SWALI: Silaha za Nuru ni zipi?
Warumi 13:12 Usiku umeendelea sana, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru
JIBU: Ni lazima tufahamu ulimwengu wa roho upo katika pande mbili,
Upande wa Nuru ni wa Kristo (Yohana 1:4-5), na upande wa giza ni wa ibilisi.
Na pande hizi hazijawahi kupatana hata kidogo, na kama hazijawahi kupatana maana yake zipo vitani na kama zipo vitani basi zote zina silaha zake, kuhakikisha zinajilinda, lakini pia kushambulia, ili kuua utawala mwingine. Ndio hapo kwanini tunaambiwa tuzivae silaha za nuru. Maana yake mtu anaweza akawa ni wa nuru lakini akawa hana/hajui kuzitumia silaha za Nuru.
Vifungu vifuatavyo ni kututhibitishia kuwa Nuru na giza vipo katika mapambano;
2Wakorintho 6:14 Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza?
Wakolosai 1:12 mkimshukuru Baba, aliyewastahilisha kupokea sehemu ya urithi wa watakatifu katika nuru.
13 Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake
Sasa silaha za Nuru ambazo mtu akiwa nazo ataweza kujilinda na mashambulizi ya giza, lakini pia ataweza kuushinda ufalme wa giza ni hizi;
Silaha hizi, ndio zile zinazotajwa pia kwenye Waefeso 6:10-18, kama silaha za haki.
Kwa maelezo marefu juu ya silaha hizi, fungua hapa usome >>> Nini maana ya Dirii, Chapeo na Utayari?
Mtu akiwa na mambo haya, ataweza kulishinda Giza, kotekote.. Ambalo, silaha zake ni kama zifuatazo;
Swali ni Je! Umejivika silaha Nuru ?
Ikiwa upo nje ya Kristo, huwezi kusimama, unahitaji wokovu kwanza, ikiwa upo tayari kufanya hivyo wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Silaha za Mkono wa kuume na za mkono wa kushoto ni zipi
Je mapepo yanakufa? Na kama hayafi, tunashindanaje vita vya kiroho?
NGUVU YA “KUKATAA” UNAPOPAMBANA VITA VYA KIROHO
SWALI: Katika sehemu nyingi kwenye maandiko tunaona, Mungu akiwaagiza watu wake Wamsifu au wamwabudu katika uzuri wa utakatifu, nini maana ya uzuri wa utakatifu?
1 Mambo ya Nyakati 16:29
[29]Mpeni BWANA utukufu wa jina lake; Leteni sadaka, mje mbele zake; Mwabuduni BWANA kwa uzuri wa utakatifu;
Zaburi 29:2
[2]Mpeni BWANA utukufu wa jina lake; Mwabuduni BWANA kwa uzuri wa utautakatifu.
Soma pia..
Zaburi 96:9, 2Nyakati 20:21
JIBU: Kuna mambo mawili hapo.
Jambo la kwanza ni “Uzuri” na jambo la pili ni “utakatifu”
Hasemi tumwabudu Bwana katika utakatifu…hapana bali anasema tumwabudu Bwana katika uzuri wa utakatifu..
Kwa namna nyingine anamaanisha hivi; tuuone uzuri ulio katika utakatifu ndio tumwabudu yeye Katika huo.
Tunaweza tukaujua utakatifu…ambao mfano wake ni kama vile maisha ya upendo, haki, usafi, adabu, amani, utu wema. n.k. Lakini tusione uzuri wa mambo kama hayo mioyoni mwetu au maishani mwetu…wengine wanaona kama utakatifu wa Mungu ni kitu cha kutisha, lakini kumbe Sio..
Siku tukiona uzuri wake ndio hatutakuwa na unafki pale tunapoambiwa tufanye jambo lolote katika utakatifu..
Kwasababu tusipoona hilo, hatma yake huwa ni kutimiza ibada kama tu agizo fulani au utaratibu wa kidini au nidhamu fulani lakini sio katika furaha na faida tuipatayo katika huo utakatifu.
Kwamfano Ibada tu yenyewe ni tendo takatifu lakini je tunaifurahia ibada na kujiona tunanufaika sana mioyoni mwetu katika hizo au tunamtimizia Mungu tu haki yake ya kuabudiwa, lakini hakuna chochote kitufurahishacho ndani yake?
Ibada ifanywayo katika uzuri wa utakatifu ni lazima itaambatana na sifa hizi;
Itakuwa Katika Roho na kweli (Yohana 4:24)
Itafanywa Katika Moyo mweupe( Zaburi 24:3-4). Mfano kusamehe, na amani moyoni.
