Swali: Kwanini Petro na Paulo walishindana na pia tunajifunza nini katika kushindana kwao?.
Jibu: Tusome,
Wagalatia 2:11 “Lakini Kefa alipokuja Antiokia, nalishindana naye uso kwa uso, kwa sababu alistahili hukumu”
Kushindana kunakozungumziwa hapo si kushindana kwa maneno ya dini kule kunakozungumziwa katika 1Timotheo 6:4, 2Timitheo 2:14 na Wafilipi 2:14, kwamba tutende mambo yote pasipo mashindano wala manung’uniko.
Wala si mashindano ya Imani, yale yanayozungumziwa katika Wafilipi 1:30 na Waebrania 12:1 ambayo tunapaswa tuwe nayo, (yaani kushindana dhidi ya nguvu za giza na kuishikilia imani).
Bali neno “mashindano” kama lilivyotumiwa hapo na Paulo lilimaanisha “kukabiliana”. Maana yake Paulo alipofika Antiokia na kukutana na Petro alikabiliana naye uso kwa uso na kumwonya kuhusiana na tabia aliyoonesha ya uvuguvugu juu ya desturi za wayahudi katika kula.
Maana yake Petro alipokuwa ameketi na wayahudi aliungana nao kwa kutokula vyakula vilivyo najisi kwa hofu ya wayahudi…lakini mahali alipoketi katika chakula pamoja na watu wa mataifa, alishirikiana nao katika vyakula hivyo vilivyo najisi kwa wayahudi.
Sasa tabia hiyo haikuwa sawa, ndipo Paulo alipoona na kumkabili na kumwambia dhahiri kuwa anachokifanya sio sawa.
Wagalatia 2:11 “Lakini Kefa alipokuja Antiokia, nalishindana naye uso kwa uso, kwa sababu alistahili hukumu
12 Kwa maana kabla hawajaja watu kadha wa kadha waliotoka kwa Yakobo, alikuwa akila pamoja na watu wa Mataifa; lakini walipokuja wao, akarudi nyuma akajitenga, huku akiwaogopa waliotahiriwa.
13 Na hao Wayahudi wengine wakajigeuza pamoja naye, hata na Barnaba pia akachukuliwa na unafiki wao.
14 Walakini, nilipoona ya kuwa njia yao haiendi sawasawa na ile kweli ya Injili, nalimwambia Kefa mbele ya wote, Ikiwa wewe uliye Myahudi wafuata desturi za Mataifa, wala si za Wayahudi, kwa nini unawashurutisha Mataifa kufuata desturi za Wayahudi?”.
Tunachoweza kujifunza kwa Paulo ni ujasiri wa kusimama kuitangaza kweli pasipo kujali cheo cha mtu wala heshima ya mtu, ikiwa na maana kwamba ikiwa yeyote ananyanyuka na kwenda kinyume na kweli basi anapaswa akabiliwe na kuonywa pasipo kujali cheo chake wala umaarufu wake lakini kwa nia ya upendo.
Vile vile tunachojifunza kwa Mtume Petro ni unyenyekevu, kwani baada ya kuonywa na Paulo alitubu na huoni popote akimkasirikia Paulo zaidi sana utaona anakuja kuwaelekeza watu kwenye nyaraka za Paulo kwamba wazisome..
2 Petro 3:15 “Nanyi uhesabuni uvumilivu wa Bwana wetu kuwa ni wokovu, kama vile na ndugu yetu mpenzi Paulo alivyowaandikia kwa hekima aliyopewa
16 vile vile kama katika nyaraka zake zote pia, akitoa humo habari za mambo hayo; katika nyaraka hizo yamo mambo ambayo ni vigumu kuelewa nayo; na mambo hayo watu wasio na elimu, wasio imara, huyapotoa, kama vile wayapotoavyo na maandiko mengine, kwa uvunjifu wao wenyewe”.
Na sisi hatuna budi kuiga ujasiri wa Paulo na unyenyekevu wa Petro, huo ndio ukristo!!!..Lakini si kuona dhambi na kuzifumbia macho au kuambiwa ukweli na kukasirika badala ya kujifunza na kubadilika.
Bwana atusaidie katika hayo yote.
Maran atha.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Rudi nyumbani
Print this post
SWALI: Wakati shetani anamjaribu Yesu, biblia inasema alimchukua na kumpandisha kwenye kinara cha hekalu, swali ni je! Alikuwa anachukuliwaje mahali pale ni njia gani ilikuwa inatumika?
JIBU: Awali ya yote ni lazima tufahamu kuwa Bwana Yesu hakupelekwa sehemu nyingine yoyote ili kujaribiwa zaidi ya pale jangwani. Hii ikiwa na maana majaribu yake yote yalimtokea akiwa palepale jangwani.
Mathayo 4:1 “Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ili ajaribiwe na Ibilisi,2 Akafunga siku arobaini mchana na usiku, mwisho akaona njaa”
Sasa kama ni hivyo iweje, shetani amtoe pale na kumpeleka kwenye kinara cha Hekalu na wakati huo huo amwonyeshe milki zote za ulimwenguni? Je! Aliondokaje pale? Au alichukuliwa kimazingara?
