Tusome,
Wafilipi 3:1 ‘Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana. Kuwaandikieni mambo yale yale hakuniudhi mimi, bali kutawafaa ninyi. 2 Jihadharini na mbwa, jihadharini na watendao mabaya, jihadharini na WAJIKATAO’’. 3 Maana sisi tu tohara, tumwabuduo Mungu kwa Roho, na kuona fahari juu ya Kristo Yesu, wala hatuutumainii mwili’.
Wafilipi 3:1 ‘Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana. Kuwaandikieni mambo yale yale hakuniudhi mimi, bali kutawafaa ninyi.
2 Jihadharini na mbwa, jihadharini na watendao mabaya, jihadharini na WAJIKATAO’’.
3 Maana sisi tu tohara, tumwabuduo Mungu kwa Roho, na kuona fahari juu ya Kristo Yesu, wala hatuutumainii mwili’.
Watu wanaojikata wanaozungumziwa hapo ni watu wa ‘Tohara’.. Yaani watu wanaofanya tohara, na hao si wengine Zaidi ya wayahudi.. limetumika neno ‘wajikatao’ kufuatia kitendo chenyewe cha Tohara, ambacho kilihusisha KUKATA sehemu ya nyama ya mbele ya viungo vya uzazi vya wanaume..
Wayahudi hawa wajikatao waliwashurutisha watu wa Mataifa, waliomwamini Mwokozi Yesu, kuwa nao pia wanapaswa watahiriwe kama wao, kulingana na Torati. Na kwamba kama hawatatahiriwa basi Mungu hatawakubali. Ikiwa na maana kuwa kigezo cha mtu kukubali wana Mungu ni kufanyiwa tohara ya mwilini.
Jambo ambalo sio kweli kwa kipindi hichi cha agano jipya.. Katika agano jipya, tohara inayokubalika na Mungu si ya mwilini tena, bali ni ya rohoni, katika mioyo yetu, ambayo tohara hiyo ni UBATIZO WA ROHO MTAKATIFU.
Roho Mtakatifu anapokuja ndani yetu, baada ya kumpokea Yesu na kutubu, anachofanya ni kuondoa sehemu ya uovu iliyoongezeka katika roho zetu, kama vile tohara ya mwilini inavyoondoa sehemu ya nyama iliyoongezeka…
Kadhalika Roho Mtakatifu anaondoa kiburi kilichoshikamanika na sisi tangu kuzaliwa, anaondoa uongo ulioshikamanika na sisi tangu kuzaliwa, anaondoa tamaa mbaya, na kila aina ya dhambi.. na kutufanya kuwa kiumbe kipya.
Kwahiyo kama vile katika Agano la kale mtu yeyote ambaye hakutahiriwa katika Mwili hakuwa mtu wa Mungu, kadhalika katika agano jipya mtu yeyote asiyetahiriwa katika roho, (maana yake asiye na Roho Mtakatifu), maandiko yanasema huyo sio wa Mungu.
Warumi 8:9 ‘Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, HUYO SI WAKE’.
Kwahiyo Mtume Paulo, aliwaonya wakristo ambao si wayahudi, kuwa Kutahiriwa katika mwili (yaani kujikata) si tiketi ya kukubaliwa na Mungu, Maana yake yule mtu aliyetahiriwa katika mwili na yule ambaye hajatahiriwa wote mbele za Mungu ni kitu kimoja…
Wagalatia 6:15 ‘Kwa sababu kutahiriwa si kitu, wala kutokutahiriwa, bali kiumbe kipya’.
Warumi 2:29 ‘bali yeye ni Myahudi aliye Myahudi kwa ndani, na tohara ni ya moyo, katika roho, si katika andiko; ambaye sifa yake haitoki kwa wanadamu bali kwa Mungu’.
Hiyo inatufundisha kuwa tujitahidi kwa hali na Mali kuzaliwa mara ya pili, kwasababu Bwana Yesu alisema, mtu yeyote asipozaliwa mara ya pili na kuwa kiumbe kipya hawezi kuuingia ufalme wa mbinguni.
Na kuzaliwa mara ya pili ni kumwamini Yesu, na kubatizwa katika ubatizo sahihi kwa maji mengi na kwa jina la Yesu, na kupokea Roho Mtakatifu.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali. Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Wote wanaokumbwa na mauti sasa ni kutokana na dhambi zao?
JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?
Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?
Mlima wa Mizeituni unaumuhimu gani kwetu?
Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni ipi?
Rudi nyumbani
Print this post
JIBU: Andiko ambalo linaonyesha kutengwa kwa mwanamke anapotokwa na damu au anapokuwa katika siku zake ni hili;
Mambo ya Walawi 15:19-33
[19]Mwanamke ye yote, kama anatokwa na kitu, na kitu chake alichokuwa nacho mwilini mwake ni damu, ataketi katika kutengwa kwake muda wa siku saba; na mtu ye yote atakayemgusa atakuwa najisi hata jioni. [20]Na kitu cho chote akilaliacho katika kutengwa kwake kitakuwa najisi; na kila kitu ambacho akiketia kitakuwa najisi. [21]Mtu ye yote atakayekigusa kitanda chake huyo mwanamke atazifua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa najisi hata jioni. [22]Mtu ye yote atakayekigusa cho chote ambacho huyo mwanamke amekiketia atazifua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa najisi hata jioni. [23]Kwamba ni katika kitanda, au cho chote alichokikalia huyo mwanamke, atakapokigusa kitu hicho, atakuwa najisi hata jioni. [24]Na mtu ye yote atakayelala na mwanamke na unajisi ukawa juu yake, atakuwa najisi muda wa siku saba; na kila kitanda alichokilalia kitakuwa najisi. [25]Na mwanamke kama akitokwa na damu yake siku nyingi, nayo si katika majira ya kutengwa kwake, au kama anatoka damu kuzidi majira ya kutengwa kwake; siku hizo zote za kutoka damu ya unajisi wake, atakuwa kama alivyokuwa katika siku za kutengwa kwake; yeye yu najisi. [26]Kila kitanda akilaliacho katika siku zote za kutoka damu kitakuwa kama kitanda cha kutengwa kwake; na kila kitu atakachokilalia kitakuwa najisi, kama unajisi wa kutengwa kwake. [27]Na mtu ye yote atakayevigusa vitu vile atakuwa najisi, naye atazifua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa najisi hata jioni. [28]Lakini huyo mwanamke kwamba ametakaswa na kule kutoka damu kwake, ndipo atakapojihesabia siku saba, na baadaye atakuwa safi. [29]Siku ya nane atajipatia hua wawili, au makinda mawili ya njiwa, na kumletea kuhani, mlangoni pa hema ya kukutania. [30]Kuhani atamsongeza mmoja kuwa sadaka ya dhambi, na wa pili kuwa sadaka ya kuteketezwa; naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za BWANA, kwa ajili ya kutoka damu ya unajisi kwake. [31]Ni hivi mtakavyowatenga wana wa Israeli na unajisi wao; ili wasife katika unajisi wao, hapo watakapoitia unajisi maskani yangu iliyo katikati yao. [32]Hii ndiyo sheria ya mwenye kisonono, na ya mtu ambaye shahawa yake yamtoka, akawa na unajisi kwa hiyo; [33]na ya mwanamke ambaye yu katika kutengwa kwake, na ya mtu ambaye ana kisonono, kama ni mtu mume, kama ni mtu mke, na ya huyo alalaye na mwanamke mwenye unajisi.
