:8-10, Yeremia 1:3 na Yeremia 52:12-30)
Mwezi wa 6: Eluli
Huu ni mwezi wa 6 kwa kalenda ya kiyahudi na unaangukia kati ya mwezi wa Agosti na Septemba katika kalenda yetu.
Katika biblia mwezi huu ndio mwezi ambao Nehemia alimaliza kati ya kuukarabati ukuta Yerusalemu..
Nehemia 6:15 “Basi huo ukuta ukamalizika siku ya ishirini na tano ya mwezi wa ELULI, katika muda wa siku hamsini na mbili”
Mwezi huu pia umetajwa kwa namba katika kitabu cha Hegai 1:14-15.
Mwezi wa 7: Ethanimu
Huu ni mwezi wa 7 kwa kalenda ya kiyahudi na kwa kalenda yetu unaangukia katika ya mwezi wa Septemba na Oktoba.
Hekalu la Sulemani liliwekwa wakfu katika mwezi huu wa Ethanimu
1Wafalme 8:1 “Ndipo Sulemani alipowakusanya wazee wa Israeli, na wakuu wote wa kabila, wakuu wa mbari za mababa wa wana wa Israeli, wamwendee mfalme Sulemani huko Yerusalemu, ili walipandishe sanduku la agano la Bwana kutoka mji wa Daudi, yaani, Sayuni. 2 Wakakutana mbele ya mfalme Sulemani watu wote wa Israeli wakati wa sikukuu, katika MWEZI WA ETHANIMU, ndio mwezi wa saba. 3 Wazee wote wa Israeli wakaja, nao makuhani wakajitwika sanduku”
1Wafalme 8:1 “Ndipo Sulemani alipowakusanya wazee wa Israeli, na wakuu wote wa kabila, wakuu wa mbari za mababa wa wana wa Israeli, wamwendee mfalme Sulemani huko Yerusalemu, ili walipandishe sanduku la agano la Bwana kutoka mji wa Daudi, yaani, Sayuni.
2 Wakakutana mbele ya mfalme Sulemani watu wote wa Israeli wakati wa sikukuu, katika MWEZI WA ETHANIMU, ndio mwezi wa saba. 3 Wazee wote wa Israeli wakaja, nao makuhani wakajitwika sanduku”
Unaweza kuusoma pia mwezi huu katika..(1Wafalme 8:2, Walawi 23:24, Nehemia 8:13-15).
Mwezi wa 8: Buli.
Mwezi huu ni mwezi wa 8 kwa kalenda ya kiyahudi na unaangukia kati ya mwezi Octoba na mwezi mwezi Novemba katika kalenda yetu ya kirumi.
Katika mwezi huu ndio mwezi ambao Sulemani alimaliza kuijenga nyumba ya Mungu (Hekalu).
1Wafalme 6:38 “Hata katika mwaka wa kumi na mmoja, katika MWEZI WA BULI, ndio mwezi wa nane, nyumba ikaisha, mambo yake yote, na sharti zake zote. Basi muda wa miaka saba alikuwa katika kuijenga.
Unaweza kusoma pia habari za mwezi huu katika (1Wafalme 12:32-33, 1Nyakati 27:11).
Mwezi wa 9: Kisleu
Huu ni mwezi wa 9 kwa kalenda ya kiyahudi na unaangukia kati ya mwezi wa Novemba na Disemba katika kalenda yetu ya sasa ya kirumi.
Katika mwezi huu Nabii Zekaria alioneshwa maono juu ya Yuda na Israeli.
Zekaria 7:1 “Ikawa katika mwaka wa nne wa mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia Zekaria, siku ya nne ya mwezi wa kenda, yaani, KISLEU”
Mwezi wa 10: Tebethi
Huu ni mwezi wa 10 kwa Wayahudi na kwa kalenda ya kirumi unaangukia kati ya mwezi Disemba na January.
Katika biblia mwezi huu ndio mwezi ambao Esta aliingizwa katika nyumba ya kifalme..
Esta 2:16 “Basi Esta alipelekwa kwa mfalme Ahasuero, katika nyumba ya kifalme, mwezi wa kumi, ndio mwezi wa Tebethi, mwaka wa saba wa kumiliki kwake. 17 Mfalme akampenda Esta kuliko wanawake wote, naye akapata neema na kibali machoni pake kuliko mabikira wote; basi akamtia taji ya kifalme kichwani pake, akamfanya awe malkia badala ya Vashti”.
Esta 2:16 “Basi Esta alipelekwa kwa mfalme Ahasuero, katika nyumba ya kifalme, mwezi wa kumi, ndio mwezi wa Tebethi, mwaka wa saba wa kumiliki kwake.