Mathayo 4:5 “Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu, akamweka juu ya kinara cha hekalu 6 akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe. 7 Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako. 8 Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake, 9 akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia. 10 Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake. 11 Kisha Ibilisi akamwacha; na tazama, wakaja malaika wakamtumikia”
Jibu ni kwamba majaribu yale yalikuwa katika roho, na sio katika mwili, Kwa ufupi yalikuwa ni mfano wa maono. Na kikawaida maono yanapokuja ikiwa ni ya kukuonyesha tukio husika utashangaa waweza kujiona kama upo pale pale eneo lenyewe, lakini sio. Kama tu vile ndoto. Unaota upo kijijini kwenu, anashughulika, unaongea na ndugu, lakini kiuhalisia kumbe umelala palepale kitandani.
Ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana Yesu, alikuwa palepale jangwani, wala hakutoka, isipokuwa alikuwa katika roho, akayaona hayo yote, aliyoonyeshwa na shetani.
Bwana akubariki.
Lakini pia ni vizuri, kutambua maana ya majaribu yale, Kwasababu hayo pia ndio shetani anayotumia kumjaribu kila mtakatifu aliyepo duniani. Kwa upana wa habari hiyo waweza fungua link hii >>> MAJARIBU MATATU YA YESU KRISTO
Shalom.
DAKIKA MOJA TU, INAKUFANYA UMWAMINI SHETANI?
Tofauti kati ya ufunuo, unabii na maono ni ipi?
NI KWA NAMNA GANI TUTASHINDA MAJARIBU?
JE! JICHO LAKO LINAONA NINI KATIKATI YA MAJARIBU?
UFUNUO: Mlango wa 11
DALILI TISA (9) ZA PEPO KUWEPO NDANI YA MTU.
KWA WINGI WA WASHAURI HUJA WOKOVU.
SWALI: Je! mstari huu unaelewekaje? Mithali 9:17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu, Na mkate ulioliwa kwa siri hupendeza”
JIBU: Mstari huo unamfunua mtu mwenye asili ya dhambi, jinsi vitu vilivyo kinyume na mapenzi ya Mungu vinavyoweza kupendeza mbele yake zaidi ya vile ambavyo ni sahihi kwake kuvifanya.
Kwamfano katika habari hiyo ukianzia vifungu vya juu utaona vinamweleza mwanamke kahaba, anavyowateka watu kuzini naye. Na mtu mjinga ataona ni sahihi kwenda kwake, lakini mwisho wake ni mbaya. Watu wengi wanaacha ndoa zao nakwenda kuzini nje! Kwasababu wanaona kile wanachokipata huko nje, kina uzuri kuliko kile walichokizoea ndani, wengine wanafanya uasherati, kwasababu wanaona wakingojea mpaka wakati wa ndoa, watakosa mambo mengi. Hao ndio wanaotembea katika usemi huo “Maji yaliyoibiwa ni matamu, Na mkate ulioliwa kwa siri hupendeza”
Wengine wanaona wakitumia njia ya udanganyifu, ndio zitawafikisha katika malengo yao kwa haraka, kuliko njia za halali, hivyo hujiingiza katika wizi, na magendo.
Lakini ukizidi kusoma mstari unaofuata anasema..
. Lakini huyo hajui ya kuwa wafu wamo humo; Ya kuwa wageni wake wamo chini kuzimuni.
Maana yake ni kuwa wote wafanyao mambo kama hayo, mwisho wao unakuwa ni kifo, na kuishia kuzimu kabisa. Dumu katika ndoa yako, kataa vya wengine, epuka mambo ya sirini. Yusufu hakukubali kuzini na mke wa boss wake. Lakini Daudi alidanganyika akazini na mke wa kijakazi wake, matokeo yake yakawa na yeye kunajisiwa wake zake vilevile, mtoto wake kufa, na ufalme wake kutikiswa na mwana wake mwenyewe aliyeitwa Absalomu, lakini zaidi sana kupoteza furaha ya wokovu kwa miaka mingi sana. Daudi alijutia makosa yake kwa muda mrefu sana.
Hivyo usipumbazwe na vivutio vyovyote vya dhambi vitakugharimu sana.
Nini maana ya Mithali 27:21 inaposema “mtu hujaribiwa kwa sifa zake?”
Fahamu maana ya Mithali 29:4 “Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.
Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)
Jicho ni nini (Yakobo 3:11)
NI NINI BWANA ANATAZAMIA KILA TUNAPOSHIRIKI MEZA YAKE.
KUWA MAKINI NA MITANDAO, NI SHIMO REFU.
Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?
SWALI: Je ni lazima nibadili jina baada ya kuokoka, na kama ni hivyo ni mazingira gani yaliyo sahihi kufanya hivyo?
JIBU: Nakusalimu katika jina la Bwana Yesu Kristo.