[19]Mwanamke ye yote, kama anatokwa na kitu, na kitu chake alichokuwa nacho mwilini mwake ni damu, ataketi katika kutengwa kwake muda wa siku saba; na mtu ye yote atakayemgusa atakuwa najisi hata jioni.
[20]Na kitu cho chote akilaliacho katika kutengwa kwake kitakuwa najisi; na kila kitu ambacho akiketia kitakuwa najisi.
[21]Mtu ye yote atakayekigusa kitanda chake huyo mwanamke atazifua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa najisi hata jioni.
[22]Mtu ye yote atakayekigusa cho chote ambacho huyo mwanamke amekiketia atazifua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa najisi hata jioni.
[23]Kwamba ni katika kitanda, au cho chote alichokikalia huyo mwanamke, atakapokigusa kitu hicho, atakuwa najisi hata jioni.
[24]Na mtu ye yote atakayelala na mwanamke na unajisi ukawa juu yake, atakuwa najisi muda wa siku saba; na kila kitanda alichokilalia kitakuwa najisi.
[25]Na mwanamke kama akitokwa na damu yake siku nyingi, nayo si katika majira ya kutengwa kwake, au kama anatoka damu kuzidi majira ya kutengwa kwake; siku hizo zote za kutoka damu ya unajisi wake, atakuwa kama alivyokuwa katika siku za kutengwa kwake; yeye yu najisi.
[26]Kila kitanda akilaliacho katika siku zote za kutoka damu kitakuwa kama kitanda cha kutengwa kwake; na kila kitu atakachokilalia kitakuwa najisi, kama unajisi wa kutengwa kwake.
[27]Na mtu ye yote atakayevigusa vitu vile atakuwa najisi, naye atazifua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa najisi hata jioni.
[28]Lakini huyo mwanamke kwamba ametakaswa na kule kutoka damu kwake, ndipo atakapojihesabia siku saba, na baadaye atakuwa safi.
[29]Siku ya nane atajipatia hua wawili, au makinda mawili ya njiwa, na kumletea kuhani, mlangoni pa hema ya kukutania.
[30]Kuhani atamsongeza mmoja kuwa sadaka ya dhambi, na wa pili kuwa sadaka ya kuteketezwa; naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za BWANA, kwa ajili ya kutoka damu ya unajisi kwake.
[31]Ni hivi mtakavyowatenga wana wa Israeli na unajisi wao; ili wasife katika unajisi wao, hapo watakapoitia unajisi maskani yangu iliyo katikati yao.
[32]Hii ndiyo sheria ya mwenye kisonono, na ya mtu ambaye shahawa yake yamtoka, akawa na unajisi kwa hiyo;
[33]na ya mwanamke ambaye yu katika kutengwa kwake, na ya mtu ambaye ana kisonono, kama ni mtu mume, kama ni mtu mke, na ya huyo alalaye na mwanamke mwenye unajisi.
Kumbuka tunapaswa tujue kuwa si kila jambo ambalo lilitendeka agano la kale, linatendeka vilevile hadi wakati wa agano jipya..mambo mengi yalikuwa ni kama kivuli tu kuwasilisha ujumbe wa rohoni kwa agano letu jipya…kwamfano kwenye suala la chakula utaona Bwana alikuja kurekebisha akasema kimwingiacho mtu hakimtii unajisi bali kumtokacho mtu kwasababu kinamtoka moyoni..hivyo chakula kwa namna yoyote hakiwezi kumfanya mtu amkosee Mungu kikilika kwa shukrani..lakini zamani kwamfano wanyama ambao walikuwa hawacheui(yaani hawawezi kurudisha tena chakula wanapokimeza) walijulikana kuwa ni najisi ikifunulia kuwa kwasasa rohoni wapo watu najisi ambao hawana tabia ya kucheua chakula cha kiroho wanacholishwa..yaani hawana muda wa kuyatafakari ya nyuma waliyofundishwa au waliyofanyiwa na Mungu, Au kutendea kazi yale waliofundishwa.
Vivyo hivyo na suala la wanawake katika siku zao kwa kawaida damu kama damu haina shida lakini jiulize kwanini hiyo inayotoka katika viungo vya uzazi ilionekana ina unajisi..Hiyo ni kufunua kuwa uchafu unazoalika kutokana na zinaa ni unajisi mkubwa sana kwa mtu.
Na ndio maana biblia inasema na malazi yawe safi.. (Waebrania 13:4)
Tunapaswa tuitunze miili yetu mbali na uasherati
Lakini haimaanishi kuwa ukitokwa na damu, wewe tayari ni najisi hapana kwasababu lile ni tendo linalokuja lenyewe halipangwi na mwanamke. Hivyo halimtoki rohoni mpaka likamtia mtu unajisi..Mungu alitumia mfano ule tu kuonyesha jinsi mambo yatokayo kule yasivyofaa(katika uzinzi)… Kwahiyo mwanamke akitokwa na damu au asipotokwa na damu hakumzuii yeye kumwomba Mungu wake au kumtumikia madhabahuni pake..
Anachopaswa kufanya ni kujiweka tu katika mazingira ya usafi na uangalifu.
Bwana akubariki.
Mada nyinginezo:
MATARAJIO YA KILA MWANADAMU DUNIANI NI YAPI?
KUNA MAJIRA MUNGU ATAIVURUGA MIPANGO YETU.
UFUNUO: Mlango wa 17
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).
Rudi Nyumbani
Tusome
Matendo 24:5 “Kwa maana tumemwona mtu huyu mkorofi, mwanzilishi wa fitina katika Wayahudi wote duniani, tena ni kichwa cha madhehebu ya Wanazorayo”.
Katika biblia kipindi ambacho Bwana Yesu yupo ulimwenguni, yalikuwepo madhehebu makuu mawili katikati ya wayahudi ambayo ni Mafarisayo na Masadukayo.
Matendo 5:17 “Akaondoka Kuhani Mkuu na wote waliokuwa pamoja naye, (hao ndio walio wa madhehebu ya Masadukayo), wamejaa wivu,”
Tusome pia..
Matendo 15:5 “Lakini baadhi ya madhehebu ya Mafarisayo walioamini wakasimama wakisema, Ni lazima kuwatahiri na kuwaagiza kuishika torati ya Musa”.
Hayo ndiyo madhehebu mawili makuu, na yote yalikuwa yanaamini katika torati ya Musa, tofauti ilikuwa ni katika kuamini kiama..Mafarisayo waliamini kuna ufufuo lakini Masadukayo walikuwa hawaamini hayo.
Lakini baada ya Bwana kuondoka lilizaliwa dhehebu lingine ambalo nalo liliamini katika torati ya Musa, lakini lilienda mbele zaidi kuamini kuwa Yesu aliyetokea Nazareti ndiye Masihi.
Hivyo dhehebu hilo likaitwa dhehebu la Wanazorayo…kufuatia mji wa Nazareti ambao Bwana alilelewa…na yeyote aliyeishi Nazareti aliitwa mnazorayo..
Mathayo 2:23 “akaenda, akakaa katika mji ulioitwa Nazareti; ili litimie neno lililonenwa na manabii, Ataitwa Mnazorayo.”