Itajaa shukrani na kumfurahia Mungu:
Zaburi 139:14
[14]Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa
Kwa jinsi ya ajabu ya kutisha. Matendo yako ni ya ajabu,
Itamwadhimisha Mungu na kumfurahia sana, kwa maajabu yake na matendo yake makuu, kwa viwango visivyo vya kawaida
Itaambatana na maisha ya utakatifu:
Warumi 12:1
[1]Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.
Maisha yetu ni ibada tosha, mwonekano wako, uvaaji wako, usemi wako, tabia yako, vitaakisi utakatifu wa Kristo.
Je umeuona uzuri wa Mungu, uzuri wa ibada, uzuri wa kukusanyika, uzuri wa uumbaji wake, ambavyo ndio uzuri wa utakatifu? Kama ni ndio basi utamsifu na kumwabudu pia katika tabia zake.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Nini maana ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli?
Ibada ni nini,Na je ili ikamilike inapaswa iwe na nini na nini?
DHABIHU ZA ROHO NI ZIPI? (1Petro 2:5)
SWALI: Nini maana ya ‘laana ya torati’, ambayo Kristo alikuja kutukomboa kutoka katika hiyo?
Wagalatia 3:13
[13]Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti;
JIBU:
Mungu alimpa Musa Torati ambayo ndani yake haikuwa na baraka tu pale Mtu alipoitii, bali pia ilikuwa na laana nyuma yake pale mtu alipoiasi..
Sasa hizo laana ndio ziliitwa “laana ya torati”, yaani adhabu, hukumu na kutengwa na uso wa Mungu.
Ukisoma Kumbukumbu la torati sura ya 27 – 28 inaeleza kwa undani juu ya baraka na laana mtu azipatapo pale anapoitii Au kunapoikataa torati..
Kwamfano
Kumbukumbu la Torati 27:26 inasema;
[26]Na alaaniwe asiyeyaweka imara maneno ya torati hii kwa kuyafanya. Na watu wote waseme, Amina.
Hivyo wanadamu, wote hawakufanikiwa kuzishika amri zile, na sheria Mungu alizowapa, na matokeo yake ikiwa ni laana juu ya kila mtu.
Warumi 3:10-12,23
[10]kama ilivyoandikwa, ya kwamba, Hakuna mwenye haki hata mmoja. [11]Hakuna afahamuye; Hakuna amtafutaye Mungu.
[12]Wote wamepotoka, wameoza wote pia; Hakuna mtenda mema, la! Hata mmoja…
[23]kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;
Sasa Kristo alipokuja, alifanywa laana kwa ajili yetu..sawasawa na hiyo Wagalatia 3:13, maana yake aliichukua hukumu yetu ya makosa kwa kupigwa na kufa kwake pale msalabani ili sisi tuponywe..
Warumi 8:1
[1]Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.
Ndio maana mtu yeyote ambaye hajamwamini Kristo bado yupo Chini ya hukumu na adhabu, kwasababu atataka kumpendeza Mungu kwa kutegemea tu nguvu zake mwenye, na hatimaye mwisho wa siku atashindwa..kwasababu hakuna mwanadamu aliyewahi kuishika torati yote…
Atasema haibi, hasemi uongolakini wakati huo huo ana mawazo mabaya, yote hayo ni makosa na dhambi…na mshahara wa dhambi sikuzote ni mauti..(Warumi 6:23)
Umeona umuhimu wa Yesu maishani mwetu?
Unasubiri nini usimwamini, akutoe katika laana hiyo, ili uhesabiwe bure kwa neema yake?
Mpokee sasa akuokoe…bofya hapa kwa mwongozo wa sala hiyo…
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
SWALI: Nini maana ya Mithali 21:3
[3]Kutenda haki na hukumu Humpendeza BWANA kuliko kutoa sadaka.
JIBU:
Mstari huo unatufundisha mambo ambayo Mungu huvutiwa nayo zaidi…
Mungu hupendezwa zaidi na sisi tunapoishi maisha ya haki, tunatenda mema, tunawajali wengine, tunaishi sawasawa ni viwango vyake vya kiroho hapa duniani..kwake hiyo ni bora zaidi ya sadaka zetu tumtoleazo.
Sadaka huwakilisha mambo yote Ya kidini tunayoweza kumfanyia Mungu, mfano ibada, fedha, mifungo, maombi, kuhubiri, kuimba n.k
Bwana huvutiwa zaidi na mioyo na tabia zetu, na sio zile Ibada za nje tu..
Haimaanishi kuwa hapendezwi na hivyo vitu hapana…bali hivyo vifanywe baada ya kutii kwanza..