Unapookoka, ni vema kufahamu Kristo akishakukomboa amekombolewa kwelikweli, Huwezi kukosa mbingu kwasababu ya jina lako, hata kama linamaana mbaya, kwasababu wapo watu waliokuwa na majina mabaya, mmojawapo ni Yabesi ambaye jina lake lilimaanisha “huzuni”, kwasababu alizaliwa katika kipindi cha huzuni, na wazazi wake wakamwita hivyo lakini alimlingana na Mungu na Mungu akambariki na kumtukuza sana (1Nyakati 4:9-10).Lakini walikuwepo pia watu wenye majina mazuri mmojawapo Yuda, lakini tabia zake hazikuendana na jina lake.
Hivyo ikiwa jina lako si zuri sana, na huoni shida kuendelea nalo, huwezi kumkosa Mungu kwasababu ya hilo. Lakini pia, yapo mazingira ambayo, inampasa mkristo abadili jina endapo kuna ulazima wa kufanya hivyo. Na mazingira yenyewe ni kama haya;
Kwahiyo hivyo ndio vigezo vya mtu kusukumwa abadili jina. Lakini usibadili kwasababu ya shinikizo la mtu, ikiwa huoni kikwacho chochote kuitwa jina hilo lako. Kwasababu wokovu wako, hauwezi kuzuiwa na jina. Hilo ulifahamu.
JINA LAKO NI LA NANI?
MAANA YA MAJINA NA TAFSIRI ZAKE.
Kula uzao wa tumbo lako maana yake nini? (Kumbukumbu 28:53)
Majina mbalimbali ya Mungu na maana zake.
Huihesabu idadi ya nyota, Huzipa zote majina.
UPEPO WA KUSI HULETA MVUA;
SWALI: Nini maana ya Zaburi 125:3 “ Kwa maana fimbo ya udhalimu Haitakaa juu ya fungu la wenye haki; Wenye haki wasije wakainyosha Mikono yao kwenye upotovu”.
JIBU: Mstari huo unatuonyesha jinsi Mungu anavyowatenga watu wake na adhabu ambazo zinawahusu waovu. Kwamba kamwe fimbo ya adhabu haiwezi kuwahusu watu wa Mungu, Ndio maana ya hilo neno ‘Kwa maana fimbo ya udhalimu Haitakaa juu ya fungu la wenye haki;.. Ni mfano tu wa wana wa Israeli wakati ule walipokuwa Misri, Mungu aliwatenga na wamisri na kuwaweka kule Gosheni, na mpigo yote yalipokuja hayakuwakuta wana wa Israeli, bali wamisri tu. Hata baadaye alipotaka kuliadhibu taifa zima, bado aliwaficha watu wake ndani ya nyumba, na Yule malaika aliyeshushwa kuwauwa watu, hakupita katika nyumba zao. Kuonyesha kuwa fimbo za makosa Mungu hana desturi ya kuzijumuisha na watu wake, isipokuwa tu wamekataa wenyewe. Ndivyo ilivyokuwa kwa Nuhu, na Lutu.
Na anafanya hivyo kwasababu gani? Ndio hapo anasema ili “Wenye haki wasije wakainyosha Mikono yao kwenye upotovu”. Kwamba anawataadharisha watu wake wasidiriki kufanya makosa kama hayo hayo ya waovu kwasababu na wenyewe adhabu inaweza kuwakuta vilevile. Na kweli ndivyo ilivyokuwa kwa wana wa Israeli baadaye, walimwacha Mungu wakaanza kuitumikia miungu, na matokeo yake Mungu akawarudisha tena utumwani, na miji yao kubomolewa.
Hivyo, ni kutuonya kuwa sisi tuliokoka, kamwe tusijichanganye na maovu kwasababu adhabu ya makosa yaweza kutupata na sisi pia, kwasababu Mungu hatazami uso wa mwanadamu, bali ulekevu wako kwake.
Kwa maana nyingine ya mistari mbalimbali ya biblia tembelea website yetu hii >>> www.wingulamashahidi.org.
Kulabu ni nini katika biblia?(2Wafalme 19:27)
Miimo ni nini na kizingiti ni nini?
Tirshatha ni nini? (Ezra 2:63)
Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma.
TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.
Je Bwana Yesu aliruhusu wanafunzi wake kubeba Fimbo au hakuwaruhusu? (Marko 6:8 na Mathayo 10:10).
Tofauti kati ya zaka na sadaka ni ipi?
UTARATIBU WA KUTOA FUNGU LA 10 UPOJE?.
SWALI: Dhabibu za roho ni zipi, zinazotajwa kwenye maandiko haya?
1Petro 2:5 “Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo”.
Dhabihu ni sadaka za kuteketezwa zilizokuwa zinatolewa katika agano la kale. Hizi zilikuwa na lengo la kufanya upatanisho wa makosa ya watu, kwamfano alipochinjwa mwanakondoo, au ng’ombe au mbuzi, au njiwa (Walawi 1:3-16) na kuteketezwa kisha ule moshi wake ukapanda juu basi huo ndio unakuwa uthibitisho wa sadaka yake kukubaliwa. Na mtu huyo makosa yake yanakuwa yamefunikwa kwa muda.