Ukweli ni kwamba mitume wa Bwana Yesu, hawakuwa wafuasi wa madhehebu yoyote ya kidini yaliyokuwa wakati ule. Wala siku ile ya Pentekoste Roho Mtakatifu hakutua, katika mojawapo ya madhehebu hayo.
Bali alitua juu ya watu waliokuwa wamefanyika wanafunzi wa Bwana Yesu, sio kwa dini bali kwa kusikia na kuyatenda yote aliyoyafundisha. Hata sasa ndivyo Roho Mtakatifu anavyofanya juu ya watu.
Hatui kwenye madhehebu ya kidini, bali kwa watu waliomtii Kristo kwa kutubu dhambi zao.
Je umempokea Yesu maishani mwako na kujazwa Roho Mtakatifu?..kama bado hujampokea ni heri ukafanya hivyo sasa maana muda uliobakia ni mchache sana.
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
KWANINI NI YESU KRISTO WA NAZARETI?
NGUVU YA MNADHIRI WA BWANA.
Kwanini wakristo walipomuona Petro akigonga walisema “Ni malaika wake”?
JE CHANJO YA KORONA NI ALAMA YA MNYAMA?
SWALI: Kwanini wakristo wa kwanza waliposikia kuwa Petro kafunguliwa hawakuamini badala yake walitumia neno “Ni malaika wake”..kwanini wawaze vile au waseme vile?
JIBU: Tusome.
Matendo ya Mitume 12:11-17
[11]Hata Petro alipopata fahamu akasema, Sasa nimejua yakini ya kuwa Bwana amempeleka malaika wake na kunitoa katika mkono wa Herode na katika kutazamia kote kwa taifa la Wayahudi. [12]Na alipokuwa akifikiri haya akafika nyumbani kwa Mariamu, mamaye Yohana, ambaye jina lake la pili ni Marko; na watu wengi walikuwa wamekutana humo wakiomba. [13]Naye alipobisha kilango cha lango, kijakazi, jina lake Roda, akaja kusikiliza. [14]Alipoitambua sauti ya Petro, hakukifungua lango, kwa ajili ya furaha, bali alipiga mbio, akaingia ndani akawaambia kwamba Petro anasimama mbele ya lango. [15]Wakamwambia, Una wazimu. Lakini yeye akakaza sana, akasema ya kwamba ndivyo hivyo. WAKANENA, NI MALAIKA WAKE. [16]Petro akafuliza kugonga, hata walipokwisha kumfungulia wakamwona, wakastaajabu. [17]Naye akawapungia mkono wanyamaze, akawaeleza jinsi Bwana alivyomtoa katika gereza. Akasema, Kampasheni Yakobo na wale ndugu habari hizi. Akaondoka, akaenda mahali pengine.
[11]Hata Petro alipopata fahamu akasema, Sasa nimejua yakini ya kuwa Bwana amempeleka malaika wake na kunitoa katika mkono wa Herode na katika kutazamia kote kwa taifa la Wayahudi.
[12]Na alipokuwa akifikiri haya akafika nyumbani kwa Mariamu, mamaye Yohana, ambaye jina lake la pili ni Marko; na watu wengi walikuwa wamekutana humo wakiomba.
[13]Naye alipobisha kilango cha lango, kijakazi, jina lake Roda, akaja kusikiliza.
[14]Alipoitambua sauti ya Petro, hakukifungua lango, kwa ajili ya furaha, bali alipiga mbio, akaingia ndani akawaambia kwamba Petro anasimama mbele ya lango.
[15]Wakamwambia, Una wazimu. Lakini yeye akakaza sana, akasema ya kwamba ndivyo hivyo. WAKANENA, NI MALAIKA WAKE.
[16]Petro akafuliza kugonga, hata walipokwisha kumfungulia wakamwona, wakastaajabu.
[17]Naye akawapungia mkono wanyamaze, akawaeleza jinsi Bwana alivyomtoa katika gereza. Akasema, Kampasheni Yakobo na wale ndugu habari hizi. Akaondoka, akaenda mahali pengine.
Wayahudi tangu zamani hadi sasa wanaamini kuwa kila mtu anaye malaika mlinzi..Na malaika hawa wanaweza kuja katika maumbile tofauti tofauti..wanaweza kuja kwa sura ya mtu mwingine au kwa sura au sauti ya yule mtu anayemlinda.
Vilevile tunaweza kulithibitisha hilo pia katika maneno ya Bwana aliyoyasema katika (Mathayo 18:10) Kwamba wapo malaika wanaosimama kwa ajili ya watu tangu wakiwa wadogo.
Sasa kulingana na hiyo habari ni kuwa Roda aliposikia sauti ya Petro, .hakuhangaika kuhakikisha kwamba yeye anayegonga ni Petro au la! bali aliamini moja kwa moja na kwenda kutoa taarifa ..Lakini alipowapelekea habari wale waliokuwa ndani haikuwa rahisi kwao kuamini moja kwa moja kama yule angeweza kuwa Petro. Kwasababu kutokana na mazingira Petro aliyofungiwa, ni ngumu kutoka kwani alikamatwa kwa amri ya mfalme, na vilevile alikuwa chini askari 16.
Hivyo jambo ambalo wangeweza kudhani ni kuwa malaika wake ndio amekuja kwa maumbile ya Petro au pengine kwa umbile lingine isipokuwa katumia sauti ya Petro labda kuwafariji au kuwapa taarifa juu ya kifo chake.
Lakini walipoona Petro anazidi kugonga mlango wakaenda kumfungulia, wakathibitisha kuwa kumbe alikuwa ni Petro na sio malaika wake.
Ni nini tunaweza kujifunza katika habari hiyo?
Ni karama ya Mungu kuwatuma malaika zake kutuhudumia.Lakini malaika hawa hawamuhudumii kila mtu tu ilimradi hapana bali ni watakatifu tu..ikiwa na maana kama wewe ni mwovu ujue kinachokulinda ni rehema za Mungu tu ili uendelee kuishi, lakini hakuna huduma yoyote unayoweza kupokea kutoka kwa malaika zake. Kinyume chake ni kuwa mapepo ndio walinzi wako.
Na ndio maana huwezi kuishi maisha ya raha au ya amani hata kama unazopesa zote ulimwenguni..ni kwasababu ufalme wa Mungu haupo wala hautembei pamoja na wewe. Ni heri ukatubu leo ukamkabidhi Yesu maisha yako. Naye atakuokoa na kuuleta ufalme wake wa mbinguni kutembea pamoja na wewe. Hapo ndipo utakapoona tofauti yako ya jana ambayo hukuokoka na leo ambayo umeokoka.
Na wokovu unakuja kwanza kwa kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuziacha na pili ni kwa kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo na kupokea Roho Mtakatifu.
Hivyo kama utapenda kumpokea Kristo leo basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi kwa msaada huo wa kiroho bure. Kumbuka saa ya wokovu ni sasa na wakati uliokubalika ni leo.
+255693036618/ +255789001312
Bwana akubariki
Mada Nyinginezo
HUDUMU YA MALAIKA WATAKATIFU.
IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.
NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.
TUSIRUHUSU MAMBO YA KUSUBIRISHA, YAVURUGE MUDA WETU NA MUNGU.
Mafundisho
Rudi Nyumbani:
SWALI: Nini maana ya kuutia moyo ufahamu? Mtu anatiaje moyo wake ufahamu?
