DON’T BE AFRAID WHEN YOU GO DOWN.

Watu wenye ulemavu wa akili, wataenda mbinguni?

Jibu: Hapana!, watu wenye ulemavu wa akili kikweli kweli, Bwana akirudi hawataenda!, watabaki kukumbana na ghadhabu ya Mungu.!.

LAKINI SISI TUNAVYOMTAFSIRI MTU MWENYE ULEMAVU WA AKILI, NI TOFAUTI NA MUNGU ANAVYOMTAFSIRI.

Sisi tunamtafsiri mtu mwenye ulemavu wa akili ni yule tunayemwona haeleweki anapozungumza, anatokwa na mate mdomoni, na hawezi kujimudu mwenyewe!..na mtu aliye na akili timamu ni yule, tunayemwona anaoga vizuri na kuwa nadhifu na mwenye utashi wa kidunia! Anayekubalika kila mahali.. lakini kwa Mungu sivyo.

1Wakorintho 3:18 “Mtu asijidanganye mwenyewe; kama mtu akijiona kuwa mwenye hekima miongoni mwenu katika dunia hii, na awe mpumbavu, ili apate kuwa mwenye hekima.

19 MAANA HEKIMA YA DUNIA HII NI UPUZI MBELE ZA MUNGU. KWA MAANA IMEANDIKWA, YEYE NDIYE AWANASAYE WENYE HEKIMA KATIKA HILA YAO”.

Sasa mtu mwenye MATATIZO YA AKILI, kibiblia ni yupi?

Tusome, mistari ifuatayo ili tuweze kujua “Mlemavu wa akili ni yupi mbele za Mungu”.

 1. MTU MZINIFU.

Mithali 6:32 “Mtu aziniye na mwanamke HANA AKILI KABISA; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake”.

Wakati unaona mtu anayedondosha mate, kama hana akili, kumbe Mungu anakuona wewe unayezini kuwa HUNA AKILI KABISA!.. Tena hasemi “huna akili” tu!..bali anamalizia na neno “kabisa”. Kwahiyo kumbe mtu anayezini ni Tahira!, mbele za Mungu… ni heri uwe unashindwa kuyamudu mate yako kuliko kuwa mzinifu.

 2. MTU ANAYEDHARAU WENGINE.

Mithali 11:12 “ASIYE NA AKILI HUMDHARAU MWENZIWE; Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza”.

Kama unamdharau huyo  unayemwona hawezi kuongea kama wewe, au hawezi kupambanua kama wewe, au hana heshima kama yako, au uwezo kama wako.. basi tambua kuwa mbele za MUNGU, Wewe ndio HUNA AKILI (Una matatizo ya akili) kuliko huyo unayemdharau.

1Wakorintho 3:18 “Mtu asijidanganye mwenyewe; kama mtu akijiona kuwa mwenye hekima miongoni mwenu katika dunia hii, na awe mpumbavu, ili apate kuwa mwenye hekima.”

 3. MTU ANAYEWAONEA WENGINE!

Mithali 28:16 “Mkuu ALIYEPUNGUKIWA NA AKILI HUWAONEA WATU SANA; Bali achukiaye kutamani ataongeza siku”

Ikiwa una cheo Fulani, au wewe ni mkubwa kicheo au kiumri, katikati ya watu, na hutendi haki bali unawaonea wengine, basi fahamu kuwa mbele za Mungu, unayo matatizo ya akili, haijalishi dunia nzima inakuona una akili, mbele za Mungu unao ulemavu wa akili.

Kwaufupi kuishi Maisha ya dhambi na ya kutomtafuta Mungu, na huku unajua kabisa kuwa unapaswa umtafute Mungu, HUKO NI KUKOSA AKILI.

Zaburi 14:2 “Toka mbinguni Bwana aliwachungulia wanadamu, Aone kama yuko mtu mwenye akili, Amtafutaye Mungu”.

Kwahiyo, kwa hitimisho ni kwamba “wale tunaowaona sisi ni walemavu wa akili, waliopo mahospitalini”..Mungu hawaoni hivyo!.. Na Bwana anateta nao!, kwa namna yao, na watahukumiwa kwa namna yao!..Wewe huwezi kuongea nao, lakini Bwana anaweza kuongea nao, kwasababu yeye ndio aliyewaumba…

Wewe huwezi kuwaelewa lakini Bwana anawaelewa, kwasababu ni yeye ndiye kawaumba..hawezi kukiumba kitu ambacho kitamshinda yeye kukielewa.

Wewe huwezi kuona kama wanamwabudu Mungu, au wanamtukuza Mungu, au wana dhambi lakini Mungu ndiye anayewajua mienendo yao…

Hivyo kwasababu Bwana ndiye anayewajua na ndiye atakayewahukumu, wapo watakaoingia mbinguni, na wapo ambao hawataingia.. (Wanadamu wote siku za mwisho watasimama mbele ya kiti cha hukumu).

Lakini sisi tunaojiona tuna akili timamu, huku tunazini, au tunafanya dhambi, huku tunatembea nusu-tupu barabarani, huku tunapaka rangi nyuso zetu, huku tunajichora Ngozi zetu, huku tunaabudu sanamu!..tujue mbele zake Mungu ni “walemavu wa akili” , haijalishi dunia nzima itatuthaminisha kiasi gani, basi mbele zake ni “walemavu wa akili”. Hivyo ili tuwe na akili hatuna budi kumtafuta Mungu, kwa kumwamini Bwana Yesu na kuyashika maneno yake.

Mathayo 7:24 “Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;

25 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia?

CHAPA YA MNYAMA

Wibari ni nani?(Mithali 30:26)

INJILI YA MANENO LAINI ITAKUGHARIMU.

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

Rudi nyumbani

Print this post

AKAJIFUNGA VAZI LAKE, AKAJITUPA BAHARINI.

Bwana Yesu asifiwe.