Hivyo katika agano jipya pia tunayo dhabihu yetu, ambayo kwa kupitia hiyo tunapokea upatanisho wa makosa yetu, na dhabihu yenyewe ni YESU KRISTO mwokozi wetu ambaye yeye kama mwanakondoo alichinjwa kwa ajili yetu ili sisi tupokee ondoleo la dhambi, hivyo yoyote ambaye yupo sasa ndani ya Kristo Yesu tayari ameshamtolea Mungu dhabihu ya upatanisho wake.
Lakini tunapokuwa ndani ya Kristo, hatuna budi kuonyesha kuwa tumekombolewa na yeye, kwa matendo yetu. Hivyo ni lazima tutaonyesha tabia kama za mtu anayekwenda kutoa dhabihu mbele za Bwana, na sio kama za mtu aliyejiamulia tu. Na tabia zenyewe ndio hizo zinazojulikana kama dhabihu za roho ambazo sisi tunazitoa.
Zifuatazo ndio dhabihu za roho zenyewe.
1) Shukrani
Zaburi 50:14 Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru; Mtimizie Aliye juu nadhiri zako.
Zaburi 50:23 Atoaye dhabihu za kushukuru, Ndiye anayenitukuza. Naye autengenezaye mwenendo wake, Nitamwonyesha wokovu wa Mungu.
Ukiwa mtu wa shukrani kwa Mungu, Ni kuonyesha kuwa umetambua kazi ya msalaba ndani yako. Na shukrani hizi ni lazima ziwe katika Sifa za kinywa chako, pamoja na matoleo kwa kile Mungu anachokubariki. Ni muhimu sana wewe kama mkristo kuwa mtu na namna hii. Wote waliokwenda kutoa sadaka za namna hii mioyo yao ilijaa shukrani kwa Mungu wao, hawakwenda hivi hivi tu.
2) Moyo uliopondeka
Zaburi 51:16 Maana hupendezwi na dhabihu, au ningeitoa, Wewe huridhii sadaka ya kuteketezwa. 17 Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika; Moyo uliovunjika na kupondeka, Ee Mungu, hutaudharau.
Moyo uliopondeka ni moyo wa toba, wa majuto ya dhambi, ambao unakufanya utaabike moyoni mwako kwasababu ya makosa yaliyotendeka, na hivyo unakufanya uwe mnyenyekevu sana mbele za Mungu.
Mtu mwenye moyo huu, mbele za Mungu anaonekana kama amejitambua yeye ni mkosaji, na hivyo Yesu amefanyika upatanisho kwa ajili yake, tofauti na mtu ambaye mambo yote kwake ni sawa, hata baada ya kuona kosa bado anaukaza moyo wake, kujifanya kama hana hatia yoyote mbele za Mungu. Yatupasa wakati wote tuwe watu wa kujinyenyekeza mbele za Mungu. Watu wa kutaka rehema zake.
3) Kuitoa miili yetu;
Warumi 12:1 “Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana. 2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.
Unapoutunza mwili wako mbali na mambo ya kidunia, kisha ukaufanya utumike kwa ajili ya kazi ya Mungu, hapo ni sawa na unamtolea Mungu dhabihu yenye kupendeza, yaani unaenda mbele za Mungu na badiliko, unasema msalaba mbele, udunia nyuma. Lakini ukiwa unavaa ovyo ovyo, unazini, unatumia mikorogo, unajichora mwili wako, unakunywa pombe, unavuta sigara, unatoa mimba, hapo hufanyi ibada yoyote mbele za Mungu. Kwasababu lazima ufahamu kuwa miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu (1Wakorintho 3:16).
Hivyo, wewe ambaye umeokoka, zangatia mambo hayo matatu, SHUKRANI, MOYO ULIOPONDEKA, NA KUUTOA MWILI WAKO. Wokovu wako utakuwa na maana sana mbele za Mungu.
Je! Umeshaokoka?. Kama bado wasubiri nini? Unatambua kuwa haya ni majira ya siku za mwisho, na Kristo amekaribia kurudi?. Dalili zote zimeshatimia, Embu tubu sasa mgeukie Kristo akuokoe uwe upande salama. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi waweza fungua hapa kwa ajili ya mwongozo was ala hiyo.>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Dhabihu ni nini?
KUTII NI BORA KULIKO DHABIHU.
Mahali pa juu palikuwa ni wapi kama tunavyosoma katika biblia?
Swali: Kurushwa upesi kunakozungumziwa katika Danieli 9:21 ndio kupi?
Mnanaa, Bizari na Jira ni viungo gani? (Mathayo 23:23)
Sadaka ya Moyo ipoje? (Walawi 22:21).
Kwanini samaki wasio na mapezi na magamba hawakuruhusiwa kuliwa?
Mara nyingi tunapojikuta tumelala tunaposoma biblia, huwa moja kwa moja tunamsingizia shetani. Lakini ukweli ni kwamba shetani anahusika kwa sehemu ndogo, sehemu kubwa ni hali zetu za kimwili ndio zinakuwa adui katika jambo hili. Mazingira ambayo ni mashambulizi kutoka kwa adui mfano wake yanakuwa ni kama haya; pengine mtu akianza tu kusoma biblia anasikia maumivu makali kwenye kichwa, au mwili, lakini akiacha tu kusoma hali yake inarudia kama kawaida, au anaona giza au vitu kama mianga mianga kwenye macho na hivyo inamfanya asiweze kuisoma biblia, au kila anapotaka kusoma anapoteza hapo hapo kumbukumbu zote kwamba alikuwa anasoma biblia, na hatimaye anajikuta yupo usingizini, au anafanya mambo mengine kabisa, hiyo ndio mfano ya mashambulizi.. Na inahitaji kuombewa, au kushindana na hiyo roho hadi ikutoke.