Tunaona jambo kama hilo amelisisitiza sehemu nyingi kwenye maandiko; Tukianzia kwa Sauli alimwambia, hivyo;
1 Samweli 15:22
[22]Naye Samweli akasema, je! BWANA huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu Sawasawa na kuitii sauti ya BWANA? Angalia, kutii ni bora kuliko dhabihu, Na kusikia kuliko mafuta ya beberu.
Mika 6:6-8 inasema;
[6]Nimkaribie BWANA na kitu gani, na kuinama mbele za Mungu aliye juu? Je! Nimkaribie na sadaka za kuteketezwa, na ndama za umri wa mwaka mmoja?
[7]Je! BWANA atapendezwa na elfu za kondoo waume, au na elfu kumi za mito ya mafuta? Je! Nimtoe mzaliwa wangu wa kwanza kwa kosa langu, mzao wa mwili wangu kwa dhambi ya roho yangu?
[8]Ee mwanadamu, yeye amekuonyesha yaliyo mema; na BWANA anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!
Soma pia..
Isaya 1:11-17 – Inasema…Bwana huchukizwa na sadaka za watu wanaishi katika dhambi
Hivyo ni lazima tujiulize Je! tunatenda haki kwa wengine?
Je! Tunatembea kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wetu?
Je! tunamtii Mungu, kuliko vitu vingine vyovyote?
Je tunawahurumia wengine…?
Mambo kama haya ndio yenye uzito zaidi kwa Mungu.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Maana ya 2Wakorintho 9:11 mkitajirishwa katika vitu vyote mpate kuwa na ukarimu wote
katika agano jipya wapo watu wanne ambao wametajwa kwa jina la Yohana.. Wawili kati ya hao ndio hujulikana sana…ambao ni Yohana mbatizaji na Yohana mtume wa Yesu ..hawa wametajwa Sehemu nyingi katika agano jipya..
Mfano vifungu ambavyo utamsoma Yohana mbatizaji ni kama vifuatavyo:
Hivi ni vifungu vinavyomtaja Yohana Mtume;
Na ndiye mwandishi wa injili ya Yohana, pia na nyaraka zote tatu (1,2, 3 Yohana, ) pamoja na kitabu cha Ufunuo.
Yohana mwingine ni Marko, ndiye mwandishi wa kitabu cha Marko,..anatajwa katika kitabu cha Matendo 12:12, 13:5, Wakolosai 4:10
Na ndiye aliyekuwa Msaidizi wa Paulo na Barnaba katika ziara zao za kupeleka injili kwa mataifa.
Yohana mwingine ni Baba wa Simoni Petro anatajwa katika;
Yohana 1:42
[42]Akampeleka kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama, akasema, Wewe u Simoni, mwana wa Yohana; nawe utaitwa Kefa (tafsiri yake Petro, au Jiwe).
Soma pia Yohana 21:15-27
Hivyo jumla Yao ni wanne…
Je ungependa kufahamu Zaidi watu wengine Katika biblia? Kama ni ndio basi jiunge tazama chini kwa makala nyingine..
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Maherodi walikuwa ni akina nani, Na kazi yao ilikuwa ni ipi?
Kwanini nguo za waliomwua Stefano ziwekwe miguuni mwa Sauli?.
Wakolosai 1:9
[9]Kwa sababu hiyo sisi nasi, tangu siku ile tuliposikia, hatuachi kufanya maombi na dua kwa ajili yenu, ili mjazwe maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote na ufahamu wa rohoni;
JIBU:
Vifungu hivyo vinaonyesha kiu ya mtume Paulo juu ya watakatifu wa kanisa la Kolosai, Kwamba wajawe kuyajua mapenzi ya Mungu katika hekima yote na ufahamu wa rohoni.
Alijua ili kanisa liweze kumpendeza Mungu na kusimama ni lazima lijue mapenzi ya Mungu makamilifu.. Hivyo Ikawa shauku yake tangu zamani lijazwe kujua mapenzi hayo.
Kuna makundi mawili (2), ya mapenzi ya Mungu.
1)Mapenzi Ya daima
2) Mapenzi Ya wakati
Mapenzi ya daima: Ni yale ambayo yapo wakati wote, na kwa wote kwamba kila mwamini lazima ayatimize..mfano wa haya ni..ni kama utakatifu (1Wathesalonike 4:3), kuhubiri Injili, kuishi kwa upendo, kukusanyika pamoja, kudumu katika maombi, kumwabudu Mungu.