Ulishawahi kulitafakari kwa ukaribu lile tukio, ambalo Bwana Yesu aliwatokea wanafunzi wake kwa sura nyingine, walipokuwa baharini wanavua?. Utaona muda wote aliokuwa anazungumza nao wasimtambue Petro alikuwa uchi, Lakini Yohana alipomtambua, kuwa ni Bwana Yesu yupo katikati yao, moja kwa moja alimwambia Petro ufunuo huo.

Na tukio lililofuata pale, utaona Petro hakwenda kumkumbatia, au kumsalimia, au kumsujudia..Bali, tukio la kwanza alilolifanya ni kuificha aibu yake mbele za Bwana. Ndio maana muda ule ule akavaa nguo zake, na akaona hilo halitoshi akajitupa kabisa baharini, kujisitiri,

Yohana 21:5 “Basi Yesu akawaambia, Wanangu, mna kitoweo? Wakamjibu, La.

6 Akawaambia, Litupeni jarife upande wa kuume wa chombo, nanyi mtapata. Basi wakatupa; wala sasa hawakuweza kulivuta tena kwa sababu ya wingi wa samaki.

7 Basi yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda akamwambia Petro, Ndiye Bwana. Naye Simoni Petro, aliposikia ya kwamba ni Bwana, akajifunga vazi lake, (maana alikuwa uchi), akajitupa baharini.

Hiyo ni kutufundisha nini? Kuwa Bwana anapenda heshima, hapendezwi na watu wasiojiheshimu miili yao, pale wanaposimama mbele yake. Petro ni mwanaume, anasimama mbele ya mwanaume mwenzake, lakini anaona aibu kukaa uchi..

Jiulize wewe mwanamke, ambaye, unajisikia amani, kuvaa vimini, Una Roho Mtakatifu kweli? Na kibaya Zaidi unamfuata Yesu kanisani, unajifanya kumlilia, na kumwimbia na mavazi ambayo huwezi kwenda nayo hata kwa wazazi wako!!. Huoni kama unamvunjia Kristo heshima?

Unajisikiaje, unapovaa suruali kama mwanaume halafu unakwenda kumwabudu Kristo?. Unavaa nguo za migongo wazi, unatembea barabarani, halafu unasema umeokoka, kivipi? Wewe sio mtumwa wa Kristo,  kwasababu watumwa wa Kristo, kama Petro huwa wanaona aibu kukaa uchi, mpaka wanajitupa baharini.

Embu kachome hizo nguo, kuonyesha kweli unamuheshimu Kristo, vaa mavazi ya kujisitiri ya kike, kwani unapunguka nini Ukivaa sketi ndefu au gauni, dada utaumwa? Sasa kwanini ufunue mapaja yako barabarani, kila mtu ayatazame?

Petro alipokwisha kujisitiri, ndipo utaona Bwana Yesu anazungumza naye, lugha ya kiutumishi.. Anamwambia Petro wanipenda? Anasema ndio, Bwana anaendelea kumwambia Chunga, kondoo wangu!, Lisha kondoo zangu!. Lakini hapo kabla hakuzungumza naye lugha kama hizo kwasababu, alikuwa uchi mbele zake.

Jitose baharini dada, Ona aibu, kuwa tayari kuacha mavazi ya kikahaba, achana na fasheni, Onekana mshamba mbele za watu, lakini kwa Kristo mwerevu. Hakuna namna vimini na suruali vitakusogeza kwa Kristo, hakuna namna dada!, ni lazima uukimbie ulimwengu tu.

1Yohana 2:15 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake”.

Injili za manabii wa uongo zinazokuambia Mungu anaangalia roho, haangalii mwili, jiangalie sana, kama ni hivyo  basi hata hiyo afya na rizki unazomuomba kila siku hana haja ya kukupa kwasababu haangalii mwili anangalia Roho yako tu, akupe uzima wa milele.

Ndugu,Vyote Bwana anavijali, isitoshe, hata siku ile ya mwisho, miili yetu pia itaokolewa, haitapotezwa na kutupwa motoni kama watu wanavyodhani, bali itaokolewa kwa kuvikwa miili ya kimbinguni(1Wakorintho 15:53-54). Yaani kwa ufupi hutakwenda mbinguni, kama mwili wako haujakombolewa.

Maandiko kama haya, hayajaandikwa kama stori kutuonyesha jinsi gani Petro anajua kujirusha baharini, na kuvaa nguo, bali ni kutufundisha sisi, tuwejeke sawa, pale tunapotaka kusimama mbele ya Bwana wetu, na mwokozi wetu.

Bwana atujalie kuliona hili.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

UVUVI BORA HAUCHAGUI, CHA KUVUA.

Kwanini wakristo walipomuona Petro akigonga walisema “Ni malaika wake”?

Je suruali ni vazi la kiume tu?

ISHARA ITAKAYONENEWA

Rudi nyumbani

Print this post

UVUVI BORA HAUCHAGUI, CHA KUVUA.

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, utukufu na heshima vina yeye milele na milele.

Utajiuliza, ni kwanini wengi wa mitume wa Bwana Yesu walikuwa ni wavuvi? Tukiachilia mbali wale wanne (yaani Petro, Yakobo, Yohana, na Andrea, ambao kazi yao rasmi ilikuwa ni uvuvi), Kulikuwa na wengine watatu, ambao walikuwa wanaifanya pia hii kazi, kama sio kuwa na uzoefu nayo (Soma Yohana 21:1-3). Hivyo tunaweza kusema, si chini ya mitume saba (7), walikuwa ni wavuvi.

Utajiuliza Ni kwanini Bwana alipendelea sana wavuvi, na sio watoza ushuru wengi, ni kwasababu kazi yake ya kuokoa watu ilifanana na hiyo, na ndio maana akamwambia Petro tangu sasa nitakufanya kuwa mvuvi wa watu, hakumwambia nitakufanya kuwa muhubiri wa watu, hapana bali mvuvi wa watu. Kuonyesha kuwa maarifa ya uvuvi, yana mchango mkubwa sana, katika kuokoa roho za watu.