Lakini ukijiona unaposoma biblia usingizi mzito umekukamata, unasinzia sinzia, unapiga piga miayo, huyo sio adui huo ni mwili wako, usiopenda mambo ya rohoni. Hivyo ni lazima uushinde huo.
Wagalatia 5:17 “Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka”
Hivyo hizi ni njia ambazo zitakusaidia usilale pale unaposoma biblia.
Usipende kufungua biblia kama kitabu cha riwaya, unasoma tu utakavyo. Kumbuka yale ni maneno ya ROHO, na hivyo inahitaji umkaribishe Roho akusaidie. Hivyo usiwe mvivu wa kuomba, pata dakika, kadhaa za kufanya hivyo. Ni jambo ambalo nimejifunza sana, wakati nasoma biblia bila kuomba, na pale ninapoomba kisha nikaisoma, kuna tofauti kubwa sana ya kiuelewa na kiutulivu. Maombi pia yanasaidia kama kuna mashambulizi yoyote, basi yanatowekea hapo.
Ikiwa umechoka sana, si lazima usome biblia muda huo huo. Pendelea kuruhusu mwili wako upumzike vizuri, kwamfano umetoka kazini, umeshughulika kutwa nzima, ni rahisi sana kukabwa na usingizi muda huo huo usomapo biblia peke yako. Hivyo tumia busara, wahi kulala, kisha amka usiku. Ukilala hata masaa 3, mwili unapokea taarifa kuwa huyu mtu tayari alishapumzika. Hivyo ukiamka ukajimwagia maji, ukaketi utajiona unafuu mkubwa, na utapata kitu kikubwa kuliko kulizimisha mwili wakati umechoka.
Tafuta meza ukae, mwili wako uwe kama mtu aliye darasani, sio kama aliye hospitalini mgonjwa unasubiriwa kuhudumiwa. Kaa kwenye meza, kisha ndio usome biblia yako
Luka 12:35 Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka
Kusoma kwa kuandika na kwa sauti, huwa kuna matokeo makubwa kuliko, kutumia tu macho yako. Hivyo andiko vifungu unavyovisoma, na ufunuo unaopata, itakuongezea umakini katika usomaji wako, na hivyo Roho Mtakatifu atapata nafasi ya kukufindisha kwa urahisi zaidi.
Ukiona huwezi kujiwekea ustaarabu wa kuzingatia ratiba yako ya usomaji, pendelea kujifunza na wengine. Kaa na familia yako, au ndugu zako, au rafiki yako katika Bwana jiwekeeni ratiba ya usomaji wa biblia pamoja, kisha mnachambua kile mlichojifunza, kwa namna hiyo itakusaidia sana kuielewa ..
Mathayo 18:20 “Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao”
Kusoma biblia sio mashindano kwamba ni lazima uimalize yote kwa siku moja, soma vifungu kadhaa, kisha tumia muda mwingi, kuvitafakari hivyo vilimaanisha nini. Roho Mtakatifu anapenda kutufundisha taratibu sana, hataki tuvuke madarasa ya juu wakati ya chini bado hatujayamaliza. Hivyo zingatia kusoma kwa muktadha wa kuelemishwa na Roho Mtakatifu, sio kumaliza silabasi. Kusoma vifungu vitano kwa dakika mbili, kisha ukavifakari kwa masaa 2, ni bora kuliko kusoma vifungu elfu kwa saa2, halafu hakuna tafakari yoyote.
Mfungo ni jambo zuri ambalo huupa mwili wepesi, kwasababu mwili unapotaabika kwa kunyimwa haja zake kwa kawaida roho yako huwa inakuja juu. Hivyo ukiwa katika kipindi cha mfungo, utaona wepesi Fulani wa kuisoma biblia kwa masafa marefu kidogo, kuliko kipindi kingine. Fungu mara kwa mara, au ukiwa unatamani wiki hiyo kuitumia vizuri usiku katika kusoma Biblia, basi hakikisha wiki hiyo yote unafunga, utajiona mwepesi sana hususani wakati wa usiku unapotulia.
Si kila jambo utaweza kulitatua tu peke yako mengine, utahitaji msaada, hivyo hakikisha maendeleo yako ya kiusomaji, kiongozi wako anayafahamu, hatua zako unamshirikisha mchungaji wako, itakusaidia sana, kupata ushauri au maombi , au ushuhuda kwa yale ambayo pengine usingeyafahamu uwapo peke yako. Na hiyo itakupa hamasa zaidi na shauku ya kusoma.
Hakikisha unasoma BIBLIA kila siku.
Jinsi ya kuandaa Somo la kufundisha
JINSI YA KUSOMA BIBLIA.
HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?