Danieli 10:12 “Ndipo akaniambia, Usiogope, Danieli; kwa maana tangu siku ile ya kwanza ulipotia moyo wako ufahamu, na kujinyenyekeza mbele za Mungu wako, maneno yako yalisikiwa; nami nimekuja kwa ajili ya maneno yako”.
JIBU: Ukisoma kitabu cha Danieli chote utagundua Danieli alikuwa ni mtu ambaye si wa kuchulia mambo juu juu tu..alikuwa ni mtu anayechunguza na kufuatilia mambo baada ya kusikia
Kwa mfano angalia ile ndoto aliyoota Nebukadreza..ndoto ile hakuota Danieli, lakini baadaye alipoona ina maana kubwa alimwomba Mungu ampe kujua zaidi..Na ndio hapo utaona Danieli akifuniliwa kwa undani mkubwa sana mambo yahusianayo na ile ndoto, Juu ya zile Milki nne za ulimwengu. Soma Danieli 2,5,7
Ukisoma tena Danieli sura ya 9 utaona..alipokuwa anasoma vitabu akagundua kuwa kumbe imeshaandikwa na nabii Yeremia kuwa Israeli watakaa Babeli kwa muda wa miaka 70 tu..Hilo jambo lilimshangaza kwasababu hakuwahi kudhani kama Israeli ingekaa utumwani kwa muda mfupi vile. Hivyo hakukaa hivyo hivyo tu..Ndipo akaanza kumlilia Mungu kwa toba..baadaye Mungu akamfunilia jinsi itakavyokuwa mpaka mwisho.
Vivyo hivyo kuna wakati mwingine mbeleni biblia inatuambia Danieli alifunuliwa jambo lingine jipya..japokuwa jambo hilo halijaandikwa katika biblia ni lipi…lakini linaonekana lilikuwa ni la kutisha na ndio maana alisema ni vita vikubwa..Sasa alipofuniliwa kwa muhtasari tu,, kama kawaida yake hakukaa tu hivi hivi..bali aliingia katika maombi ya mfungo na maombolezo kwa muda wa wiki tatu nzima kumsihi Mungu amfunulie..
Tusome..
Danieli 10:1-3,
[1]Katika mwaka wa tatu wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, Danieli, ambaye jina lake aliitwa Belteshaza, alifunuliwa neno; na neno lile lilikuwa kweli; maana ni vita vikubwa; naye akalifahamu neno lile, akaelewa na maono hayo. [2]Katika siku zile mimi, Danieli, nalikuwa nikiomboleza muda wa majuma matatu kamili. [3]Sikula chakula kitamu, wala nyama wala divai haikuingia kinywani mwangu, wala sikujipaka mafuta kabisa, hata majuma matatu kamili yalipotimia”.
[1]Katika mwaka wa tatu wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, Danieli, ambaye jina lake aliitwa Belteshaza, alifunuliwa neno; na neno lile lilikuwa kweli; maana ni vita vikubwa; naye akalifahamu neno lile, akaelewa na maono hayo.
[2]Katika siku zile mimi, Danieli, nalikuwa nikiomboleza muda wa majuma matatu kamili.
[3]Sikula chakula kitamu, wala nyama wala divai haikuingia kinywani mwangu, wala sikujipaka mafuta kabisa, hata majuma matatu kamili yalipotimia”.
Unaona…Sasa tukiendelea kusoma mbeleni ndio tunaona akitokewa na yule malaika. Na kumwambia maneno haya;
Danieli 10:12
[12]Ndipo akaniambia, Usiogope, Danieli; kwa maana tangu siku ile ya kwanza ulipotia moyo wako ufahamu, na kujinyenyekeza mbele za Mungu wako, maneno yako yalisikiwa; nami nimekuja kwa ajili ya maneno yako.
Kumbe kitendo cha Danieli kuzingatia jumbe alizopewa..mbinguni alikuwa anaonekana kama mtu aliyetia moyo wake ufahamu ili kutaka kujua.
Ni nini tunajifunza kwa Danieli?
Hata sasa, Mungu anatafuta watu kama hawa. Ni mara ngapi watu wanamsikia Mungu akizungumza nao kwa njia mbalimbali hususa kwa Neno lake lakini hawataki kutia mioyo yao ufahamu kusikia?.
Na ndio hapo utashangaa mtu anaona kila kitu ni sawa tu. Hajui kuwa ni Mungu anataka kumpigisha hatua nyingine..lakini yeye anaenda kwa desturi na mazoea ..kila siku kanisani ni kusikia tu Neno basi hatii moyo wake ufahamu wa kutaka kusikia sauti ya Mungu inamwambia nini nyuma yake(Maana yake kuwa hatilii maanani).
Na ndio maana hakuna badiliko lolote la maisha yake.
Mungu huwa anataka tutie mioyo yetu ufahamu kwanza ndipo aseme na sisi zaidi au kutuhudumia, kama alivyokuwa akifanya Danieli.
Shalom
KWANINI NI NUHU, AYUBU NA DANIELI?
HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?
TUSIWE WATU WA KUPUNGUKIWA AKILI.
Je! Watu ambao hawajawahi kusikia injili kabisa siku ya mwisho watahukumiwa?
Yohana 9:39 “Yesu akasema, Mimi nimekuja ulimwenguni humu kwa hukumu, ili wao wasioona waone, nao wanaoona wawe vipofu”
Jibu: Ukisoma habari za Bwana Yesu utaona kuwa alikubaliwa na watu wanyonge na wenye dhambi lakini alikataliwa na watu wa Imani na wa dini (yaani Makuhani, waandishi, mafarisayo pamoja na masadukayo)..ambao wao walikuwa wanajiona wenye haki..
Sasa ili tuelewe vizuri hebu tujifunze katika mfano wa kawaida wa maisha.
Mtu anayetembea gizani na tochi yake mkononi, ule mwanga wa tochi akiutumia kumulika mbele yake katika njia anayoiendea utamfanya aone gizani, lakini akiigeuza ile tochi na kuyamulika macho yake, ule mwanga utamuathiri, utamfanya asione..
Ndivyo Mafarisayo na Masadukayo kilichowapata, walikuwa wanaenda kinyume na Nuru na maandiko yanasema Yesu ndiye Nuru ya ulimwengu (Yohana 8:12).Hivyo ile nuru ikawapofusha macho.
Laiti mafarisayo na Masadukayo wangeitumia nuru hiyo kumulika njia zao,wasingekuwa vipofu lakini kwasababu walikuwa wanaenda kinyume na ile Nuru, ikawapofusha macho kama ilivyompofusha Sauli alipokuwa anakwenda Dameski kuwaua watakatifu. (Soma Matendo 9:1-19).
Hiyo inatufundisha kuwa wanyenyekevu na kulitii Neno la Mungu..Tukijiona kuwa tunajua kila kitu au tunajua zaidi ya wengine wote, kama Mafarisayo na Makuhani na wala hatuhitaji kujua zaidi, wala kujifunza zaidi basi tujue tunakwenda kinyume na ile Nuru,Basi tufahamu kuwa Neno la Mungu litatupofusha macho, kama lilivyowapofusha mafarisayo, makuhani na Masadukayo.
1 Wakorintho 8:2 “Mtu akidhani ya kuwa anajua neno, hajui neno lo lote bado, kama impasavyo kujua”
Roho Mtakatifu atusaidie na kutubariki.
Ni nani aliye kipofu, ila mtumishi wangu?