Sasa tabia mojawapo ya mvuvi, ni kuwa hachagui cha kuvua pindi anapotupa nyavu yake baharini, huwa kichani pake anajua kabisa, vitakavyokuja juu, sio  Samaki tu peke yake, bali pia na viumbe vingine vingi vya majini, Pamoja na takataka nyingi.

Ndio maana Bwana Yesu alitoa mfano huu, akasema;

Mathayo 13:47 “Tena ufalme wa mbinguni umefanana na juya, lililotupwa baharini, likakusanya samaki wa kila namna;

48 hata lilipojaa, walilivuta pwani; wakaketi, wakakusanya walio wema vyomboni, bali walio wabaya wakawatupa”.

Umeona? Samaki waliovuliwa, inaweza ikawa ni asilimia 20 tu, lakini 80 yote iliyobakia, ni konokono, kobe, nyoka, magugu, minyoo n.k.

Hivyo akishafika ufukweni, kazi yake inakuwa ni kukusanya Samaki, lakini hao wengine anawatupa, kesho tena anaendelea na uvuvi wake huo huo, anatoa tena vitu kama hivyo. Lakini hilo halimfanyi akate tamaa. Kwasababu Neti/Nyavu yake ndio ilivyotengenezwa, kuvua kila kitu.

Anajua ndio hali halisi ilivyo.

Kuonyesha kuwa na sisi kama wavuvi wa rohoni, tunaowahubiria watu Habari njema ili waokoke, si kazi yetu, kuchunguza chunguza kama huyu ni wa Mungu kweli au sio, ukifanya hivyo, utakata tamaa mapema. Watu mia, utakaowahubiria Kristo, pengine ni kumi tu, wakawa na matokeo unayoyatazamia.

Kinyume chake wengine ndio wanakuwa mwiba kwako, badala ya faraja. Bwana Yesu alipochagua mitume wake, mmoja wao alikuwa mwizi na msaliti, Lakini hiyo haikumaanisha kuwa hakuwa makini katika uchaguzi wake, au alifanya hitilafu. Hapana, neti yake ilikuwa bora kabisa.

Vivyo hivyo na wewe ndugu, ikiwa upo katika kazi ya uvuvi wa watu wa Mungu, basi leweke akilini, hilo, utumishi wa kweli wa Mungu hauchagui, cha kuvua. Si kila utakayemshuhudia, atapokea ujumbe wako, hivyo usikate tamaa ukadhani kuwa kuna dosari katika utumishi wako, hapana, bali, ndivyo uvuvi ulivyo. Endelea kuwashuhudia wengine, ukijua kabisa kati ya mia hutakosa wachache watakaoponyeka. Na hao ndio Samaki.

Bwana alitaka hilo likae katika vichwa vya mitume wake,kabla ya kazi kuanza, ili wasikatishwe tamaa katika shamba la Bwana, pindi wakutanapo na wasivyovitarajia.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Juya ni nini kwenye biblia? (Mathayo 13:47)

TENGENEZA  NYAVU ZAKO, OSHA NYAVU ZAKO.

CHAMBO ILIYO BORA.

Je! Ni kweli kuna samaki mtu (Nguva) Baharini.

Nini maana ya kuokoka katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

TATIZO LA VISIGINO KUUMA KIBIBLIA

Tatizo la visigino kuuma ni ishara ya nini kibiblia?..Au visigino kuwaka moto?.

1) Visigino kuuma.

Kama unafanya shughuli yenye kuhusisha miguu, kwamfano kulima au kutembea umbali mrefu, au michezo..basi ni jambo la kawaida visigino kuuma, au visigino kuwaka moto.

Suluhisho la tatizo hilo ni kupunguza shughuli hizo zinazohusisha miguu, na miguu itarudia hali yake.

Lakini kama huna shughuli zozote unazozifanya na umeenda hospitali na hujapata suluhisho, na hujui sababu, na pengine umeshafanyiwa hata na maombezi, na tatizo bado lipo palepale..

Basi suluhisho la tatizo hilo,linaweza kuwa la kimaandiko,na maandiko yafuatayo yatakufungua…

Yeremia 13:22 “Nawe ukisema moyoni mwako, Mbona mambo haya yamenipata mimi? Ni kwa sababu ya WINGI WA UOVU WAKO, marinda yako yamefunuliwa, na visigino vya miguu yako vimeumia”.

Jiangalie maisha yako ni wapi hapako sawa na Mungu..tubu makosa yako kwa Mungu kwa kumaanisha kuyaacha.

Angalia mahali unapofanyia kazi, au mahali unapoishi, jinsi unavyoenenda, tafakari mawazo ya mioyo yako, je yanampendeza Mungu?..

Je unao upendo?, Wewe ni mvumilivu, ni mtu wa kusamehe au wa vinyongo?, Je ni mtu unayemcha Mungu na kumwogopa?.

Kama sio basi hiyo ndio sababu kwanini visigino vyako vinauma, au vinawaka moto, na umekosa ufumbuzi kila mahali.

Litafakari sana hilo na Mungu akusaidie, yeye ni mwaminifu tukiungama dhambi zetu kwa lengo la kuziacha kabisa, anatusamehe na kuponya magonjwa yetu na majeraha yetu, kwasababu lengo lake sio sisi tuteseke, bali tuwe na furaha na tupate mema, ndio maana saa nyingine anaruhusu vitu fulani vitutokee ili tutubu, na mwishoni atubariki zaidi.

Maran atha!.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

JE TATIZO LA KULA KUCHA NI ISHARA YA KUWA NA MAPEPO?

EE MUNGU, MUNGU WANGU, NITAKUTAFUTA MAPEMA:

TATIZO LA NDANI LINALOWASUMBUA VIJANA, WALIOOKOKA.

WITO WA MUNGU

Kulabu ni nini katika biblia?(2Wafalme 19:27)

Rudi nyumbani

Print this post

FANYA KAMA UONAVYO VEMA.