UFUNUO NI NINI, NA NITAPOKEAJE UFUNUO KUTOKA KWA MUNGU?
Biblia inamaana gani inaposema tutoapo unabii tutoe kwa kadiri ya imani?
Ni kanuni gani ya kuzingatia wakati wa kuhubiri/kufundisha ili usimzimishe Roho?.
Kuna vita vikubwa sana vya kiroho vinavyoinuka muda mchache kabla ya kusimama kufundisha/kuhubiri ambavyo ni lazima mkristo avijue na ajue jinsi ya kuvishinda ili injili ya Bwana isizuilike.
Baada ya kuandaa somo kwa kuongozwa na Roho Mtakatifu, hatua inayofuata ni wewe kwenda kuwasilisha ujumbe ulioupokea mbele ya mtu au watu. Sasa ni muhimu kujua kanuni za kuwasilisha ujumbe ili usije ukamzimisha Roho, kwasababu Roho Mtakatifu pia anaweza kuzimishwa ndani ya mtu na mtu mwenyewe, na shetani ndicho anachokitafuta hicho, lengo lake Injili isiwafikie wengine.
(Kumbuka shetani mwenyewe hawezi kumzimisha Roho Mtakatifu, kwasababu Roho Mtakatifu ana nguvu kuliko yeye), anachokifanya shetani ni kuzikoroga hisia za mtu ili zisiruhusu Roho Mtakatifu kufanya kazi ndani yake. Na neno linatuambia kuwa “tusimzimishe Roho”
1Wathesalonike 5:19 “Msimzimishe Roho”.
Wengi huwa wanamzimisha Roho Mtakatifu wakati wa kusimama kufundisha/kuhubiri pasipo wao kujijua..unakuta wakati wanaandaa somo/mahubiri wanakuwa katika uwepo mkubwa sana lakini wakati wa kufundisha au kuhubiri ule uwepo au ile hali ya kutiririka inapotea, na hivyo kumfanya huyu mtu ajihisi Mungu hayupo naye au kamwacha.
Kiuhalisia huyu mtu hajaachwa na Roho Mtakatifu, isipokuwa hali yake ya ndani imezuia utendaji kazi wa Roho Mtakatifu.
Sasa yafuatayo ni mambo ya kuzingatia ili Roho asizime ndani yako, (kule kutiririka kusikome), na ule ujumbe wa Roho Mtakatifu ulioupokea ufike kwa walengwa kama Roho alivyokufunulia.
1.Usijipange kwa maneno mengi.
Epuka kujipanga kwa maneno mengi; Maneno mengi yanazuia kutiririka kwa Roho Mtakatifu, wengi wanadhani kuwa na maneno mengi ndiko kueleweka, pasipo kujua kuwa anayewagusa watu na kuwafanya waelewe ni Roho Mtakatifu, hivyo ukifuata kanuni ya Roho Mtakatifu utaeleweka tu na utakuwa na matunda.
Unapojiandaa kwa maneno mengi, utajikuta unategemea yale maneno yako, na hivyo wakati Roho Mtakatifu anataka kuingiza mada nyingine katika akili yako wakati wa kufundisha ule ukuta wa maneno uliojiwekea unazuia kinywa cha Roho Mtakatifu kifanye kazi, na hivyo utajikuta unafundisha kwa akili zako, na yale maneno uliyoyaandaa yanapokwisha unajikuta na wewe umekauka, huna cha kusema Zaidi.
Kwahiyo jiandae kwa maneno machache tu!, hata kama unaona somo litakuwa ni fupi sana, Roho Mtakatifu ndio anataka iwe hivyo, ili hayo maneno mengine ayajazie yeye, ukiweka desturi hiyo siku zote utaona muda hautoshi, utaona daftari lako lina maneno machache uliyoyaandaa, lakini muda uliofundisha ni madakika mengi au masaa mengi, ukiona hiyo hali imekutokea jua sio wewe uliyekuwa unafundisha bali ni Roho Mtakatifu ndani yako.
2. Usifikiri fikiri.
Kufikikri fikiri ni nini utaenda kusema au kuhubiri, kunazima kinywa cha Roho Mtakatifu. Unapofika wakati wa kwenda kufundisha wengi huwa wanapaniki na kuwaza mara nyingi nyingi ni nini wataenda kusema, na hivyo kujikuta kulazimisha kupanga maneno ya kuzungumza kuanzia mwanzo hadi mwisho. Ukiona hiyo hali inakujua ndani yako dakika chache kabla ya kusimama kufundisha au kuhubiri ikatae!. Kwani ni adui anataka kutumia fikra zako kumzimisha Roho ndani yako.
Siku zote usijiangalie hali uliyonayo kifikra wakati wa kwenda kufundisha, hata kama hukumbuki chochote, wewe tulia mpaka wakati utakapofika wa kusimama, funga fikra zako kufikiri ni nini utaenda kufundisha au kuhubiri, ukiona mawazo hayo yanakujia hamisha fikra zako kwa kutafakari mambo mengine ya kiMungu au soma Neno, kwasababu wakati huo ndio wakati wa vita vikali, shetani anatumia nguvu kubwa sana kumshambulia mtu katika hii hatua.