Lakini mapenzi ya wakati: Ni yale ambayo Mungu anakusudia uyafanye katika kipindi fulani tu, ni mapenzi yasiyo na mfanano, au mwendelezo fulani.. Kwamfano Mungu anakutaka leo usihubiri, bali uende kumtembelea yatima mmoja kijijini. Mfano wa kama alivyoambiwa Filipo awaache makutano aende jangwani kwa ajili ya yule mtu mmoja mkushi.(matendo Matendo 8:26)
Au wakati mwingine unapitishwa katika jaribu fulani, halafu pasipo kujua kuwa hilo ni darasa la Mungu ili kutumiza kusudi fulani, unajikuta unakemea na kushindana nayo…Ndio maana Bwana Yesu alipoomba juu ya kuondolewa kikombe cha mateso, alimalizia kwa kusema Baba mapenzi yako yatimizwe.
Sasa yote haya yanahitaji hekima na maarifa kuyatambua na kuyatimiliza. Si rahisi kuyatambua kwa akili za kibinadamu au kuyatimiliza.
Jambo la kwanza Paulo analitaja ni kuomba, aliwaombea watakatifu Wa Kolosai kwasababu alijua uwezekano wa kupokea Maarifa hayo upo katika maombi.
Yakobo 1:5
[5]Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.
Maombi hufungua mlango wa Mungu kuyaingilia maisha yetu na kututia katika kusudi Lake kamilifu. Mungu anafanya kazi ndani yetu kupitia maombi…Bila uombaji haiwezekani kutembea ndani ya mapenzi yote ya Mungu.
Kwa kusoma Neno ndipo unapojua Tabia za Mungu, nini anataka na nini hataki. Sauti ya Mungu, maagizo ya Mungu ya moja kwa moja yasiyohitaji usaidizi ni biblia takatifu.
Zaburi 119:105
[105]Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.
Mtu ajijengeaye tabia ya kusoma biblia, si rahisi kuanguka au kutoka nje ya mpango wa Mungu. Kwasababu lile neno linakaa ndani yake kama mafuta kumfundisha.
Bwana anafunua mapenzi yake tuwapo katika mabaraza yetu kutafakari maneno yake.. alisema wawili watatu kwa jina lake yupo hapo hapo katikati yao…Wale watu wawili waliokuwa wanakwenda Emau, tunaona walikuwa zaidi ya mmoja, ndipo wakiwa katika kutafakari habari za Kristo, Aliungana nao bila hata wao kujua akaanza kuwafundisha, na mwisho wote kujua mapenzi makamilifu ya Mungu ni nini..(Luka 24)
Na ndio maana hatupaswi kulikwepa kanisa kwasababu huko tunaungana na viungo vingi katika Mwili wa Kristo, na hivyo kujengana na kuonyana. Hatimaye mapenzi ya Mungu yanafunuliwa kwetu.
Hata wakati ule kulipotokea sintofahamu ndani ya kanisa kuhusu vyakula na sheria..baraza lilikalishwa kule Yerusalemu kisha mahojiana mengi yakaendelea …lakini mwishoni Mungu alitoa maarifa kwa kusema wajiepushe.na damu na uasherati lakini sio mataifa watwikwe tena kongwa la torati lililowashinda wao.(Matendo 15 )
Hivyo ni vema kumshirikisha pia mpendwa mwenzako/ kanisa mpango wako, yapo mashauri ya ki-Mungu ndani yao yaliyojaa hekima yatakusaidia.
Huu ni uwezo wa Mungu ambao mtu humwingia kutokana na kiwango chake cha juu cha ukuaji wa kiroho (Waebrania 5:14).. Bila kutegemea kuomba au kumuuliza Mungu mtu hutambua lililo la kweli na lililo la uongo.. lililosahihi na lisilosahihi, la rohoni au la mwilini, lenye Mwongozo wa ki- Mungu au kibinadamu. Tunaweza kujua mapenzi ya Mungu kwa ujuzi huu, unaozalika kutokana na ukomavu wetu wa kiroho.
Hivyo wewe kama mwana wa Mungu, kumbuka ni sharti kutembea ndani ya mapenzi yake…madhara ya kutembea nje ya hayo ndio kama yale aliyoyasema Bwana kwenye Mathayo Mathayo 7:21..
[21]Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha kwanza cha Petro.(1Petro)
SWALI: Je ni kitu gani hasaa kilikuwa kinatokea mpaka wafikie hatua kama ile, je! Ni utahira ulikuwa unawapata au ni nini hasaa?
JIBU: Silaha mojawapo ambayo tuona Mungu alikuwa akiitumia kuwashindania watu wake mara myingi wawapo vitani, Ni hii ya “machafuko” yaani Ni kuwavuraga maadui washindwe kuelewana na hatimaye kuanza kushambuliana wao kwa wao.