Moja ya mambo ambayo yanadhoofisha karama, au yanamchelewesha mtu kuifanya kazi ya Mungu, ni tabia ya kusubiria Mungu amwambie jambo Fulani, au Mungu amwoneshe jambo kwanza.

Watu wengi sana leo hii wamekuwa watu wa kungojea ngojea!.. Utamwuliza mtu kwanini huanzi kuifanya  kazi ya Mungu?.. Jibu atakalokupa ni “nangojea wakati wa Bwana” au “Nangoja Bwana aniambie kwanza au anioneshe kwanza”. Na ilihali kashamwamini Yesu na kupokea Roho Mtakatifu.

Leo nataka nikuambie ndugu yangu.. Usiendelee kungoja!!.. Nenda kaanze kumtumikia Bwana, maadamu umeshamwamini Bwana Yesu, na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu, usisubiri maono, wala sauti ikuambie nenda kanitumikie!.. “Hiyo utaingoja sana”.. Anza sasa.

Utauliza nitaanzaje anzaje sasa?

Usiogope, Roho Mtakatifu aliye ndani yako atakufundisha na kukuongoza!.. hutaanza katika ukamilifu wote lakini utaishia katika ukamilifu, kwasababu Roho Mtakatifu yu Pamoja nawe, kukufundisha cha kusema au cha kufanya, anachosubiri kutoka kwako ni wewe tu kuchukua hatua ya kuanza.

Luka 12:11 “Na watakapowapeleka ninyi mbele ya masinagogi na maliwali na wenye mamlaka, msifadhaike kwa kuwaza maneno yenu jinsi mtakavyojibu au kusema;

12 kwa kuwa Roho Mtakatifu atawafundisha saa ile ile yawapasayo kuyasema”.

Hakikisha unamtumikia Mungu tu! Katika Neno lake, hayo mengine mwachie yeye!.

Sasa utazidi kuuliza ni kwa namna gani??..kama sipaswi kungoja kusikia sauti, nitasemaje au nitafanyaje?..

Jibu ni rahisi, kama tayari umeshampokea Roho Mtakatifu, Songa mbele, FANYA KAMA UONAVYO VYEMA!

 1. Kama unaona ni vema wewe kumwimbia Mungu, Basi fanya hivyo kwa bidii.. usisubiri uambiwe au uone maono, au Malaika akutokee.

 2. Kama unaona ni vema wewe kuhubiri, basi anza kufanya hivyo hata kama unajiona huna ujasiri, Bwana atakupa ujasiri pale tu utakapotia nia ya kuanza kuwahubiria watu.

 3. Kama unaona ni vema wewe kuishikilia kazi ya Mungu kwa maombi au michango!, usingoje uwekewe mikono, au Roho Mtakatifu akuambie, wewe fanya na Bwana atakuwa na wewe, na kukupa kibali.

 4. Kama unaona ni vema wewe kuwafundisha Watoto, basi usingoje ngoje, anza kufanya kazi hiyo,. Kwasababu ni Roho Mtakatifu kaliweka hilo ndani yako.

 5. Kama unaona ni vema wewe kuhubiri mitaani, au mitandaoni, usisubiri utokewe na Bwana, wala usiseme ngoje, wakati Fulani ufike ndio uanze!, anza sasa!

 6. Kama unaona vema kuandaa Makala mbali mbali au kuchapisha vitabu vya mahubiria au mafundisho, basi fanya hivyo usingoje ngoje, usizidi kupoteza muda, kwasababu Muda haukungoji wewe. Na mambo mengine yote!, usingoje.. FANYA KAMA UONAVYO VEMA.

Ili tujifunze Zaidi, hebu tuutazame wito wa Mfalme Sauli, jinsi Mungu alivyompaka mafuta, na jinsi alivyoagizwa namna ya kuuongoza ufalme aliopewa!.

Sauli baada ya kupakwa mafuta na nabii Samweli ya kuwa mfalme wa kwanza wa Israeli, alikuwa anajiuliza uliza atawezaje kutawala, atafanyaje fanyaje!. Lakini Nabii Samweli alimpa maneno makubwa sana yaliyompatia Mwanga!.. na maneno hayo ni kwamba.. “BAADA TU YA KUPOKEA ROHO, BASI AFANYE KAMA AONAVYO VEMA”.

Tusome,

1Samweli 10:1 “Ndipo Samweli akatwaa kichupa cha mafuta, akayamimina kichwani pake, akambusu, akasema, Je! Bwana hakukutia mafuta [uwe mkuu juu ya watu wake Israeli? Nawe utamiliki watu wa Bwana, na kuwaokoa na mikono ya adui zao; kisha hii itakuwa ishara kwako ya kuwa Bwana amekutia mafuta] uwe mkuu juu ya urithi wake.

2 Utakapoondoka kwangu leo, utakutana na wanaume wawili karibu na kaburi la Raheli, katika mpaka wa Benyamini huko Selsa; nao watakuambia, Punda hao uliokwenda kuwatafuta wameonekana; na tazama, baba yako ameacha kufikiri habari za punda, anafikiri habari zenu, akisema, Nifanye nini kwa ajili ya mwanangu?

3 Kisha utakwenda mbele kutoka hapo, na kufika kwa mwaloni wa Tabori, na hapo watu watatu watakutana nawe, wanaokwea kumwendea Mungu huko Betheli, mmoja anachukua wana-mbuzi watatu, na mwingine anachukua mikate mitatu, na mwingine anachukua kiriba cha divai;

4 nao watakusalimu na kukupa mikate miwili; nawe utaipokea mikononi mwao.

5 Baada ya hayo utafika Gibea ya Mungu, hapo palipo na ngome ya Wafilisti; kisha itakuwa, utakapofika mjini, utakutana na kundi la manabii wakishuka kutoka mahali pa juu, wenye kinanda, na tari, na kinubi, na filimbi mbele yao, nao watakuwa wakitabiri;

6 na roho ya Bwana itakujilia kwa nguvu, nawe utatabiri pamoja nao, nawe utageuzwa kuwa mtu mwingine.