Hivyo funga fikra zako na subiri ule wakati wa kufundisha Roho Mtakatifu atakupa cha kusema wakati ule ule utakaposimama kufundisha.
Kanuni kama hii Bwana Yesu aliwafundisha wanafunzi wake wakati wakipelekwa mbele ya watu wa Mataifa, akawaambia wasifikiri fikiri watakavyojibu kwani watapewa kinywa saa ile ile watakaposimamishwa.
Mathayo 10:19 “ Lakini hapo watakapowapeleka, msifikiri-fikiri jinsi mtakavyosema; maana mtapewa saa ile mtakayosema
20 Kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu”.
Kwahiyo na wewe usiwe mtu wa kufikiri fikiri utakavyosema, subiri ule muda utakapofika utapewa kinywa cha kusema, ambacho hata wewe mwenyewe utajishangaa.
3. Usijiangalie udhaifu wako na Jiachilie
Usijipime kwa kujiangalia udhaifu wako, kama unajua kuhubiri au la!, kama una kigugumizi au la!, kama una uzoefu au la!..Kwani kinywa chochote kilichovuviwa na Roho Mtakatifu kina nguvu kwasababu kimebeba ujumbe wa Roho Mtakatifu.
Hivyo kabla ya kwenda kufundisha weka kando udhaifu wako, weka kando kumbukumbu za nyuma ambazo unahisi uliwahi kukosea, weka kando hisia kwamba husikilizwi au hueleweki, au unapotezea watu muda.
Zungumza kile kinachokuja kinywani mwako muda ule kwa ujasiri wote, (achilia moyo wako na fikra zako), wala usijilinganishe na yeyote wala usitafute kufundisha kama mtu Fulani unayemjua, hapo utaona Roho Mtakatifua atakavyokutumia na utakavyomhisi akitenda kazi ndani yako kwa viwango vingine.
4. Usiongozwe na muda.
Ukiona hofu ya kuwahi kumaliza inaingia ndani yako, ikatae hiyo hali!.. Kwasababu ni mbinu nyingine ya shetani kumzimisha Roho Mtakatifu ndani yako (Kumbuka tena shetani mwenyewe hawezi kumzimisha Roho Mtakatifu, kwasababu Roho Mtakatifu ana nguvu kuliko yeye), anachokifanya shetani ni kuzikoroga hisia zako ili zisiruhusu Roho Mtakatifu kufanya kazi ndani yako.
Kwahiyo hofu ya muda ikatae. Kama umepewa lisaa la kufundisha, usianze kuwaza utasema nini kwenye hilo lisaa lote (hiyo sio kazi yako) ni kazi ya Roho Mtakatifu, ukianza kuwaza utasema nini muda wote huo wakati utakapofika hofu iliyopo ndani yako itamzuia Roho Mtakatifu kusema kupitia wewe. Wewe anza kufundisha kana kwamba utamaliza dakika tano zijazo, na utaona Roho Mtakatifu atakachokifanya!.. Kama atapenda umalize ujumbe kwa dakika hizo hizo tano, wala usiogope!, ndivyo alivyotaka yeye, na kama atakusudia ufundishe kwa kwa lisaa au masaa mawili, atakupa maneno na utashangaa yametoka wapi.. Kwahiyo ondoa hofu ya muda!.
5. Wahusishe watu katika kufundisha kwako
Hii ni njia nyingine ya kuendeleza uwepo uwepo wa Roho Mtakatifu usikatike ndani yako, tumia muda kuwauliza maswali unaowafundisha kama unaweza kufanya hivyo, au kuwapa jukumu la kusoma mistari ya biblia n.k
Hizi ni baadhi ya njia chache utakazoweza kuzitumia ili Kile Roho Mtakatifu alichokufunulia kiweze kuwafikia walengwa.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba kabla ya kwenda kusimama kufundisha ZILINDE SANA FIKRA ZAKO!.. Kwasababu hizo ndizo shetani anashughulika nazo kuharibu mambo.
Ikiwa hukupata somo la “Jinsi ya kuandaa somo basi wasiliana nasi kwa njia ya inbox”
Wanikolai ni watu gani? Katika biblia?
JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?
Roho Mtakatifu ni nani?.
MASOMO MAALUMU KWA WANAWAKE.
Neno hili utalipata katika vifungu hivi kwenye biblia.
Ezra 2:63 Na huyo Tirshatha akawaambia wasile katika vitu vitakatifu sana ,hata atakaposimama kuhani mwenye urimu na Thumimu.
Nehemia 8:9 Naye Nehemia, ndiye aliyekuwa Tirshatha, na Ezra kuhani, mwandishi, na Walawi waliowafundisha watu, wakawaambia watu wote, Siku hii ni takatifu kwa Bwana, Mungu wenu; msiomboleze wala msilie. Maana watu wote walilia, walipoyasikia maneno ya torati
Nehemia 10: 1 Basi hawa ndio waliotia muhuri; Nehemia, ndiye Tirshatha, mwana wa Hakalia, na Sedekia;
Soma pia Nehemia 7:65
Tirshatha ni neno la kiajemi, ambalo linamaanisha mtawala aliyeteuliwa kuongoza uyahudi chini ya ufalme wa uajemi. Kwa jina lingine ni gavana/ liwali, Katika vifungu hivyo vinamwonyesha Nehemia alikuwa kama Tirshatha/Mtawala. Soma pia (Nehemia 5:18).