Kwamfano wa matukio kama hayo tunaweza kuyathibitisha katika habari hizi;
Wana wa Israeli Walipoizunguka Yeriko.
Waamuzi 7:22
[22]Wakazipiga zile tarumbeta mia tatu, naye BWANA akaufanya upanga wa kila mtu uwe juu ya mwenziwe, na juu ya jeshi lote, jeshi likakimbia mpaka Bethshita, kuendelea Serera, hata mpaka wa Abel-Mehola, karibu na Tabathi.
Sasa tuone ni njia zipi alikuwa anazitumia Mungu mpaka wauane wao kwa wao, watu ambao walikuwa wamekubaliana kabisa kwenda vitani?
Hii ni hali ya kutoweza fikiri vema, kuwa kama mtu fulani nusu aliyerukwa na akili.
Kumbukumbu la Torati 28:28
[28]BWANA atakupiga kwa wazimu, na kwa upofu, na kwa bumbuazi la moyoni;
Hii ni hali yakutokuwa sawa katika ufahamu, unamwona mwenzako kuwa ndiye adui, na hatimaye vita vinaanza kabla hata ya maadui wenyewe kufika..hili ndio yamkini Bwana alilowapiga watu wa Yeriko.
Kama tu vile Mungu alivyowapiga upofu watu wa Sodoma na Gomora wasione mlango wa Lutu, vivyo hivyo hawa wanapigwa katika eneo la fikra wasifiri vema wauane, wao kwa wao.
Hii ni namna ambayo mnapisha usemi. Kiasi kwamba hakuna mtu wa kumsikiliza mwenzake, huyu anataka hili, Yule hili, kila mmoja haafikiani na mwenzake hatimaye chuki inatokea, matengano na mwisho kuanza kupigana wao kwa wao.
Watu wa Babeli walipigwa ‘usemi’ isipokuwa tu wao hawakufikia hatua ya kuuana, lakini ni namna tu hii hii .(Mwanzo 10)
Hii ni hali ya kuwashuku wenzako kuwa ni wasaliti, hivyo ghafla kupoteza imani nao, na kuanzisha vita ili kujilinda…mfano wa hili tunaliona kwenye ile vita ya Yuda na majeshi ya wamoabu, waamoni na wameuni walipokutanika kupigana na taifa la Mungu..ghafla moabu Na amoni wakaipiga Seiri, halafu baadaye wakarudiana Wao kwa wao.
2 Mambo ya Nyakati 20:22-23
[22]Nao walipoanza kuimba na kusifu, BWANA akaweka waviziao juu ya wana wa Amoni, na Moabu, na wa mlima Seiri, waliokuja juu ya Yuda; nao wakapigwa.
[23]Kwani wana wa Amoni na wa Moabu waliwaondokea wenyeji wa mlima Seiri kuwaulia mbali na kuwaharibu; nao walipokwisha kuwakomesha hao wakaao Seiri, wakajitia kuharibu kila mtu mwenziwe.
Hii ya visasi inatokeaje?
Labda mmoja alikuwa na chuki na mwenzake, hivyo unamlipizia kisasi, na huyu naye kaona ndugu yake kauliwa anaamka kumtetea, mara kabila hili na hili hatimaye taifa zima linaiingia katika kujiharibu.
Hivyo Mungu anapotaka kutupigania, silaha hii huwa anaitumia hata katika agano jipya hususani hapo kwenye kugonganisha ndimi.
Kwamfano mtume Paulo alipokamatwa awekwe barazani ili ahukumiwe…kwa hekima ya Roho alipewa kujua kuwa katikati ya baraza wapo mafarisayo na masadukayo. Hivyo alilolifanya ni kuwachonganisha ndimi, badala ya kumshambulia yeye..wakaanza kushambuliana wao kwa wao…hiyo ni silaha ya Bwana ambayo kwa hekima ya Roho aliitamka..
Matendo ya Mitume 23:6-7
[6]Paulo alipotambua ya kuwa sehemu moja ni Masadukayo, na sehemu ya pili ni Mafarisayo, akapaza sauti yake katika ile baraza, Ndugu zangu, mimi ni Farisayo mwana wa Farisayo; mimi ninahukumiwa kwa ajili ya tumaini la ufufuo wa wafu.
[7]Alipokwisha kunena hayo palikuwa na mashindano baina ya Mafarisayo na Masadukayo, mkutano ukafarakana.
Ni vema kufahamu aina hii ya silaha ni mbaya kuliko ile ya kushindana na adui yako.
Lakini ni vema kufahamu kuwa hata shetani hutumia silaha hii, pale tunapotoka nje ya mpango wa Mungu.
Israeli iliingia kwenye vita vya wao kwa wao, na kupelekea mauaji mengi sana…
Ni nini kilitokea?