7 Basi, hapo ishara hizi zitakapokutukia, FANYA KAMA UONAVYO VEMA; KWA KUWA MUNGU YU PAMOJA NAWE”.

Umeona hapo mstari wa 7??.. Samweli hakuendelea kumpa maagizo kwamba, baada ya ishara hizo, aende akatwae jeshi, au aende akatawale watu kwa namna hii au ile, bali alimwambia tu maneno haya machache… “hapo ishara hizi zitakapokutukia, FANYA KAMA UONAVYO VEMA; KWA KUWA MUNGU YU PAMOJA NAWE”.

Maana yake jinsi ya kutawala, afanye jinsi aonavyo, kwasababu Mungu yu Pamoja naye..hataruhusu ajikwae wala akose, atamlinda na mashauri ya adui, hivyo yeye kile kijacho kichwani mwake maadamu ni cha kujenga, basi akifanye asiogope!, asianze kusubiri maono na ishara!.

Hali kadhalika na wewe leo!… Umeshamwamini Bwana Yesu, umeshabatizwa na tena umepokea Roho Mtakatifu.. unachosubiria ni nini???..Ishara ya mwisho ya Roho Mtakatifu imeshatimia juu yako unachosubiri ni nini??...HARAKA SANA FANYA UONAVYO VEMA, KWASABABU ROHO MTAKATIFU HAKUDHARAU.

Lakini kama bado hujampokea Yesu usifanye lolote kwanza!!..kwasababu utaharibu badala ya kujenga!.. Mpokee Yesu kwanza, na ubatizwe kwa ubatizo sahihi wa maji tele (Yohana 3:23), na kwa jina la BWANA YESU KRISTO (Matendo 2:38). Baada ya hapo Roho Mtakatifu ataingia ndani yako na kukuongoza katika kweli yote!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

kwanini Yakobo amefananishwa na mdudu?(Isa 42:14)

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

AHADI YA ROHO ILIYOSALIA SASA KWA KIPINDI CHETU.

YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.

Rudi nyumbani

Print this post

Je Malaika Mikaeli ndiye Yesu mwenyewe?

JIBU: Hakuna mahali popote katika biblia inamtaja Mikaeli kuwa ndiye Bwana Yesu. Kinyume chake, maandiko yanamtofautisha Yesu na Malaika hata kwa asili aliyoitwaa,  Biblia inasema.

Waebrania 2:16 “Maana ni hakika, hatwai asili ya malaika, ila atwaa asili ya mzao wa Ibrahimu”.

Ikiwa na maana, kudhihirishwa kwa Bwana Yesu kwa mara ya kwanza, kulikuwa ni katika asili ya mwanadamu na sio Malaika. Na ndio maana utaona, Malaika nao, walimwona na kumtambua kwa mara ya kwanza, siku ile alipozaliwa katika mwili.

1Timotheo 3:16 “Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu”.

Ni kweli Mikaeli ni mmoja wa Malaika wakuu mbinguni,na pengine Zaidi ya wote, Lakini hana sifa yoyote ya kudhaniwa kuwa yeye ndiye Kristo, kwani  biblia inatuambia kuwa Kristo anaabudiwa sio tu na wanadamu, bali pia na malaika wote mbinguni(Waebrania 1:6), Lakini  hakuna Malaika yoyote anayeabudiwa.

Pia Kristo alikuwa na mamlaka ya kusamehe dhambi, Pamoja na kukemea pepo kwa uweza wake,lakini Malaika (akiwemo Mikaeli), hawana uwezo huo, wanajiona hawastahili mpaka wanasema Bwana mwenyewe na awakemee mashetani (Yuda 1:9)..

Na mwisho biblia inasema, hakuna mahali popote, Mungu alimwita Malaika yoyote “Mwanangu”, bali hao ni watumishi wake, watumikao kuwahudumia watakatifu, lakini kwa Bwana Yesu, Mungu alimwita mwana, kumtofautisha yeye na Malaika zake.

Waebrania 1:5 “Kwa maana alimwambia malaika yupi wakati wo wote, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa? Na tena, Mimi nitakuwa kwake baba, Na yeye atakuwa kwangu mwana?

Hivyo, Mikaaeli ni Malaika wa Bwana na atabakia kuwa hivyo. Lakini ikiwa utatamani kujua Zaidi aina za Malaika wa Mungu, na kazi zao na idadi zao, Fungua hapa >> Je! Kuna malaika wangapi mbinguni?

Swali Je! Unatambua kuwa Mungu ameshawaweka tayari Malaika zake kwa ajili ya mapigo ya siku hizi za mwisho? Una Habari kuwa unyakuo upo karibuni sana kutokea, kuliko unavyoweza kudhani?

Kumbuka paraparanda ya Mungu ikilia leo, basi, Malaika hao wa mapigo, Mungu atawaachilia ulimwenguni mwote, wataipiga dunia kwa kwa zile baragumu saba, na vitasa saba. Wakati huo kutakuwa ni nyakati za shida sana ulimwenguni. Soma Ufunuo 8 &16, ujionee mpendwa. Ni Malaika mahususi wa kuleta mabaya duniani.

Zaburi 78:49 “Akawapelekea ukali wa hasira yake, Ghadhabu, na uchungu, na taabu, Kundi la malaika waletao mabaya”.

Usitamani uwepo wakati huo ndugu yangu, Ni heri leo ukatubu na kumrudia muumba wako. Upokee uhakika wa kuurithi uzima wa milele. Ikiwa utataka kusoma juu ya mapigo hayo, fungua link hii>>

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Neno Saumu lina maana gani katika biblia?

UNYAKUO.

Ninawi ni nchi gani kwasasa?

AINA SABA (7) ZA UNAFIKI, AMBAZO UNAPASWA UJIEPUSHE NAZO.

Rudi nyumbani

Print this post

USICHELEWE KUMPAKA BWANA MARHAMU!

Jina la Bwana, Yesu libarikiwe.