Maherodi walikuwa ni akina nani, Na kazi yao ilikuwa ni ipi?
NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.
Hanithi ni nini katika biblia? (kumbukumbu 23:17)
Shalom tukisoma Mathayo 25:8 na Marko 16:8, tunaona habari mbili zinachanganya, kuhusu wale wanawake, sehemu moja inasema walikwenda kutangaza na sehemu nyingine inasema walikaa kimya hawakumwambia mtu, je ipi ni sahihi?
Jibu: Tusome.
Mathayo 25:5 “Malaika akajibu, akawaambia wale wanawake, Msiogope ninyi; kwa maana najua ya kuwa mnamtafuta Yesu aliyesulibiwa. 6 Hayupo hapa; kwani amefufuka kama alivyosema. Njoni, mpatazame mahali alipolazwa. 7 Nanyi nendeni upesi, mkawaambie wanafunzi wake, Amefufuka katika wafu. Tazama, awatangulia kwenda Galilaya; ndiko mtakakomwona. Haya, nimekwisha waambia. 8 WAKAONDOKA UPESI KUTOKA KABURINI, KWA HOFU NA FURAHA NYINGI, WAKAENDA MBIO KUWAPASHA WANAFUNZI WAKE HABARI”.
Mathayo 25:5 “Malaika akajibu, akawaambia wale wanawake, Msiogope ninyi; kwa maana najua ya kuwa mnamtafuta Yesu aliyesulibiwa.
6 Hayupo hapa; kwani amefufuka kama alivyosema. Njoni, mpatazame mahali alipolazwa.
7 Nanyi nendeni upesi, mkawaambie wanafunzi wake, Amefufuka katika wafu. Tazama, awatangulia kwenda Galilaya; ndiko mtakakomwona. Haya, nimekwisha waambia.
8 WAKAONDOKA UPESI KUTOKA KABURINI, KWA HOFU NA FURAHA NYINGI, WAKAENDA MBIO KUWAPASHA WANAFUNZI WAKE HABARI”.
Tusome tena habari hiyo hiyo katika Marko…
Marko 16:7 “Lakini enendeni zenu, mkawaambie wanafunzi wake, na Petro, ya kwamba awatangulia kwenda Galilaya; huko mtamwona, kama alivyowaambia. 8 Wakatoka nje, wakakimbia kutoka kaburini; KWA MAANA WAMEINGIA TETEMEKO NA USHANGAO; WALA HAWAKUMWAMBIA MTU NENO, MAANA WALIOGOPA”.
Marko 16:7 “Lakini enendeni zenu, mkawaambie wanafunzi wake, na Petro, ya kwamba awatangulia kwenda Galilaya; huko mtamwona, kama alivyowaambia.
8 Wakatoka nje, wakakimbia kutoka kaburini; KWA MAANA WAMEINGIA TETEMEKO NA USHANGAO; WALA HAWAKUMWAMBIA MTU NENO, MAANA WALIOGOPA”.
Hapo tunasona habari mbili zinazoelezea tukio moja, lakini ni kama vile habari hizo zinajichanganya, kwamba iweje Mathayo aseme ”wanawake walikwenda kuwapasha wanafunzi habari” na Marko aseme “hawakumwambia mtu neno”.. Swali ni je! Biblia inajichanganya?.
Jibu ni la! Biblia haijichanganyi hata sehemu moja, isipokuwa ni fahamu zetu ndizo zinazojichangaya…
Awali ya yote ikumbukwe kuwa kifo cha Bwana Yesu, kilihusisha Dini na vile vile kilihusisha Serikali. Kwa maana ya kuwa viongozi wa dini (yaani Makuhani na Waandishi) walimshitaki Bwana kwa Serikali(ambayo ilikuwa ni serikali ya kirumi), na Serikali hiyo ndiyo iliyomsulubisha Bwana Yesu. Na baada ya Bwana Yesu kufa kaburi lake liliwekewa walinzi kulilinda!. Lengo ni ili wanafunzi wake wasije wakamwiba na kusingizia kafufuka.
Hivyo kulikuwa na hofu kubwa sana, kwa mtu yeyote ambaye angezusha kuwa Kristo kafufuka!. Kwasababu Serikali ya kirumi ndio iliyokuwa inatawala, na ilikuwa ni serikali ya kikatili, endapo kingezushwa kitu chochote kilicho kinyume na itikadi zao au taratibu zao, sheria ilikuwa ni moja tu! Nayo ni Kifo.
Kwahiyo hata hawa wanawake ambao walitokewa na Malaika na kuwaambia kwamba Bwana kafufuka, wao waliamini, lakini haikuwa vyepesi kwenda kutangaza kwa watu wa nje!. Huko na huko kama Yule mwanamke Msamaria alivyofanya… Isipokuwa kwa watu wachache tu! Wenye imani moja na wao, ambao ndio wakina Petro na mitume wa Yesu.. Hao ndio wanawake waliwapelekea habari za kufufuka kwa Yesu, lakini watu wengine wa nje, kama Mafarisayo au masadukayo, maakida, au ndugu zao ambao hawakumwamini Bwana hawakuwapa taarifa zozote, zilibaki kuwa siri, ndio maana maandiko yanasema hapo hawakusema Neno kwa mtu yeyote.
Kwasababu hata katika hali ya kawaida, Mariamu Magdalena ataogopa vipi kumwambia Petro kwamba Bwana kafufuka?.. Kwani Petro angewafanya nini hao wanawake baada ya kupewa taarifa hizo?, angewapiga? Au angewashitaki kwa Herode?, bila shaka hilo ni jambo ambalo haliwezekani, kwasababu wote hao walikuwa upande mmoja, na tumaini lao ni moja..
Haiwezekani kuogopa kuambiana mambo yaliyojiri kumhusu Bwana wao… isipokuwa kwa watu wa nje, itabaki kuwa siri na fumbo.. ndio maana hata huyo Malaika hakuwaambia wakatangaze habari hizo kwa kila mtu tu!, bali kwa wanafunzi wa Yesu peke yao.
Hivyo hawa wanawake waliificha Siri kwa watu wa nje lakini waliiweka wazi kwa wanafunzi wa Yesu, kama maandiko yanavyosema hapo kwenye Mathayo.
Na hawakuwaambia watu wa nje kwasababu waliogopa!, aidha kuuawa, au kupitia dhiki fulani, kwasababu makuhani na maakida wangewasumbua kuwahoji ni wapi walipomficha..Ndio maana utaona sehemu zote baada ya kufufuka kwa Bwana, mitume pamoja na wanawake hawa, walikuwa wanajificha ndani na kujifungia kutokana na hofu ya kukamatwa, unaweza kuyathibitisha hayo katika mistari hii> Yohana 20:19, Yohana 20:26 na Matendo 2:1
Ni lipi tunaloweza kujifunza?
Kama kufufuka kwake Bwana Yesu kulivyokuwa kwa siri, kiasi kwamba ni watu wachache sana ndio waliojua na kuthibitisha kwamba Bwana kafufuka, wengine wote hawakujua chochote, Herode na Pilato hawakutokewa na Bwana wala malaika, hivyo hawakujua chochote, vile vile na watu wengine hawakutokewa na Bwana wala Malaika wake kuwajuza kuwa kafufuka, maandiko yanasema watu 500 tu ndio waliotokewa na Bwana baada ya kufufuka kwake kati ya Mamilioni waliokuwa wanaishi duniani,siku hizo..