Baadhi ya wana wa Benyamini waliendekeza dhambi ya uasherati mpaka ikafikia hatua inayokaribia ile ya sodoma Na Gomora na Israeli yote ilipopata taarifa, wakataka wawatoe hao watu wauliwe, lakini wabenyamini wakawaficha kwasababu ni watu wa kabila lao. Machafuko yakaanzia hapo, hatimaye wakauana Sana. (Waamuzi 19-21)
Hata sasa silaha hii shetani hupenda kuirusha kwenye kanisa la Mungu, watu wapoteze upendo na utakatifu ili waanze kulana na kung’atana..kwasababu ya wivu, visasi na vinyongo.
Wagalatia 5:14-15
[14]Maana torati yote imetimilika katika neno moja, nalo ni hili, Umpende jirani yako kama nafsi yako.
[15]Lakini mkiumana na kulana, angalieni msije mkaangamizana.
Lazima tuijue hila hii ya shetani na kukataa kuipa nafasi.. Na Bwana atatuhifadhi, na matokeo itakuwa ni yeye kuleta machafuko kwa maadui zetu wanaposimama Kinyume na sisi.
Shalom
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je mapepo yanakufa? Na kama hayafi, tunashindanaje vita vya kiroho?
SWALI: Tukisoma Kitabu cha Waebrania tunaona mwandishi akitaja vitu viwili vya Mungu visivyoweza Kubadilika ambavyo tumepewa viwe kama nanga ya Roho, je ni vipi hivyo? Au Maana yake ni nini?
Waebrania 6:17-19
[17]Katika neno hilo Mungu, akitaka kuwaonyesha zaidi sana warithio ile ahadi, jinsi mashauri yake yasivyoweza kubadilika, alitia kiapo katikati;
[18]ili kwa vitu viwili visivyoweza kubadilika, ambavyo katika hivyo Mungu hawezi kusema uongo, tupate faraja iliyo imara, sisi tuliokimbilia kuyashika matumaini yale yawekwayo mbele yetu;
[19]tuliyo nayo kama nanga ya roho, yenye salama, yenye nguvu, yaingiayo hata mle mlimo ndani ya pazia,
JIBU: Ukisoma hiyo habari vifungu vya juu na vile vinavyoendelea mbele yake. Habari inayozungumziwa pale ni ya Ibrahimu na jinsi Mungu alivyompa ahadi ya mbaraka pamoja na uzao wake. Na jinsi alivyokuja kuitimiza
Lakini tunaonyeshwa ahadi ile pekee aliyopewa, haikutosha kumfanya Ibrahimu, aamini bali Mungu Ili kumthibitishia kuwa atavipokea kweli kweli basi aliongezea Na kiapo.
Mwanzo 22:15-17
[15]Malaika wa BWANA akamwita Ibrahimu mara ya pili kutoka mbinguni
[16]akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema BWANA, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee,
[17]katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao;
Kwasababu kiapo ni kifungo cha mwisho ambacho Mtu humaliza shuku zote, mashaka yote mijadala yote..
Ilimbidi Mungu aweke kiapo ijapokuwa angetimiza Ahadi zake bila kiapo. Lakini ilimbidi afanye vile ili kumpa uthabiti Ibrahimu juu ya maadhimio yake.
Hivyo mambo hayo mawili yasiyoweza Kubadilika ya Mungu ni;
1)Neno lake(ambalo lilikuja kama ahadi),
2) lakini pia Kiapo, ambacho hukata maneno yote.
Na kweli tunakuja kuona yote Mungu aliyomuahidi Ibrahimu yalitokea kama yalivyo..
Lakini Ahadi hiyo haikuishia kwa Ibrahimu, bali ilitimilizwa yote na Bwana wetu Yesu Kristo.
Ambao sisi tuliomwamini, tunaingizwa Katika ahadi hizo..alizozithibitisha Kwa kiapo kupitia Bwana wetu Yesu Kristo. Ambaye Mungu alimthibitisha kama kuhani mkuu wa milele mfano wa Melkizedeki kuhani Wa Ibrahimu (rohoni)..
Waebrania 7:21-25
[21](maana wale walifanywa makuhani pasipo kiapo; bali yeye, pamoja na kiapo, kwa yeye aliyemwambia, Bwana ameapa wala hataghairi, Wewe u kuhani milele;)
[22]basi kwa kadiri hii Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.
[23]Tena wale walifanywa makuhani wengi, kwa sababu wazuiliwa na mauti wasikae;
[24]bali yeye, kwa kuwa akaa milele, anao ukuhani wake usioondoka.