Kuna tofauti ya Marhamu na Manukato, kujua tofauti yake fungua hapa >> Marhamu na manukato ni nini?.

Lakini kwaufupi ni kwamba Marhamu ni pafyumu.

Sasa maandalio ya wayahudi kabla ya kuzika, ilikuwa ni desturi ya kumpaka maiti Marhamu kichwani, kisha Manukato yanafungiwa katika sehemu nyingine ya mwili. Na manukato hayakuwa katika mfumo wa kimiminika.

Lakini tunaona Bwana Yesu alipokufa, Yusufu yule mtu Tajiri Pamoja na Nikodemo waliandaa tu Manukato!, bila Marhamu na kwenda kuyafungia ndani ya mwili wa Bwana Yesu.

Yohana 19:38 “Hata baada ya hayo Yusufu wa Arimathaya, naye ni mwanafunzi wa Yesu, (lakini kwa siri, kwa hofu ya Wayahudi), alimwomba Pilato ruhusa ili auondoe mwili wake Yesu. Na Pilato akampa ruhusa. Basi akaenda, akauondoa mwili wake.

39 Akaenda Nikodemo naye, (yule aliyemwendea usiku hapo kwanza), AKALETA MACHANGANYIKO YA MANEMANE NA UUDI, YAPATA RATLI MIA.

40 Basi wakautwaa mwili wake Yesu, wakaufunga sanda ya kitani pamoja na YALE MANUKATO, kama ilivyo desturi ya Wayahudi katika kuzika”.

Lakini desturi ni kwamba, Maiti lazima apakwe pia Marhamu.. Lakini hapa tunaona hawakufanya hivyo!. Na utaona wale wanawake  walipanga kurudia hilo zoezi la kuupaka uso wa Bwana Marhamu siku ya kwanza ya juma baada ya sabato kuisha!…wangeupaka siku ile ile lakini tayari sabato, ilikuwa imeshaingia na kulingana na desturi za wayahudi, ilikuwa si ruhusa kufanya shughuli yoyote siku ya sabato!, hivyo ikawapasa wasubiri mpaka jumapili asubuhi.

Lakini chaajabu ni kwamba asubuhi walipokwenda wakiwa na Marhamu zao, Pamoja na manukato mengine hawakumkuta Bwana kaburini..Hivyo Marhamu zao zikawa hazina kazi tena!.

Luka 23:54 “Na siku ile ilikuwa siku ya Maandalio, na sabato ikaanza kuingia.

55 Na wale wanawake waliokuja naye toka Galilaya walifuata, wakaliona kaburi, na jinsi mwili wake ulivyowekwa.

56 Wakarudi, wakafanya tayari MANUKATO NA MARHAMU. Na siku ya sabato walistarehe kama ilivyoamriwa.

Luka 24:1 “Hata siku ya kwanza ya juma, ilipoanza kupambazuka, walikwenda kaburini, wakiyaleta manukato waliyoweka tayari.

2 Wakalikuta lile jiwe limevingirishwa mbali na kaburi,

3 Wakaingia, wasiuone mwili wa Bwana Yesu”.

Umeona hapo?.. wenyewe walikuja kwa lengo la kuupaka uso wa Bwana Yesu  marhamu na  mwili wake kuufungia manukato!, lakini hawakumkuta!..walikuwa wamechelewa.. Kumbe nafasi ya kumpaka Marhamu kichwani ilikuwa ni kipindi yupo hai!, si kipindi amekufa kama wafu wengine wanavyofanyiwa..

Na utaona yule mwanamke wa kwanza alipata huo ufunuo, na akawahi kumpaka Bwana Marhamu ya thamani kichwani mwake, na Bwana Yesu akawaambia watu “AMEFANYA VILE KUMWEKA TAYARI KWA MAZIKO YAKE”..Na popote injili itakapohubiriwa.. itahubiriwa kwa kumbukumbu lake!.

Mathayo 26:6 “Naye Yesu alipokuwapo Bethania katika nyumba ya Simoni mkoma,

7 MWANAMKE MWENYE KIBWETA CHA MARHAMU YA THAMANI KUBWA ALIMKARIBIA AKAIMIMINA KICHWANI PAKE ALIPOKETI CHAKULANI.

8 Wanafunzi wake walipoona, wakachukizwa, wakasema, Ni wa nini upotevu huu?

9 Maana marhamu hii ingaliweza kuuzwa kwa fedha nyingi wakapewa maskini.

10 Yesu akatambua akawaambia, Mbona mnamtaabisha mwanamke? Maana ni kazi njema aliyonitendea mimi.

11 Kwa maana siku zote mnao maskini pamoja nanyi; lakini mimi hamnami siku zote.

12 MAANA KWA KUNIMWAGIA MWILI WANGU MARHAMU HIYO, AMETENDA HIVYO ILI KUNIWEKA TAYARI KWA MAZIKO YANGU.

13 Amin, nawaambieni, Kila patakapohubiriwa Injili hii katika ulimwengu wote, tendo hilo alilolitenda huyu litatajwa pia kwa kumbukumbu lake”.

Na kwa heshima yake, utaona Bwana Yesu alipofufuka, vile vitambaa vya sanda vilifunguliwa na kuachwa pale, lakini ile LESO ya kichwani, maandiko yanasema “ilizongwa zongwa pembeni (Yohana 20:7)”.. maana yake ilikunjwa vizuri na kuwekwa pembeni..

Sasa kwanini ikunjwe na kuwekwa pembeni?, ni kuonesha uthamani wa leso ile, kwamba isitupwe, bali iwekwe ije itumike tena!!..kwasababu bado inafaa kwa matumizi, na kufaa huko ni kutokana pia na ile Marhamu yule Mwanamke aliyompaka Bwana siku chache nyuma kabla ya kufa kwake!

Nini tunajifunza hapo?