Lakini pia Zerubabeli, alipewa nafasi hii kama tunavyosoma hapo kwenye Ezra 2:63, Hivyo wote hawa walisimama kama wakuu wa majimbo hayo wayaangalie, na kusimamia kazi zote walizoagizwa na mfalme.
Tazama pia maana ya maneno mengine ya kibiblia chini.
Je! Umeokoka? Je, unatambua kuwa Kristo anakaribia kurudi? Umejiandaaje? Tubu dhambi zako ukabatizwe upokee Roho Mtakatifu uwe salama zizini mwa Bwana. Muda ni mfupi sana tuliobakiwa nao, huu si wakati wa kubembelezewa wokovu, ni wewe mwenyewe kuona na kugeuka upesi. Ikiwa upo tayari kuyakabidhi maisha yako kwa Bwana basi fungua hapa ili upate mwongozo wa sala ya toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Maana Ya Maneno Katika Biblia.
Ayari ni nini kama tunavyosoma katika biblia?
Jabari ni nini, kama linavyotumika kwenye biblia?
Kisima cha joka na lango la jaa ni nini?(Nehemia 2:13)
HAPAKUWA NA NAFASI YA KUPITA KWA YULE MNYAMA ALIYEKUWA CHINI YANGU.
NI MAONO YAPI HAYO UNAYOSUBIRIA?
FUMBO ZA SHETANI.
SWALI: Nini maana ya Neno hili; Mithali 22:29 “Je! Wamwona mtu mwenye bidii katika kazi zake? Huyo atasimama mbele ya wafalme; Hatasimama mbele ya watu wasio na cheo”.
JIBU: Neno la Mungu linatuonyesha kuwa ‘bidii’ humkweza mtu. Na bidii inayozungumziwa kibiblia ni zaidi ile inayodhaniwa kufanya tu kazi sana kwa muda mrefu, hapana, bali ni pamoja na kutumia ujuzi wako wote na ufanisi ili kutimiza kusudi ulilowekewa ndani ya muda. Watu wa namna hii mara nyingi huwa wanateka macho ya watu wenye vyeo au wakuu wa nchi.
Kwamfano Wafanyakazi wanaoonyesha ufanisi katika utendaji kazi, na kutimiza malengo ya shirika lao ndani ya wakati waliowekewa, huwa wanapendwa na ma-boss wao, na mara nyingi hupandishwa vyeo kama sio kupewa zawadi. Wagunduzi wa mipango ambayo inaleta mabadiliko chanya kwenye jamii, huwa wanaalikwa na viongozi wakubwa na maraisi kupongezwa na wakati mwingine kufanywa washauri wao.
Vivyo hivyo kiroho pia, ili tupate kibali kwa aliye Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana, zaidi ya wakuu wote duniani (yaani YESU KRISTO), hatuna budi kuwa na bidii katika kumtumikia yeye, na kuyafanya mapenzi yake.
Anasema,..
Kumbukumbu 28:1 Itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu wako, KWA BIDII, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo Bwana, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani;
Umeona? Tusipokuwa walegevu, Bwana atatunyanyua juu sana tena sana kwasababu ni ahadi yake na haiwezi kutanguka..
Warumi 12:11 ‘kwa bidii, si walegevu; mkiwa na juhudi katika roho zenu; mkimtumikia Bwana;’
Hivyo, hakikisha, kile ulichopewa na Bwana unakitendea kazi, zaidi sana angalia ni kwa namna gani utakiweka ili kilete matokeo mazuri katika ufalme wa Bwana, usikifanye bila maarifa, hakikisha unatumia vyote yaani; nguvu zake zote, akili zako zote, roho yako yote, na moyo wako wote kwa pamoja bila kusahau kimoja wapo, ndani ya muda huu mchache uliopewa na Mungu hapa duniani. Na hakika kitakapochipuka kama Bwana alivyokusudia, Bwana atakutukuza sana.
Lakini ikiwa upo nje ya Kristo, tambua kuwa bado huwezi kumtumikia Bwana, na hata ukifa sasa ni moja kwa moja unaenda katika jehanamu ya moto. Kwanini usiyapange upya maisha yako leo kwa kufanya uamuzi wa busara wa kumkabidhi Kristo maisha yako?
Ikiwa upo tayari kufanya hivyo sasa, basi fungua hapa kwa mwongozo huo wa sala.>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Nini maana ya Mithali 5:15-18 anaposema Unywe maji ya birika lako mwenyewe?
USINIPE UMASKINI WALA UTAJIRI. (Mithali 30)
Je! Wamwona mtu mwenye bidii katika kazi zake?
TULITAFUTE KWA BIDII TUNDA LA ROHO.
HAKUVAA NGUO SIKU NYINGI.
KUWA MAKINI, HATUA ZA UNYAKUO ZINAENDELEA.