Ndivyo itakavyokuwa katika siku ya unyakuo.. Itakuwa ni tendo la ghafla na la siri!. Siku parapanda ya mwisho itakapolia, kundi la watu wachache sana duniani litaondoka na kwenda mbinguni, na wengine wote hawatajua kitu…Hivyo hatuna budi kusimama imara katika Imani, ili siku hiyo ya unyakuo itakapofika tusiukose.
Marana atha
TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI:
MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.
KIKWAZO CHA EUODIA NA SINTIKE.
NAMNA YA KUMTAMBUA BIBI ARUSI WA KWELI WA KRISTO.
SWALI: Paulo alimaanisha nini kusema…”Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia;?
1Wakorintho 14:14 “Maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda. 15 Imekuwaje, basi? Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia; mtaimba kwa roho, tena nitaimba kwa akili pia”.
1Wakorintho 14:14 “Maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda.
15 Imekuwaje, basi? Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia; mtaimba kwa roho, tena nitaimba kwa akili pia”.
JIBU: Hapa mtume Paulo alikuwa anaondoa mkanganyiko uliokuwa unaendelea katika kanisa kuhusiana na karama za rohoni, hususani karama ya lugha. Na mkanganyiko huu unaendelea hata sasa katika kanisa la Mungu.
Lakini kabla ya kufahamu mtume Paulo alikuwa anamaanisha nini hasaa hapo, ni vizuri tukajua jinsi hii karama inavyofanya kazi. Lugha zinazozungumziwa katika maandiko, ambazo Roho Mtakatifu anazishusha juu ya mtu kwa jinsi apendavyo yeye, zimegawanyika katika makundi mawili.
Kundi la kwanza: Ni lugha za kibinadamu. Mfano kichini, Kiswahili, kimasai n.k.
Kundi la Pili: Ni Lugha za malaika. Hizi hazijulikani na wanadamu,.
Sasa lengo kuu la hizi lugha ni kama zifuatavyo:
Mtu yeyote akimwomba Mungu ampe kunena kwa lugha, atapewa, (1Wakorintho 14:5).. Lakini pia haiwezi kuwa wakati wote, au ikaja kwa wepesi kama vile mtu yule aliyejaliwa karama hii na Mungu. Mtu aliyepewa karama hii, inakuwa ni rahisi sana kwake kunena, hususani pale anapoanza tu kuomba, hatumii nguvu nyingi, anashangaa ulimi wenyewe unaanza kuzungumza lugha nyingine gheni. Sasa kwa mtu kama huyu anapaswa kujua hiyo ni sehemu ya karama yake, na hivyo anapaswa aelewe ni nini anatakiwa afanye baada ya pale ili karama hiyo iwe ina manufaa kwa ajili ya kanisa la Mungu.
Sasa, jambo ambalo watu wengi hawajui ni kuwa hizi lugha zinaposhushwa ndani ya mtu, kwa kipindi cha mwanzoni, huwa haziji na tafsiri yoyote, zinakuwa ni kwa ajili ya yule mtu tu husika (mnenaji), na sio kwa kanisa, hapo ndipo utaona mtu anaweza kunena kwa lugha usiku kucha. Lakini kusiwe na kitu chochote unachokielewa yeye, au yule mwingine anayesikia.
Lakini baadaye kama ataichochea karama yake, kwa kumwomba Mungu, amjalie na tafsiri, ndio inapokuja na tafsiri ndani yake. Na hiyo inakuwa ni kwa faida ya kanisa la Kristo. Hivyo mtu ambaye karama yake inatenda kazi ni yule ambaye akinena katika kanisa, basi na Mungu anamfunulia tafsiri ya maneno yale aliyoyanena, kisha analiambia kanisa.. Na kanisa linajengwa, kwasababu hiyo.
Sasa tukirudi katika jambo ambalo Paulo alilisema.. kuhusiana na upungufu wa maarifa kuhusu karama hizi, ni kwamba watu walikuwa wananena kwa lugha mbele ya kanisa, lakini hakuna tafsiri yoyote ile. Ndipo hapo mtume Paulo akasema, Je! Yule anayesikia, ataelewaje?si atakuona wewe ni mwendawazimu? Akaongezea kusema, kama hutakuwa na tafsiri ya lugha hiyo, basi ni heri ukae kimya uombe kivyako vyako. Kuliko kusimama mbele ya kanisa na huku unatoa lugha ambazo hazieleweki kwa wasikiaji.
Ndipo hapo akasema..
Imekuwaje, basi? Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia; mtaimba kwa roho, tena nitaimba kwa akili pia..
Yaani, nitaomba kwa lugha, halafu wakati huo huo ninaomba kwa akili zangu, na sio tena tafsiri ya ile lugha niliyoizungumza bali maneno yangu mengine ya sikuzote.. kwamfano, mtu aanze kuzungumza kiharabu katikati ya mahubiri, bila kutolea tafsiri yoyote halafu anaendelea kuzungumza Kiswahili chake..wewe kama msikiaji utaelewa nini hapo?..
Ndicho kinachoendelea leo hii, mtu atasema ananena kwa lugha, anapohubiri, lakini hatoi tafsiri ya kile anachokisema, anaendelea na maneno yake ya Kiswahili. Katika mazingira kama hayo, wewe msikiaje unajengekaje?
Vilevile Roho Mtakatifu atakujalia kuimba hata wimbo katika lugha nyingine ya rohoni, halafu hutoi tafsiri yake, Je! Msikaji atajengekaje?
Naamini, kama na wewe ni mmojawapo mwenye karama hii, utafanya marekebisho katika hilo. Na kama umekuwa ukinena tu, huoni tafsiri, basi unawajibu wa kumwomba Mungu kwa bidi akupe na tafsiri, pindi uwapo mbele ya kanisa lake. Kwa msingi huu sasa, naomba upitie vifungu hivi hapa chini, ili uelewe Zaidi.
1Wakorintho 14:10 “Yamkini ziko sauti za namna nyingi duniani, wala hakuna moja isiyo na maana. 11 Basi nisipoijua maana ya ile sauti nitakuwa kama mjinga kwake yeye anenaye; naye anenaye atakuwa mjinga kwangu. 12 Vivyo hivyo na ninyi, kwa kuwa mnatamani sana kuwa watu wenye karama za roho, takeni kwamba mzidi sana kuwa nazo ili kulijenga kanisa. 13 KWA SABABU HIYO YEYE ANENAYE KWA LUGHA NA AOMBE APEWE KUFASIRI. 14 Maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda. 15 Imekuwaje, basi? NITAOMBA KWA ROHO, TENA NITAOMBA KWA AKILI PIA; MTAIMBA KWA ROHO, TENA NITAIMBA KWA AKILI PIA. 16 Kwa maana wewe ukibariki kwa roho, yeye aketiye katika mahali pa mjinga ataitikaje, Amina, baada ya kushukuru kwako, akiwa hayajui usemayo? 17 Maana ni kweli, wewe washukuru vema, bali yule mwingine hajengwi. 18 Namshukuru Mungu ya kuwa nanena kwa lugha zaidi ya ninyi nyote; 19 lakini katika kanisa napenda kunena maneno matano kwa akili zangu, nipate kuwafundisha wengine, zaidi ya kunena maneno kumi elfu kwa lugha. 20 Ndugu zangu, msiwe watoto katika akili zenu; lakini katika uovu mgeuzwe watoto wachanga, bali katika akili zenu mkawe watu wazima. 21 Imeandikwa katika torati, Nitasema na watu hawa kwa watu wa lugha nyingine, na kwa midomo ya wageni, wala hata hivyo hawatanisikia, asema Bwana. 22 Basi, hizi lugha ni ishara, si kwao waaminio, bali kwao wasioamini lakini kuhutubu si kwa ajili yao wasioamini, bali kwa ajili yao waaminio”.