Kuna wakati unaofaa wa kumfanyia jambo Bwana, na pia upo wakati usiofaa!!.. Ukipata nafasi ya kumtolea Bwana fedha zako, au mali zako, au muda wako.. Mtolee sasa usingoje siku Fulani mbeleni ifike. Huo muda unaoungoja ukifika, utakapokwenda kumfanyia Bwana huduma utakuwa sio muda unaofaa..

Akina Mariamu Magdalene na wenzake, ni kweli walikuwa wana nia nzuri ya kwenda kumpaka Bwana Marhamu lakini walikuwa wamechelewa, Bwana havihitaji tena hivyo vitu kwa wakati huo!!…

Aliwaambia wale watu, “maskini mnao siku zote, lakini mimi hamnami siku zote”.

Ndugu, Watoto wako unao siku zote, ndugu zako wenye shida unao siku zote, Rafiki zako wenye matatizo unao siku zote, lakini kazi ya Bwana haipo kwako siku zote!, mfanyie Bwana kitu leo usingoje kesho.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

LIPI TUNAJIFUNZA KWA WALIOMWONA YESU ALIYEFUFUKA?

LIPI TUNAJIFUNZA KWA WALIOMWONA YESU ALIYEFUFUKA?

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.

Naivera ni nini? Kwanini Daudi aliihitaji alipomtafuta Mungu?

Rudi nyumbani

Print this post

Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

1) Marhamu ni nini?

Marhamu kwa lugha ya kiingereza ni “perfume”..kwa lugha ya kiswahili iliyozoeleka ni “pafyumu”. Pafyumu inatengenezwa kutoka katika mimea mbali mbali na inakuwa katika mfumo wa kimiminika, matumizi yake ni kukifanya kitu kiwe  chenye kutoa harufu nzuri, na kufukuza wadudu na baadhi ya viumbe viharibifu, Viwango na ubora wa pafyumu (marhamu) unatofautiana.

Zipo Marhamu za gharama kubwa, ambazo hazipungui nguvu yake ya harufu haraka! (Mfano wa hizo ndio zile Bwana Yesu alizopakwa kichwani na yule mwanamke, kipindi yupo nyumbani mwa Simoni, mkoma).

Mathayo 26:6 “Naye Yesu alipokuwapo Bethania katika nyumba ya Simoni mkoma,

7 mwanamke mwenye KIBWETA CHA MARHAMU YA thamani kubwa alimkaribia akaimimina kichwani pake alipoketi chakulani.

8 Wanafunzi wake walipoona, wakachukiwa, wakasema, Ni wa nini upotevu huu?

9 Maana marhamu hii ingaliweza kuuzwa kwa fedha nyingi wakapewa maskini”.

Na zile akina Mariamu, Magdalene walizoziandaa kwaajili ya kumpaka Bwana siku ile ya kwanza ya juma

Luka 23:56 “Wakarudi, wakafanya tayari manukato na MARHAMU. Na siku ya sabato walistarehe kama ilivyoamriwa”.

Lakini pia zipo Marhamu za gharama ndogo!, ambazo hazidumu sana katika mwili wa mtu.

Kwa urefu juu ya Marhamu Mwanamke aliyompaka Bwana kichwani na ujumbe wake kiroho unaweza kufungua hapa>> MARHAMU KICHWANI MWA BWANA

2) Manukato ni nini?

Manukato ni viungo ambavyo havipo katika mfumo wa kimiminika, ambavyo vikichomwa, au kupikwa au kuwekwa mahali basi vinatoa harufu Fulani inayovutia, au inayowakilisha jambo Fulani. Mfano wa manukato ni UDI, UVUMBA, na MANEMANE.. Kwasasa kuna maelfu ya aina za Manukato!

Kwa maelezo marefu kuhusu Manukato aina ya UVUMBA, na jinsi wakuhani walivyofukiza uvumba na ujumbe wake kiroho unaweza kufungua hapa >> KUVUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

LIPI TUNAJIFUNZA KWA WALIOMWONA YESU ALIYEFUFUKA?

MUNGU HATAZAMI MOTO WA KIGENI,KUWA MAKINI!

Ratli/ Ratili ni nini katika biblia?

NAMNA YA KUMTAMBUA BIBI ARUSI WA KWELI WA KRISTO.

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

Rudi nyumbani

Print this post

Moabu ni nchi gani kwasasa?

 1) Moabu ni nchi gani kwasasa? 2) Wamoabu walikuwa ni akina nani? 3) Na waamoni walikuwa ni watu gani na wa nchi gani?


1) Moabu ni nchi gani kwasasa?

Moabu ni Mji uliokuwepo maeneo ya nchi ya YORDANI kwasasa. Yordani ni nchi iliyopakana na Nchi ya Israeli kwa upande wa Mashariki.

2) Wamoabu walikuwa ni akina nani?

Asili ya Wamoabu na Waamoni ni kutoka kwa LUTU, aliyekuwa ndugu yake Ibrahimu (Baba wa imani). Mabinti wawili wa Lutu, walilala na Baba yao na kila mmoja kubeba mimba, Watoto hao waliozaliwa mmoja aliitwa MOABU na wa PILI aliitwa AMONI.

Mwanzo 19:30 “Lutu akapanda kutoka Soari akakaa mlimani, na binti zake wawili pamoja naye, kwa sababu aliogopa kukaa katika Soari. Akakaa katika pango, yeye na binti zake wawili.

 31 Yule mkubwa akamwambia mdogo, Baba yetu ni mzee, wala hakuna mtu mume katika nchi atuingilie kama ilivyo desturi ya dunia yote.

32 Haya, na tumnyweshe baba yetu mvinyo, tukalale naye, ili tumhifadhie baba yetu uzao.

 33 Wakamnywesha baba yao mvinyo usiku ule, akaondoka huyo mkubwa akalala naye, wala yeye hana habari alipolala wala alipoondoka.

34 Ikawa siku ya pili, mkubwa akamwambia mdogo, Tazama, nimelala jana na baba yangu, tumnyweshe mvinyo tena usiku huu, ukaingie ukalale naye.