[25]Naye, kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai sikuzote ili awaombee.
Hivyo sisi tuna Neno la ahadi..kwamba tunaomwamini tunapokea uzima wa milele kama yeye.. Lakini pia jambo Hilo amelikolezea Kwa kiapo kuwa hatalibatilisha..Ni hakikisho kubwa sana..Haleluya!
Hivyo ni wajibu wetu kuendelea mbele kwaujasiri na bidiii katika imani na kumtumikia yeye kwasababu yupo pamoja nasi, wala kamwe hawezi kutuacha hata Iweje.
Kwasababu Neno lake ni hakika, alilotuahikikishia Na kiapo juu.
Je umempokea Bwana Yesu kwenye Maisha yako?. Fahamu kuwa hakuna tumaini lolote nje ya Kristo. Okoka leo.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
SWALI: Yule tajiri alimaanisha nini kumwambia Lazaro, achovye ncha ya kidole chake majini uuburudishe ulimi wake?
Luka 16:24
[24]Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.
JIBU:
Habari hiyo la Tajiri na Lazaro, Bwana Yesu aliieleza kufunua uhalisia wa jehanamu jinsi ulivyo… Na mambo ambayo mtu aliyeukataa wokovu atakutana nayo baada ya kifo.
Anaeleza jinsi yule tajiri alivyokufa katika hali ya dhambi..na hatimaye akajikuta mahali pale pa mateso, ambapo hakutana hata ndugu zake wafike, tunaona hata alipoomba mtu atokaye kwa wafu aende kuwahubiria ndugu zake akaambiwa hawatashawishwa…Ni kuonyesha kuwa mahali pale palikuwa pa mateso Sana, kiasi cha kutaka mwingine yeyote kufika.
Lakini tukio lingine tunaonyeshwa akimwomba Ibrahimu Amruhusu Lazaro achovye ncha ya kidole Chake majini amburudishe ulimi wake, nalo pia akaambiwa haiwezekaia kwasababu kuna kizuizi kikubwa Sana katikati yao.
Sasa swali linakuja tukio lile linamaana gani Je kiu kile ni halisi au ni ufunuo?.
Bwana Yesu alipokuja duniani.. aliona Dunia nzima ina Kiu kikubwa sana.. na hivyo inahitaji maji ya kuweza iponya.
Sasa maji inayohitaji sio haya ya mtoni..bali maji ya rohoni ambayo ni ya uzima, na mtu pekee awezayo kutoa hayo ni yeye mwenyewe..hakuwahi kutokea mtu aliyeweza kuyatoa.
Kama tunavyojua mwili ukikosa maji, mwishowe utakufa..Ndivyo ilivyokuwa sisi sote, hapo mwanzo kabla ya Kristo, Wote tulikuwa wafu kiroho..
Utauliza vipi kwa watakatifu wa kale kama akina Musa na Eliya?…Wale walikuwa wanaishi kwa ahadi ya Kristo, Hivyo walitii madhihirisho yake aliyokuwa akijifunua kwao kwa namna mbalimbali huku wakiiongejea ahadi kamili ya ukombozi ambayo alikuja kuikamilisha yeye mwenyewe (Yesu Kristo) alipofufuka Katika wafu..(waebrania 11)
Yeye mwenyewe Alisema..
Yohana 7:37-39
[37]Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe.
[38]Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.
[39]Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.
Sasa kiu hii ni ya nini?
Ya maisha….
Tangu zamani mwanadamu amekuwa akitafuta ‘maisha’ ambayo hata sasa hajayapata…ndio maana wengi wanakimbilia kutafuta elimu, fedha na utajiri wakidhani kuwa ndio wamepata maisha, lakini hivyo vipo mbali sana na maisha …vitakufanya ule vizuri tu, unywe vizuri, ulale vizuri kama maandalizi ya heri ya kifo chako baadaye..kwasababu Haviwezi kukudumishia maisha.. vinapooza tu kiu..lakini haviondoi kiu.
Yesu amekuja kuondoa kiu.
Sasa watu Ambao watapuuzia kuyapokea maji hayo ambayo Yesu anatupa…wakifa Katika hali hiyo hiyo huko waendapo ni majuto makubwa.
Kwasababu watataka hata tone dogo la maji hawatapata…yaani kiwango kidogo tu cha neema ya uzima hawatapata…
Leo Yesu hatupi maji tu, kwa kipimo fulani bali anapanda kabisa chemchemi za maji ndani yetu Ambazo zinabubujika uzima wa milele.
Yohana 4:14
[14]walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.