1Wakorintho 14:10 “Yamkini ziko sauti za namna nyingi duniani, wala hakuna moja isiyo na maana.
11 Basi nisipoijua maana ya ile sauti nitakuwa kama mjinga kwake yeye anenaye; naye anenaye atakuwa mjinga kwangu.
12 Vivyo hivyo na ninyi, kwa kuwa mnatamani sana kuwa watu wenye karama za roho, takeni kwamba mzidi sana kuwa nazo ili kulijenga kanisa.
13 KWA SABABU HIYO YEYE ANENAYE KWA LUGHA NA AOMBE APEWE KUFASIRI.
14 Maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda.
15 Imekuwaje, basi? NITAOMBA KWA ROHO, TENA NITAOMBA KWA AKILI PIA; MTAIMBA KWA ROHO, TENA NITAIMBA KWA AKILI PIA.
16 Kwa maana wewe ukibariki kwa roho, yeye aketiye katika mahali pa mjinga ataitikaje, Amina, baada ya kushukuru kwako, akiwa hayajui usemayo?
17 Maana ni kweli, wewe washukuru vema, bali yule mwingine hajengwi.
18 Namshukuru Mungu ya kuwa nanena kwa lugha zaidi ya ninyi nyote;
19 lakini katika kanisa napenda kunena maneno matano kwa akili zangu, nipate kuwafundisha wengine, zaidi ya kunena maneno kumi elfu kwa lugha.
20 Ndugu zangu, msiwe watoto katika akili zenu; lakini katika uovu mgeuzwe watoto wachanga, bali katika akili zenu mkawe watu wazima.
21 Imeandikwa katika torati, Nitasema na watu hawa kwa watu wa lugha nyingine, na kwa midomo ya wageni, wala hata hivyo hawatanisikia, asema Bwana.
22 Basi, hizi lugha ni ishara, si kwao waaminio, bali kwao wasioamini lakini kuhutubu si kwa ajili yao wasioamini, bali kwa ajili yao waaminio”.
FAHAMU TAFSIRI ZA NDOTO MBALIMBALI.
Nini maana ya “wazimu” katika biblia?
NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.
USINIE MAKUU.
Jina kuu la Bwana na Mwokozi wetu na wa ulimwengu, Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze Neno la Mungu ambalo ndio taa iongozayo miguu yetu na mwanga wa njia yetu. (Zab 119:105).
Je unafanya kazi yoyote ya mikono?, ya kujiajiri au kuajiriwa?.. labda una shamba, au mifugo, au biashara, ambayo katika hiyo unategemea kukuingizia kipato?…
Je unayo shughuli ambayo ghafla umeshangaa mambo yameharibika!, yameenda kombo!..wakati mwingine unaweza kujiuliza ni nini chanzo, na ukashinda kujua..Leo nataka uone sababu ya mambo hayo kupitia maandiko?
Kama upo ndani ya Kristo, umesimama vizuri na ni mwaminifu kwa Bwana na mambo yamekuharibikia ghafla!, tambua kuwa chanzo ni kama kile kile cha Ayubu na wala si kingine..
Kwamba Shetani amekwenda kukushitaki mbele za Bwana, kwasababu ya haki yako, na hivyo Bwana akamruhusu aiharibu kazi yako,.. Na majaribu hayo mwisho wake ni mzuri, kwasababu ukiisha kuyashinda basi Bwana atakunyanyua mara dufu.. Ni majaribu ya kuwavusha watu wa Mungu kutoka hatua moja hadi nyingine.
Lakini kama upo nje ya Kristo (Yaani hujampokea Yesu na kumwamini, na kubatizwa, na kuishi maisha ya utakatifu yanayompendeza yeye), na ghafla umeona mambo yako yameharibika, kwa uharibifu usio wa kawaida..nataka nikuambie kuwa jambo ni lile lile lililomtokea Ayubu limekutokea na wewe, isipokuwa katika pande tofauti.
Ni kwamba shetani, au mapepo yake yamekwenda mbele za Mungu na kukushitaki na hivyo kupewa ruhusa ya kuja kuharibu kazi yako, au biashara yako au mifugo yako..na mwisho wa uharibifu huo ni mbaya kwasababu hauna tumaini la kuvipata tena vile ulivyopoteza.
Sasa hebu tusome habari moja katika biblia ambayo hiyo itatusaidia kuelewa vizuri.. tumsome mtu mmoja tajiri, ambaye alikuwa na biashara yake kubwa ya mifugo lakini iliharibika ghafla na wala hakupata kurejeshewa..
Marko 5:6 “Na alipomwona Yesu kwa mbali, alipiga mbio, akamsujudia; 7 akapiga kelele kwa sauti kuu, akasema, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu? Nakuapisha kwa Mungu usinitese. 8 Kwa sababu amemwambia, Ewe pepo mchafu, mtoke mtu huyu. 9 Akamwuliza, Jina lako nani? Akamjibu, Jina langu ni Legioni, kwa kuwa tu wengi. 10 Akamsihi sana asiwapeleke nje ya nchi ile. 11 NA HAPO MILIMANI PALIKUWA NA KUNDI KUBWA LA NGURUWE, WAKILISHA. 12 PEPO WOTE WAKAMSIHI, WAKISEMA, TUPELEKE KATIKA NGURUWE, TUPATE KUWAINGIA WAO. 13 AKAWAPA RUHUSA. WALE PEPO WACHAFU WAKATOKA, WAKAINGIA KATIKA WALE NGURUWE; NALO KUNDI LOTE LIKATELEMKA KWA KASI GENGENI, WAKAINGIA BAHARINI, WAPATA ELFU MBILI; WAKAFA BAHARINI. 14 Wachungaji wao wakakimbia, wakaieneza habari mjini na mashambani. Watu wakatoka walione lililotokea”.
Marko 5:6 “Na alipomwona Yesu kwa mbali, alipiga mbio, akamsujudia;
7 akapiga kelele kwa sauti kuu, akasema, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu? Nakuapisha kwa Mungu usinitese.
8 Kwa sababu amemwambia, Ewe pepo mchafu, mtoke mtu huyu.
9 Akamwuliza, Jina lako nani? Akamjibu, Jina langu ni Legioni, kwa kuwa tu wengi.
10 Akamsihi sana asiwapeleke nje ya nchi ile.
11 NA HAPO MILIMANI PALIKUWA NA KUNDI KUBWA LA NGURUWE, WAKILISHA.
12 PEPO WOTE WAKAMSIHI, WAKISEMA, TUPELEKE KATIKA NGURUWE, TUPATE KUWAINGIA WAO.
13 AKAWAPA RUHUSA. WALE PEPO WACHAFU WAKATOKA, WAKAINGIA KATIKA WALE NGURUWE; NALO KUNDI LOTE LIKATELEMKA KWA KASI GENGENI, WAKAINGIA BAHARINI, WAPATA ELFU MBILI; WAKAFA BAHARINI.