35 Wakamnywesha tena baba yao mvinyo usiku ule, akaondoka mdogo akalala naye, wala yeye hana habari alipolala wala alipoondoka.

36 Basi hao binti wote wawili wa Lutu wakapata mimba kwa baba yao.

37 Yule mkubwa akazaa mwana, akamwita jina lake Moabu; huyo ndiye baba wa Wamoabi, hata leo.

38 Na yule mdogo naye akazaa mwana akamwita jina lake Benami; huyo ndiye baba wa Waamoni hata leo”.

3) Na waamoni walikuwa ni watu gani na wa nchi gani?

Kama tulivyosoma hapo Mwanzo 19:38, kwamba walikuwa ni kutoka uzao wa Lutu.

Taifa la Moabu ni moja ya mataifa yaliyolisumbua sana Taifa la Israeli, hususani katika safari yao ya kutoka Misri, utakumbuka Mfalme wa Moabu alimwajiri BALAAMU MCHAWI ili awalaani Israeli (yaani awaloge!).. lakini mpango huo ulishindikana!.

Bwana hakupendezwa na Taifa hilo, na alililaani.

Kwa maelezo marefu kuhusu Balaamu na uchawi wake unaweza kufungua hapa >> Balaamu mchawi

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

USIJITUMAINISHE JUU YA SIRA YAKO ANGALI UPO KATIKA DHAMBI.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

Ninawi ni nchi gani kwasasa?

Babeli ni nchi gani kwasasa?

KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini Yakobo na Yohana waliitwa “Wana wa Ngurumo”?

Marko 3:16 “Akawaweka wale Thenashara; na Simoni akampa jina la Petro;

17 na Yakobo, mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye Yakobo, akawapa jina la Boanerge, maana yake, wana wa ngurumo”.

Wana wa Zebedayo (yaani Yakobo na Yohana), walipewa jina hilo la Boarnege kwasababu ya ukaribu wao kwa Bwana.

Ikumbukwe kuwa ni wanafunzi watatu tu! Peke,e ndio waliobadilishwa majina na Bwana, na hao ni Petro, Yohana na Yakobo, Ambao biblia inawataja kama NGUZO! (Soma Wagalatia 2:9). Wakati Bwana akienda mlimani kusali hawa nao walikuwa Pamoja naye! (Soma Mathayo 17:1)..hawa walimpenda Bwana sana kuliko wale wanafunzi wengine 9 waliosalia.

Yakobo na Yohana ulifika wakati walikwenda kumwomba Bwana awaketishe mkono wa kuume na wa kushoto katika ufalme wake siku ile.

Mathayo 20:20 “Ndipo mama yao wana wa Zebedayo akamwendea pamoja na wanawe, akamsujudia, na kumwomba neno.

21 Akamwambia, Wataka nini? Akamwambia, Agiza kwamba hawa wanangu wawili waketi mmoja mkono wako wa kuume, na mmoja mkono wako wa kushoto, katika ufalme wako.

22 Yesu akajibu akasema, Hamjui mnaloliomba. Je! Mwaweza kunywea kikombe nitakachonywea mimi? Wakamwambia, Twaweza.

23 Akawaambia, Hakika mtakinywea kikombe changu; lakini kuketi mkono wangu wa kuume na mkono wangu wa kushoto, sina amri kuwapa, bali watapewa waliowekewa tayari na Baba yangu”.

Umeona?

Hivyo hawa wana wa Zebedayo Pamoja na Petro siku zote walikuwa wanatamani kumsogelea Bwana sana, na Bwana aliijua mioyo yao!.

Kutokana na mapenzi hayo kwa Bwana, walikuwa ni watu wasiopenda kuona Bwana anakataliwa mahali popote!.. Utaona Petro, alimkata mtumwa wa kuhani mkuu sikio, kipindi ambacho walikwenda kumkamata Bwana. Halikadhalika Yohana na Yakobo walitaka Bwana ashushe moto kuwaangamiza watu wa Samaria kipindi kile walichomkataa.

Luka 9:51 “Ikawa, siku za kupaa kwake zilipokuwa karibu kutimia, yeye aliukaza uso wake kwenda Yerusalemu;

52 akatuma wajumbe kutangulia mbele ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha Wasamaria, ili kumtengenezea mahali.

53 Lakini wenyeji hawakumkaribisha kwa vile alivyouelekeza uso wake kwenda Yerusalemu.

54 wanafunzi wake YAKOBO NA YOHANA walipoona hayo, walisema, BWANA, WATAKA TUAGIZE MOTO USHUKE KUTOKA MBINGUNI, UWAANGAMIZE; [KAMA ELIYA NAYE ALIVYOFANYA]?

55 Akawageukia, akawakanya. [Akasema, Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo.]

56 Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine”.

Umeona hapo?.. Tabia hiyo ya “kutaka Moto ushuke kutoka mbinguni” ni tabia za KUNGURUMA.. Moto hauwezi kushuka kabla mbingu hazijanguruma, sauti ya Ngurumo ni sauti ya Hukumu iliyokaribu au ya adhabu!.

Hivyo Bwana aliiona tabia hiyo ndani yao, kwamba siku za mbeleni baada ya kuondoka kwake, watakuja kunguruma juu ya kazi zote za shetani, na kuziteketeza!.. kipindi hicho watakuwa hawafanyi vita juu ya damu ya nyama, kama walivyotaka kufanya juu ya hawa watu wa Samaria,(kutaka kuwaua kwa moto) bali wakati huo, watanguruma juu ya kazi zote za shetani katika ulimwengu wa roho na kuzichoma na kuwaacha watu wa Bwana huru!.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

NGURUMO SABA NI NINI?

KAMA VILE UMEME UTOKAVYO MASHARIKI UKAONEKANA HATA MAGHARIBI.

Je kauli ya Bwana Yesu inajichanganya? Katika Yohana 8:14 na Yohana 5:31?

UFUNUO: Mlango wa 1

Maswali na Majibu

Rudi nyumbani

Print this post