17 Mfalme akampenda Esta kuliko wanawake wote, naye akapata neema na kibali machoni pake kuliko mabikira wote; basi akamtia taji ya kifalme kichwani pake, akamfanya awe malkia badala ya Vashti”.
Na ndio mwezi ambao Nebukadreza aliuhusuru Yerusalemu (2Wafalme 25:1, Yeremia 52:4).
Mwezi wa 11: Shebati
Mwezi huu unaangukia kati ya mwezi Januari na mwezi Februari kwa kalenda ya kirumi na katika kalenda ya kiyahudi ni mwezi wa 11.
Katika mwezi huu ndio mwezi ambao Zekaria aliona maono tena juu ya Yerusalemu..
Zekaria 1:7 “Siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, yaani, mwezi uitwao Shebati, katika mwaka wa pili wa Dario, neno la Bwana lilimjia Zekaria, mwana wa Berekia, mwana wa Ido, nabii, kusema, 8 Naliona wakati wa usiku, na tazama, mtu amepanda farasi mwekundu, akasimama kati ya mihadasi iliyokuwa mahali penye uvuli; na nyuma yake walikuwapo farasi wengine wekundu, na wa rangi ya kijivujivu, na weupe”.
Zekaria 1:7 “Siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, yaani, mwezi uitwao Shebati, katika mwaka wa pili wa Dario, neno la Bwana lilimjia Zekaria, mwana wa Berekia, mwana wa Ido, nabii, kusema,
8 Naliona wakati wa usiku, na tazama, mtu amepanda farasi mwekundu, akasimama kati ya mihadasi iliyokuwa mahali penye uvuli; na nyuma yake walikuwapo farasi wengine wekundu, na wa rangi ya kijivujivu, na weupe”.
Mwezi wa 12: Adari I.
Huu ni mwezi wa 12 na wa mwisho kwa kalenda za kiyahudi, ambapo kwa kalenda ya kirumi unaangukia kati ya Mwezi Februari na mwezi Machi.
Esta 3:7 “Basi mwezi wa kwanza, ndio mwezi wa Nisani, mwaka wa kumi na mbili wa mfalme Ahasuero, wakapiga Puri, yaani kura, mbele yake Hamani; siku kwa siku, na mwezi kwa mwezi, hata mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari”.
Kutokana na kuwepo na miaka mirefu na mifupi, Marabi wa kiyahudi katika karne ya 4, wakiongozwa na Rabbi Hillel II, waliongeza mwezi mmoja wa 13, katika kalenda ya kiyahudi ambao waliuita mwezi ADARI II (Adari wa pili).
Lengo la kuongeza mwezi huu ni ili kuziweka sikukuu za kiyahudi katika majira halisia, vinginevyo sikukuu za kiyahudi zingeangukia misimu ambayo sio, kwamfano sikukuu ya pasaka ambayo kwa wayahudi inaseherekewa katika mwezi wa March au April kwa kalenda yetu, kama kusingekuwepo huu mwezi wa 13, basi huenda miaka mingine sikukuu hii ingeangukia mwezi wa 8 kwa kalenda yetu, jambo ambalo lingekuwa halina uhalisia hata kidogo.
Lakini swali ni je!, sisi wakristo tunapaswa kuifuata kalenda ipi?, ya kiyahudi au hii inayotumika sasa ya kirumi?
Jibu ni kuwa Kalenda hazitusogezi karibu na Mungu wala hazipeleki mbali na Mungu, tukitumia kalenda ya kiyahudi, au ya kirumi au ya kichina au hata ya kichaga haituongezei chochote, kilicho cha muhimu ni kuishi kwa kuukomboa wakati kama biblia inavyosema katika..
Waefeso 5:15 “Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; 16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu”
Waefeso 5:15 “Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;
16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu”
Na tunaukomboa wakati kwa kufanya yale yanayotupasa kufanya, ikiwemo Kujitakasa, kufanya ibada, kuomba, kusoma Neno, kuifanya kazi ya Mungu kupitia karama iliyo ndani yako kabla ya ule mwisho kufika na mambo mengine yote yanayohusiana na hayo.
Mwandamo wa mwezi/Mwezi mpya Ni nini kibiblia?
UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?
Je! kuna sikukuu za pasaka mbili? (Hesabu 9:11)
Je! ni sahihi kwa Mkristo kusherekea siku yake ya kuzaliwa.[Birth day]?
Nini maana ya wokovu watoka kwa Wayahudi? (Yohana 4:22)