14 Wachungaji wao wakakimbia, wakaieneza habari mjini na mashambani. Watu wakatoka walione lililotokea”.
Umeona hapo?.. huyu mtu pengine alikuwa tajiri sana mwenye nguruwe wengi (biblia inasema walikuwa nguruwe elfu 2), na akaajiri wachungaji wakawachunge kondoo wale milimani.. Na siku hiyo ghafla anakuja kuletewa taarifa kuwa nguruwe wake wote elfu mbili wamekimbilia baharini na wamekufa huko.
Bila shaka kwa haraka haraka angeweza kusema ni uchawi, au ana gundu!.. Lakini kumbe kuna jambo lililokuwa linaendelea katika roho juu yake na mali zake bila yeye kujua. Kwamba mapepo yalikwenda kwanza mbele za Bwana Yesu kuomba ruhusa yaingie kwenye kitega uchumi chake, ili yaiharibu kazi yake! Na Bwana Yesu akayapa ruhusa na wala hakuyakataza..
Kama vile tu!, shetani alivyokwenda mbele za Bwana kuomba ruhusa aharibu mifugo ya Ayubu, na Mungu akampa ruhusa wala hakumkataza.(Ayubu 1:9-12). Ndicho kilichomtokea huyu mtu mwenye nguruwe Elfu 2.
Lakini cha ajabu ni kwamba hatusomi tena habari za huyo tajiri aliyepoteza nguruwe wake, (hao elfu mbili kwa siku moja) kwamba alikuja kuwapata tena.. maana yake ni kwamba hakuja kuwapata tena.. kama ilivyokuwa kwa Ayubu.. Ayubu yeye alipopoteza mifugo yake maandiko yanasema alikuja kupata mara dufu.. Lakini huyu tajiri wa nguruwe hakuna chochote alichoambulia..zaidi ya kupata hasara tu!
Na kinachoshangaza zaidi ni kwamba hata Bwana hakumhurumia wala hakusikitika, yeye kupoteza nguruwe wote wali, Zaidi ya yote aliruhusu mapepo yaingie nguruwe wake.
Sasa ni kwasababu gani hatusomi ushuhuda wowote wa huyu tajiri kuja kupata tena alichokipoteza kama Ayubu?.. Jibu ni rahisi, ni kwasababu hakuwa ndani ya wokovu kama aliokuwa nao Ayubu.. hakutubu!, wala hakumwamini Yesu kabla wala baada ya hapo.. Zaidi ya yote maandiko yanasema wakuu wa miji pengine na yeye akiwemo miongoni mwao, walimfukuza Bwana Yesu atoke katika mipaka yao.
Ndugu unayesoma ujumbe huu, jitafakari je!, hiyo kazi unayoifanya ina usalama kiasi gani?..je upo ndani ya Kristo au nje!.. Unaweza kufikiri mali zako zitakusaidia, au mifugo yako..lakini nataka nikuambie mapepo kila siku yanazitaja hizo mali zako mbele za Mungu.. Na cha kuogopesha ni kwamba Mungu anaweza kuyaruhusu yazichukue au waziue ndani ya siku moja..
Kwasababu kama aliruhusu kwa mtumishi wake Ayubu, ambaye alikuwa mkamilifu mbele zake, wewe na mimi ambaye pengine si wakamilifu mbele zake ni wakina nani, Mungu asiruhusu mabaya hayo?
Jiulize je!, siku ya uharibifu itakapokuja ghafla kama ilivyokuja kwa huyu Tajiri wa nguruwe na Ayubu, utakuwa wapi?.. utakuwa na tumaini kama Ayubu au utapotea moja kwa moja kama huyu Tajiri.
Kama bado hujampokea Yesu, ni vyema ukampokea sasahivi, kwa usalama wa Roho yako na watoto wako, na mali zako na mifugo yako. Kwani usipofanya hivyo kuna hatari ya kukosa tumaini katika siku za kujaribiwa.
Kwanini Bwana aliwalenga mbwa na nguruwe tu katika Mathayo 7:6?
Nini maana ya “kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi?”
KWANINI MIMI?
WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.
Katika Mathayo 9:2 tunasoma Bwana anamwita “Mkuu” Yule mtu aliyepooza ?.. Je ni sahihi na sisi kuitana wakuu?
Jibu: Tusome,
Mathayo 9:2 “Na tazama, wakamletea mtu mwenye kupooza, amelala kitandani; naye Yesu, alipoiona imani yao, ALIMWAMBIA YULE MWENYE KUPOOZA, JIPE MOYO MKUU, MWANANGU, umesamehewa dhambi zako”.
Hapo ukisoma vizuri utaona Bwana hakumwita Yule mtu “Mkuu”.. Bali alimaanisha “ajipe Moyo Mkuu” yaani “moyo ulio mkuu”. Kwahiyo ni moyo mkuu ndio uliotajwa hapo, na si Mkuu kama mtu. Kristo hana Mkuu juu yake zaidi ya Baba, hivyo hawezi kumwita mtu yeyote duniani Mkuu, zaidi sana anatuita sisi WANAWE, kama mwishoni hapo alipomalizia.. “jipe moyo mkuu, MWANANGU, umesamehewa dhambi zako”
Kadhalika biblia haijaruhusu sisi kwa sisi kuitana “Wakuu”, kwasababu aliye Mkuu wetu sisi sote ni mmoja tu naye ni Kristo, (Soma Matendo 3:15 na Ufunuo 1:5). Sisi tukiitana majina yetu kama ndugu inatosha!..Vyeo vingine vya juu zaidi ya hivyo vinamhusu Bwana wetu Yesu peke yake (Mathayo 23:8-11).
Sasa hivi upo mtindo wa sisi kwa sisi kuitana “wakuu”, utaona mtu atazungumza maneno mawili matatu na mwenzie na katikati atataja neno “mkuu” kama kionjo cha kumpandisha hadhi Yule anayezungumza naye. Si sawa kufanya hivyo!.. Ni mtindo ambao chanzo chake ni kutoka kwa Yule adui yetu shetani.
Lakini pamoja na hayo, tunaweza kujifunza kitu kupitia hiyo habari!.. Bwana alimwambia Yule aliyepooza kwamba “jipe moyo mkuu ” na si “ajipe tu moyo”..bali “moyo mkuu”.. Maana yake tunapokuwa katika dhiki fulani, au tatizo fulani, au ugonjwa fulani.. Hatuna budi kujipa moyo mkuu wenyewe!.. Maana yake hatupaswi kukata tamaa.. Tunapaswa kuamini mpaka mwisho, ili tupokee uponyaji wetu, au Baraka zetu. Kama ni kuomba tunapaswa tuendelee kuomba kwa Moyo Mkuu, kama kutafuta tunapaswa tuendelee kutafuta kwa Moyo Mkuu, mpaka tukipate. Lakini tunapokata tamaa kirahisi ni ngumu kupokea au kupata kile tulichokuwa tunakitafuta.
Bwana atubariki.
Kwanini ndugu wanaokaa pamoja wawe kama mafuta ya Haruni?
Nini tofauti kati ya moyo na roho?
SHETANI ANAPOKUINGIA, ANATIA MOYO MGENI NDANI YAKO.
Je kualikwa kwenye sherehe za watu ambao si wakristo ni dhambi?
JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.
MPAKA UTIMILIFU WA MATAIFA UTAKAPOWASILI.