Madhara ya kukosa maji ya uzima si tu baada ya kufa…hata hapa Hapa duniani.. mtu ambaye hana Kristo rohoni anajulikana kama nchi kamena matokeo yake ni kuwa makao ya mapepo yanakuwa Ndani yake hata kama hujui..
Angalia Yesu alichokisema juu ya hilo.
Mathayo 12:43-45
[43]Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, asipate.
[44]Halafu husema, Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa, na kupambwa.
[45]Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya.
Yanakwenda mahali pasipo na maji…yaani moyo ambao hauna Kristo ndani yake.
Ndugu…umeona hatari waliyonao wenye dhambi, hapa duniani na baada ya kifo?
Shetani asikupumbaze, tubu leo kwa kumpokea Bwana Yesu katika maisha yako ili upate ondoleo la dhambi zako haraka sana.
Hizi ni siku za mwisho, dunia hii inakwisha…vilevile hujui ni siku Gani utakufa…Acha kuchezea maisha yako, ukafanana na yule tajiri aliyekosa maji ya uzima angali akiwa hai.
Okoka leo..
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
SWALI: Bwana Yesu alikuwa na maana gani kusema ‘haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu’.
Luka 13:33
[33]Pamoja na hayo imenipasa kushika njia yangu leo na kesho na kesho kutwa; kwa kuwa haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu.
JIBU: Bwana Yesu alikuwa anaeleza asili ya mji wa Yerusalemu nyakati zote ulivyokuwa wa mauaji, mji ambao ungepaswa uwe wa kupokea manabii wa Mungu, lakini kinyume chake uligeuka mji wa kuwaua Manabii…
Sasa kusema maneno yale ni kutokana na taarifa aliyoletewa na wale mafarisayo kuwa Herode anataka kumwangamiza, hivyo aondoke pale aende mji mwingine…ndipo Bwana Yesu akawaambia ‘haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu’ yaani haipaswi nabii afe nje ya Yerusalemu…
Manabii wengi wa Mungu, waliuliwa pale pale Yerusalemu hivyo hata na yeye kuangamia hapo si jambo geni, …
Na ndivyo ilivyokuwa
Mfano wa hao katika maandiko alikuwa;
Zekaria mwana wa Yehoyada (2Nyakati 24:20-21). Ambaye aliuliwa hekaluni
Mwingine ni Uria nabii (Yeremia 26:20 – 24)
Na manabii wengine wengi ambao hawajatajwa, moja kwa moja katika maandiko waliuawa Yerusalemu…ndio sababu ya Yesu kusema maneno Haya;
Mathayo 23:37-39
[37]Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka!
[38]Angalieni, nyumba yenu mmeachiwa hali ya ukiwa.
[39]Kwa maana nawaambia, Hamtaniona kamwe tangu sasa, hata mtakaposema, Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana.
Jambo hili hujirudi sasa rohoni..
Watu wote ambao wanaipinga injili mioyoni mwao leo, hata kama hawajashiriki moja kwa moja kuwarushia mawe watu wa Mungu, ni shirika moja tu na wale waliokuwa wanawaua manabii wa Bwana zamani.
Ndivyo walivyodhani mafarisayo kwamba wenyewe hawahusiki na mauaji ya manabii wa Bwana, angali wanampinga yeye waziwazi, kwa unafiki wao aliwaambia maneno haya..
Mathayo 23:29-36
[29]Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnayajenga makaburi ya manabii, na kuyapamba maziara ya wenye haki,
[30]na kusema, Kama sisi tungalikuwako zamani za baba zetu, hatungalishirikiana nao katika damu ya manabii.
[31]Hivi mwajishuhudia wenyewe, ya kwamba ninyi ni wana wao waliowaua manabii.
[32]Kijazeni basi kipimo cha baba zenu.
[33]Enyi nyoka, wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanum?
[34]Kwa sababu hiyo, angalieni, mimi natuma kwenu manabii na wenye hekima na waandishi; na wengine wao ninyi mtawaua na kuwasulibisha, na wengine wao mtawapiga katika masinagogi yenu, na kuwafukuza mji kwa mji;
[35]hivyo ije juu yenu damu yote ya haki iliyomwagika juu ya nchi, tangu damu ya Habili, yule mwenye haki, hata damu ya Zakaria bin Barakia, mliyemwua kati ya patakatifu na madhabahu.
[36]Amin, nawaambieni, Mambo hayo yote yatakuja juu ya kizazi hiki.
Hii ni hatari kubwa sana kwa walio nje ya Kristo.
Mwamini Yesu leo uoshwe dhambi zako. Upokee uzima wa milele. Kwingineko si salama.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Yesu alikuwa na maana gani aliposema ‘tena siku ile hamtaniuliza neno lolote (Yohana 16:23)
MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.